CHADEMA acheni ujinga wa Kujihami!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,042
33,527
Ninaposema CHADEMA, hapa namaanisha viongozi wenye dhamana ya kuzungumza kwa niaba ya wanachama wenzao, kwa maana nyingine wao ndiyo chama na wanaposema wao chama huwa kinakuwa kimesema. CHADEMA kila mara hujiweka kwenye kujihami badala ya kushambulia.

Kwa mfano mpaka sasa wapinzani wa CHADEMA wamefanikiwa kuwaaminsha watu kwamba CHADEMA ni chama kinachodhibitiwa na Wakristu na watu Kaskazini. Lakini wakati inashutumiwa hivyo, CCM inashutumiwa asilimia zaidi ya 60 Makatibu wa CCM walikuwa ni waislamu lakini CCM haikuitwa ni chama cha Waislamu!

Wakati huu ambapo CHADEMA inaitwa ya "kikanda" Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano ameteua watu wengi toka Kanda ya Ziwa na mikoa ya Jirani lakini CCM haiitwi ya Kikanda wala Magufuli hasemwi kuwa anateu watu wa "kwao" kama ambavyo inasemwa kwa Mbowe kuhusu CHADEMA na Uchaga.

Tatizo la CHADEMA ni kwamba wao huchukulia vitu vinavyoharibu chama kama ni vitu "vitu vidogo" kwa hivyo hawajishughulishi navyo. Leo mtu akiwa ni mchaga anataka kugombea nafasi ya uongozi wa chama huko mtwara anashindwa kugombea kwa kuwa itaonekana kwamba wachaga wanapandikiza watu wao kila sehemu ya nchi. Viongozi wanafanyaje kuondoa hizi propaganda kwamba bila kuwa mchaga au mtu wa kaskazini huwezi kuwa kiongozi ndani ya CHADEMA?

Wakati watu wa Kaskazini waliopo CCM wanaweza kuwa viongozi mahala popote ndani ya Tanzania, CHADEMA mtu ukiwa wa Kaskazini na ukiwa kiongozi nje ya mikoa ya kaskazini inajengwa picha na CCM kwamba CHADEMA ni ya watu wa Kaskazini na viongozi wa CHADEMA wanabaki wameduwaa hawana la kufanya! Ni lini CHADEMA itatoka na kuwaambia watu kwamba nchi hii mtu anaweza kuwa kiongozi wa chama cha siasa mahala popote bila ya kujali asili wala dini yake?

Ukiangalia suala la Ben Saanane, Mikutano ya hadhara, kufukuzwa Bungeni, CHADEMA siku zote huamini kwamba wananchi "wataelewa tu" kwamba CCM ni chama kibaya bila ya kufanya juhudi za kuonesha kwamba CCM ni chama kibaya na mabaya ya watanzania chanzo chake ni CCM!
 
Ninaposema CHADEMA, hapa namaanisha viongozi wenye dhamana ya kuzungumza kwa niaba ya wanachama wenzao, kwa maana nyingine wao ndiyo chama na wanaposema wao chama huwa kinakuwa kimesema. CHADEMA kila mara hujiweka kwenye kujihami badala ya kushambulia.

Kwa mfano mpaka sasa wapinzani wa CHADEMA wamefanikiwa kuwaaminsha watu kwamba CHADEMA ni chama kinachodhibitiwa na Wakristu na watu Kaskazini. Lakini wakati inashutumiwa hivyo, CCM inashutumiwa asilimia zaidi ya 60 Makatibu wa CCM walikuwa ni waislamu lakini CCM haikuitwa ni chama cha Waislamu!

Wakati huu ambapo CHADEMA inaitwa ya "kikanda" Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano ameteua watu wengi toka Kanda ya Ziwa na mikoa ya Jirani lakini CCM haiitwi ya Kikanda wala Magufuli hasemwi kuwa anateu watu wa "kwao" kama ambavyo inasemwa kwa Mbowe kuhusu CHADEMA na Uchaga.

Tatizo la CHADEMA ni kwamba wao huchukulia vitu vinavyoharibu chama kama ni vitu "vitu vidogo" kwa hivyo hawajishughulishi navyo. Leo mtu akiwa ni mchaga anataka kugombea nafasi ya uongozi wa chama huko mtwara anashindwa kugombea kwa kuwa itaonekana kwamba wachaga wanapandikiza watu wao kila sehemu ya nchi. Viongozi wanafanyaje kuondoa hizi propaganda kwamba bila kuwa mchaga au mtu wa kaskazini huwezi kuwa kiongozi ndani ya CHADEMA?

Wakati watu wa Kaskazini waliopo CCM wanaweza kuwa viongozi mahala popote ndani ya Tanzania, CHADEMA mtu ukiwa wa Kaskazini na ukiwa kiongozi nje ya mikoa ya kaskazini inajengwa picha na CCM kwamba CHADEMA ni ya watu wa Kaskazini na viongozi wa CHADEMA wanabaki wameduwaa hawana la kufanya! Ni lini CHADEMA itatoka na kuwaambia watu kwamba nchi hii mtu anaweza kuwa kiongozi wa chama cha siasa mahala popote bila ya kujali asili wala dini yake?

Ukiangalia suala la Ben Saanane, Mikutano ya hadhara, kufukuzwa Bungeni, CHADEMA siku zote huamini kwamba wananchi "wataelewa tu" kwamba CCM ni chama kibaya bila ya kufanya juhudi za kuonesha kwamba CCM ni chama kibaya na mabaya ya watanzania chanzo chake ni CCM!
Chadema kuitwa chama cha wachaga ni sawa kabisa.Kiliasisiwa na wachaga na ndio wanaokimiliki hata wagombea wao Tanzania nzima asilimia kubwa ni chagas.Hata wanaojaribu kuibomoa cuf nyuma ya Profesa ni chagas ili chadema itamalaki na hata wanaozishikilia rasilimali za CCM mikoani kwa mikataba ya kijanjajanja yenye lengo la kuua chama ukiwaangalia kwa umakini ndio haohao ili chama cha home kikamate fursa.So ukabila na ukanda ni ngumu sana kuvitenganisha na chadema.Hilo la udini siwezi kulisemea maana hata ccm kuna wabunge na DC ambao ni wachungaji.
 
Unashindwa kuirudisha CDm kwenye Ajenda ya ufisadi unakalia ngonjera du!!

Ukanda na udini ni pete na kidole kwa chadema.
Unapo isema ccm vibaya ujue unamkera sana Lowassa
 
Hayo masuala madogo sana,mi nachukia sana fisadi na mafisadi..!!na wote wanaowakumbatia!Agenda yetu imeenda wapi?
Agenda bado ipo bali wao wenyewe mpaka sasa wameshindwa kuwaeleza wananchi jambo ambalo lipo wazi kuhusu Lowassa na ufisadi wa Richmond. Hawasemi ni "Ushahidi" gani waliokuwa nao hadi wakamwita Lowassa "fisadi" na ni ushahidi gani waliioupata baadaye uliohalalisha wao kukubali kumpitisha Lowassa kuwa mgombea Urais kwenye uchaguzi wa Mwaka 2015. Wako kimya tu.
 
Ninaposema CHADEMA, hapa namaanisha viongozi wenye dhamana ya kuzungumza kwa niaba ya wanachama wenzao, kwa maana nyingine wao ndiyo chama na wanaposema wao chama huwa kinakuwa kimesema. CHADEMA kila mara hujiweka kwenye kujihami badala ya kushambulia.

Kwa mfano mpaka sasa wapinzani wa CHADEMA wamefanikiwa kuwaaminsha watu kwamba CHADEMA ni chama kinachodhibitiwa na Wakristu na watu Kaskazini. Lakini wakati inashutumiwa hivyo, CCM inashutumiwa asilimia zaidi ya 60 Makatibu wa CCM walikuwa ni waislamu lakini CCM haikuitwa ni chama cha Waislamu!

Wakati huu ambapo CHADEMA inaitwa ya "kikanda" Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano ameteua watu wengi toka Kanda ya Ziwa na mikoa ya Jirani lakini CCM haiitwi ya Kikanda wala Magufuli hasemwi kuwa anateu watu wa "kwao" kama ambavyo inasemwa kwa Mbowe kuhusu CHADEMA na Uchaga.

Tatizo la CHADEMA ni kwamba wao huchukulia vitu vinavyoharibu chama kama ni vitu "vitu vidogo" kwa hivyo hawajishughulishi navyo. Leo mtu akiwa ni mchaga anataka kugombea nafasi ya uongozi wa chama huko mtwara anashindwa kugombea kwa kuwa itaonekana kwamba wachaga wanapandikiza watu wao kila sehemu ya nchi. Viongozi wanafanyaje kuondoa hizi propaganda kwamba bila kuwa mchaga au mtu wa kaskazini huwezi kuwa kiongozi ndani ya CHADEMA?

Wakati watu wa Kaskazini waliopo CCM wanaweza kuwa viongozi mahala popote ndani ya Tanzania, CHADEMA mtu ukiwa wa Kaskazini na ukiwa kiongozi nje ya mikoa ya kaskazini inajengwa picha na CCM kwamba CHADEMA ni ya watu wa Kaskazini na viongozi wa CHADEMA wanabaki wameduwaa hawana la kufanya! Ni lini CHADEMA itatoka na kuwaambia watu kwamba nchi hii mtu anaweza kuwa kiongozi wa chama cha siasa mahala popote bila ya kujali asili wala dini yake?

Ukiangalia suala la Ben Saanane, Mikutano ya hadhara, kufukuzwa Bungeni, CHADEMA siku zote huamini kwamba wananchi "wataelewa tu" kwamba CCM ni chama kibaya bila ya kufanya juhudi za kuonesha kwamba CCM ni chama kibaya na mabaya ya watanzania chanzo chake ni CCM!
Wanasiasa wote ni ndugu,

Mkuu naomba unitajie majina ya wabunge wa viti maalumu kutoka CDM.
 
Agenda bado ipo bali wao wenyewe mpaka sasa wameshindwa kuwaeleza wananchi jambo ambalo lipo wazi kuhusu Lowassa na ufisadi wa Richmond. Hawasemi ni "Ushahidi" gani waliokuwa nao hadi wakamwita Lowassa "fisadi" na ni ushahidi gani waliioupata baadaye uliohalalisha wao kukubali kumpitisha Lowassa kuwa mgombea Urais kwenye uchaguzi wa Mwaka 2015. Wako kimya tu.
Pesa pesa ndugu
 
Agenda bado ipo bali wao wenyewe mpaka sasa wameshindwa kuwaeleza wananchi jambo ambalo lipo wazi kuhusu Lowassa na ufisadi wa Richmond. Hawasemi ni "Ushahidi" gani waliokuwa nao hadi wakamwita Lowassa "fisadi" na ni ushahidi gani waliioupata baadaye uliohalalisha wao kukubali kumpitisha Lowassa kuwa mgombea Urais kwenye uchaguzi wa Mwaka 2015. Wako kimya tu.
'Wao' sawa .Sisi je tuliozunguka mikoa yote na list of shame tukilaani ufisadi na mifano tukatoa Mh akiwamo bado tu tunabeba iyo ajenda?tukisema tunayo ajenda iyo watu watatuamini?
 
Back
Top Bottom