CHADEMA, CUF: Mpinzani halisi atajulikana kesho

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233

CHADEMA, CUF: Mpinzani halisi atajulikana kesho

Na Yusuf Aboud

NIMEMSIKILIZA vema Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa Wawi, akizungumza katika mdahalo wa wazi ulioandaliwa na Vox Media na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI), kwa ufadhili wa ITV, mwishoni mwa wiki.

Katika mdahalo huo, alikuwa akichuana na Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe, ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Majadala ulihusu mwelekeo wa upinzani, na waliulizwa maswali mengi kwa pamoja, kubwa likihusu azima yao kuungana ili kuwa na upinzani imara.

Lakini Hamd Rashid alipotosha wasikilizaji katika hoja nyingi alizojenga, huku akishangiliwa na kundi la mashabiki wake, kuhusu haja ya wapinzani wote kuungana.

Kwanza, alikosea kusema CUF inakataa kuunda kambi na CHADEMA kwa sababu wao wanaitambua serikali, na CHADEMA haiitambui serikali.

Lakini palepale, Mwenyekiti wa CHADEMA aliposema chama chake kinaitambua serikali, bali kinashinikiza mabadiliko makubwa ya kimfumo, alikuwa ameimaliza nguvu hoja ya Hamad Rashid.

Lakini upotoshaji wa Hamad Rashid unasisitizwa na ukweli kwamba anajipendekeza kwa CCM. Zipo sababu. Kwa miaka 15 mfululizo, CUF hawakuitambua serikali ya Zanzibar. Lakini waliunda upinzani ndani ya Baraza la wawakilishi, chini ya uongozi wa Abubakari Khamis Bakari.

Pili, kwa muda wa miaka 15 CUF hawakuitambua serikali ya Zanzibar inayoundwa na CCM. Lakini, katika Bunge la Muungano, waliweza kushirikiana na CHADEMA na vyama vingine ambavyo havikujiingiza katika mgogoro wa Zanzibar. Sasa huu unafiki wa sasa wa CUF unatoka wapi?

Tatu, Hamad anataka upinzani ushirikishe vyama vyote vya upinzani bungeni. Lakini mwaka 1995, CUF walishirikiana na UDP na kuacha NCCR-Mageuzi nje ya kambi, huku wakijua NCCR-Mageuzi ilikuwa na wabunge 19; na CUF haikuwa na mbunge hata mmoja kutoka Bara.

Fatuma Maghimbi ndiye alikuwa kiongozi wa upinzani na John Cheyo naibu wake. Sasa kama aliweza kuacha vyama vingine nje, kwa nini analazimisha CHADEMA waingize vyama vingine katika kambi yao?

Hamad Rashid anataka gari, nyumba, posho na kuwatumia wabunge wa CCM kushinikiza mabadiliko ya baadhi ya vifungu vya kanuni za Bunge. Analilia posho na marupurupu kutoka serikalini, ambayo ameyafaidi kwa miaka mingi iliyopita.

Hakuwa amefikiria kwamba CHADEMA wangeweza kupata wabunge wengi wa kutosha kukiondoa chama chake katika uongozi wa upinzani. Sasa anataka kufuta kifungu kilekile ambacho alikiasisi mwenyewe wakati CUF kikiwa na wabunge wengi kuliko vingine.

Lakini kinachomuuma zaidi ni kwamba viongozi wenzake wa CUF, huko Visiwani, walijiandaa kuingia serikalini, wakati yeye akijiandaa kuendelea na uongozi wa upinzani bungeni.

Inamuuma kwanza yeye kakosa, wenzake wamepata; na sasa anataka kubadilisha vifungu ili kujipatia fursa nyingine. Kwa nini tusiseme anaonyesha ubinafsi wa hali ya juu?

Kifungu ambacho Hamad anashinikiza kubadilishwa ni kanuni ya 14 (3), 14 (4) na 113 (11) za Kanuni za Bunge za mwaka 2007.

Kanuni ya 14 (3) ambayo CUF na washirika wake wanashinikiza kubadilishwa inataka chama cha upinzani kitakachoruhusiwa kuchagua kiongozi wa upinzani bungeni, kiwe na wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili ya wabunge wote.

Vyama vya CUF, NCCR- Mageuzi na TLP vina wabunge 42 ambao hawakidhi matakwa hayo ya sheria, huku CUF ikiongoza kundi la vyama hivyo kwa kuwa na wabunge 36.

Kanuni za Bunge kwanza zinatoa fursa ya chama chenye wabunge wengi, kabla ya kuzungumzia muungano wa vyama. Anataka kuondoa maneno – Kambi rasmi ya upinzani bungeni ili kuipora CHADEMA haki yake ya kushikilia nyadhifa za uongozi ndani ya Bunge.

Kwa mujibu wa kumbukumbu za Bunge, Hamadi mwenyewe ndiye alipendekeza maneno “kambi rasmi ya upinzani bungeni.”

Kumbukumbu za Bunge zinaonyesha kuwa Kamati ya Kanuni ilikuwa chini ya uongozi wa Job Ndugai ambaye sasa ni naibu spika wa Bunge.

Wakati ule, Bunge lilikuwa linafanyia marekebisho kanuni za mwaka 2002, na kwamba kuwekwa kwa neno “kambi rasmi” kulitokana na Hamad kushindwa katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alishindwa na John Cheyo ambaye wakatio huo hakuwa katika kambi ya upinzani iliyokuwa inaundwa na CUF pekee.

Nne, Hamad amewasaidia Watanzania kutambua kirahisi kwamba hivi sasa, chama cha upinzani kilichobaki Tanzania, ni CHADEMA.

CCM inashambulia CHADEMA. CUF wanashambulia CHADEMA. NCCR-Mageuzi wanashambulia CHADEMA. TLP wanashambulia CHADEMA. UDP wanashambulia CHADEMA.

Na katika mazingira ambamo CUF ina ushirikiano wa kikatiba na CCM, huko visiwani, chama hicho kinapoteza sifa na nguvu ya kuwa chama cha upinzani kinachopaswa kuaminiwa na wapinzani wa kweli.

Wala hakina haki ya kweli ya kushinikiza kushirikishwa katika masuala ya upinzani, kwa maana kitawahujumu. Hakitaweza kutunza siri za wapinzani.

Na hata kama Hamad Rashid angependa kuzitunza, kwa maelezo kuwa Zanzibar wana katiba yao, serikali yao, mahakama yao; na kwamba masuala ya Muungano yazingatie msingi tofauti, ukweli unabaki kuwa Katibu Mkuu wa CUF ni mmoja, na ndiye anaandaa mikutano ya vikao vyote vikuu vya chama; na ndiye kiongozi mkuu mwenye sauti kuu kuliko wote; na huyuhuyu ndiye Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

CUF kinamuamini Seif kwa sababu ni kiongozi wake. Kwanini kinalazimisha CHADEMA nao wamuamini Seif?

Na ingawa alitaka kutushawishi Watanzania tuwalazimishe CHADEMA iwashirikishe wabunge wa vyama vingine, Hamad Rashid hajui kwamba hawezi kusemea vyama vingine?

Lakini kikubwa zaidi, hajui kwamba wanasiasa hawa wanaoshirikiana na CCM kukichukia CHADEMA, wanapata wapi ujasiri wa kutaka CHADEMA kiwaamini? Na kama hawaaminiani, kwa nini wanafikiri kwamba wanaweza kuunda ushirikiano ukadumu, bila kuhujumiana?

Je, CUF rafiki wa CCM kiutawala, anaweza kukaa meza moja na CHADEMA wakakipinga CCM kwa dhati? Haiwezekani. Na CHADEMA kama wanajua, ni vema waendeelee na msimamo wao, waongoze upinzani, wahamasishe umma.

Na wala CHADEMA wasitumie mfano wa ushirikiano wa CHADEMA na CCM Kigoma (2005-2010) kama kisingizio. Huu wa CUF na CCM ni wa kikatiba; na wote wako madarakani. Wamegawana vyeo, wakaridhika.

Kule Kigoma, CHADEMA na CCM walitofautiana, walipingana; na hawakuongoza serikali moja kwa wakati mmoja, bali walipeana miaka miwili na nusu kila chama.

Tusidanganyane. Vyama hivi havina nia moja. Haviaminiani. Kinachounganishwa ni nia, si idadi ya wabunge. Hawa hawana nia moja. Wanahujumiana. Na wengine wanatumiwa na CCM kumaliza nguvu za upinzani.

Ushauri wangu ni huu: Kila chama kiende vyake. Mpinzani wa kweli atajulikana baadaye.




