Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Akitangaza kuvuliwa kwa uachama wa Chama hicho leo, mbele ya waandishi kaimu mwenyekiti wa Chama hicho wilaya ya Hai Dr Joe Nkya amesema kamati tendaji ya Chama wilaya ya Hai imechukua uamuzi huo baada ya kutokuridhishwa na matendo ya mwenyekiti huyo wa zama.
Amesema bwana James Mushi amekua akiwakashifu viongozi wa Chama hicho kuanzia Wilaya hadi Taifa kwa kutoa kauli za kejeli na matusi kinyume na katiba ya Chama. Pia amekua akikihujumu chama hicho katika sekta mbalimbali kwa ajili ya manufaa yake binafsi na washirika wake.
Amesema kuwa kamati tendaji imejiridhisha pasipo shaka kwamba bwana James ametenda makosa hayo hata alipokemewa aliendelea kukiuka maagizo ya Chama na hivyo kuanzia leo amefukuzwa rasmi ndani ya CHADEMA.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai mh Helga Mchomvu amewashutumu madiwa watatu wa Chama hicho waliojiuzulu hivi karibuni kwa kununuliwa bila kujali kwamba wanawaongezea mzigo wananchi waliyowapa ridhaa ya kuwaongoza katika kata zao.
Mh Helga amesema kuwa madiwani hao walikua wameshaanza kuonyesha viashiria vya kwenda kinyume na maadili ya ki - upinzani hata katika uwajibikaji kwa muda mrefu.
Amesema kwamba madiwani hao wanawaongezea mzigo wananchi wao kwa kuingia kwenye uchaguzi ambao unagharimu fedha nyingi ambazo zingeingia kwenye matumizi mengine mfano kuongeza madawa Hospitalini nk.
Mh Helga amesema madiwani hao waliokubali kununuliwa hawajawatendea haki wapiga kura wao na kusema Chama km Chama kitaingia kwenye uchaguzi kwa kujiamini na kitashinda kwakua kimepeleka maendeleo katika Halmashauri katika maeneo yote kulingana na Bajeti ya serikali.
Katika mkutano na waandishi wa habari, baadhi ya madiwani wanaosadikiwa nao wako mbioni kuondoka ndani ya CHADEMA wamekanusha vikali kuondoka ndani ya CHADEMA na kusema wanaoneza uvumi huo ni mawakala wa CCM.
Wamesema ni kweli baadhi yao wamekua wakifuatwa hadi usiku wa manane baadhi ya watu wasiojulikana wakishirikiana na diwani mmoja aliyeachia ngazi kwa kigezo cha kupewa Mil 30 lkn wamekua wakiwakatalia.
Baadhi ya madiwani hao wameomba CHADEMA kuwawekekea ulinzi kwani wanahofia maisha yao kutokana na kufuatwa nyumbani usiku wa manane usiku wakishawishiwa wapokee mil 30 ili wajivue udiwani pamoja uanachama ndani ya CDM.
Amesema bwana James Mushi amekua akiwakashifu viongozi wa Chama hicho kuanzia Wilaya hadi Taifa kwa kutoa kauli za kejeli na matusi kinyume na katiba ya Chama. Pia amekua akikihujumu chama hicho katika sekta mbalimbali kwa ajili ya manufaa yake binafsi na washirika wake.
Amesema kuwa kamati tendaji imejiridhisha pasipo shaka kwamba bwana James ametenda makosa hayo hata alipokemewa aliendelea kukiuka maagizo ya Chama na hivyo kuanzia leo amefukuzwa rasmi ndani ya CHADEMA.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai mh Helga Mchomvu amewashutumu madiwa watatu wa Chama hicho waliojiuzulu hivi karibuni kwa kununuliwa bila kujali kwamba wanawaongezea mzigo wananchi waliyowapa ridhaa ya kuwaongoza katika kata zao.
Mh Helga amesema kuwa madiwani hao walikua wameshaanza kuonyesha viashiria vya kwenda kinyume na maadili ya ki - upinzani hata katika uwajibikaji kwa muda mrefu.
Amesema kwamba madiwani hao wanawaongezea mzigo wananchi wao kwa kuingia kwenye uchaguzi ambao unagharimu fedha nyingi ambazo zingeingia kwenye matumizi mengine mfano kuongeza madawa Hospitalini nk.
Mh Helga amesema madiwani hao waliokubali kununuliwa hawajawatendea haki wapiga kura wao na kusema Chama km Chama kitaingia kwenye uchaguzi kwa kujiamini na kitashinda kwakua kimepeleka maendeleo katika Halmashauri katika maeneo yote kulingana na Bajeti ya serikali.
Katika mkutano na waandishi wa habari, baadhi ya madiwani wanaosadikiwa nao wako mbioni kuondoka ndani ya CHADEMA wamekanusha vikali kuondoka ndani ya CHADEMA na kusema wanaoneza uvumi huo ni mawakala wa CCM.
Wamesema ni kweli baadhi yao wamekua wakifuatwa hadi usiku wa manane baadhi ya watu wasiojulikana wakishirikiana na diwani mmoja aliyeachia ngazi kwa kigezo cha kupewa Mil 30 lkn wamekua wakiwakatalia.
Baadhi ya madiwani hao wameomba CHADEMA kuwawekekea ulinzi kwani wanahofia maisha yao kutokana na kufuatwa nyumbani usiku wa manane usiku wakishawishiwa wapokee mil 30 ili wajivue udiwani pamoja uanachama ndani ya CDM.