CHADEMA fanyeni walichofanya Kinana na Migiro kuelekea Oktoba 2015

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,489
13,608
Miezi kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015 katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Mama Asha Migiro walitembea nchi nzima kwa lengo maalum. Walikwenda kuiombea msamaha CCM mbele ya wananchi, walijaribu kadri walivyoweza kuirudisha CCM kwenye fikra za wananchi wa kawaida. Mzee Kinana hakusita kuwaita mizigo baadhi ya mawaziri waliyoonekana kutokuwa na msaada kwa serikali ya awamu ya nne. Wasomi wakagawanyika kimawazo kuhusiana na ziara zile za viongozi wa juu wa CCM nchi nzima.

Wapo walioamini kwamba Kinana anaongea lugha ya upinzani ambayo itachangia kukibomoa kabisa chama cha mapinduzi, lakini alichofanya kilikuwa ni sawa na mtu aliyegombana na mchumba/mke halafu akaanza kumtimia zawadi nyingi tu ili kuuteka tena moyo wa mpenzi wake.

Wakati wa kampeni kazi iliyofanywa na Kinana pamoja na migiro ikawa imeshapunguza makali ya chuki waliyokuwa nayo wananchi kwa CCM. JPM akatumia ujanja wa kujitambulisha yeye badala ya CCM huku akifanya kampeni akiwa amevaa mavazi ya CCM. Kinana na Migiro walitumia ukongwe wao kwenye siasa katika angalau kujaribu kurudisha hali kwenye ubora uliokuwepo miaka mingi nyuma kabla mafisadi hawajakichafua chama cha mapinduzi.

CHADEMA wamepata katibu mkuu mpya, wanao muda wa kutosha kuelekea 2020, huu sasa ni wakati muafaka wa kutengeneza mikakati ya ushindi sio kuendelea kutegemea kura za huruma (mahaba). CCM kwa sasa wanafanya kila njia ili waweze kuwa karibu na wananchi wa kawaida, wamelibomoa daraja lililokuwa linawatenganisha wao na wananchi wa kawaida. Waziri mkuu akiona bango njiani anasimamisha msafara na kuwasikiliza wananchi, akibipiwa anapiga muda ule ule. Hakuna tena muda wa kuunda tume za ajabuajabu kwa ajili ya kutafutia ufumbuzi mambo yanayoweza kutatuliwa ndani ya siku moja ya kazi.

CHADEMA wautambue mkakati mpya wa CCM na wajipange kisayansi katika kuukabili, ili wasipotee machoni na mioyoni mwa watu ambao walikuwa sehemu ya wahudhuriaji wa mikutano yao ya kampeni. Awamu ya tano imekuja kivingine, JPM sio JK ambaye aliruhusu uzembe ambao ulitumika vizuri katika kuifanya heshima ya CCM ikapotea. JPM na wasaidizi wake wanapaswa kuwafumbua macho CHADEMA ili waje kivingine yaani kisasa zaidi kwa faida ya mtanzania wa kawaida. Ni mawazo yangu tu.
 
Absalom Kibanda aliwatahadharisha kuwa Utawala wa CCM chini ya Kinana ni tofauti na wa Makamba hivyo wabadilike. Ghafla watu wanaosadikiwa kuwa Majambazi wakamtoa Jicho Absalom.
Uwe makini na Wanasadikiwa kuwa Majambazi.
 
Absalom Kibanda aliwatahadharisha kuwa Utawala wa CCM chini ya Kinana ni tofauti na wa Makamba hivyo wabadilike. Ghafla watu wanaosadikiwa kuwa Majambazi wakamtoa Jicho Absalom.
Uwe makini na Wanasadikiwa kuwa Majambazi.
Duh kaka nimelisoma onyo lako. Lakini naamini Mungu yupo na ananisimamia. Asante kwa ushauri.
 
Tokalini fisi akamuhurumia binadamu na yeye ananjaa
Akili yako fupi kama mkia wa mbuzi inaangalia mambo kichama, soma hoja na angalia jinsi gani inaweza ikawa na msaada, usiletee ujuaji wa watoto wachanga wanabebwa na wazazi lakini kondakta akikaribia wanataka wao ndio wamlipie nauli mtu mzima aliyewabeba.
 
Akili yako fupi kama mkia wa mbuzi inaangalia mambo kichama, soma hoja na angalia jinsi gani inaweza ikawa na msaada, usiletee ujuaji wa watoto wachanga wanabebwa na wazazi lakini kondakta akikaribia wanataka wao ndio wamlipie nauli mtu mzima aliyewabeba.
unaona ulivyo mtupu...eti unaangalia mambo kichama....kwani hapo wewe umeongelea vyama vya ndondi?
 
Miezi kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015 katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Mama Asha Migiro walitembea nchi nzima kwa lengo maalum. Walikwenda kuiombea msamaha CCM mbele ya wananchi, walijaribu kadri walivyoweza kuirudisha CCM kwenye fikra za wananchi wa kawaida. Mzee Kinana hakusita kuwaita mizigo baadhi ya mawaziri waliyoonekana kutokuwa na msaada kwa serikali ya awamu ya nne. Wasomi wakagawanyika kimawazo kuhusiana na ziara zile za viongozi wa juu wa CCM nchi nzima.
Kawaita mzigo wakati mwenyekiti wake amewaona majembe...
 
unaona ulivyo mtupu...eti unaangalia mambo kichama....kwani hapo wewe umeongelea vyama vya ndondi?
Wewe ndio wale wale wenye upeo mdogo. Kaka zako na Baba zako ambao wamenielewa wamewakilisha hisia zako kistaarabu, nyinyi mnaodanganyiwa pipi hamuwezi kuelewa ujumbe wenye maana nyingi zinazohitaji tafakuri pana ya fikra, matokeo yake mnaongea kwa kutegemea mihemko wala sio ile nia ya kutaka kujifunza kitu fulani. Freeland nilishakwambia, yule anayejiona anajua kila kitu huwa kwenye nafasi ya kuonekana mjinga kuliko wajinga wote. Take my advice and change your attitude.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Duh kaka nimelisoma onyo lako. Lakini naamini Mungu yupo na ananisimamia. Asante kwa ushauri.
Wewe unaongea kama mwanaCCM, mwanaCHADEMA, au raia wa kawaida? Maana siku hizi CHADEMA ina bahati sana ya kupata washauri wazuri kutoka ndani ya CCM
 
CDM wawashauri CCM kuwa ikiwezekana kikatiba, wananchi wawe wanachagua wabunge, madiwani na viongozi wengine wa chini. Urais CCM wapange jinsi kuchaguana nani anakuwa Rais wa TZ kila baada ya miaka 5 au 10.
 
Kawaita mzigo wakati mwenyekiti wake amewaona majembe...
Lengo lilikuwa ni zaidi ya maoni ya mwenyekiti, lengo lilikuwa ni kukikomboa chama ambacho kilishageuka kuwa mali ya wezi wachache. Na lengo lilifanikiwa kwani JPM aliweza kukaa mbali na wafanyabiashara wenye sifa mbaya kwa kutumia msingi mzuri uliowekwa na kina Kinana na Migiro.
 
Umetoa ushauri mzuri, tatizo linakuwa hapa; CHADEMA wanajiona wao wasafi hawana makosa. Kwa hiyo kuiga waliyofanya Kinana na Migiro, naona itakuwa kibarua kigumu kwa CHADEMA.
Kinana na Migiro walifanya sanaa, na hakuna ambaye yupo tayari kuiga sanaa. Kwani walifanya kitu gani cha ziada? Mbona walipokutana na wananchi wanaokumbuka mambo wakawahoji maswali walipanic na kuwaita wanywa viroba?
 
Wewe unaongea kama mwanaCCM, mwanaCHADEMA, au raia wa kawaida? Maana siku hizi CHADEMA ina bahati sana ya kupata washauri wazuri kutoka ndani ya CCM
It doesn't matter naongea kama nani, kilicho muhimu ni nchi hii. Mwalimu alisema "CCM sio Mama yangu" lakini kumbuka kwamba bila ya Mwalimu CCM isingekuwa ni chama kikongwe barani Afrika. Wakati mwingine tujifunze kuiangalia Tanzania kwanza kabla hatujajidanganya kwamba vyama vinaanza halafu nchi inafuata, ukweli ni kwamba nchi inaanza halafu siasa za vyama ndio hufuatia.
 
Lengo lilikuwa ni zaidi ya maoni ya mwenyekiti, lengo lilikuwa ni kukikomboa chama ambacho kilishageuka kuwa mali ya wezi wachache. Na lengo lilifanikiwa kwani JPM aliweza kukaa mbali na wafanyabiashara wenye sifa mbaya kwa kutumia msingi mzuri uliowekwa na kina Kinana na Migiro.
Basi na tujivunie kuwa na mzalendo Kinana anayeipenda nchi yake.
 
It doesn't matter naongea kama nani, kilicho muhimu ni nchi hii. Mwalimu alisema "CCM sio Mama yangu" lakini kumbuka kwamba bila ya Mwalimu CCM isingekuwa ni chama kikongwe barani Afrika. Wakati mwingine tujifunze kuiangalia Tanzania kwanza kabla hatujajidanganya kwamba vyama vinaanza halafu nchi inafuata, ukweli ni kwamba nchi inaanza halafu siasa za vyama ndio hufuatia.
CCM imewekwa sawa na Kinana na Migiro kwa kauli yako. Let's move on then. CHADEMA watajijua.
Na kuhusu nini kinaanza kati ya chama na nchi,tell it to any politician uone kama atakubaliana na wewe. Kama na wewe ni politician, nina hakika pia haukubaliani na maneno hayo unayosema. Hata JPM ambaye akiwa kwenye jukwaa neutral anasema kuwa hahitaji kushabikia CCM, anapokuwa kwenye uwanja sahihi lazima atasimama na chama kwanza kabla ya nchi. Nasikia juzi amesema atapendelea jimbo ambalo mbunge wake ni wa CCM maana hawezi kumpa chakula mtoto wa jirani kabla wake hajashiba. Hii inatosha kukupa picha kwamba hata Rais ambaye tunamtumainia sana amepotoka kusimama na chama akasahau kwamba hapa anayetakiwa kusaidiwa si Mbunge (ambaye ni wa CCM), ni wananchi ambapo hata kama ingekuwa ni huo upendeleo, nina hakika hata huko anakoongoza mtoto wa jirani au mtoto wa kambo bado wapo 'watoto' wake pia. Cutting it short, wanasiasa huwezi kuwatenga na vyama vyao...na kwao Chama kinakuja kabla ya nchi. Ni mtizamo uliopotoka lakini ndivyo ilivyo.
 
Kinana na Migiro walifanya sanaa, na hakuna ambaye yupo tayari kuiga sanaa. Kwani walifanya kitu gani cha ziada? Mbona walipokutana na wananchi wanaokumbuka mambo wakawahoji maswali walipanic na kuwaita wanywa viroba?

Uhitaji kuumiza kichwa kujua kazi waliyofanya Kinana na Migori...hawa wamefanya kazi kubwa ya kurudisha matumaini ya wananchi kwa CCM. Hayo ya sanaa muulizeni Lowassa maana huyu ndio msanii mkubwa.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom