CHADEMA ikishinda vita ya propaganda itachukua nchi 2015

meningitis

JF-Expert Member
Nov 17, 2010
8,349
4,674
Umebakia muda mchache tu kabla ya CHADEMA kutangaza ushindi 2015.

Kwa sasa CCM imeamua kuanzisha vita ya kipropaganda kupitia mitandao ya kijamii na magazeti. Nina hakika hii ni silaha ya mwisho kwa CCM na pale tutakapoweza kuishinda basi njia ya CHADEMA kushika nchi 2015 itakuwa nyeupe.

CCM imeshakataliwa mjini na vijijni, pia imekataliwa na waislamu kwa wakristo,wazee kwa vijana, tunahitaji busara za hali ya juu kupambana na propaganda.

Tumeanza na mungu tutamaliza na mungu.
 
Ni wazi kwamba CCM sasa imeingia kwenye vita mpya na CDM.Vita hiyo ni ya Propaganda na inapiganiwa kwenye mlango wa CDM.

CCM sasa imeamua kuwanunua baadhi ya vijana waliofukuzwa CDM na kupita huku na huko wakijitambulisha eti ni viongozi wa CDM na wanawachafua viongozi wa CDM hasa Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Katika hali ya kushangaza vijana hao wanapata Airtime ya kutosha kwenye TV,Radio na Magazeti Maalum.

Ni wakati sasa wa kitengo cha habari na uenezi CDM kuwa imara kupambana na Propaganda hizi chafu ambazo zinaweza kukiathiri chama hasa kwa watu wasio waelewa sana.

Nawaalika wanajamvi kutoa mchango wa mawazo kwa kitengo hicho kinachoongozwa na John Mnyika na Tumaini Makene.

Lakini mwisho niseme mdharau mwiba mguu huota tende.CDM wameshauriwa mara nyingi kupambana na waasi ndani ya Bavicha wakawadharau,sasa waasi hao wameota mapembe wanaitisha mikutano ya waandishi kumtisha Dr Slaa.Kama Baba mwenye nyumba anatishwa tuzidi kukaa kimya?
 
Hali si shwari ndani Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA).Makundi ya wahuni yameanza kujitokeza ama kupandikizwa,msipokuwa makini hakika hamfiki mbali.Katiba ya Vyama hivi vyote vya siasa hakuna sehemu inayosema mtu akihama chama fulani kwenda chama kingine lazima arudishe kadi yake.

Pia nawaasa vijana hawa wanao jiita BAVICHA kama kweli elimu yao ni kwa faida ya umma wajaribu kuisoma katiba ya chama chao kabla ya kuita press conference na kuropoka.Ki kawaida kuna vikao vya chama ambavyo ni halali ambavyo vinaweza kusikiliza hoja zao kuliko njia ya kihuni ambayo mwisho wa siku inaonekana ni kikundi fulani kilicho kosa nidhamu nadni ya jamii na kupokea mlungula ambao si tu kuupoza njaa zao bali ni pamoja na kuwa dhalilisha.

Kiko wapi kigezo cha elimu ikiwa wanashindwa kufuata taratibu ambazo zinazo kubalika kisheria kwa mujibu wa kanuni na sheria walizojiwekea ndani ya katiba inayoongoza chama chao.

Kamati kuu naamini haijafikishiwa scandal hii ,lakini ikiachiwa ikapita hivi hivi bila kurugenzi ya habari kulizungumzia suala hili kwa usafaha , wananchi watakuwa njia panda.Lakini haitoshi kulalamika kwenye vyombo vya habari bila kulifikisha ndani ya vikao halali vya chama na kutolewa maamuzi hapo ndipo tutakuwa na imani kuwa vijana hawa ni wanachama wa CDM na wana fahamu taratibu za chama .

CHADEMA hii ni assignment msiipuuze inataka itolewa ufafanuzi wa kina.
 
Kweli mkuu umesema kweli tatizo la vijana njaa kali! Ila kama watapewa elimu ya kutosha ni kwa jinsi gani tupigane hadi kumwondoa huyu mkoloni mweusi tutashinda. Ona wenzetu Kenya wanakoelekea wametoka mbali na nina uhakika watafika mbali. Ukija huku nje wazungu wamesha wagrade wakenya, na wanasema kabisa Kenyans will go far because they have shown struggle. NAPE HIZI DAMU ZINA KULILIA I AM TELLING YOU YOU WILL REMEMBER THIS!!! TIME WILL TELL
 
Vita tupiganavyo si ya damu na nyama bali vita dhidi ya falme za nguvu za giiza!
 
Viongozi wote wa cdm kuweni makini wakati huu,sisi wapenda mabadiliko tuko nyuma yenu. Kama kuna waasi wasiofuata taratibu za chama waanzishe chama chao. Suala la dr kuwa na kadi,mbona vijana wa uvccm hawajashinikiza nape kuachia ngazi? Kwa kuwa na kadi ya ccj? Wana chadema tusidanganyike hiyo ni janja ya ccm!
 
