Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,428
Yaani kila kitu kinachotokea ndani ya Chama, hatuna hata muda wa kufanya uchunguzi, moja kwa moja tunakimbilia tu ni CCM.
Hivi inawezekana je mwanao akiugua homa; haraka tu wewe unasema ni jirani, mwanao akilalamika njaa ;unakimbilia ni jirani kamtuma, akisema anataka kusoma arts na si sayansi ;unasema lazima katumwa na jirani, akiuliza sasa baba kwa nini tusifungue duka badala ya kununua bajaji; unasema atakuwa katumwa na wenye maduka jirani wanaogopa ushindani: Yaani bila hata kutafakari na kuopata muunganiko wa kimantiki!
Inaniuma sana katika hili kwa kuwa muaminifu tu. Ni mfano wa mtu mwenye tongo tongo usoni. Ni vigumu kwa mtu mwenye kujiona, ila mwezake anaweza kumuona kiurahisi.Sasa kama anaemuona akimuambia "Ndugu yangu una uchafu usoni" mwenye uchafu anakuwa mkali kweli!, kitakachotokea watu watanyamaza tu!. Hata hivyo kunyamaza kwao hakutasababisha uchafu ule kwenye uso wa ndugu yao kuondoka (ikiwa upo). Hatimae kila watakakopita; jamii yote itakuwa inauona hali aliye nao hauoni!, alieongozana naye naye atakuwa anauona ila kwa kuwa akisema anagombezwa basi ataamua kukauka kana kwamba haoni.Mwishowe walioongozana wote wataishangaza jamii itakayokuwa inawatazama.
Ni bora tukaamua kuondoa "impurities" ambazo tayari ziko kwenywe vichwa vyetu, ili tuweze kupokea maarifa zaidi na mapya kutoka nje ya vichwa vyetu wakati huo huo tukipata fursa ya kusoma kutoka kwenye uzoefu wa watu wengine.
Na ili kujua ni kwa jinsi gani tatizo hili ni kubwa; utaona hata kwenye uzi huu, kuna watu bila hata kusoma uzi wote, watakurupuka na kuanza kusema "Wewe sio CCM kweli!" "Umetumwa!" "unatumika!" n.k
- Kila tukikubwa na Tatizo lolote bila hata uchunguzi na tafakuri ya kina;haraka tunakimbilia ni CCM tu hao!.
- Mtu akitukosoa kwa lolote bila hata kulitafakari kwa makini kwanza; haraka tunakimbilia lazima katumwa tu na CCM huyo.Wala hata hatuna muda wa kutafakari hoja yake na kuipima misingi na mantiki yake!.
- Mtu akilalamika kidogo tu ndani ya chama kwamba kuna jambo haliendi sawa, moja kwa moja tunakimbilia mbona huyu katumwa na CCM na kesha hongwa wala hata hatuangalii analalamikia nini!.
- Mtu akijitokeza tu na kutoa wazo linaloonekana kutofautiana na baadhi ya watu basi utasikia kesha hongwa huyo, kazi ya CCM hiyo na kinachofuata ni kejeli!
Hivi inawezekana je mwanao akiugua homa; haraka tu wewe unasema ni jirani, mwanao akilalamika njaa ;unakimbilia ni jirani kamtuma, akisema anataka kusoma arts na si sayansi ;unasema lazima katumwa na jirani, akiuliza sasa baba kwa nini tusifungue duka badala ya kununua bajaji; unasema atakuwa katumwa na wenye maduka jirani wanaogopa ushindani: Yaani bila hata kutafakari na kuopata muunganiko wa kimantiki!
Inaniuma sana katika hili kwa kuwa muaminifu tu. Ni mfano wa mtu mwenye tongo tongo usoni. Ni vigumu kwa mtu mwenye kujiona, ila mwezake anaweza kumuona kiurahisi.Sasa kama anaemuona akimuambia "Ndugu yangu una uchafu usoni" mwenye uchafu anakuwa mkali kweli!, kitakachotokea watu watanyamaza tu!. Hata hivyo kunyamaza kwao hakutasababisha uchafu ule kwenye uso wa ndugu yao kuondoka (ikiwa upo). Hatimae kila watakakopita; jamii yote itakuwa inauona hali aliye nao hauoni!, alieongozana naye naye atakuwa anauona ila kwa kuwa akisema anagombezwa basi ataamua kukauka kana kwamba haoni.Mwishowe walioongozana wote wataishangaza jamii itakayokuwa inawatazama.
Ni bora tukaamua kuondoa "impurities" ambazo tayari ziko kwenywe vichwa vyetu, ili tuweze kupokea maarifa zaidi na mapya kutoka nje ya vichwa vyetu wakati huo huo tukipata fursa ya kusoma kutoka kwenye uzoefu wa watu wengine.
Na ili kujua ni kwa jinsi gani tatizo hili ni kubwa; utaona hata kwenye uzi huu, kuna watu bila hata kusoma uzi wote, watakurupuka na kuanza kusema "Wewe sio CCM kweli!" "Umetumwa!" "unatumika!" n.k