CHADEMA chama njaa, nani apendaye njaa?

The Giantist

JF-Expert Member
Dec 12, 2018
214
86
Habari ya leo tena wanabodi wenzangu. Kwa mara nyingine tena, nimekuja kuwaeleza machache ya muhimu yenye muelekeo wa kisiasa katika siasa ya nchi yetu.

Kabla sijaendelea mbele zaidi, ni muhimu wote tukakubaliana kuhusu Shibe na Njaa. Shibe na Njaa ni majina mawili ama mambo mawili ambayo yanategemeana. Ijapokuwa Njaa ndiye mwenye umaarufu zaidi kuliko Shibe. Kwa nini Njaa? Ni kwa sababu binadamu kwa asili ni mwenye matamanio chanya katika yote yamuhusuyo na amekuwa akipendelea zaidi raha kuliko karaha.

Na ndio maana katika Shibe kuna Raha na katika Njaa kuna karaha! Mtu mwenye njaa anaweza akaonekana kwenye maneno na matendo yake yenye udhaifu mkubwa na yaliyokosa afya na matumaini. Bila shaka mtu mwenye Shibe atafahamika kwa maneno na matendo yake yenye uchangamfu na yenye afya na matumaini.

Na katika siasa hivyo hivyo, vipo vyama vya siasa baadhi ambavyo ni vyenye Njaa na vipo vyama vya siasa baadhi ambavyo ni vyenye Shibe. Sasa basi, sio wajibu wangu wa kusema kwa kuhitimisha kwamba chama fulani ni chenye Njaa na chama fulani ni chenye Shibe. Wenye wajibu huo ni wananchi wenyewe, ambao wao ndio walengwa haswa wa vyama hivyo vya siasa.

Wananchi wanasema:


Katika siasa ya Tanzania ni afadhali Chama cha Mapinduzi. Kwa sababu ni CCM ambayo kinawapa Shibe wananchi kwa maana ya kuwatimizia mahitaji yao ya msingi ya kila siku. Wao wanasema kwa kuwa wameshuhudia kwamba; barabara sio shida tena Kama sehemu muhimu ya uchukuzi, Huduma ya Afya sio kero tena kwa wananchi wa maeneo yote, Wafanyabiashara ndogondogo (al-maarufu wamachinga) wanafanya shughuli zao kwa raha mustarehe bila karaha na kubughudhiwa, makundi maalum (wanawake, vijana na waremavu) wameshuhudia raha tele katika uongozi wa CCM, wanasema ni kijana aliyechanganyikiwa tu ndiye atashindwa kung'amua ukweli huo; umeme sio tena mjini, hata vijijini upo sasa; wananchi wameshuhudia usawa kwa walionacho na wasionacho, kwa wenye mamlaka na wasio kuwa na mamlaka katika uongozi wa CCM n.k.

Lakini kubwa zaidi na la muhimu ni kule kuendelea kuulinda na kuudumisha uhuru wa nchi yetu, na Muungano wetu. Ambapo hatukuwahi kuuza heshima yetu kwa ajili ya kujitafutia maendeleo yetu wala kuuyumbisha Muungano wetu kwa sababu Muungano wetu ni alama ya Uhuru wetu. Na katika kukuunga mkono hoja hiyo, wananchi wameona jinsi ambavyo sekta ya madini imeweza kupambana na kuzuia kabisa ukiritimba uliokuwa ukifanywa na wazungu katika sekta hiyo. Ijapokuwa kuna waganga wa kisiasa ambao walipiga Ramli zao na kutaka kujaribu kuwaongopea watanzania kwamba, tutakiona cha mtema kuni, kwa sababu ya kuwazuia wazungu wasiendelee kutunyonya kupitia sekta ya madini (hayo yalisemwa na mganga wa siasa nchini Tundu Lissu). Hivyo CCM ni chama chenye Shibe kwa wananchi.

Wananchi wanaendelea kusema:

Vyama vya siasa nchini, ukiiondoa CCM, ni vyama vyenye Njaa! Huku wakisema CHADEMA ndio top leader wao (yaani kiongozi wao). Kwa nini wao wanasema: ni kwa sababu vinapiga kelele mno kuliko kutekeleza yale wanayoyapigia kelele, kwa mfano ni wahubiri wazuri wa maendeleo na demokrasia lakini sio watekelazaji wa demokrasi na maendeleo; viongozi wake hawaoneshi nia ya dhahiri ya kulinda na kuudumisha uhuru na Muungano wetu; sio wenye nia ya dhati ya kuwapa Shibe wananchi kwa matendo, kwani kama wangekuwa na nia hiyo kweli, inakuwaje wanashindwa kuunga mkono juhudi za CCM za kuwaletea wananchi Maendeleo, badala yake wamgeuka kuwa wapinzani wa CCM. Hata hivyo wanaendelea kusema kuwa, ni vyama vyenye Njaa kwa sababu vipo pale kwa ajili kula ruzuku tu za serikali.

Wananchi wanaendelea kusema:


Hata katika suala la Covid-19, viongozi wa vyama Njaa walipiga Ramli na wakaona vifo vingi zaidi kuliko ushindi; Waliwajaza hofu kuliko matumaini. Wakati huo CCM kama chama kiongozi, kiliendelea kuonesha njia maridhawa kwa wananchi, kwamba ni jinsi gani wanaweza wakaishi na kuendelea kufanya kazi bila vifo wala hofu ya Covid-19.

Mwisho, wananchi wanagundua kuwa, ikiwa wataruhusu chama Njaa kiongozi (yaani CHADEMA) kiwaongoze, basi wapo kwenye hatari ya kurudishwa kwenye Njaa. Njaa ya Uhuru, Njaa ya uchumi, Njaa ya kujiamini, Njaa ya maendeleo.

Wananchi hao, wanahitimisha na kusema:

Mwaka wa 2020-2025 ni wa CCM tena na Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI TENA!!! Hakuna anayependa Njaa kwa kujitakia, na kwamba wao wanataka Shibe.

Karibu 2020!
Sauti ya Mdodomia
 
Bandiko ndefu la kijinga kama hili atasoma Nani?
Nendeni mkadukue account ya kigogo kwanza kule Twitter
 
Mwamba kala ruzuku peke yake? 8b wapi? Mpunga wa kubadilisha gia angani, za mzee mamvi?? 12B zote kapiga peke yake, bado michango ya wabunge kila mwezi! DJ ni noma sana
 
Moderator naomba uwe unaunganisha thread zote za watu wa lumumba kila thread ni CHADEMA tu.
 
Habari ya leo tena wanabodi wenzangu. Kwa mara nyingine tena, nimekuja kuwaeleza machache ya muhimu yenye muelekeo wa kisiasa katika siasa ya nchi yetu.

Kabla sijaendelea mbele zaidi, ni muhimu wote tukakubaliana kuhusu Shibe na Njaa. Shibe na Njaa ni majina mawili ama mambo mawili ambayo yanategemeana. Ijapokuwa Njaa ndiye mwenye umaarufu zaidi kuliko Shibe. Kwa nini Njaa? Ni kwa sababu binadamu kwa asili ni mwenye matamanio chanya katika yote yamuhusuyo na amekuwa akipendelea zaidi raha kuliko karaha.

Na ndio maana katika Shibe kuna Raha na katika Njaa kuna karaha! Mtu mwenye njaa anaweza akaonekana kwenye maneno na matendo yake yenye udhaifu mkubwa na yaliyokosa afya na matumaini. Bila shaka mtu mwenye Shibe atafahamika kwa maneno na matendo yake yenye uchangamfu na yenye afya na matumaini.

Na katika siasa hivyo hivyo, vipo vyama vya siasa baadhi ambavyo ni vyenye Njaa na vipo vyama vya siasa baadhi ambavyo ni vyenye Shibe. Sasa basi, sio wajibu wangu wa kusema kwa kuhitimisha kwamba chama fulani ni chenye Njaa na chama fulani ni chenye Shibe. Wenye wajibu huo ni wananchi wenyewe, ambao wao ndio walengwa haswa wa vyama hivyo vya siasa.

Wananchi wanasema:

Katika siasa ya Tanzania ni afadhali Chama cha Mapinduzi. Kwa sababu ni CCM ambayo kinawapa Shibe wananchi kwa maana ya kuwatimizia mahitaji yao ya msingi ya kila siku. Wao wanasema kwa kuwa wameshuhudia kwamba; barabara sio shida tena Kama sehemu muhimu ya uchukuzi, Huduma ya Afya sio kero tena kwa wananchi wa maeneo yote, Wafanyabiashara ndogondogo (al-maarufu wamachinga) wanafanya shughuli zao kwa raha mustarehe bila karaha na kubughudhiwa, makundi maalum (wanawake, vijana na waremavu) wameshuhudia raha tele katika uongozi wa CCM, wanasema ni kijana aliyechanganyikiwa tu ndiye atashindwa kung'amua ukweli huo; umeme sio tena mjini, hata vijijini upo sasa; wananchi wameshuhudia usawa kwa walionacho na wasionacho, kwa wenye mamlaka na wasio kuwa na mamlaka katika uongozi wa CCM n.k.

Lakini kubwa zaidi na la muhimu ni kule kuendelea kuulinda na kuudumisha uhuru wa nchi yetu, na Muungano wetu. Ambapo hatukuwahi kuuza heshima yetu kwa ajili ya kujitafutia maendeleo yetu wala kuuyumbisha Muungano wetu kwa sababu Muungano wetu ni alama ya Uhuru wetu. Na katika kukuunga mkono hoja hiyo, wananchi wameona jinsi ambavyo sekta ya madini imeweza kupambana na kuzuia kabisa ukiritimba uliokuwa ukifanywa na wazungu katika sekta hiyo. Ijapokuwa kuna waganga wa kisiasa ambao walipiga Ramli zao na kutaka kujaribu kuwaongopea watanzania kwamba, tutakiona cha mtema kuni, kwa sababu ya kuwazuia wazungu wasiendelee kutunyonya kupitia sekta ya madini (hayo yalisemwa na mganga wa siasa nchini Tundu Lissu). Hivyo CCM ni chama chenye Shibe kwa wananchi.

Wananchi wanaendelea kusema:

Vyama vya siasa nchini, ukiiondoa CCM, ni vyama vyenye Njaa! Huku wakisema CHADEMA ndio top leader wao (yaani kiongozi wao). Kwa nini wao wanasema: ni kwa sababu vinapiga kelele mno kuliko kutekeleza yale wanayoyapigia kelele, kwa mfano ni wahubiri wazuri wa maendeleo na demokrasia lakini sio watekelazaji wa demokrasi na maendeleo; viongozi wake hawaoneshi nia ya dhahiri ya kulinda na kuudumisha uhuru na Muungano wetu; sio wenye nia ya dhati ya kuwapa Shibe wananchi kwa matendo, kwani kama wangekuwa na nia hiyo kweli, inakuwaje wanashindwa kuunga mkono juhudi za CCM za kuwaletea wananchi Maendeleo, badala yake wamgeuka kuwa wapinzani wa CCM. Hata hivyo wanaendelea kusema kuwa, ni vyama vyenye Njaa kwa sababu vipo pale kwa ajili kula ruzuku tu za serikali.

Wananchi wanaendelea kusema:

Hata katika suala la Covid-19, viongozi wa vyama Njaa walipiga Ramli na wakaona vifo vingi zaidi kuliko ushindi; Waliwajaza hofu kuliko matumaini. Wakati huo CCM kama chama kiongozi, kiliendelea kuonesha njia maridhawa kwa wananchi, kwamba ni jinsi gani wanaweza wakaishi na kuendelea kufanya kazi bila vifo wala hofu ya Covid-19.

Mwisho, wananchi wanagundua kuwa, ikiwa wataruhusu chama Njaa kiongozi (yaani CHADEMA) kiwaongoze, basi wapo kwenye hatari ya kurudishwa kwenye Njaa. Njaa ya Uhuru, Njaa ya uchumi, Njaa ya kujiamini, Njaa ya maendeleo.

Wananchi hao, wanahitimisha na kusema:

Mwaka wa 2020-2025 ni wa CCM tena na Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI TENA!!! Hakuna anayependa Njaa kwa kujitakia, na kwamba wao wanataka Shibe.

Karibu 2020!
Sauti ya Mdodomia
Wewe utakuwa umetokea zile pande ambazo ccm imeloga watu mpaka wanafikiri ccm ni nchi. Angalia maendeleo duni ya mkoa unakotoka ni kwasababu ya kukumbatia ccm lakini kamwe hamuiachi ccm. Na wewe ndio ka-msomi ka huko kwenu upo hivi je uliwaacha kijijini sijui watakuwa vipi?
 
Habari ya leo tena wanabodi wenzangu. Kwa mara nyingine tena, nimekuja kuwaeleza machache ya muhimu yenye muelekeo wa kisiasa katika siasa ya nchi yetu.

Kabla sijaendelea mbele zaidi, ni muhimu wote tukakubaliana kuhusu Shibe na Njaa. Shibe na Njaa ni majina mawili ama mambo mawili ambayo yanategemeana. Ijapokuwa Njaa ndiye mwenye umaarufu zaidi kuliko Shibe. Kwa nini Njaa? Ni kwa sababu binadamu kwa asili ni mwenye matamanio chanya katika yote yamuhusuyo na amekuwa akipendelea zaidi raha kuliko karaha.

Na ndio maana katika Shibe kuna Raha na katika Njaa kuna karaha! Mtu mwenye njaa anaweza akaonekana kwenye maneno na matendo yake yenye udhaifu mkubwa na yaliyokosa afya na matumaini. Bila shaka mtu mwenye Shibe atafahamika kwa maneno na matendo yake yenye uchangamfu na yenye afya na matumaini.

Na katika siasa hivyo hivyo, vipo vyama vya siasa baadhi ambavyo ni vyenye Njaa na vipo vyama vya siasa baadhi ambavyo ni vyenye Shibe. Sasa basi, sio wajibu wangu wa kusema kwa kuhitimisha kwamba chama fulani ni chenye Njaa na chama fulani ni chenye Shibe. Wenye wajibu huo ni wananchi wenyewe, ambao wao ndio walengwa haswa wa vyama hivyo vya siasa.

Wananchi wanasema:


Katika siasa ya Tanzania ni afadhali Chama cha Mapinduzi. Kwa sababu ni CCM ambayo kinawapa Shibe wananchi kwa maana ya kuwatimizia mahitaji yao ya msingi ya kila siku. Wao wanasema kwa kuwa wameshuhudia kwamba; barabara sio shida tena Kama sehemu muhimu ya uchukuzi, Huduma ya Afya sio kero tena kwa wananchi wa maeneo yote, Wafanyabiashara ndogondogo (al-maarufu wamachinga) wanafanya shughuli zao kwa raha mustarehe bila karaha na kubughudhiwa, makundi maalum (wanawake, vijana na waremavu) wameshuhudia raha tele katika uongozi wa CCM, wanasema ni kijana aliyechanganyikiwa tu ndiye atashindwa kung'amua ukweli huo; umeme sio tena mjini, hata vijijini upo sasa; wananchi wameshuhudia usawa kwa walionacho na wasionacho, kwa wenye mamlaka na wasio kuwa na mamlaka katika uongozi wa CCM n.k.

Lakini kubwa zaidi na la muhimu ni kule kuendelea kuulinda na kuudumisha uhuru wa nchi yetu, na Muungano wetu. Ambapo hatukuwahi kuuza heshima yetu kwa ajili ya kujitafutia maendeleo yetu wala kuuyumbisha Muungano wetu kwa sababu Muungano wetu ni alama ya Uhuru wetu. Na katika kukuunga mkono hoja hiyo, wananchi wameona jinsi ambavyo sekta ya madini imeweza kupambana na kuzuia kabisa ukiritimba uliokuwa ukifanywa na wazungu katika sekta hiyo. Ijapokuwa kuna waganga wa kisiasa ambao walipiga Ramli zao na kutaka kujaribu kuwaongopea watanzania kwamba, tutakiona cha mtema kuni, kwa sababu ya kuwazuia wazungu wasiendelee kutunyonya kupitia sekta ya madini (hayo yalisemwa na mganga wa siasa nchini Tundu Lissu). Hivyo CCM ni chama chenye Shibe kwa wananchi.

Wananchi wanaendelea kusema:

Vyama vya siasa nchini, ukiiondoa CCM, ni vyama vyenye Njaa! Huku wakisema CHADEMA ndio top leader wao (yaani kiongozi wao). Kwa nini wao wanasema: ni kwa sababu vinapiga kelele mno kuliko kutekeleza yale wanayoyapigia kelele, kwa mfano ni wahubiri wazuri wa maendeleo na demokrasia lakini sio watekelazaji wa demokrasi na maendeleo; viongozi wake hawaoneshi nia ya dhahiri ya kulinda na kuudumisha uhuru na Muungano wetu; sio wenye nia ya dhati ya kuwapa Shibe wananchi kwa matendo, kwani kama wangekuwa na nia hiyo kweli, inakuwaje wanashindwa kuunga mkono juhudi za CCM za kuwaletea wananchi Maendeleo, badala yake wamgeuka kuwa wapinzani wa CCM. Hata hivyo wanaendelea kusema kuwa, ni vyama vyenye Njaa kwa sababu vipo pale kwa ajili kula ruzuku tu za serikali.

Wananchi wanaendelea kusema:


Hata katika suala la Covid-19, viongozi wa vyama Njaa walipiga Ramli na wakaona vifo vingi zaidi kuliko ushindi; Waliwajaza hofu kuliko matumaini. Wakati huo CCM kama chama kiongozi, kiliendelea kuonesha njia maridhawa kwa wananchi, kwamba ni jinsi gani wanaweza wakaishi na kuendelea kufanya kazi bila vifo wala hofu ya Covid-19.

Mwisho, wananchi wanagundua kuwa, ikiwa wataruhusu chama Njaa kiongozi (yaani CHADEMA) kiwaongoze, basi wapo kwenye hatari ya kurudishwa kwenye Njaa. Njaa ya Uhuru, Njaa ya uchumi, Njaa ya kujiamini, Njaa ya maendeleo.

Wananchi hao, wanahitimisha na kusema:

Mwaka wa 2020-2025 ni wa CCM tena na Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI TENA!!! Hakuna anayependa Njaa kwa kujitakia, na kwamba wao wanataka Shibe.

Karibu 2020!
Sauti ya Mdodomia
Upuuzi mtupu kutoka kwa mla viwavijeshi
 
Back
Top Bottom