Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,337
- 51,848
Salama Wakuu!
Kwa jinsi mambo nilivyoyakuta na yalivyosasa kuhusiana na Siasa za nchi hii, nadiriki kusema kuwa CHADEMA bado Sana katika kuchukua nchi.
Nimeanza kufuatilia Siasa mwaka 2005, mpaka sasa ni miaka 16. Sio miaka mingi ila pia sio michache Sana. Inatosha Kueleza Jambo.
Nikiwatazama CHADEMA, kisha nikiwaangalia Watanzania, alafu nikamalizia na CCM wenyewe. Ni wazi kuwa, CHADEMA bado Sana kuchukua nchi hii.
Hawana uwezo Kwa sababu, hawana uwezo wa kukaza, hawana uwezo wa mapambano makali ya Muda mrefu.
CHADEMA ni Kama watoto, ambao Sisi wanafasihi tunasemaga Ngoma ya watoto haikeshi.
Kama ni kwenye riadha CHADEMA wanaziweza mbio fupi za Mita Mia, hapo wanaouwezo wa kukimbia Kwa Kasi kubwa wakashinda. Lakini mbio ndefu hakika CHADEMA wamethibitisha kuwa hawaziwezi. CCM wao wamejithibitishia kuwa wao ni mabingwa wa mbio ndefu.
CHADEMA kwenye Uwanja WA vita wapo kwenye kundi ambalo wanapenda ukanda wenye mashambulizi yaliyopoa, hawahimili ukanda wenye mashambulizi makali yasiyokoma.
CHADEMA wamepoa Kama uji wa dundi.
Mengi wanayoyapigania wameshindwa kuyapata, wanaishia kulalamika tuu.
Siku zote kwenye maisha, ukishakuwa upande wa mlalamikaji basi jua umekwisha.
CCM wao ni watu wakuchukua hatua. Hawalalamiki.
CHADEMA mkiendelea hivi kuwa Kama uji wa dundi, mtakatika vipande vipande.
Nawasilisha
Kwa jinsi mambo nilivyoyakuta na yalivyosasa kuhusiana na Siasa za nchi hii, nadiriki kusema kuwa CHADEMA bado Sana katika kuchukua nchi.
Nimeanza kufuatilia Siasa mwaka 2005, mpaka sasa ni miaka 16. Sio miaka mingi ila pia sio michache Sana. Inatosha Kueleza Jambo.
Nikiwatazama CHADEMA, kisha nikiwaangalia Watanzania, alafu nikamalizia na CCM wenyewe. Ni wazi kuwa, CHADEMA bado Sana kuchukua nchi hii.
Hawana uwezo Kwa sababu, hawana uwezo wa kukaza, hawana uwezo wa mapambano makali ya Muda mrefu.
CHADEMA ni Kama watoto, ambao Sisi wanafasihi tunasemaga Ngoma ya watoto haikeshi.
Kama ni kwenye riadha CHADEMA wanaziweza mbio fupi za Mita Mia, hapo wanaouwezo wa kukimbia Kwa Kasi kubwa wakashinda. Lakini mbio ndefu hakika CHADEMA wamethibitisha kuwa hawaziwezi. CCM wao wamejithibitishia kuwa wao ni mabingwa wa mbio ndefu.
CHADEMA kwenye Uwanja WA vita wapo kwenye kundi ambalo wanapenda ukanda wenye mashambulizi yaliyopoa, hawahimili ukanda wenye mashambulizi makali yasiyokoma.
CHADEMA wamepoa Kama uji wa dundi.
Mengi wanayoyapigania wameshindwa kuyapata, wanaishia kulalamika tuu.
Siku zote kwenye maisha, ukishakuwa upande wa mlalamikaji basi jua umekwisha.
CCM wao ni watu wakuchukua hatua. Hawalalamiki.
CHADEMA mkiendelea hivi kuwa Kama uji wa dundi, mtakatika vipande vipande.
Nawasilisha