Ukweli ni kwamba CCM imeshajua kuwa hali yake ni mbaya na Dr Slaa ni silaha ya maangamizi kwao, kwahiyo wameamua kutumia kila silaha waliyonayo kupambana na CHADEMA! Tunahitaji kujipanga kwani silaha yao kubwa ni fedha, kwa kutumia fedha watanunua vijana wetu, watanunua vyombo vya habari kusambaza uongo wao! Tunahitaji kuendelea kuwa Imara na tumuombe Mungu zaidi kwa tunapambana na SHETANI CCM uso kwa usa sasa! Propaganda zao nyingi zimeshindwa kufanikiwa sasa wanaanza kutengeneza uadui ndani ya CHADEMA kwa kuwatumia wananchadema wenyewe! Mungu Ibariki Tanzania, Mungu ibariki CHADEMA.
 
Ni wazi kwamba CCM sasa imeingia kwenye vita mpya na CDM.Vita hiyo ni ya Propaganda na inapiganiwa kwenye mlango wa CDM.

CCM sasa imeamua kuwanunua baadhi ya vijana waliofukuzwa CDM na kupita huku na huko wakijitambulisha eti ni viongozi wa CDM na wanawachafua viongozi wa CDM hasa Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Katika hali ya kushangaza vijana hao wanapata Airtime ya kutosha kwenye TV,Radio na Magazeti Maalum.

Ni wakati sasa wa kitengo cha habari na uenezi CDM kuwa imara kupambana na Propaganda hizi chafu ambazo zinaweza kukiathiri chama hasa kwa watu wasio waelewa sana.

Nawaalika wanajamvi kutoa mchango wa mawazo kwa kitengo hicho kinachoongozwa na John Mnyika na Tumaini Makene.

Lakini mwisho niseme mdharau mwiba mguu huota tende.CDM wameshauriwa mara nyingi kupambana na waasi ndani ya Bavicha wakawadharau,sasa waasi hao wameota mapembe wanaitisha mikutano ya waandishi kumtisha Dr Slaa.Kama Baba mwenye nyumba anatishwa tuzidi kukaa kimya?

-Propaganda chafu ndiyo nguzo yao.Kwa bahati mbaya sana CCM wamekua wakitumia vijana ambao uwezo wao tunaujua.Hata vibaraka wao waliobaki ni harmless.Naendelea kutoa wito.Tuchukue hatua kali

-Juzi wameleta.machafuko facebook hasa TANURU LA FIKRA,Cha motto wamekiona.

Tusikubali kukaa nabtraitors miongoni mwetu.Tuwapeleke kunakostahili
 
Hao mamluki wanaopandikizwa na Magamba ya ccm watambue kuwa Mwisho wa Ubaya ni Aibu!!!! chadema tutachukua Nchi na kila fisadi alie fisidi mali ya Umma atarudisha mpaka ile sent ya Mwisho Hili halipingiki kwa vyovyote...
 
kama tuliweza kupambana na matusi kwa dr slaa 2010 kwa nini ishindikane leo hii.M4C iongezewe kasi.
 
M4C go... nawaamini makamanda wangu kwani hizo hila waliwafanyia kina mrema enzi zile, wakasambaratika kule Tanga. tena wakaleta hila za kidini kwa cuf wakafifia kwa kukosa namna ya kujinasua hadi cuf wakabaki kukubali hali hiyo ya kuwa ya udini. sasa hapa wamepiga ngoma ya sikinde kwa wamakonde. wataipenda!
 
Watashindana na CHADEMA lakini hawatashinda,
watawanunua na kuwadanganya wachache kwa muda mchache,hawawezi kudanganya watu wote kwa muda wote.Hakuna silaha wala jeshi lolote Duniani linaloweza kushindana na nguvu ya umma,wala kuzuia mabadiliko.Mabadiliko ni sasa,na hakuna wa kuzuia
 
-Propaganda chafu ndiyo nguzo yao.Kwa bahati mbaya sana CCM wamekua wakitumia vijana ambao uwezo wao tunaujua.Hata vibaraka wao waliobaki ni harmless.Naendelea kutoa wito.Tuchukue hatua kali

-Juzi wameleta.machafuko facebook hasa TANURU LA FIKRA,Cha motto wamekiona.

Tusikubali kukaa nabtraitors miongoni mwetu.Tuwapeleke kunakostahili

...Taratibu unaelekea kwenye "akili ndogo" kisiasa, geuka kabla haujazama, Siasa za Ufuasi hazidumu lakini siasa za fikra huru zitadumu ata pale wabebaji watakapogota, hii ndio tofauti ya vijana makini wanaoweza kusimama kwa miguu yao wenyewe na vijana hohehahe wanaosubiri tu kubebwa kwenye mbeleko...
 
