zema21
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 619
- 251
Binafsi huwa nashangazwa saana vitendo vinavyofanywa na serikali ya CCM kwa kutumia jeshi la polisi. Huwa mara nyingi wamekuwa wakizuia maandamano ya vyama vya upinzani kwa madai ya kuwa wamepata taarifa za kiitelijensia kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani.
Awali nilifikiria kuwa ni kweli kwamba vana dhamira safi ya kuwalinda wananchi wake lakini kumbe laa! Hao hao endapo chama kitakaidi huwa wanaenda eneo la tukio na kuanzisha vurugu kubwa ambayo inaleta uvunjifu wa amani na matukio ya mauaji.. sote tumeshudia matukio kadhaa likiwemo la arusha, ambapo polisi waliosema kuwa wanawakataza chadema ili kuzuia uvunjifu wa amani walienda wakaleta vurugu kubwaa, kujeruhi wananchi pamoja na mauaji ya wasiokuwa na hatia…
Tukio la juzi morogoro la polisi kuleta vurugu, kujeruhi na kuua ni kitu cha kushangaza sana! Badala yake baada ya polisi kuzidiwa nguvu, chadema waliandamana kwa amani, wakafika uwanjani, wakafanya mkutano na kumaliza kwa amani bila vurugu!!!
Kuna wakati polisi huzuia mikutano kwa kisingizio kuwa hawana polisi wakutosha kuwalinda chadema katika mkutano wao lakini ikitokea chadema wakasema wanaandama basi polisi na vifaa vingi utadhani wako vitani hutembea mitaani kwa ajili ya kuwadhibiti chadema, ebu jiulize hawa polisi huwa wanapatikana wapi? Iweje chadema wanambiwa kuwa hakuna askari wa kutosha kuwalinda katika maandamano yao hivyo wasiandamane lakini wakikaidi na kuandamana huwa askari lukuki hujazwa mitaani ili kuja kuwadhibiti? Huwa wanatoka wapi hawa?
Kwanini zile risasi za moto huwa hazielekezwi kwa akina dr slaa, au lisu au myika au mbowe bali ni kwa raia wa chini wasiokuwa hata na magwanda?
Tujiulize
Awali nilifikiria kuwa ni kweli kwamba vana dhamira safi ya kuwalinda wananchi wake lakini kumbe laa! Hao hao endapo chama kitakaidi huwa wanaenda eneo la tukio na kuanzisha vurugu kubwa ambayo inaleta uvunjifu wa amani na matukio ya mauaji.. sote tumeshudia matukio kadhaa likiwemo la arusha, ambapo polisi waliosema kuwa wanawakataza chadema ili kuzuia uvunjifu wa amani walienda wakaleta vurugu kubwaa, kujeruhi wananchi pamoja na mauaji ya wasiokuwa na hatia…
Tukio la juzi morogoro la polisi kuleta vurugu, kujeruhi na kuua ni kitu cha kushangaza sana! Badala yake baada ya polisi kuzidiwa nguvu, chadema waliandamana kwa amani, wakafika uwanjani, wakafanya mkutano na kumaliza kwa amani bila vurugu!!!
Kuna wakati polisi huzuia mikutano kwa kisingizio kuwa hawana polisi wakutosha kuwalinda chadema katika mkutano wao lakini ikitokea chadema wakasema wanaandama basi polisi na vifaa vingi utadhani wako vitani hutembea mitaani kwa ajili ya kuwadhibiti chadema, ebu jiulize hawa polisi huwa wanapatikana wapi? Iweje chadema wanambiwa kuwa hakuna askari wa kutosha kuwalinda katika maandamano yao hivyo wasiandamane lakini wakikaidi na kuandamana huwa askari lukuki hujazwa mitaani ili kuja kuwadhibiti? Huwa wanatoka wapi hawa?
Kwanini zile risasi za moto huwa hazielekezwi kwa akina dr slaa, au lisu au myika au mbowe bali ni kwa raia wa chini wasiokuwa hata na magwanda?
Tujiulize