CHADEMA huu ndio uwe moja ya misingi ya kudai mabadiliko ya katiba

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,346
6,469
:target:Misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 (Toleo la 20 Juni 2005)

KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani.

NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia, ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na serikali yenye kufuata misingi ya kidemokrasia, ujamaa na isiyokuwa na dini.

{kwa misingi hii ya katiba yetu basi masharti au ibara zote zisizofuata misingi hii minne uhuru, haki, udugu na amani yafutwe mara moja kwa kutumia Bunge Maalum kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015 bila mjadala mrefu baada ya kukusanya maoni ya wananchi kutoka kwenye kila jimbo la uchaguzi}

Baadhi ya masharti au ibara zinazofuata misingi ya katiba

Ibara ya 3
(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, isiyokuwa na dini, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa

Ibara ya 8
(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya kidemokrasia na haki ya jamii; na kwa hiyo:
(a) Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa katiba hii
(b) Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi

Ibara ya 13
(1) watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kuptata haki sawa mbele ya sheria
(2) ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake

Ibara ya 107A
(1) Mamlaka yenye kauli ya mwisho ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa in Mahakama.

Baadhi ya masharti/ vifungu/ibara ambazo hazifuati misingi ya katiba

Ibara ya 41
(7) Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.

[ibara hii inapinga ibara ya 3(1), 8(1), 13 (1) and (2), na 107A(1) na kwa maana hiyo inapinga misingi ya katiba yetu bila kuwa na sababu yoyote aidha ya sababu ya ovyo au msingi.

Maswali ya Msingi: Je, wagombea wa Urais wa vyama vingine kama ibara ya 3 (1) inavyosema wakinyimwa haki waitafute vipi wakati/ waipate vipi? Kwenda msituni? Kuandamana barabarani? Wabunge wao kutoka nje ya Bunge wakati Rais akitoa hotuba? Matokeo ya Udiwani na Ubunge yanachunguzwa mahakamani kwa sababu wagombea ni zaidi ya mmoja, sasa iweje haya ya Urais yenye mgombea zaidi ya mmoja yasichunguzwe kama haki ambayo ni msingi wa katiba kama imetendeka?]

Ibara ya 74
(12) Hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza jambo lolote lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya katiba hii.

[ibara hii inapingana na ibara ya 3(1), 8(1), 13 (1) and (2), 74 (5) na 107A(1) lakini hasa ibara ya 107A(1) bila sababu yoyote aidha ya msingi au ya ovyo.
Maswali ya Msingi: Je, haki isipotendeka itajulikana vipi, na itatafutwa vipi hasa kwa wagombea Urais wakati mahakama ndio chombo cha kutoa haki (ibara ya 107A(1)? Sasa kama mahakama ndio chombo chenye kauli ya mwisho kwenye utoaji haki, haki ya hawa wagombea wa Urais iliyopokonywa itatolewa na nani? Rais? Kama Rais, mbona katiba haisemi? Je, Tume ya Uchaguzi inaendeshwa na ‘malaika wema waliotelemka kutoka Mbinguni’? Kama ndio, misingi ya katiba inasema nchi yetu aina dini! Rais atajuaje kama Tume ya Uchaguzi haitendi haki bila mahakama ili aweze kutimiza masharti ya ibara ya 74 (5)? ]
 
Back
Top Bottom