Cecil Mwambe: Nitajenga ofisi mpya ya CHADEMA. CHADEMA kimepokea zaidi ya shilingi bilioni 13

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Mgombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa, Cecil David Mwambe ameahidi kujenga jengo jipya la Ofisi ya Makao Makuu ya CHADEMA pindi atakapochaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na kuachana na jingo la sasa ambalo halina hadhi ya CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani.

Hayo ameyasema baada ya kufanya mahojiano na mwandishi wa habari na mtandao wa DarMpya nchini.

Mgombea huyo amedai mpaka sasa CHADEMA kimepokea kutoka serikalini kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 13 kama ruzuku lakini pesa hizo hazikupangiwa mipango mizuri ya kukiendeleza chama.

Mgombea huyo amedai kama atachaguliwa atahakikisha Makatibu wa Majimbo, Mikoa na Wilaya wanapata posho zitakazowawezesha kutimiza majukumu yao tofauti na sasa ambapo hawalipwi.

Amemaliza kwa kusema, atahakikisha mapato na matumizi ya pesa za chama yanakuwa wazi tofauti na sasa ambapo ni siri ya viongozi wachache.

Screenshot (10).png


Screenshot (11).png


Screenshot (12).png



 
@ChademaTz mpaka sasa wamepewa BILIONI 13 kama Ruzuku na michango mwingine ,lakini wameshindwa kujenga ofisi yenye hadhi ya Chama kinachojiandaa kushika Dola.

jengo hili (chini)limejengwa kwa gharama ya BILIONI 1 yaani kama wangetumia ruzuku vizuri wangeyajenga kama haya 13 lakini kwa sasa hata chumba kimoja hawana, na wanachama wala hawana muda wa kuhoji zaidi kuitukana serikali .
IMG_20191216_195756.jpeg
 
..kwanini chama kiwe na ofisi za kifahari za mabilioni ya shilingi?

..ruzuku wanayopewa waitumie ktk program za kuwafikia Watanzania wengi zaidi.

..kwa taarifa tu, TANU ilileta uhuru wa Tanganyika bila kuwa na majengo ya kifahari yanayogharimu mabilioni ya fedha.
 
Bado zile milioni moja moja kwa kila mbunge kwa kila mwezi! Sijui nazo zinatumika kwa matumizi gani! Naangalia taarifa ya habari muda huu naona majina mawili yamepitishwa kwa ajili ya mpambano kwenye nafasi ya Mwenyekiti!

Kwa haraka haraka unaona kabisa Kamanda Mkuu lazima tu atatetea nafasi yake kwa mhula wa nne mfululizo, huku Cecil Mwambe akienda kupata kura kiduchu na huku akihukumiwa kama pandikizi la ccm! ingawa ukimsikiliza kwa umakini utagundua hoja zake zina mashiko kwa mustakabali mpana wa chama.
 
Wakijenga ofisi unazodai niza ''kifahari'' utakuja tena hapa Jamiiforums na kuanza kuwapongeza!

Kwa hiyo CHADEMA unawalinganisha na TANU? Kwani TANU walikuwa wanapokea mabilioni ya pesa kutoka serikalini kwa njia ya ruzuku?

Hii nchi ina vituko!

..hii ni imani tu mmejijengea kuwa chama lazima kimiliki jengo, tena la kifahari.

..kwani wakiwa na makao makuu ktk jengo walilopanga kuna tatizo gani?

..Je, kwa sasa hivi kipi ni kipaumbele kwa cdm? Cdm watumie ruzuku kujenga makao makuu ya kifahari, au watumie kusaka wanachama nchi nzima?

..Ofisi walizonazo sasa hivi zinakwamisha kazi za chama kufanyika?
 
Cecil Mwambe hajui kuwa kuweka wazi mapato ya CHADEMA ni kosa kubwa sana kwa wenye chama? Kuweka wazi mapato ya CHADEMA ni kosa linafukuzisha uanachama!!

Huyu Mwambe hana historia ya kile kilimkuta Zitto Kabwe mwaka 2014 baada ya kutaka mapato ya CHADEMA yawe wazi?

Huyu Mwambe baada ya Uchaguzi ndani ya CHADEMA ataundiwa ''zengwe' na kufukuzwa uanachama kwa sababu fikra zake ni sumu/kansa kwa wenye chama ndani ya CHADEMA!

Mradi wa kisiasa anataka kuuweka wazi? Hawezi kusalimika baada ya uchaguzi ndani ya CHADEMA!
 
Huyu kaandikiwa dondoo na Lumumba team. Naona mikakati ya tume ya uchaguzi na wasio julikana kuweka mtu wao pale. Vila najua Chadema wanajitambua

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo aliyoongea ni uongo au yana ukweli?

Tuanzie hapa ili tujue ana hoja ? Je ni propaganda za Ccm ,tusikimbilie kumu attack mtu bila kujibu hoja yake
 
Back
Top Bottom