Chadema Iendelee Kufanya Iliyoyafanya Hadi Kufika Hapa Ilipo Sasa…….

VoiceOfReason

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
5,194
1,355
Mimi kama mtu ninayeamini nchi haiwezi kufika popote bila upinzani wa kweli Ninaomba Chadema iendelee kufanya mambo iliyoyafanya (with less MPS) hadi kukua kwa kasi kwa muda mfupi na iendelee kuyafanya hayo hayo…. na sio hii media frenzy inayotokea sasa na behind the scenes issue kuleak…. wananchi don’t need to know misukosuko ya kawaida ndani ya Chama (Dirty Linens should not be washed in Public)

Wananchi waliipenda Chadema Kwa yafuatayo Na Haya ndio inabidi iconcentrate kufanya:-

Kwa kutumia makamanda wake wabunge walionyesha kufatilia kwa karibu serikali na kuwa vocal kwa kuibana serikali pale inapokosea…..

Wabunge kuwa karibu na wananchi wake na kuleta maendeleo kwa wananchi….

Kuwa mwiba wa mafisadi na kuwafichua kila inapobidi… kuleta hoja zinazojenga nchi (na sio kwenda kwenye media na kusema sijui nani ni dikteta kwenye chama changu.... au sikubaliani na maamuzi ya fulani ndani ya Chama)

Waliweza kufanya hayo juu wakiwa na makamanda wachache (kati yao ni Slaa, Zitto, na Mdee) sasa wana makamanda 500% zaidi kwahiyo impact inabidi iwe multiplied by 500.

Pia kama kuna jambo la kufanya la kuwajibisha mtu inabidi lifanyika ndani ya chama as soon as possible na limelizike ili watu waendelee na kazi sio kila siku same stories ambazo hazina tija..... Pia waache kuongea na Media kama tunavyojua media zetu bongo food poisoning inaweza ikabadilishwa ikawa mtu kanyeshwa sumu
 
I agree with you that your are the voice of reason.Cdm now is a time for making things move for 2015. Muachane na migogoro kwani inapoteza muda
 
Yaani walichofanya Chadema na wale wabunge wachache kilikuwa bora kuliko sasa yanayofanyika wakiwa na wabunge lukuki... (mifarakano ipo kila mahali hata kwenye familia zetu, lakini wananchi hatuhitaji kuyajua hayo)
 
Kwa mtaji wa wabunge walionao its a perfect combination..... they just need to be utilised.....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom