celebritydidie drogba amewapa pete za diamond wachezaj wake wa chelsea zenye thaman ya pound 800,000

Money Stunna

JF-Expert Member
Aug 9, 2011
13,054
6,281
kweli ukishangaa ya beyonce,utayaona ya drogba,drogba amewazawadia wachezaj wa chelasea pete zenye thaman ya pound 800,000 wachezaj wa chelsea.

Drogba1_1633990a.jpg


Drogba_1633989a.jpg


drogba-rings-2.jpg


Drogba+Ring


wapo watu wamesema hiyo pesa angesaidia nchi yake kutokana na umasikin mkubwa uliopo
 
Duh! Pesa si mchezo. Ukipata tumia ukikosa jutia. Hapo unaweza kuta hata baadhi ya nduguze huko kwao mlo mmoja kwa siku ni shida.
 
Maskini akipata ... M.a.t.ako hulia mbwata.... maana yake atavimbiwa na ushuzi juu juu.... habari mbaya hiii kwa Ivory Coast ....
 
Miafrika ndivyo tulivo.let the guy live his life.tutakua omba omba hadi lini? Tafakari,chukua hatua.
 
Duh! Pesa si mchezo. Ukipata tumia ukikosa jutia. Hapo unaweza kuta hata baadhi ya nduguze huko kwao mlo mmoja kwa siku ni shida.

Sawa na ni kweli ila Chelsea ndiyo iliyompatia jina na ukwasi zaidi ya aliokuwa nao..
Anaipenda Chelsea,na Chelsea kama taasisi pia ilimpenda,achilia mbali mashabiki. Nadhani anawatia sumu ya kuipenda na kuichezea kwa moyo klabu yao.
 
Sawa na ni kweli ila Chelsea ndiyo iliyompatia jina na ukwasi zaidi ya aliokuwa nao..
Anaipenda Chelsea,na Chelsea kama taasisi pia ilimpenda,achilia mbali mashabiki. Nadhani anawatia sumu ya kuipenda na kuichezea kwa moyo klabu yao.

lakin mkuu hizo pesa ni ela nyingi sana ata kwa ulaya,zingetumika kusaidia watu ingekuwa vizuri zaidi,lakin ni zake ana haki ya kuamua namna ya kutumia
 
Acheni attitude, hata Yesu alipowekewa marashi wapambe walisema hela ingewalisha maskini. Na Yesu akawajibu maskini mnao siku zote. Wenyewe mnaendesha ma-benz na maprado mjini hapa na baba zenu wanakaa nyumba za tope hazina umeme. Na binamu zenu hawajaenda shule kisa ada. Muacheni atumie hela zake apendavyo.
Hivi diaspora wabongo wakiamua kuchangana wakaleta hata millioni 100 zijengwe shule ya walemavu unajua wizi gani utakaotokea? Not even 20% of the money will be put into correct use. Muacheni ajitengenezee marafiki wa badae, siku akifulia walau atazengea ofa za bia banaa, kwani ni nini? ??
 
Mnaacha kuwajibisha serikali yenu mnataka kuwajibisha mtu binafsi alietoa jasho kusaka hela yake. Waafrika bwana. Wyclef Jean alienda kugombea urais kwao na wakamnyima. Drogba akienda kugombea urais kwao watamuona mhuni aliekaa ulaya. Afu hela yake akawape mafisadi wa kwao wajengee nyumba maskini. Kha!
 
Mnaacha kuwajibisha serikali yenu mnataka kuwajibisha mtu binafsi alietoa jasho kusaka hela yake. Waafrika bwana. Wyclef Jean alienda kugombea urais kwao na wakamnyima. Drogba akienda kugombea urais kwao watamuona mhuni aliekaa ulaya. Afu hela yake akawape mafisadi wa kwao wajengee nyumba maskini. Kha!

umeongea ukweli kabisa,watu atusaidiani kutafuta pesa,lakin ukipata wanataka kukusaidia namna ya kuzitumia,hizo ni pesa kidogo sana kwa didie,kama anaweza kulipwa pound 250,000 kwa week,acheze asi cheze bado mikataba kibao ya matangazo,kama samsung,pepsi na mengineyo,hiyo pesa kwake ni kidogo sana,sisi wenyewe kabla ya kupiga domo tujiulize namna tunavyosaidia wenzetu kwanza
 
Acheni attitude, hata Yesu alipowekewa marashi wapambe walisema hela ingewalisha maskini. Na Yesu akawajibu maskini mnao siku zote. Wenyewe mnaendesha ma-benz na maprado mjini hapa na baba zenu wanakaa nyumba za tope hazina umeme. Na binamu zenu hawajaenda shule kisa ada. Muacheni atumie hela zake apendavyo.
Hivi diaspora wabongo wakiamua kuchangana wakaleta hata millioni 100 zijengwe shule ya walemavu unajua wizi gani utakaotokea? Not even 20% of the money will be put into correct use. Muacheni ajitengenezee marafiki wa badae, siku akifulia walau atazengea ofa za bia banaa, kwani ni nini? ??
Bonge la point!
 
Acheni kumpangia mtu matumizi ya pesa yake. Anafanya kazi kwaajili ya maisha yake siyo kusaidia maskini. Wangapi humu mmefunga Harusi za mamilioni wakati nduguzenu wengi tu wanakosa ada za shule na fedha za matibabu au hata makazi bora. Pendeni kufanya kazi acheni kufikiria kwamba kunawatu wapo kufanya kazi ili kusaidia watu.
 
Very smart points


Acheni attitude, hata Yesu alipowekewa marashi wapambe walisema hela ingewalisha maskini. Na Yesu akawajibu maskini mnao siku zote. Wenyewe mnaendesha ma-benz na maprado mjini hapa na baba zenu wanakaa nyumba za tope hazina umeme. Na binamu zenu hawajaenda shule kisa ada. Muacheni atumie hela zake apendavyo.
Hivi diaspora wabongo wakiamua kuchangana wakaleta hata millioni 100 zijengwe shule ya walemavu unajua wizi gani utakaotokea? Not even 20% of the money will be put into correct use. Muacheni ajitengenezee marafiki wa badae, siku akifulia walau atazengea ofa za bia banaa, kwani ni nini? ??
 
Lakini ana foundation inayofanya kazi nzuri kuboresha maisha ya watoto huko ivory coast. Pia nadhani alijenga hospital. After all ni pesa yake anawajibu kuitumia anavyotaka yeye sio tunavyotaka sisi.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
tuna matatizo aisee yaani kazitafuta kwa juhudi zake na wakati anaanza kucheza nahisi kuna baadhi ya mijitu ilikuwa inamkatisha tamaa ila sasa hivi kafika hapo watu mnataka kumpangia hela zake jinsi ya kuzitumia?? yale yale ya hashim thebeet wakati anaanza watu anajifanya sasa hivi wanasema anatumia pesa vibaya, tuacheni haya mawivu wajameni tufanye kazi na sisi tufikie hapo walipo ingawa ni ndoto za alinacha.
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom