CHADEMA hubirini dhambi ya CCM kwa chopa kijiji hadi kijiji

dr. gracemary

Member
Jul 7, 2011
32
6
Kwa vyovyote vile mwaka 2015 tunahitaji rais mpya, na maandalizi ni lazima yaanze sasa, wanachi wameisha ichoka ccm, huko kanda ya kati tumeshuhudia wenyewe...watu wameuwawa ili wengine washinde HADI WANAWAKE WENZANGU, inauma sana!. Nawaomba sana CDM anzeni sasa hivi kuzunguka kijiji hadi kijiji ili kuwaambia wananchi makosa ya CCM na sababu kwa nini hawafai tena kuiongoza nchi, kisha elezeni mtashirikiana na wanachi kufanya nini, fungueni matawi na mweke uongozi huko vijijini. Wananchi wapo tayari kuchangia pesa kwa hali na mali .ili kuliwezesha Chopa kuruka. Wananchi tunataka ukombozi na tuko tayari kuchangia kwa wazi ama kwa siri, CDM anzishe akaunti yenu ya M-PESA na mtujulishe tuwawezeshe.
 
Nipo tayari kuchangia hili.CCM kimekuwa genge la mauaji.
Wananchi wanapaswa kuchukua maamuzi mazito dhidi ya CCM vinginevyo hiki chama kitatumaliza.
UKIPENDA HAKI KUWA MAKINI NA CCM.
 
CDM tunawangoja...tuko tayari kuchangia sio tu pesa bali hata damu...mashijaa wameuliwa Igunga sasa hakuna kulala
 
Dada,
Cdm wanatakiwa kunadi sera tu kwenye kila kona ya nchi. Kijiji kwa kijiji!. Swala la kuwaambia wananchi makosa ya ccm kwasasa sioni uzito wake kwa sasa maana watz wanayafahamu makosa ya ccm vzur kabisa. Cdm wanatakiwa kuwaonesha mwanga mpya wa maisha kwa kuwaeleza sera zenye tumaini ili wakiamini maana tatizo la watz wengi hawajapata imani ya kutosha kwamba kuna maisha mazuri sana ndani ya cdm!
 
siasa bila propaganda haziendi. Sera na propaganda ni muhimu. Ccm waliitumia, cdm nao waitumie ila kwa malengo
 
siasa bila propaganda haziendi. Sera na propaganda ni muhimu. Ccm waliitumia, cdm nao waitumie ila kwa malengo

Hapana kama ni Propaganda no no .Chadema wawe wakweli tu hakuna haja ya kuunga unga .Wao waasema ukweli na wananchi watapima na kuamua .Nakubaliana na matawi kufunguliwa yes na michango itapatikana kwa masikini na sala zao Mbinguni zitapokelewa .Michango ya Manji hapana .
 
damu utachangia wewe mwenyewe. Ulaaniwe.

acha utani bana.....laana unatoa wewe? kuna watu wanauwawa kila siku huja walaani wauaji then unalaani wapigania ukombozi? wapinania ukombozi mara zote huchangia ukombozi hadi kwa damu...laana ina wewe bila shaka kwa sababu unashiba vya dhuluma. Hao wamama wenzangu waliouwawa Igunga hujawaona?
 
Kwa vyovyote vile mwaka 2015 tunahitaji rais mpya, na maandalizi ni lazima yaanze sasa, wanachi wameisha ichoka ccm, huko kanda ya kati tumeshuhudia wenyewe...watu wameuwawa ili wengine washinde HADI WANAWAKE WENZANGU, inauma sana!. Nawaomba sana CDM anzeni sasa hivi kuzunguka kijiji hadi kijiji ili kuwaambia wananchi makosa ya CCM na sababu kwa nini hawafai tena kuiongoza nchi, kisha elezeni mtashirikiana na wanachi kufanya nini, fungueni matawi na mweke uongozi huko vijijini. Wananchi wapo tayari kuchangia pesa kwa hali na mali .ili kuliwezesha Chopa kuruka. Wananchi tunataka ukombozi na tuko tayari kuchangia kwa wazi ama kwa siri, CDM anzishe akaunti yenu ya M-PESA na mtujulishe tuwawezeshe.
Tupo pamoja Mkuu, ni wazo zuri sana hili ila uchangiaji wake si lazima uwe kwa M-pesa unaweza ukamwona Mbunge yeyote wa CDM au Diwani Makini wa CDM then akakupa utaratibu wa kufuata.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom