Dumelambegu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,052
- 257
Ndiyo hivyo jamani, kama shamba lisilo na mwenyewe vile! Wajanja wanakuja na mbegu chache lakini wanazalisha na kuvuna kwa kutumia watumishi walewale na shamba lilelile kisha wanakula, wanashiba halafu wanaondoka na mbegu nyingi mara dufu ya kiasi walichokuja nacho. Kabla ya kuondoka wanawapigia miluzi wajanja wenzao wengine kuashiria kwamba wao wamevimbiwa. Hao nao wakija wanatumia shamba lilelile na watumishi walewale kwa staili ileile mpaka wanavimbiwa na kuondoka. Kila anapoingia mjanja mpya lazima amwalike kiongozi mkuu wa wamiliki wa shamba kwenye hafla ya kubadilishana uendeshaji wa shamba na wamiliki wanashangilia na kugonganisha bilauli zilizojaa vinywaji vya bei mbaya!