CHADEMA: Hiki ndicho kitakachotumaliza!

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Yaani kila kitu kinachotokea ndani ya Chama, hatuna hata muda wa kufanya uchunguzi, moja kwa moja tunakimbilia tu ni CCM.

  • Kila tukikubwa na Tatizo lolote bila hata uchunguzi na tafakuri ya kina;haraka tunakimbilia ni CCM tu hao!.
  • Mtu akitukosoa kwa lolote bila hata kulitafakari kwa makini kwanza; haraka tunakimbilia lazima katumwa tu na CCM huyo.Wala hata hatuna muda wa kutafakari hoja yake na kuipima misingi na mantiki yake!.
  • Mtu akilalamika kidogo tu ndani ya chama kwamba kuna jambo haliendi sawa, moja kwa moja tunakimbilia mbona huyu katumwa na CCM na kesha hongwa wala hata hatuangalii analalamikia nini!.
  • Mtu akijitokeza tu na kutoa wazo linaloonekana kutofautiana na baadhi ya watu basi utasikia kesha hongwa huyo, kazi ya CCM hiyo na kinachofuata ni kejeli!
Amin! Amin nawaambia: Kwa kusoma mazingira tu, Utaratibu huu ndio utakaotumaliza!. Kuna jambo linatufunga macho na tunashindwa kuona mbele katika mwanga bora. Jambo hilo si jingine zaidi ya kujiaminisha kwamba tuko "Absolutely perfect" Wakati watu wengine wote nje ya CHADEMA, au hata baadhi ya wanachadema wenzetu Wako "Absolutely wrong" na kudhani kuwa hali hiyo ni "constant " kana kwamba ni hali ya kimaumbile! kitu ambacho kiuhalisia si kweli. Hali hii inatuponza na itatusababishia masikitiko makubwa sisi wenyewe na Watanzania wanaoitegemea CHADEMA na hatmae kwa taifa zima.

Hivi inawezekana je mwanao akiugua homa; haraka tu wewe unasema ni jirani, mwanao akilalamika njaa ;unakimbilia ni jirani kamtuma, akisema anataka kusoma arts na si sayansi ;unasema lazima katumwa na jirani, akiuliza sasa baba kwa nini tusifungue duka badala ya kununua bajaji; unasema atakuwa katumwa na wenye maduka jirani wanaogopa ushindani: Yaani bila hata kutafakari na kuopata muunganiko wa kimantiki!

Inaniuma sana katika hili kwa kuwa muaminifu tu. Ni mfano wa mtu mwenye tongo tongo usoni. Ni vigumu kwa mtu mwenye kujiona, ila mwezake anaweza kumuona kiurahisi.Sasa kama anaemuona akimuambia "Ndugu yangu una uchafu usoni" mwenye uchafu anakuwa mkali kweli!, kitakachotokea watu watanyamaza tu!. Hata hivyo kunyamaza kwao
hakutasababisha uchafu ule kwenye uso wa ndugu yao kuondoka (ikiwa upo). Hatimae kila watakakopita; jamii yote itakuwa inauona hali aliye nao hauoni!, alieongozana naye naye atakuwa anauona ila kwa kuwa akisema anagombezwa basi ataamua kukauka kana kwamba haoni.Mwishowe walioongozana wote wataishangaza jamii itakayokuwa inawatazama.

Ni bora tukaamua kuondoa "impurities" ambazo tayari ziko kwenywe vichwa vyetu, ili tuweze kupokea maarifa zaidi na mapya kutoka nje ya vichwa vyetu wakati huo huo tukipata fursa ya kusoma kutoka kwenye uzoefu wa watu wengine.


Na ili kujua ni kwa jinsi gani tatizo hili ni kubwa; utaona hata kwenye uzi huu, kuna watu bila hata kusoma uzi wote, watakurupuka na kuanza kusema "Wewe sio CCM kweli!" "Umetumwa!" "unatumika!" n.k
 
Mkuu betlehem,
Vp kuhusu angalizo la Bandiko lako la hatari kwa CHADEMA na kuwataka wakutane kwa haraka
 
Last edited by a moderator:
Mkuu bado unajadili tu mambo ya chama Marehemu Chadema,tunatafuta mahala pa kumzikia tu cjui Arusha,au kilimanjaro kwani ndugu wa marehemu chadema wengi wako wapi vile?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
hali hiyo imekuwa ikitokea kwenye migomo hata vyuoni na makazini, mnapokuwa kwenye mjadala especially wale jamaa wanaohamasisha huwa wanapenda kutumia maneno yanayoshabihiana na you are either with us or against us. Sasa ole wako uhoji chochote......, ndivyo ilivyo katika mchakato huu wa kuiondoa CCM madarakani CDM wanataka kutuaminisha kuwa we should concentrate only on that matter and not otherwise. Hivyo basi ukiutaka uenyekiti, wewe ni mhaini, ukihoji kuhusu matumisi wewe ni mzandiki na bila kusahau zidumu fikra sahihi za mwenyekiti
 
Hakika umenena, vitabu vya Mwenyezii Mungu vimeeleza wazi kuwa mwanaadam kaumbwa na udhaifu.

Lakini kwa wapenzi wa Chadema huona wamekamilika, hebu jitazameni. Ninyi si malaika.

Waungwana hukosolewa na kuchukulia positive, kisha hujirekebisha pasipo kuparuana. Kwa Chadema kwao ni HAPANA KABISA.

Jitazameni.
 
Sijui kama wataelewa na hata wakielewa hawatakiri na wakikiri watakiri kwa vinywa na hawatoyafanyia kazi!!!!!!!
 
Yaani kila kitu kinachotokea ndani ya Chama, hatuna hata muda wa kufanya uchunguzi, moja kwa moja tunakimbilia tu ni CCM.

  • Kila tukikubwa na Tatizo lolote bila hata uchunguzi na tafakuri ya kina;haraka tunakimbilia ni CCM tu hao!.
  • Mtu akitukosoa kwa lolote bila hata kulitafakari kwa makini kwanza; haraka tunakimbilia lazima katumwa tu na CCM huyo.Wala hata hatuna muda wa kutafakari hoja yake na kuipima misingi na mantiki yake!.
  • Mtu akilalamika kidogo tu ndani ya chama kwamba kuna jambo haliendi sawa, moja kwa moja tunakimbilia mbona huyu katumwa na CCM na kesha hongwa wala hata hatuangalii analalamikia nini!.
  • Mtu akijitokeza tu na kutoa wazo linaloonekana kutofautiana na baadhi ya watu basi utasikia kesha hongwa huyo, kazi ya CCM hiyo na kinachofuata ni kejeli!
Amin! Amin nawaambia: Kwa kusoma mazingira tu, Utaratibu huu ndio utakaotumaliza!. Kuna jambo linatufunga macho na tunashindwa kuona mbele katika mwanga bora. Jambo hilo si jingine zaidi ya kujiaminisha kwamba tuko “Absolutely perfect” Wakati watu wengine wote nje ya CHADEMA, au hata baadhi ya wanachadema wenzetu Wako “Absolutely wrong” na kudhani kuwa hali hiyo ni “constant " kana kwamba ni hali ya kimaumbile! kitu ambacho kiuhalisia si kweli. Hali hii inatuponza na itatusababishia masikitiko makubwa sisi wenyewe na Watanzania wanaoitegemea CHADEMA na hatmae kwa taifa zima.

Hivi inawezekana je mwanao akiugua homa; haraka tu wewe unasema ni jirani, mwanao akilalamika njaa ;unakimbilia ni jirani kamtuma, akisema anataka kusoma arts na si sayansi ;unasema lazima katumwa na jirani, akiuliza sasa baba kwa nini tusifungue duka badala ya kununua bajaji; unasema atakuwa katumwa na wenye maduka jirani wanaogopa ushindani: Yaani bila hata kutafakari na kuopata muunganiko wa kimantiki!

