Wana JF, Tangu mashindano ya Celtel Universities Challenge yaanze nilikua nayafuatilia kwa kina. Mashindano hayo huusisha vyuo vingi vikiwemo vya Africa Mashariki. Cha kusikitisha sana baadhi ya vyuo vyetu vikuu vya Kitanzania vimekua vikifanya vibaya sana ukilinganisha Uganda na Kenya. Mfano mzuri ni Jana Jumapili tarehe 9/2/2008, Chuo Kikuu DSM kikipambana na Egaton University from Kenya. UDSM walibwagwa kwa kiajabu na Egaton. UDSM walionekana kama watoto wa sekondari, walikua wanaduaa kujibu maswali, wakati mwingine walikua wa wanashituka ikifika wakati wao, kujiamini kulikua sifuri kabisa. Mimi nashindwa kuelewa tatizo ni nini hasa, je ni mfumo wa elimu mbovu au wliochagulia kuiwakilisha UDSM kulikua na harufu ya RichMond? Wana JF nisaidie hapo. Hata St Agustin kilifanya vibaya. Matokeo ya Jana, UDSM=340 point wakati Egaton ni 940 points, ni aibu kubwa kwa UDSM. Kulikoni?