mwakatundu
Member
- Jan 1, 2010
- 15
- 0
Hawa CHADEMA wamekata tamaa ya kuunda serikali hata kabla ya mpambano wenyewe? Afadhali chama wangemwachia Zitto kumbe.
Chadema yapania kunyakua majimbo 80
Daniel Mjema, Moshi
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimejiwekea mkakati wa kunyakua majimbo 80 katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Tayari Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ametangaza azma ya kugombea ubunge katika Jimbo la Hai.
Mkakati huo ulitangazwa juzi na Mbowe alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa madiwani wote wa Chadema kote nchini, waliokutana mjini Moshi.
Kwa mujibu wa Mbowe lengo la chama chake katika uchaguzi huo ni kupata angalau theluthi moja ya wabunge wote.
"Kama kuna eneo CCM inajidanganya ni Bunge la Jamhuri. Chadema mwaka 2010 lazima tuingize angalau theluthi moja ya wabunge ili tukate ngebe ya CCM katika maamuzi ndani ya chombo hiki muhimu,"alisema.
Mbowe alisema ana uhakika chama hicho kinaweza kunyakua majimbo 80 na kukifanya kiwe na nguvu katika maamuzi ya bunge kwa maslahi ya wananchi wengi.
"Kama CCM wanafikiri tunakwenda katika uchaguzi huu kuwasindikiza, wanajidanganya kwa sababu tuna uhakika wa wabunge 80 na hakuna mkoa ambao hautatoa madiwani wanaotokana na Chadema,"alisema Mbowe.
Alisema malengo ya chini ya chama chake ni kushinda na kushika hatamu ya kuongoza ya mabaraza ya madiwani katika halmashauri 30 na kwamba kinaweka wagombea wanaokubalika kwa wananchi.
Aliwahakikishia madiwani hao kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Hai anakokwenda kugombea ubunge na Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, zitakuwa chini ya Chadema.
Alisema Chadema ni chama kinachokua ndani ya upinzani uliosinyaa na kutoa takwimu kuwa mwaka 1994 kilikuwa na madiwani 42 na idadi hiyo ikapanda mwaka 2000 na kufikia 56 na uchaguzi wa 2005 ikapata madiwani 103.
Hata hivyo alisema pamoja na mafanikio hayo lakini chama hicho kimekuwa kikipandikiziwa matatizo na mikasa mbalimbali ili kukidhoofisha.
"Mmesikia kwa muda mrefu kuwa Chadema ni chama cha Wachaga nawaambieni leo hii ni propaganda iliyopikwa na kupandikizwa ili kutugombanisha ndani ya chama lakini siku zote ukweli hudumu na uongo husinyaa"alisema.
Mbowe alisema anashangazwa na kauli hizo na kuwataka madiwani wa mkoa wa Kilimanjaro wanaohudhuria mkutano huo kusimama na waliposimama walifikia nane kati ya madiwani 103 nchi nzima.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shirika la Ujerumani la Conrad Adeneur Stiftung (CAS), Anke Lensh alisema japokuwa mfumo wa vyama vingi nchini uliingia 1992 lakini baadhi ya Watanzania hawafahamu haki yao. "Japokuwa mfumo huu uliingia Tanzania mwaka 1992, lakini sidhani kama wananchi wamejengewa vya kutosha uwezo wa kuamua kwani bado wapo wanaoona kuchagua chama kingine nje ya CCM ni kusaliti nchi,"alisema.
Chadema yapania kunyakua majimbo 80
Daniel Mjema, Moshi
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimejiwekea mkakati wa kunyakua majimbo 80 katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Tayari Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ametangaza azma ya kugombea ubunge katika Jimbo la Hai.
Mkakati huo ulitangazwa juzi na Mbowe alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa madiwani wote wa Chadema kote nchini, waliokutana mjini Moshi.
Kwa mujibu wa Mbowe lengo la chama chake katika uchaguzi huo ni kupata angalau theluthi moja ya wabunge wote.
"Kama kuna eneo CCM inajidanganya ni Bunge la Jamhuri. Chadema mwaka 2010 lazima tuingize angalau theluthi moja ya wabunge ili tukate ngebe ya CCM katika maamuzi ndani ya chombo hiki muhimu,"alisema.
Mbowe alisema ana uhakika chama hicho kinaweza kunyakua majimbo 80 na kukifanya kiwe na nguvu katika maamuzi ya bunge kwa maslahi ya wananchi wengi.
"Kama CCM wanafikiri tunakwenda katika uchaguzi huu kuwasindikiza, wanajidanganya kwa sababu tuna uhakika wa wabunge 80 na hakuna mkoa ambao hautatoa madiwani wanaotokana na Chadema,"alisema Mbowe.
Alisema malengo ya chini ya chama chake ni kushinda na kushika hatamu ya kuongoza ya mabaraza ya madiwani katika halmashauri 30 na kwamba kinaweka wagombea wanaokubalika kwa wananchi.
Aliwahakikishia madiwani hao kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Hai anakokwenda kugombea ubunge na Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, zitakuwa chini ya Chadema.
Alisema Chadema ni chama kinachokua ndani ya upinzani uliosinyaa na kutoa takwimu kuwa mwaka 1994 kilikuwa na madiwani 42 na idadi hiyo ikapanda mwaka 2000 na kufikia 56 na uchaguzi wa 2005 ikapata madiwani 103.
Hata hivyo alisema pamoja na mafanikio hayo lakini chama hicho kimekuwa kikipandikiziwa matatizo na mikasa mbalimbali ili kukidhoofisha.
"Mmesikia kwa muda mrefu kuwa Chadema ni chama cha Wachaga nawaambieni leo hii ni propaganda iliyopikwa na kupandikizwa ili kutugombanisha ndani ya chama lakini siku zote ukweli hudumu na uongo husinyaa"alisema.
Mbowe alisema anashangazwa na kauli hizo na kuwataka madiwani wa mkoa wa Kilimanjaro wanaohudhuria mkutano huo kusimama na waliposimama walifikia nane kati ya madiwani 103 nchi nzima.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shirika la Ujerumani la Conrad Adeneur Stiftung (CAS), Anke Lensh alisema japokuwa mfumo wa vyama vingi nchini uliingia 1992 lakini baadhi ya Watanzania hawafahamu haki yao. "Japokuwa mfumo huu uliingia Tanzania mwaka 1992, lakini sidhani kama wananchi wamejengewa vya kutosha uwezo wa kuamua kwani bado wapo wanaoona kuchagua chama kingine nje ya CCM ni kusaliti nchi,"alisema.