kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,732
Ben Saanane, Habib Nchange, Juliana Shonza, Mwampamba, Exaud Mamuya, Gwakisa, Sanga na Zitto ZK
Nimejitahidi sana kupitia post zilizowekwa humu jukwaani, kwa mtazamo wangu hawa vijana hapo juu wapo katika kundi maalum lililoandaliwa kuihujumu na kuiua CHADEMA nayasema haya kwa sababu zifuatazo
1. Tumeshuhudia kundi moja likitoa maelezo likijionyesha moja kwa moja linatumika na viongozi wakuu kwa ajili ya kumuangamiza Zitto ikiwa ni pamoja na kutaka kumuua tuuma ambayo ni kubwa sana na ni mbaya sana kwa uhai wa chama
2. Pia tumeona kundi lingine likiwa limeegemea upande wa Zitto na likionyesha mbinu na mawasiliano yaliyokuwa yakifanyika eti kuleta Demokrasia katika Chama na hili likionyesha Zitto alikuwa akubaliana na viongozi wenzake wa Juu (Mwenyekiti na Katibu Mkuu)na akiwa katika mbinu ya kuanzisha chama kingine (CHAUMA)
3. Hii inaonyesha hawa vijana wamejipanga vyema kulitumia hili jukwaa ili kuuchonganisha uongozi wote wa Juu wa CDM na mwisho wa siku wakose kuaminiana, kuheshimiana.kwani haiingii akilini kama kweli ni mwanachama muadilifu wa CHADEMA watoe maelezo kama haya tuliyoyasoma humu ambayo yalitakiwa yawe siri na utatuzi wake ufanyike kwenye vikao vya ndani vya chama.
4. Pia ningependa kukumbushia ile kauli ya Ndg. Steven Wassira kuwa CDM itakufa kabla ya 2013 hii inajionyesha haya mambo yamepangwa na waliopewa jukumu hilo ni hawa vijana akiwemo na ZITTO kwani tumeshuhudia wengine wakiingiza suala la Ukanda ambalo limezungumzwa sana na Viongozi wa CCM wakati wakiishambulia CDM
5. Pia nimeshuhudia pale Ben Saanane alipokuwa akisakamwa na hawa wenzake yeye alikuwa anagonga Like! Ikimaanisha anawaunga mkono kwa kutoa hicho walichopanga.
** Wito na maoni yangu Uongozi wa Juu wa chama ulitafakari hili na ikiwezekana kuchukua maamuzi magumu ambayo yatakitetelesha chama kwa muda mfupi lakini kukifanya kuwa Imara kwa muda Mrefu na kuheshimika kuliko kama ilivyo sasa ambapo chama kimekuwa kama jumuiya ya Kambale hajulikani baba, mama wala mtoto wote wana masharubu.
Nawasilisha!!!!
Nimejitahidi sana kupitia post zilizowekwa humu jukwaani, kwa mtazamo wangu hawa vijana hapo juu wapo katika kundi maalum lililoandaliwa kuihujumu na kuiua CHADEMA nayasema haya kwa sababu zifuatazo
1. Tumeshuhudia kundi moja likitoa maelezo likijionyesha moja kwa moja linatumika na viongozi wakuu kwa ajili ya kumuangamiza Zitto ikiwa ni pamoja na kutaka kumuua tuuma ambayo ni kubwa sana na ni mbaya sana kwa uhai wa chama
2. Pia tumeona kundi lingine likiwa limeegemea upande wa Zitto na likionyesha mbinu na mawasiliano yaliyokuwa yakifanyika eti kuleta Demokrasia katika Chama na hili likionyesha Zitto alikuwa akubaliana na viongozi wenzake wa Juu (Mwenyekiti na Katibu Mkuu)na akiwa katika mbinu ya kuanzisha chama kingine (CHAUMA)
3. Hii inaonyesha hawa vijana wamejipanga vyema kulitumia hili jukwaa ili kuuchonganisha uongozi wote wa Juu wa CDM na mwisho wa siku wakose kuaminiana, kuheshimiana.kwani haiingii akilini kama kweli ni mwanachama muadilifu wa CHADEMA watoe maelezo kama haya tuliyoyasoma humu ambayo yalitakiwa yawe siri na utatuzi wake ufanyike kwenye vikao vya ndani vya chama.
4. Pia ningependa kukumbushia ile kauli ya Ndg. Steven Wassira kuwa CDM itakufa kabla ya 2013 hii inajionyesha haya mambo yamepangwa na waliopewa jukumu hilo ni hawa vijana akiwemo na ZITTO kwani tumeshuhudia wengine wakiingiza suala la Ukanda ambalo limezungumzwa sana na Viongozi wa CCM wakati wakiishambulia CDM
5. Pia nimeshuhudia pale Ben Saanane alipokuwa akisakamwa na hawa wenzake yeye alikuwa anagonga Like! Ikimaanisha anawaunga mkono kwa kutoa hicho walichopanga.
** Wito na maoni yangu Uongozi wa Juu wa chama ulitafakari hili na ikiwezekana kuchukua maamuzi magumu ambayo yatakitetelesha chama kwa muda mfupi lakini kukifanya kuwa Imara kwa muda Mrefu na kuheshimika kuliko kama ilivyo sasa ambapo chama kimekuwa kama jumuiya ya Kambale hajulikani baba, mama wala mtoto wote wana masharubu.
Nawasilisha!!!!