Travelogue_tz
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 848
- 1,212
Habari JF
Kumekuwa na mtazamo tofauti juu ya kuhama Kwa Mhe Laurance Masha ambae ameamua kurudi CCM.
Licha ya kwamba ni haki yake kikatiba, ukweli ni kwamba zipo sababu nyingine zinazoweza kurudisha Masha Lau CCM.
1. Kwa kuwa Masha amekuwa sehemu ya utawala, inawezekana njia zake sio Safi na hivyo kutoa fursa kwa maadui zake (CCM) kumtisha na akatishika.
2. Kupoteza fursa za kimaisha - Masha alipata kizingiti kutoka kwa CCM wenzake wakati wa kutafuta uteuzi wa Ubunge wa Afrika Mashariki - pengine vizingiti hivi vimeendelea katika baadhi ya fursa zake zenye mafungamano na chama tawala.
3. Hofu ya jaribio LA kuuwawa kwa Tundu Lissu na Kulipuliwa kwa EMMMA Advocates inawezekana pia kuchochea hofu dhidi ya maisha yake binafsi.
4. Vitisho dhidi ya wakosoaji na wanaohama CCM, Kama jinsi Lazaro Nyalandu anavyobambikiziwa baada tu ya kuhama chama?
Katika hali hii ni vyema chadema kufungua fursa zaidi kwa wana CCM, tofauti na hapo kutapelekea CCM kuwa na nguvu zaidi ya kimaamuzi dhidi ya wakosoaji wake kwa kujua kwamba baada ya kuwafukuza watakuwa hawana pa kukimbilia.
Magufuli angependa kuwa na mamlaka ya kuamua hatma ya wanasiasa wote, hili la kuhamia chadema linamkera zaidi.
Kumekuwa na mtazamo tofauti juu ya kuhama Kwa Mhe Laurance Masha ambae ameamua kurudi CCM.
Licha ya kwamba ni haki yake kikatiba, ukweli ni kwamba zipo sababu nyingine zinazoweza kurudisha Masha Lau CCM.
1. Kwa kuwa Masha amekuwa sehemu ya utawala, inawezekana njia zake sio Safi na hivyo kutoa fursa kwa maadui zake (CCM) kumtisha na akatishika.
2. Kupoteza fursa za kimaisha - Masha alipata kizingiti kutoka kwa CCM wenzake wakati wa kutafuta uteuzi wa Ubunge wa Afrika Mashariki - pengine vizingiti hivi vimeendelea katika baadhi ya fursa zake zenye mafungamano na chama tawala.
3. Hofu ya jaribio LA kuuwawa kwa Tundu Lissu na Kulipuliwa kwa EMMMA Advocates inawezekana pia kuchochea hofu dhidi ya maisha yake binafsi.
4. Vitisho dhidi ya wakosoaji na wanaohama CCM, Kama jinsi Lazaro Nyalandu anavyobambikiziwa baada tu ya kuhama chama?
Katika hali hii ni vyema chadema kufungua fursa zaidi kwa wana CCM, tofauti na hapo kutapelekea CCM kuwa na nguvu zaidi ya kimaamuzi dhidi ya wakosoaji wake kwa kujua kwamba baada ya kuwafukuza watakuwa hawana pa kukimbilia.
Magufuli angependa kuwa na mamlaka ya kuamua hatma ya wanasiasa wote, hili la kuhamia chadema linamkera zaidi.