-Wanaofanya siasa za ufuasi wanajulikana

-Kama fikra huru ni kutukana matusi badala ya kujenga hoja basi sitaki kuwa na fikra hizo

-Narudia hakuna msaliti atakayeambatana nasi katika mapambano haya
 
kinachonifurahisha ni kwamba ccm inapambana na nguvu ya umma na sio chadema.
 
-Wanaofanya siasa za ufuasi wanajulikana

-Kama fikra huru ni kutukana matusi badala ya kujenga hoja basi sitaki kuwa na fikra hizo

-Narudia hakuna msaliti atakayeambatana nasi katika mapambano haya

....Wenye fikra za kifuasi wapo wazi,na wanaonekana kwa maneno na matendo yao, wapo tayari ata kurusha ngumi ilmuradi wamtetee "mtu" badala ya "fikra", na upo katikati ya kundi hilo sasa, ukishakuwa ana "akili ndogo hizi" hauwezi kusimama kwa miguu yako, tegemea mbebaji tu...

....Umaarufu wa Chadema ukiyeyuka, wanasiasa wengi waliopo Chadema leo ndio utakuwa mwisho wa fani yao ya siasa kwa sababu hawajajipambanua kwa wananchi kama wanaweza kusimama wenyewe, ata akina Masumbuko Lamwai wanalijua hili...

...LAKINI ata ANC ikifa leo-Kijana Malema atabaki, ata Kibaki alipomgeukia ndani ya NARC-Raila Odinga alibaki, ata ODM ilipomgeukia-Ruto alibaki, na ata changamoto ya ICC ilipokuja-Uhuru Muigai alibaki, ata Chadema ikifa leo-Zitto atabaki, kwanini? hawategemei upepo wa "mtu" wala "matukio", wanaweza kusimama kwa miguu yao...
 
....Wenye fikra za kifuasi wapo wazi,na wanaonekana kwa maneno na matendo yao, wapo tayari ata kurusha ngumi ilmuradi wamtetee "mtu" badala ya "fikra", na upo katikati ya kundi hilo sasa, ukishakuwa ana "akili ndogo hizi" hauwezi kusimama kwa miguu yako, tegemea mbebaji tu...

....Umaarufu wa Chadema ukiyeyuka, wanasiasa wengi waliopo Chadema leo ndio utakuwa mwisho wa fani yao ya siasa kwa sababu hawajajipambanua kwa wananchi kama wanaweza kusimama wenyewe, ata akina Masumbuko Lamwai wanalijua hili...

...LAKINI ata ANC ikifa leo-Kijana Malema atabaki, ata Kibaki alipomgeukia ndani ya NARC-Raila Odinga alibaki, ata ODM ilipomgeukia-Ruto alibaki, na ata changamoto ya ICC ilipokuja-Uhuru Muigai alibaki, ata Chadema ikifa leo-Zitto atabaki, kwanini? hawategemei upepo wa "mtu" wala "matukio", wanaweza kusimama kwa miguu yao...

-Badala ya kujenga hoja unajiropokea tu.Unadhihirisha ulivyo narrow minded kwa kutaja majina ya watu.Huu ndio ufuasi kipofu(blind follower) tunaousema hapa.Grow up.I think i should ignore you hadi pale utakapojenga hoja ambazo ni credible
 
....Wenye fikra za kifuasi wapo wazi,na wanaonekana kwa maneno na matendo yao, wapo tayari ata kurusha ngumi ilmuradi wamtetee "mtu" badala ya "fikra", na upo katikati ya kundi hilo sasa, ukishakuwa ana "akili ndogo hizi" hauwezi kusimama kwa miguu yako, tegemea mbebaji tu...

....Umaarufu wa Chadema ukiyeyuka, wanasiasa wengi waliopo Chadema leo ndio utakuwa mwisho wa fani yao ya siasa kwa sababu hawajajipambanua kwa wananchi kama wanaweza kusimama wenyewe, ata akina Masumbuko Lamwai wanalijua hili...

...LAKINI ata ANC ikifa leo-Kijana Malema atabaki, ata Kibaki alipomgeukia ndani ya NARC-Raila Odinga alibaki, ata ODM ilipomgeukia-Ruto alibaki, na ata changamoto ya ICC ilipokuja-Uhuru Muigai alibaki, ata Chadema ikifa leo-Zitto atabaki, kwanini? hawategemei upepo wa "mtu" wala "matukio", wanaweza kusimama kwa miguu yao...

-Badala ya kujenga hoja unajiropokea tu.Unadhihirisha ulivyo narrow minded kwa kutaja majina ya watu.Huu ndio ufuasi kipofu(blind follower) tunaousema hapa.Badala ya kujenga taasisi unataka watu wajijenge.Grow up.I think i should ignore you hadi pale utakapojenga hoja ambazo ni credible
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom