Central Police - Mbeya inawaka moto

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,385
jengo liliungua floo ya kwanza tu na zimamoto wamefanikiwa kuuzima moto ..hakuna majeruhi

Source: JF
 
Ntashangaa kama fire watashindwa kuuzima huo moto kutokana na ukaribu.

Chanzo ni nini tena shoti ya umeme au kuna afande aliacha jiko linawaka?
 
What is going ön? Umecema inawaka moto then mwenye updates, haya yamekuwaje!
 
News alert halafu mwenye habari atujuze, hapo naona haijatulia kidogo lakini hakuna shida hii tutaichukilia kama tetesi hivyo inahitaji prove kupitia vyanzo mbali mbali. Ngoja nizame chimbo nikirudi niko na full story.
 
Hii mioto ya Mbeya!. Sii bure!.
Lilianza soko, likajengwa upya likaungua tena!. Lijafuatiwa na soko jingine na jingine tena!. Sasa ndio kituo cha polisi!. Basi ofisi ya RC wajiandae!. Itambidi mbunge wa Mbeya Mhe. Sugu, akifute kabisa kile kibwagizo chake (Sugu Moto Chini!) cha wakati wa kampeni kilichompa ushindi kwa sababu sasa moto chini unafanya kweli!.

Kituo cha polisi kilichostahili kuungua ni kile cha Arusha kufidia damu za raia wakaida wasio na hatia waliopoteza maisha kwa kumiminiwa risasi na polisi wakiwa Stendi Kuu na wengine Unga Limited lakini wakasingiziwa eti wanefyatuliwa risasi kwa kutaka kuvamia kituo cha Polisi!.

Poleni wana Mbeya!.
 
Ni ile Police Welfare Canteen almaarufu kama "CHIZIKA"... Maarufu kwa Bia za Buku buku ndio imeshika moto... Natumai kutokana na Police wengi kupata Mishahara yao Ijumaa patakuwa pamejaa sana... poleni WAPENDA MTEREMKO aka KITONGA wa Mbeya... Bia za Buku mtapata wapi...
 
..Jamani hebu walioko Mbeya walete kitu cha kueleweka manake Mbeya imekuwa MOTO..MOTO..MOTO..MOTO..Kulikoni??
 
Ni ile Police Welfare Canteen almaarufu kama "CHIZIKA"... Maarufu kwa Bia za Buku buku ndio imeshika moto... Natumai kutokana na Police wengi kupata Mishahara yao Ijumaa patakuwa pamejaa sana... poleni WAPENDA MTEREMKO aka KITONGA wa Mbeya... Bia za Buku mtapata wapi...
tupe habari iliyosimama maana naona kimyaji kimekolea halafu inaonekana unachukia nao........hahahahaah
 
Nilikua nasikiliza Clouds, wakatangaza kua kuna moto unawaka pale Central Polisi jijini Mbeya, wakasema wanatuma mwakilishi wao ili alete taarifa zaidi, hee cjakaa sawa Mzee wa Megawatt akachukua chake.
 
Nilikua nasikiliza Clouds, wakatangaza kua kuna moto unawaka pale Central Polisi jijini Mbeya, wakasema wanatuma mwakilishi wao ili alete taarifa zaidi, hee cjakaa sawa Mzee wa Megawatt akachukua chake.
hata mimi kuna jamaa hapa kasema amesikia kwenye radio. dah wakuu kweli zama hizi za mtandiowazi hakuna hata mwana JF mmoja Mbeya akatupatia kitu kamili?
 
Habari nilizozinasa hivi punde zinasema kituo cha polisi kikuu cha Mbeya kinawaka moto.

UPDATES
Nimeweza kuwasiliana na kamanda wangu Mh. Mbilinyi (Mb) na amethibitisha kutokea ajali ya moto kwenye makazi ya polisi yaliyopo katika kituo kikuu cha polisi.
 
Mbona matatizo ya moto Mbeya hayaishi? Tujuze chanzo cha huo moto mkuu
 
Back
Top Bottom