Inaniuma sana katika hili kwa kuwa muaminifu tu. Ni mfano wa mtu mwenye tongo tongo usoni. Ni vigumu kwa mtu mwenye kujiona, ila mwezake anaweza kumuona kiurahisi.Sasa kama anaemuona akimuambia "Ndugu yangu una uchafu usoni" mwenye uchafu anakuwa mkali kweli!, kitakachotokea watu watanyamaza tu!. Hata hivyo kunyamaza kwao
hakutasababisha uchafu ule kwenye uso wa ndugu yao kuondoka (ikiwa upo). Hatimae kila watakakopita; jamii yote itakuwa inauona hali aliye nao hauoni!, alieongozana naye naye atakuwa anauona ila kwa kuwa akisema anagombezwa basi ataamua kukauka kana kwamba haoni.Mwishowe walioongozana wote wataishangaza jamii itakayokuwa inawatazama.

Ni bora tukaamua kuondoa "impurities" ambazo tayari ziko kwenywe vichwa vyetu, ili tuweze kupokea maarifa zaidi na mapya kutoka nje ya vichwa vyetu wakati huo huo tukipata fursa ya kusoma kutoka kwenye uzoefu wa watu wengine.


Na ili kujua ni kwa jinsi gani tatizo hili ni kubwa; utaona hata kwenye uzi huu, kuna watu bila hata kusoma uzi wote, watakurupuka na kuanza kusema "Wewe sio CCM kweli!" "Umetumwa!" "unatumika!" n.k

Mi naona its better kujadili mambo ya msingi hawa jamaa wameshajifia,maovu yao yameanikwa hadharani,na hawana kitu kinachoitwa political tolerance kwa sababu kile sio chama cha kisiasa.
 
Hivi we unataka kuzunguka nini, nani asiyejua na akili zake timamu kuwa CCM hawalali kuangalia watasambaratisha vipi CDM, kwa mantiki hiyo lazima tu tuwaangalie sana kwenye nafasi ya first suspect.
Ebo, akina Mwigulu, Wassira hawalali kwa ajili ya CDM we unajifanya huoni. CHADEMA komaeni tu inaelekea kila mbinu sasa zinagonga, ushindi unakaribia........
 
Nafikiri hili Mkuu Nguruvi3 alishalijadili vizuri sana akisaidia na Mchambuzi kutoka chama cha CCM.

Wengine naona kama mnarudia tu yaleyale ambayo mlishayaandika mapema. Wewe Betlehem mwenyewe juzi tu hapa ulikuja na makala nzuri tu inayofanana na hii. Nafikiri wengi walikuelewa na kukupa hongera kwa mchango na mawazo yako. Hao wanaosema kuwa mtu kanunuliwa wataendelea kusema na hakuna jinsi ya kuwazuia ili muradi si viongozi wa juu wa CDM.

Kama unaongelea hili la huyu Mwenyekiti wa CDM huko Singida, kuna kitu Nguruvi3 na wenzake na haswa kaka Kichuguu alikiandika kwamba lugha za hawa wanaojiondoa kwenye chama kwa sasa, zinafanana sana na lugha iliyotumika kwenye waraka wa siri wa Mkumbo na ndiyo lugha wanayotumia akina Shonza na Mwampamba et el... Hapo unashindwa kuamini kama hawa watu hawafahamiani na wanajua meli yao inakwenda chini.

Kichuguu anasema:
Uroho wa madaraka na mali ndio unaosababisha Tanzania tuendelee katika hali ya ufukara tulio nao. Kila mtu anafikiria ya kwake tu; hata watu tuliodhani wanatutetea kama akina Zito kumbe nao wanatutetea kwa sababu ya maslahi yao binafsi.

Kitila anaonyesha ana akili sana na anajua sana kupanga maneno yake kwa makini kuliko Zitto ila nadhani naye alishindwa kujua njia nzuri ya kupamabana.

Ni kwa bahati mbaya sana kuwa watu hawa, kama ilivyokuwa kwa wafuasi wao akina Shonza (something like that) nao watahamia CCM na na kupewa ukumbi mkubwa sana wa kutangaza kuwa matatazio ya Tanzania yanatokana na CHADEMA. CCM siyo chama imara ila kina raslimali nyingi sana zitokanazo na utaratibu mbovu wa serikali yetu, halafu kinapowapata watu wenye uchu wa madaraka na tamaa kubwa kama hawa basi wanatumiwa kwa nguvu sana kuibakisha CCM madarakani. Angalia Tambwe Hiza leo sijui yuko wapi, na wapo wengi sana katika historia: Nzanzugwaku, Lamwai, Kaburu, Jidulamabambasi (something like that), na wengine wengi sana. Ni kweli kuwa wanatumia haki zao za kikatiba lakini hawazitumii haki hizo kwa manufaa ya nchi.

Migogoro ya uongozi CDM ilikuwa na njia nyingi za kuitatua kitaasisi, lakini timu hii ilipoamua kuwa confrotational basi inawezekana sana kuwa ilichangia sana kutibua kila kitu kwani ni hulka ya binadamu kutotaka kushindwa. Waraka wao ulikokuwa na observations nzuri lakini ni observations ambazo hawakuonyesha kuzichannel vizuri, kwani ningekuwa katika positions zao nisingefanya hivyo na huenda ningefanikiwa sana. CDM wamekuwa wanatumia sana public opinion kumsimamisha mgombea wao. Hakukuwa na ulazima wa kusema hatumtaki huyu tunamtaka yule, wangetumia vigezo vile vile walivyotumia kumsimamisha Slaa mwaka 2010 wangeweza kufanikiwa malengo bila kuvuruga chama chao

Hata hivyo ya ngoswe tumwachie ngoswe, ila ngoswe huyo akikata mti ukaangukia nyumba yetu inabidi tulalamike. Mgogoro huu umeirahisishia sana CCM kurudi madarakani kwa kutumia mtu yeyote watakayemsimamisha hata kama ana uchafu wa namna gani.

Tafadhali ipitie hii makala na utaona umerudia kilekile ambacho wenzako wamekichambua kwa upana zaidi kuliko wewe ambavyo umekuja kwa upande mmoja tu.

Soma hapa: https://www.jamiiforums.com/great-t...pecial-mgogoro-kambi-ya-upinzani-chadema.html
 
Last edited by a moderator:
Hivi we unataka kuzunguka nini, nani asiyejua na akili zake timamu kuwa CCM hawalali kuangalia watasambaratisha vipi CDM, kwa mantiki hiyo lazima tu tuwaangalie sana kwenye nafasi ya first suspect.
Ebo, akina Mwigulu, Wassira hawalali kwa ajili ya CDM we unajifanya huoni. CHADEMA komaeni tu inaelekea kila mbinu sasa zinagonga, ushindi unakaribia........

Mzee uko pepo ipi,nakuhurumia kama umelala hamka,au uko kwenye paylaw ya Dj joker.
 
Mkuu betlehem sisi watani wako ambao tumekuwa wote muda mrefu hapa jukwaani tunajua kuwa unaongea kutoka moyoni.

Tatizo ni watu ambao hawajui mbele wala nyuma.

Umeona leo Ben Saanane anasema Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Singida ni useless. Just imagine mtu amejitolea nyumba yake iwe ofisi lakini kijana kama Ben anamvunjia heshima just because yeye Ben yuko karibu na Dr. Slaa.

Endelea kutoa elimu. Najua utalaumiwa na kupigwa madongo just because umeungwa mkono na Zemarcopolo, lakini siwezi kuacha kukuunga mkono wakati ninaona ndugu yangu unaonewa.

Washauri wasome kitabu ulichoandika.
 
Last edited by a moderator:
Maelezo ya Nguruvi3: (ukiyasoma, utaona uhusika wa CCM. Bado wewe unataka watu wasiamini?)

Mkuu
Mkandara huo waraka umeandikwa muda sasa na kinachofanyika ni uekelezaji wake ambao Zitto anaufanyia kazi ikiwa ushahidi kuwa alishakubali jukumu kama waraka ulivyosema. Hakuondolewa katika hao watatu bali alijiondoa, soma maneno haya
Mwaka huu viongozi wetu wamekuja na ugatuaji madaraka kutoka makao makuu ya taasisi na kupeleka madaraka kwenye kanda mbalimbali.

Zitto hawezi kusema viongozi wetu yeye akiwemo! Kama hakushirikisha hiyo ilikuwa fursa ya kueleza na si kutumia mitandao.

Hao watu watatu wametajwa katika waraka kuwa ni Mbowe, Dr Slaa na mtunza fedha. Hakuna sababu za kufikiri kuna wengine zaidi

Kuhusu watu kulalamika sehemu kama hapa JF nakubalina nawe kuwa wameanza muda mrefu kidogo.
Tena malalamiko yako yanafanana sana na malalamiko yaliyopo katika waraka.

Mathalan, kuna mwana CCM lakini kwa kusukumwa na utashi wa demokrasia nchi nzima ameamua kuwaasa wana CDM. Ushauri wake umefanyiwa kazi na waandika waraka kwasababu yeye aliandika muda mrefu kabla ya waraka.

Nadhani tuangalie malalmiko haya na ya waraka tuone kama yanatupa jingine zaidi ya kuuona waraka kama ulivyo ili
Waraka:Mpinzani wetu (Mbowe)ni mtu aliyezaliwa kwenye utajiri na anadhani pesa ni kila kitu
HAMY-D(July 2013): Mbowe ni mtoto wa kishua, unadhani atakuwa na huruma na watanzania?Mbowe kama hajawahi kuonja suruba ya umaskini, uchungu kwa watu maskini ataupata wapi?



Waraka:Simtu wa kujipenda nafsi na katika kupambana umaskini wa watu badala ya umaskiniwake

HAMY-D :
sisi tunataka maskini wenzetu ndio watutoe hapa tulipo na kutupeleka mbele. Birds of the same feathers, flock together!!


Waraka: Matukiomawili yanamwacha uchi katika hili pale alipolitangazia taifa kwambawawakilishi wetu wote hawatachukua posho za vikao halafu yeye na wengine wotewanazichukua hadi leo na kumwacha mtendaji msaidizi peke yake. Na la pililinalofanana na hilo ni pale alipotangaza kutotumia gari la serikali ambalo nila kifahari kisha akalirudia kimya kimya

HAMY-D: Pia, kama Mbowe ana stahili kuliendesha hilo gari, huoni ndio maana serikali ilimpa hili awe nalo? sasa kwanini yeye alirudishe? haafu sasa hizo sababu zake utasikia mara uzalendo, mara nawaulumia wananchi kwani serikali ina matumizi makubwa. Sasa kwanini alichukue wakati tayari alitoasababu za kulikataa? Nikisema Mbowe hana msimamo nitakuwa nimekosea?Last edited by HAMY-D; 12th July 2013 at 11:26.


Waraka:Nikubadilisha uongozi wa taasisi haraka iwezekanavyo

HAMY-D: Fanyeni uchaguzi haraka wa ndani ya CDM mumtoe huyu Mbowe, mauaji aliyofanya kwa vijana wetu chini ya uongozi wake yanatosha.


Waraka: Tutahakikisha tuko busy kupost mambo mema na mazuri yatakayokuwa yakifanywa na MM kila wakati na kuzidi kusambaza sifa zake njema kila inapotokea nafasi. Atakayefanya kazi hiyo ni sisi wengine wala si yeye! Pia tutahakikisha kila post ya kumchafua inapatiwa majibu bila kutumia ID yake inayojulikana.

HAMY-D WanaJF, hivi ni kwanini Mbowe asiige siasa za Zitto?
Sikuwahi kumuona Zitto kwenye maandamano yaliyo husisha mauaji au uvunjifu wa amani wa aina yoyote!


Waraka: Uongozi wa sasa wa taasisi yetu umefanya tuonekana kwamba taasisi yetu ipo kwa ajili ya kuvuruga amani ya nchi, Yote hii ni kwa sababu tumekuwa hatuna mbinu mpya za mapambano zinabadilikabadilika zaidi ya maandamano ya kila mara.

Hamy-D: Utajadili maendeleo wakati amani na utulivu vipo hatarini?
Hatuwezi kuijenga nchi wakati kuna kundi la watu linaibomoa nchi kwa kasi.
Amani ni tunu ya taifa letu, ikipotea kuirudisha si jambo dogo.
Ni bora tubaki na dhiki na ufukara wetu ila amani idumishwe. Jambo ambalo MBOWE na Dr Slaa hawaoni kama ni muhimu.
 
Nafikiri hili Mkuu Nguruvi3 alishalijadili vizuri sana akisaidia na Mchambuzi kutoka chama cha CCM.

Wengine naona kama mnarudia tu yaleyale ambayo mlishayaandika mapema. Wewe Betlehem mwenyewe juzi tu hapa ulikuja na makala nzuri tu inayofanana na hii. Nafikiri wengi walikuelewa na kukupa hongera kwa mchango na mawazo yako. Hao wanaosema kuwa mtu kanunuliwa wataendelea kusema na hakuna jinsi ya kuwazuia ili muradi si viongozi wa juu wa CDM.

Kama unaongelea hili la huyu Mwenyekiti wa CDM huko Singida, kuna kitu Nguruvi3 na wenzake na haswa kaka Kichuguu alikiandika kwamba lugha za hawa wanaojiondoa kwenye chama kwa sasa, zinafanana sana na lugha iliyotumika kwenye waraka wa siri wa Mkumbo na ndiyo lugha wanayotumia akina Shonza na Mwampamba et el... Hapo unashindwa kuamini kama hawa watu hawafahamiani na wanajua meli yao inakwenda chini.

Kichuguu anasema:

Tafadhali ipitie hii makala na utaona umerudia kilekile ambacho wenzako wamekichambua kwa upana zaidi kuliko wewe ambavyo umekuja kwa upande mmoja tu.

Soma hapa: https://www.jamiiforums.com/great-t...pecial-mgogoro-kambi-ya-upinzani-chadema.html
Mkuu kwa hili nazungumzia ujumla wa mambo na sizungumzii mtu mmoja mmoja wala tukio moja.Sizungumzii viongozi bali sisi wanachama kwa ujumla na wapenzi wote na wengi tuko humu JF.Hata hivyo sikuona huo uzi wa nguruvi3.Samahani kwa hilo
 
Mkuu bado unajadili tu mambo ya chama Marehemu Chadema,tunatafuta mahala pa kumzikia tu cjui Arusha,au kilimanjaro kwani ndugu wa marehemu chadema wengi wako wapi vile?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Mkuu unaukumbuka ule wimbo tuliokuwa tunaimba zamani, "Iddi Amin akifa,mimi siwezi kulia, nitamtupa kagera,awe chakula cha mamba"! The same tu saccos ya chadema.
 
Hii ni sauti iliyayo nyikani. Tatizo la wafuasi wengi wa Chadema ni Upofu, ushabiki, kufa na tai shingoni hata kama kila kitu kiko wazi mbele yao. hawahoji matumizi halali ya pesa za Chama. badala ya kuwasulubu wababaishaji, wanawasulubu watu wanaotaka uwajibikaji ndani ya chama
 
Mkuu katika lile mimi nimefikisha, wajibu wangu nimetimiza na historia itaandika hivyo.

Hivi kwanini kila anayepingwa humu anaamini anapingwa na watu wa CDM? Kwa mfano mimi MTAZAMO sina kadi ya CDM wala sina uhusiano na mwanachama yeyote wa CDM ninayemfahamu vizuri fika ni mwanachama, je kelele zangu ndio kelele za CDM?
 
Hii ni sauti iliyayo nyikani. Tatizo la wafuasi wengi wa Chadema ni Upofu, ushabiki, kufa na tai shingoni hata kama kila kitu kiko wazi mbele yao. hawahoji matumizi halali ya pesa za Chama. badala ya kuwasulubu wababaishaji, wanawasulubu watu wanaotaka uwajibikaji ndani ya chama

Mzee kuna husemi unasema waarabu wa pemba hujuana kwa vilemba,unashabiana na huu the birds of the same feathers fly together,usipofanana na wale watu wa kaskazini wenye mioyo kandamizi,wenye kuwaza kujitjirisha wao wenyewe,wasiowajali wanyonge hadi inafikia wakati wanawalia hata miambili zao,hakika usipofanana nao hamtakaa pamoja!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom