Haya yote mabaya wanayofanyiwa CHADEMA na serikali ya CCM hivi kwanini CCM mnaichukia CHADEMA?
=====
=====
Tokea kuanzishwa siasa za Vyama vingi CCM haijawahi kupata upinzani wa kweli kama kipindi hiki
Tukiondoa Upinzani wa Visiwani hapa Bara lilikuwa ni Shamba la bibi kwa CCM hata wakati wa Mrema na Nccr-Mageuzi ilikuwa ni rahisi kupenyeza Mamluki na Mapandikizi
Ila Chadema kimetumwa kuichukua Ikulu hakuna uchaguzi CCM ilikuwa na hofu kama 2015 haijawahi kutokea mimi mwenyewe nilikuwa CCM kabla sijakihama
Hali ilikuwa mbaya sana ndani ya CCM na makada walikuwa wakisema waziwazi kuwa bila kuiba kura CCM kijiandae kisaikolojia
Na wizi mkubwa wa kura wa kutisha ulifanyika trust me
Bila wizi CCM ingepigwa chini hilo halina mjadala
Baada ya ushindi haramu wa 2015 CCM ikapanga mikakati ya kukimaliza Chama cha Demokrasia na Maendeleo huku wakijipa moyo kuwa watakimaliza kama walivyokiua chama cha Nccr-Mageuzi
Lakini ilikuwa ni kujidanganya na kushindwa kusoma alama za nyakati
Chadema ni Chama pekee cha Upinzani ambacho kiko Well organized na CCM imetumia mbinu zote zimegonga mwamba
Ukweli ni kwamba tokea CCM iasisiwe hakijawahi kupata mpinzani serious kama Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
Chadema nacho kinatakiwa kishikilie hapo hapo