Chanzo; MwanaHALISI.
 
Yaani Mwanahalisi wamekuwa too desperate. Hii article iko empty kabisa. Kwanza haiendani na kichwa chake cha habari!
 
Hii ni mojawapo ya makala nzuri sana katika gazeti hilo wiki hii. Anachosema mwandishi ni cha ukweli -- kwamba mpinzani halisi huku Tanzania Bara atajulikana siku zinavyozidi kuyoyoma. Mpinzani ni yue atakeyeanza kukubalika na wananchi wengi, pamoja na maneneo ya kenye migahawa, midahalo, humu JF etc. Na dalili za ujio wa mpinzani wa aina hiyo zaanza kuonekana -- na kwa Tz bara, nina hakika haitakuwa CUF.
 
Pamoja na changamoto zao zinazowakabili sasa hivi, kikitulia baada ya kusafisha safu zake na kujipanga upya, Chadema ni zaidi ya mbadala kwa CCM. CCM imepata mtikisiko mkubwa kutoka kwa CDM, si kutoka kwa CUF na ndo maana silaha zao sasa zaelekezwa kwao, na si kwa CUF.
 
Pamoja na changamoto zao zinazowakabili sasa hivi, kikitulia baada ya kusafisha safu zake na kujipanga upya, Chadema ni zaidi ya mbadala kwa CCM. CCM imepata mtikisiko mkubwa kutoka kwa CDM, si kutoka kwa CUF na ndo maana silaha zao sasa zaelekezwa kwao, na si kwa CUF.

Penye rangi: Hivi kura walizopata Wabunge wote wa CUF kule Visiwani zinazidi kura za Halima Mdee na Mnyika? Nasikia kule Mbunge huchaguliwa kwa kura kati ya 3,000 na 6,000 tu, wakati huku bara Mbunge huchaguliwa kwa maelfu ya kura. Halafu eti CUF ndo wanataka kuendelea kuwa wasemaji wakubwa wa wapinzani wa Bara. Inaingia akilini? Wapinzani bara sasa wameamka!
 
Yaani Mwanahalisi wamekuwa too desperate. Hii article iko empty kabisa. Kwanza haiendani na kichwa chake cha habari!
watu wengine kwa kuropoka ni wazuri. Ebu mkuu soma vizuri makala ya mwandishi kisha jadili hoja........

Nampongeza mwandishi wa makala hii kwa kuwa ameeleza ukweli. Vyama vijipange, viwe na hoja na hapo ndipo tutakapoona mpinzani wa kweli anavyopatikana. Najua Kikwete anaweza kuteua watu wa CUF kuwa wabunge ili wapate kuunda kambi ya upinzani na kuua nguvu za Chadema bungeni lakini hoja na mwelekeo wa vyama ndo vinatakiwa!!!
 
CUF ni mpinzani halisi miaka ming na ndio chama kilicho ipeleka ccm puta mpaka kupata baadhi ya mabadilko yaliyo kuwepo leo hii, huwezi kulinganisha na chama cha mtandao, kikabila na kidini ambacho kinapata coverage kubwa kwa sababu ya mitandao

Chadema bado hawaja komaa kisiasa, M/kiti na Katibu wao hawana uzowefu ya kisiasa, just aliacha kuhubiri hivi karibunu na mwingine kuacha u-DJ wa night club, unategemea nini ?

Leo hatumtambui raisi wa tanzania , mara kesho tunamtambua, leo walkout bungeni, kesho sitting in bungeni. Chadema walete mabadiliko na democracia ya kweli ndani ya chama chake

Chadema uwezi linganisha na CUF au CCM, ndani ya vyama hivi kuna democrasi, hakuna ukabila wala udini
 
CHADEMA, CUF: Mpinzani halisi atajulikana kesho

Na Yusuf Aboud

NIMEMSIKILIZA vema Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa Wawi, akizungumza katika mdahalo wa wazi ulioandaliwa na Vox Media na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI), kwa ufadhili wa ITV, mwishoni mwa wiki.

Katika mdahalo huo, alikuwa akichuana na Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe, ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Majadala ulihusu mwelekeo wa upinzani, na waliulizwa maswali mengi kwa pamoja, kubwa likihusu azima yao kuungana ili kuwa na upinzani imara.

Lakini Hamd Rashid alipotosha wasikilizaji katika hoja nyingi alizojenga, huku akishangiliwa na kundi la mashabiki wake, kuhusu haja ya wapinzani wote kuungana.

Kwanza, alikosea kusema CUF inakataa kuunda kambi na CHADEMA kwa sababu wao wanaitambua serikali, na CHADEMA haiitambui serikali.

Lakini palepale, Mwenyekiti wa CHADEMA aliposema chama chake kinaitambua serikali, bali kinashinikiza mabadiliko makubwa ya kimfumo, alikuwa ameimaliza nguvu hoja ya Hamad Rashid.

Lakini upotoshaji wa Hamad Rashid unasisitizwa na ukweli kwamba anajipendekeza kwa CCM. Zipo sababu. Kwa miaka 15 mfululizo, CUF hawakuitambua serikali ya Zanzibar. Lakini waliunda upinzani ndani ya Baraza la wawakilishi, chini ya uongozi wa Abubakari Khamis Bakari.

Pili, kwa muda wa miaka 15 CUF hawakuitambua serikali ya Zanzibar inayoundwa na CCM. Lakini, katika Bunge la Muungano, waliweza kushirikiana na CHADEMA na vyama vingine ambavyo havikujiingiza katika mgogoro wa Zanzibar. Sasa huu unafiki wa sasa wa CUF unatoka wapi?

Tatu, Hamad anataka upinzani ushirikishe vyama vyote vya upinzani bungeni. Lakini mwaka 1995, CUF walishirikiana na UDP na kuacha NCCR-Mageuzi nje ya kambi, huku wakijua NCCR-Mageuzi ilikuwa na wabunge 19; na CUF haikuwa na mbunge hata mmoja kutoka Bara.

Fatuma Maghimbi ndiye alikuwa kiongozi wa upinzani na John Cheyo naibu wake. Sasa kama aliweza kuacha vyama vingine nje, kwa nini analazimisha CHADEMA waingize vyama vingine katika kambi yao?

Hamad Rashid anataka gari, nyumba, posho na kuwatumia wabunge wa CCM kushinikiza mabadiliko ya baadhi ya vifungu vya kanuni za Bunge. Analilia posho na marupurupu kutoka serikalini, ambayo ameyafaidi kwa miaka mingi iliyopita.

Hakuwa amefikiria kwamba CHADEMA wangeweza kupata wabunge wengi wa kutosha kukiondoa chama chake katika uongozi wa upinzani. Sasa anataka kufuta kifungu kilekile ambacho alikiasisi mwenyewe wakati CUF kikiwa na wabunge wengi kuliko vingine.

Lakini kinachomuuma zaidi ni kwamba viongozi wenzake wa CUF, huko Visiwani, walijiandaa kuingia serikalini, wakati yeye akijiandaa kuendelea na uongozi wa upinzani bungeni.

Inamuuma kwanza yeye kakosa, wenzake wamepata; na sasa anataka kubadilisha vifungu ili kujipatia fursa nyingine. Kwa nini tusiseme anaonyesha ubinafsi wa hali ya juu?

Kifungu ambacho Hamad anashinikiza kubadilishwa ni kanuni ya 14 (3), 14 (4) na 113 (11) za Kanuni za Bunge za mwaka 2007.

Kanuni ya 14 (3) ambayo CUF na washirika wake wanashinikiza kubadilishwa inataka chama cha upinzani kitakachoruhusiwa kuchagua kiongozi wa upinzani bungeni, kiwe na wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili ya wabunge wote.

Vyama vya CUF, NCCR- Mageuzi na TLP vina wabunge 42 ambao hawakidhi matakwa hayo ya sheria, huku CUF ikiongoza kundi la vyama hivyo kwa kuwa na wabunge 36.

Kanuni za Bunge kwanza zinatoa fursa ya chama chenye wabunge wengi, kabla ya kuzungumzia muungano wa vyama. Anataka kuondoa maneno – Kambi rasmi ya upinzani bungeni ili kuipora CHADEMA haki yake ya kushikilia nyadhifa za uongozi ndani ya Bunge.

Kwa mujibu wa kumbukumbu za Bunge, Hamadi mwenyewe ndiye alipendekeza maneno “kambi rasmi ya upinzani bungeni.”

Kumbukumbu za Bunge zinaonyesha kuwa Kamati ya Kanuni ilikuwa chini ya uongozi wa Job Ndugai ambaye sasa ni naibu spika wa Bunge.

Wakati ule, Bunge lilikuwa linafanyia marekebisho kanuni za mwaka 2002, na kwamba kuwekwa kwa neno “kambi rasmi” kulitokana na Hamad kushindwa katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alishindwa na John Cheyo ambaye wakatio huo hakuwa katika kambi ya upinzani iliyokuwa inaundwa na CUF pekee.

Nne, Hamad amewasaidia Watanzania kutambua kirahisi kwamba hivi sasa, chama cha upinzani kilichobaki Tanzania, ni CHADEMA.

CCM inashambulia CHADEMA. CUF wanashambulia CHADEMA. NCCR-Mageuzi wanashambulia CHADEMA. TLP wanashambulia CHADEMA. UDP wanashambulia CHADEMA.

Na katika mazingira ambamo CUF ina ushirikiano wa kikatiba na CCM, huko visiwani, chama hicho kinapoteza sifa na nguvu ya kuwa chama cha upinzani kinachopaswa kuaminiwa na wapinzani wa kweli.

Wala hakina haki ya kweli ya kushinikiza kushirikishwa katika masuala ya upinzani, kwa maana kitawahujumu. Hakitaweza kutunza siri za wapinzani.

Na hata kama Hamad Rashid angependa kuzitunza, kwa maelezo kuwa Zanzibar wana katiba yao, serikali yao, mahakama yao; na kwamba masuala ya Muungano yazingatie msingi tofauti, ukweli unabaki kuwa Katibu Mkuu wa CUF ni mmoja, na ndiye anaandaa mikutano ya vikao vyote vikuu vya chama; na ndiye kiongozi mkuu mwenye sauti kuu kuliko wote; na huyuhuyu ndiye Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

CUF kinamuamini Seif kwa sababu ni kiongozi wake. Kwanini kinalazimisha CHADEMA nao wamuamini Seif?

Na ingawa alitaka kutushawishi Watanzania tuwalazimishe CHADEMA iwashirikishe wabunge wa vyama vingine, Hamad Rashid hajui kwamba hawezi kusemea vyama vingine?

Lakini kikubwa zaidi, hajui kwamba wanasiasa hawa wanaoshirikiana na CCM kukichukia CHADEMA, wanapata wapi ujasiri wa kutaka CHADEMA kiwaamini? Na kama hawaaminiani, kwa nini wanafikiri kwamba wanaweza kuunda ushirikiano ukadumu, bila kuhujumiana?

Je, CUF rafiki wa CCM kiutawala, anaweza kukaa meza moja na CHADEMA wakakipinga CCM kwa dhati? Haiwezekani. Na CHADEMA kama wanajua, ni vema waendeelee na msimamo wao, waongoze upinzani, wahamasishe umma.

Na wala CHADEMA wasitumie mfano wa ushirikiano wa CHADEMA na CCM Kigoma (2005-2010) kama kisingizio. Huu wa CUF na CCM ni wa kikatiba; na wote wako madarakani. Wamegawana vyeo, wakaridhika.

Kule Kigoma, CHADEMA na CCM walitofautiana, walipingana; na hawakuongoza serikali moja kwa wakati mmoja, bali walipeana miaka miwili na nusu kila chama.

Tusidanganyane. Vyama hivi havina nia moja. Haviaminiani. Kinachounganishwa ni nia, si idadi ya wabunge. Hawa hawana nia moja. Wanahujumiana. Na wengine wanatumiwa na CCM kumaliza nguvu za upinzani.

Ushauri wangu ni huu: Kila chama kiende vyake. Mpinzani wa kweli atajulikana baadaye.




Chanzo; MwanaHALISI.

Kweli vita vya panzi ni furaha ya kunguru. Badala ya kuungana ndio kila mtu awe kivyake. Kwa mtaji huu CCM itatawala Tanzania mpaka mwisho wa dunia hii wana JF wenzangu
 
Wakuu naomba sana JF isigeuzwe kuwa uwanja wa udini na ukabila bila hata kuonyesha vithibitisho ili kama ni kweli tukemee hayo mmbo kwa pamoja. Kuna watu kila kitu hapa huunganishwa na udini na ukabila. Sasa wengine tunakereka sana kiasi inakuwa kama kuandika matusi hapa kila mara. Hebu tuonyeshe ukomavu wa akili zaidi.
 

Penye rangi: Hivi kura walizopata Wabunge wote wa CUF kule Visiwani zinazidi kura za Halima Mdee na Mnyika? Nasikia kule Mbunge huchaguliwa kwa kura kati ya 3,000 na 6,000 tu, wakati huku bara Mbunge huchaguliwa kwa maelfu ya kura. Halafu eti CUF ndo wanataka kuendelea kuwa wasemaji wakubwa wa wapinzani wa Bara. Inaingia akilini? Wapinzani bara sasa wameamka!

Mngemplekea Halima Mdee mmoja na John Mnyika mmoja akashinde, kitu gani kiliwazuia?
 

Penye rangi: Hivi kura walizopata Wabunge wote wa CUF kule Visiwani zinazidi kura za Halima Mdee na Mnyika? Nasikia kule Mbunge huchaguliwa kwa kura kati ya 3,000 na 6,000 tu, wakati huku bara Mbunge huchaguliwa kwa maelfu ya kura. Halafu eti CUF ndo wanataka kuendelea kuwa wasemaji wakubwa wa wapinzani wa Bara. Inaingia akilini? Wapinzani bara sasa wameamka!
hapa tuko pamoja nadhani kuna haja ya kuliangalia na hili, hivi mimi nichanguliwe na watu 40000 na wewe uchaguliwe na watu 2800 halafu tuwe sawa hapo kuna haki gani?
 
Kweli vita vya panzi ni furaha ya kunguru. Badala ya kuungana ndio kila mtu awe kivyake. Kwa mtaji huu CCM itatawala Tanzania mpaka mwisho wa dunia hii wana JF wenzangu
kama mwisho wa dunia ni ndani ya miaka kumi sawa wanaweza lakini kama nitofauti na hapo...you are wrong
 
Devide and rule!
Kuna aina nyingi za kufikiri...
hata kuota nako ni kufikiri, mtu anaweza kulala na akaamka akisema ameota kajenga ghorofa!
Yuko mmoja aliota kaokota fuko la pesa, akawa anakwenda fuko likatoboka akatia kidole ile fedha zake zisidondoke.. aliposhtusha asubuhi alikojikuta kajiweka dole hakutamani hata kumsimulia mtu....
(Mtaniwia radhi nasema kwa mithali sasa)
Jambo jema ni mtu kuwa mweledi, ikishindikana kuwa mjuzi, ikishindikana kuwa mwenye kujifunza, ikishindikana kuwa mwenye kuuliza....
... MTU YEYOTE ANAEDHANI ANAJUA KULIKO WENZAKE BASI HUYO NDIYE ASIEJUA CHOCHOTE KULIKO WATU WOTE.
 
hapa tuko pamoja nadhani kuna haja ya kuliangalia na hili, hivi mimi nichanguliwe na watu 40000 na wewe uchaguliwe na watu 2800 halafu tuwe sawa hapo kuna haki gani?
hapo kwenye watu Napenda niseme hivi: Ni bora mtu kuchaguliwa na watu 10 walio macho kuliko kuchaguliwa na watu 1000 walioko usingizini! (mtanisamehe kwa hili) Wingi si hoja bali ubora. ndio maana tunasema ni bora wakafa wajinga elfu moja kuliko kufa msomi mmoja.
Nimesomeka
 
Naam,mwandishi anasema, "Ushauri wangu ni huu: Kila chama kiende vyake. Mpinzani wa kweli atajulikana baadaye."

Time will tell,tusubiri tuone, mwisho wa ngebe utaonekana!
 
hapo kwenye watu Napenda niseme hivi: Ni bora mtu kuchaguliwa na watu 10 walio macho kuliko kuchaguliwa na watu 1000 walioko usingizini! (mtanisamehe kwa hili) Wingi si hoja bali ubora. ndio maana tunasema ni bora wakafa wajinga elfu moja kuliko kufa msomi mmoja.
Nimesomeka
umesomeka mkuu lakini haiwezekani wafe wasomi 40000 kwa ajili ya wajinga 2800
 
Goood!!!!!!!!11 Ni uchambuzi mzuri ambao unaweza kuonyesha sura halisi za watu. Hamad Rashid toka asamehewe deni lake na Savings and Finance Bank kawa zuzu kweli, may be serikali ilimlipia ndio maana kawa hivi, walitaka kupiga mnada nyumba yake!!!!!!!!!!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom