CDM kuing'oa CCM kama itawaelimisha Watz ukweli suala la kupanda bei ya umeme

Erwin Rommel

JF-Expert Member
Dec 1, 2013
429
115
Suala la bei ya umeme laweza kuiondoa CCM madarakani mwaka 2015 iwapo CDM itauelezea umma kuhusu uhusiano mkubwa kati ya ufisadi ndani ya serikali ya CCM na bei ya umeme.


Na ni rahisi kabisa. Kwanza kabisa Ewura wanaendeshwa na serikali, na haipo kwa masilahi ya wananchi kwani Mkurugenzi wake ni mteule wa Rais.


Serikali inataka kuwaficha Watz kwa kujaribu kutuaminisha kwamba hasara ya mabilioni ndani ya Tanesco kwa asilimia kubwa ni hasara halali na haitokani na ufisadi, na uzembe/mapungufu ya kiutendaji ndani ya Tanesco.


Wananchi wajiulize, vipi wakati wa Mwalimu Nyerere, kiongozi huyo aliweza kujenga mabwawa matano ya uzalishaji umeme – yote mali ya Tanesco, na kuifanya Tanesco kutolazimishwa kununua umeme kutoka popote?


Lakini katika awamu zilizofuata mitambo yote iliyojengwa ya kuzalisha umeme eg IPTL na ile ya dharura (eg Songas, Richmond/Dowans/Symbion, Aggreko rtc) yote ya watu binafsi na hivyo kulazimisha Tanesco kununua umeme kutoka kwao kwa mikataba kandamizi.


Na hii mitambo lilitokana na wazo (brainchild) ya JK kuanzia awamu ya Mwinnyi wakati yeye (JK) akiiongoza Wizara ya Nishati. Hivyi ikaletwa IPTL ambapo Tanesco ililazimishwa kuingia mkataba nao, mkataba ambao hadi leo unaiumiza Tanesco na kesi kuozea mahakamani.


Mkapa awamu yake hakutaka ufisadi wa aina hii – hakuleta/kujenga mitambo yoyote ya kuzalisha umeme. Lakini alipoingia JK kule Ikulu, basi yeye na EL wake wakafufua mipango wa ki-IPTL – kwa kuanzia Richmond ambapo ufisadi ndani yake ulikuwa dhahiri kabisa pamoja na jitihada nyingi za kufunika.


Ndiyo ikafuata ile mitambo mingine ambapo yote yanailazimisha Tanesco kununua umeme kutoka kwao – mpango ambao umeiua kabisa Tanesco na kuwa katika hali iliyo nayo na sasa serikali kulazimisha mzigo wa hasara ubebeshwe wateja.
Zipo hasara zingine za kawaida kama vile upoteaji umeme wakati wa kuusafirisha kupitia miundo mbinu chakavu, au wizi wa umeme unaofanywa na wateja, ingawa hili la wizi pia unachangiwa na ufisadi wa baadhi ya maafisa wa shirika.


Lakini kuna jingine ambalo linatia hasara sana Tanesco – kuharibika mara kwa mara kwa network yao ya kuuza umeme kupitia mawakala wao eg Maxcom, Selcom etc. hazipiti siku mbili lazima network itakuwa down na kuwafanya wateja walioishiwa umeme majumbani mwao kukaa bila umeme kwa masaa kadha. Fikiria – ni wateja wangapi nchini kote, na kilowatthours milioni ngapi kila siku hazinunuliwi kutokana na sababu hii ya network inapokuwa down.


Kwa kuhitimisha tu naweza kusema hasara iliyo "halali" ya Tanesco ni asilimia 25 tu na iliyobaki – asilimia 75 – ni hasara "isiyo halali" -- yaani inayotokana na ufisadi wa watendaji wa serikali ya CCM wanaosimamia sekta ya nishati.


Ingawa sijaandika kwa mpangilio ulio bora na kutokuwa na ufasaha nawaomba Chadema wawaeleze wananchi ukweli huu kwa nini Watz wanabebeshwa mzigo wa Tanesco.
 
Mkuu hapa unaongelea chadema ipi ya zito au chadema ya slaa.
 
Kwa nini sikumzote chadema mipango yenu imekaa kimapinduzi wala siyo kimaendeleo? Kila kina choletwa na chadema ni mapambano ya kuvuruga na kuviziana kwa kiasi kikubwa ccm waharibu wao wapate hoja ila siyo wao wasaidie kuleta maendeleo.
 
Kwa nini sikumzote chadema mipango yenu imekaa kimapinduzi wala siyo kimaendeleo? Kila kina choletwa na chadema ni mapambano ya kuvuruga na kuviziana kwa kiasi kikubwa ccm waharibu wao wapate hoja ila siyo wao wasaidie kuleta maendeleo.

Kwa maneno mengine unakubaliana kabisa kwamba hasara ya Tanesco ni halali -- haihusikani kabisa na ufisadi wa serikali ya CCM, na kwamba ni halali wa wateja wa Tanesco kubebeshwa hasara hiyo?
 
Suala la bei ya umeme laweza kuiondoa CCM madarakani mwaka 2015 iwapo CDM itauelezea umma kuhusu uhusiano mkubwa kati ya ufisadi ndani ya serikali ya CCM na bei ya umeme.


Na ni rahisi kabisa. Kwanza kabisa Ewura wanaendeshwa na serikali, na haipo kwa masilahi ya wananchi kwani Mkurugenzi wake ni mteule wa Rais.


Serikali inataka kuwaficha Watz kwa kujaribu kutuaminisha kwamba hasara ya mabilioni ndani ya Tanesco kwa asilimia kubwa ni hasara halali na haitokani na ufisadi, na uzembe/mapungufu ya kiutendaji ndani ya Tanesco.


Wananchi wajiulize, vipi wakati wa Mwalimu Nyerere, kiongozi huyo aliweza kujenga mabwawa matano ya uzalishaji umeme – yote mali ya Tanesco, na kuifanya Tanesco kutolazimishwa kununua umeme kutoka popote?


Lakini katika awamu zilizofuata mitambo yote iliyojengwa ya kuzalisha umeme eg IPTL na ile ya dharura (eg Songas, Richmond/Dowans/Symbion, Aggreko rtc) yote ya watu binafsi na hivyo kulazimisha Tanesco kununua umeme kutoka kwao kwa mikataba kandamizi.


Na hii mitambo lilitokana na wazo (brainchild) ya JK kuanzia awamu ya Mwinnyi wakati yeye (JK) akiiongoza Wizara ya Nishati. Hivyi ikaletwa IPTL ambapo Tanesco ililazimishwa kuingia mkataba nao, mkataba ambao hadi leo unaiumiza Tanesco na kesi kuozea mahakamani.


Mkapa awamu yake hakutaka ufisadi wa aina hii – hakuleta/kujenga mitambo yoyote ya kuzalisha umeme. Lakini alipoingia JK kule Ikulu, basi yeye na EL wake wakafufua mipango wa ki-IPTL – kwa kuanzia Richmond ambapo ufisadi ndani yake ulikuwa dhahiri kabisa pamoja na jitihada nyingi za kufunika.


Ndiyo ikafuata ile mitambo mingine ambapo yote yanailazimisha Tanesco kununua umeme kutoka kwao – mpango ambao umeiua kabisa Tanesco na kuwa katika hali iliyo nayo na sasa serikali kulazimisha mzigo wa hasara ubebeshwe wateja.
Zipo hasara zingine za kawaida kama vile upoteaji umeme wakati wa kuusafirisha kupitia miundo mbinu chakavu, au wizi wa umeme unaofanywa na wateja, ingawa hili la wizi pia unachangiwa na ufisadi wa baadhi ya maafisa wa shirika.


Lakini kuna jingine ambalo linatia hasara sana Tanesco – kuharibika mara kwa mara kwa network yao ya kuuza umeme kupitia mawakala wao eg Maxcom, Selcom etc. hazipiti siku mbili lazima network itakuwa down na kuwafanya wateja walioishiwa umeme majumbani mwao kukaa bila umeme kwa masaa kadha. Fikiria – ni wateja wangapi nchini kote, na kilowatthours milioni ngapi kila siku hazinunuliwi kutokana na sababu hii ya network inapokuwa down.


Kwa kuhitimisha tu naweza kusema hasara iliyo “halali” ya Tanesco ni asilimia 25 tu na iliyobaki – asilimia 75 – ni hasara “isiyo halali” -- yaani inayotokana na ufisadi wa watendaji wa serikali ya CCM wanaosimamia sekta ya nishati.


Ingawa sijaandika kwa mpangilio ulio bora na kutokuwa na ufasaha nawaomba Chadema wawaeleze wananchi ukweli huu kwa nini Watz wanabebeshwa mzigo wa Tanesco.
haiitaji kueleweshwa kila mtu anajua kwamba, serikali iliyokubali bei ya umeme ni serikali ya ccm
 
Maandamano ya kupinga kupanda kwa bei a umeme ni haki ya kila mwananchi bila ya kujali itikadi yake, dini yake wala kabila lake. Nikweli kuwa CDM inatakiwa iongoze maandamano haya lakini kwa kuwashirikisha viongozi wa vyama vya wafanyakazi na taasisi zisizo za kiserikali... Gharama za maisha tayari ziko juu sana, wananchi, wafanyakazi, wafanyabiashara wanazidi kukamuliwa kodi na malipo ghali ili makampuni ya Symbion, IPTL, Agreco na SONGAS zaidi ya Million 700 kila siku... Hii haikubaliki asilani... Tunahitaji hadi watu wa boda boda na daladala kugoma ....ushirikishwaji na ushiriki wa kila mmoja wetu ni silaha pekee ya kuonyesha hasira zetu kwa watawala... Tunajua huu ni mpango mkakati wa kuidhoofisha TANESCO ili baadae SYMBION waichukue ili tuendelee kuendeshwa kwa msaada wa watu wa Marekani...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom