Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,830
Ujumbe wangu ni mfupi tu kwa viongozi wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA.
Jitafakarini upya kuhusu mwenendo wa chama, mifumo ya uongozi, sera za Chama, namna mnavyoshughulika na masuala ya ndani ya chama, masilahi ya mtu mmoja mmoja chamani, umoja wa chama n.k. Haya mambo yaangaliwe kwa jicho la tatu.
Ni dhahiri sasa kuwa hawa wabunge,madiwani na wanachama wenu wanao hama chama kila siku si kwa sababu wananunulia kama mnavyoamini/kuaminisha watu, kutakuwa na tatizo la kiuongozi.
Katika hili wala msitafute mchawi, ni ninyi wenyewe ndio sababu na msipo badilika mtaendelea kupoteza watu wengine makini chamani.
Hivi karibuni mmekuwa mkifanya maamuzi ya kushangaza sana kwenye mambo ya msingi mfano.
Kumchagua Lissu kuwa makamo mweyekiti wakati mtu hayupo hata nchini na anadai hatorudi nchini kuhofia usalama wake.
Alafu yeye ndio makamo mwenyekiti, katika hili mmekosea sana. Sijui kama wote mlikubaliana hili sina hakika.
Uamuzi wa kuondoka bungeni kisa Covid-19, huu uamuzi kwa asilimia mia moja mlikurupuka haukuwa uamuzi sahihi na sina hakika pia kama ulikubaliwa na wengi ndani ya chama.
Tuhuma za ubadhilifu na ufisadi ndani ya chama, hili nalo ni tatizo kubwa sana hili ambalo linaendelea kuota mizizi ndani ya chama mfano mweyekiti anatuhumiwa kwa matumizi mabaya na upotevu wa bil 8.
Malalamiko ya wabunge kukatwa mishara yao kwa kiwango kikubwa, hili pia linawaumiza wengi ndani ya chama.
Kujiingiza kwenye kesi zisizokuwa za lazima na kutia hasara chama, mfano kufanya fujo gerezani kule segerea.
Kauli zisizokuwa na mipangilio mfano kauli ya mch Msigwa kusema kuwa alimsingizia kinana ujangili, anaomba radhi inamaana kuna mengi pia waliwasingizia viongozi wa serikali? Ester Bulaya kuwatumikia mabeberu n.k
Kuja na majina ya uteuzi mifukoni, ubabe wa mwenyekiti n.k
Kutokuwepo kwa Uhuru wa maoni ndani ya chama, mwenyekiti kudaiwa kuwaburuza tu wajumbe kwenye maamuzi.
Matamko wanayo yatoa hasa kwenye kipindi hiki cha Janga la Covid-19.
Hayo yote yanaweza kuwa sababu ya mpasuko wa chama kwa wale wenye nia ya mabadiliko ya kweli wanaweza kukihama chama na wala si kununuliwa kama inavodaiwa sasa.
Niwakati sasa wakukaa pamoja muyaangalie madhaifu yenu muone wapi mnakosea ili msizidi kupoteza Imani kwa watanzania.
Jitafakarini upya kuhusu mwenendo wa chama, mifumo ya uongozi, sera za Chama, namna mnavyoshughulika na masuala ya ndani ya chama, masilahi ya mtu mmoja mmoja chamani, umoja wa chama n.k. Haya mambo yaangaliwe kwa jicho la tatu.
Ni dhahiri sasa kuwa hawa wabunge,madiwani na wanachama wenu wanao hama chama kila siku si kwa sababu wananunulia kama mnavyoamini/kuaminisha watu, kutakuwa na tatizo la kiuongozi.
Katika hili wala msitafute mchawi, ni ninyi wenyewe ndio sababu na msipo badilika mtaendelea kupoteza watu wengine makini chamani.
Hivi karibuni mmekuwa mkifanya maamuzi ya kushangaza sana kwenye mambo ya msingi mfano.
Kumchagua Lissu kuwa makamo mweyekiti wakati mtu hayupo hata nchini na anadai hatorudi nchini kuhofia usalama wake.
Alafu yeye ndio makamo mwenyekiti, katika hili mmekosea sana. Sijui kama wote mlikubaliana hili sina hakika.
Uamuzi wa kuondoka bungeni kisa Covid-19, huu uamuzi kwa asilimia mia moja mlikurupuka haukuwa uamuzi sahihi na sina hakika pia kama ulikubaliwa na wengi ndani ya chama.
Tuhuma za ubadhilifu na ufisadi ndani ya chama, hili nalo ni tatizo kubwa sana hili ambalo linaendelea kuota mizizi ndani ya chama mfano mweyekiti anatuhumiwa kwa matumizi mabaya na upotevu wa bil 8.
Malalamiko ya wabunge kukatwa mishara yao kwa kiwango kikubwa, hili pia linawaumiza wengi ndani ya chama.
Kujiingiza kwenye kesi zisizokuwa za lazima na kutia hasara chama, mfano kufanya fujo gerezani kule segerea.
Kauli zisizokuwa na mipangilio mfano kauli ya mch Msigwa kusema kuwa alimsingizia kinana ujangili, anaomba radhi inamaana kuna mengi pia waliwasingizia viongozi wa serikali? Ester Bulaya kuwatumikia mabeberu n.k
Kuja na majina ya uteuzi mifukoni, ubabe wa mwenyekiti n.k
Kutokuwepo kwa Uhuru wa maoni ndani ya chama, mwenyekiti kudaiwa kuwaburuza tu wajumbe kwenye maamuzi.
Matamko wanayo yatoa hasa kwenye kipindi hiki cha Janga la Covid-19.
Hayo yote yanaweza kuwa sababu ya mpasuko wa chama kwa wale wenye nia ya mabadiliko ya kweli wanaweza kukihama chama na wala si kununuliwa kama inavodaiwa sasa.
Niwakati sasa wakukaa pamoja muyaangalie madhaifu yenu muone wapi mnakosea ili msizidi kupoteza Imani kwa watanzania.