My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,283
Nakikumbuka Kitabu cha" Bush at war" kilichoandikwa na mwandishi wa Marekani, Bob Woodward.
Mara baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Sept 11, Mwandishi Woodward anasimulia jinsi Bush alivyokuwa Kachanganyikiwa mara baada ya mashambulizi yale .
Hasa baada ya hatua za kiusalama zilizolenga kunusuru maisha yake, Bush alikimbizwa haraka kutoka Florida alikokuwa kaenda kwa ziara hadi kwenye kambi kubwa ya kijeshi iliyopo ktk jimbo la Louisiana nchini humo, akiwa kwenye kambi hiyo ya kijeshi, Rais Bush alifichwa kwenye handaki.
"Mr President, America is under attack,you'll have to stay here until the situation calms down "
Kiongozi wa walinzi wa Rais Bush, alimweleza Rais.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, Rais Bush alielezwa kuwa, "Bwana Rais, Marekani imevamiwa, itakulazimu ukae hapa hadi hapo hali itakavyotulia ".
Rais Bush alikaa hapo kwa masaa kadhaa, kisha akaondolewa na kurudishwa Washington, kisha baada ya muda mfupi alitoa hotuba fupi kwa taifa akiwa na hasira ,namnukuu kwa ufupi.
"The great nation is attacked,now we want to show the world that we pass this test".
Kwa tafsiri isiyo rasmi Rais Bush alisema.
"Taifa kubwa limepigwa, sasa tunataka kuionyesha Dunia kwamba tunafaulu huu mtihani ".
Mwisho wa kunukuu.
Chadema imepigwa na imepigika hasa, chadema iko vitani, adui kalenga kusambaratisha chama hiki chenye nguvu kubwa kuliko vyote Tanzania kwa sasa.
Adui huwa hachagui staili ya kukupiga, anakupiga kwa staili zote anazojua yeye, lengo lake ni kupata ushindi.
Mapandikizi ya wanausalama ndani ya Chadema ni jambo la kawaida kabisa hasa kwa chama ambacho hakina ndoto ya kuachia madaraka hata Kama kitaangushwa kwenye sanduku la kura.
Vitani hata majenerali wanaoongoza vikosi huwa inatokea wakatekwa au kujisalimisha kwa adui, lakini hiyo huwa haitoi marks za ushindi kwa adui.
ANC ilikuwa na vita kubwa mara 100 ya Chadema, lakini ilishinda hii vita.
Chadema is attaked, now we want show the world that we pass this test.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mara baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Sept 11, Mwandishi Woodward anasimulia jinsi Bush alivyokuwa Kachanganyikiwa mara baada ya mashambulizi yale .
Hasa baada ya hatua za kiusalama zilizolenga kunusuru maisha yake, Bush alikimbizwa haraka kutoka Florida alikokuwa kaenda kwa ziara hadi kwenye kambi kubwa ya kijeshi iliyopo ktk jimbo la Louisiana nchini humo, akiwa kwenye kambi hiyo ya kijeshi, Rais Bush alifichwa kwenye handaki.
"Mr President, America is under attack,you'll have to stay here until the situation calms down "
Kiongozi wa walinzi wa Rais Bush, alimweleza Rais.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, Rais Bush alielezwa kuwa, "Bwana Rais, Marekani imevamiwa, itakulazimu ukae hapa hadi hapo hali itakavyotulia ".
Rais Bush alikaa hapo kwa masaa kadhaa, kisha akaondolewa na kurudishwa Washington, kisha baada ya muda mfupi alitoa hotuba fupi kwa taifa akiwa na hasira ,namnukuu kwa ufupi.
"The great nation is attacked,now we want to show the world that we pass this test".
Kwa tafsiri isiyo rasmi Rais Bush alisema.
"Taifa kubwa limepigwa, sasa tunataka kuionyesha Dunia kwamba tunafaulu huu mtihani ".
Mwisho wa kunukuu.
Chadema imepigwa na imepigika hasa, chadema iko vitani, adui kalenga kusambaratisha chama hiki chenye nguvu kubwa kuliko vyote Tanzania kwa sasa.
Adui huwa hachagui staili ya kukupiga, anakupiga kwa staili zote anazojua yeye, lengo lake ni kupata ushindi.
Mapandikizi ya wanausalama ndani ya Chadema ni jambo la kawaida kabisa hasa kwa chama ambacho hakina ndoto ya kuachia madaraka hata Kama kitaangushwa kwenye sanduku la kura.
Vitani hata majenerali wanaoongoza vikosi huwa inatokea wakatekwa au kujisalimisha kwa adui, lakini hiyo huwa haitoi marks za ushindi kwa adui.
ANC ilikuwa na vita kubwa mara 100 ya Chadema, lakini ilishinda hii vita.
Chadema is attaked, now we want show the world that we pass this test.
Sent using Jamii Forums mobile app