CD za ngono ni dhambi kwenye ndoa?

Ndumbayeye

JF-Expert Member
Jan 31, 2009
7,333
3,896
Jamani nipo kwenye ndoa zaidi ya miaka 10, nilikuwa na package ya cd mbali za ngono na tulikuwa tunafurahia na mywife. Jana nimezikuta zimesagwasagwa...eti zinanichochea niwe na wanawake wengi, je wakuu sijapokonywa haki yangu?
 
Mkuu heshima mbele kwanza,hakuna mchezo usiokuwa na mazoezi,Mazoezi maana yake ni kuona na kujifunza halafu ku practise.Ulimwengu wa sasa mambo yote tunajifunza kwa mtandao/mitandao kinyume na enzi za Adam na Hawa walifundishwa na Mungu na wajukuu wao wakafunzwa na wao.Sasa kizazi cha dot.com kinajifunza huko huko kwenye dot.com.

Binafsi sioni ubaya wala siiiamini kama ni dhambi kuangalia mikanda hiyo na mwandani wako, ambaye ni halali kufanya naye mchezo huo.Kinyume cha hapo nadhani itakuwa ni dhambi.Lakini kama mwenzi wako hapendi basi huna budi kukubaliana naye atakavyo.Mimi kusema kweli mikanda hiyo hainibariki kabisa kwani nakiangalia inanitia hasira zaidi ya kujua hali ya ufuska ilivyo duniani.Ni mtizamo wangu tu!!
 
cd nyingi za ngono hazifundishi kitu...kwanza nyingi zimejaa mapenzi ya tigo.....tusiige wazungu kwa kila kitu...
...wewe dumbayeye mwanzoni mlipooana miaka 10 iliyopita mlikuwa mnaangalia cd za ngono?
 
Kwakweli CD za Ngono ni Mbaya sana tena zinachochea ngono ya mara kwa mara, maana ya tendo la ndoa ni kwa ajili ajili ya reproduction na tunafanya makosa tukizani ni mchezo wa kujiburudisha! Ni sawasawa na kujisaidia tu. Huwezi kusema unafanya mazoezi ya kujisaidia! Unaweza!!!

Ni Mawazo tu.
 
ulikuwa unaangalia ili iweje?Kuamsha hisia?kuigiza unayoyaona?au zilikuwa zinakusaidiaje kwa kipindi chote ulipokuwa waziangalia?Binafsi sizani km ni Heshima na inajenga chochote ktk ndoa,sanasana utamuomba mkeo akufanyie km wanavyofanya hao porn stars then ikawa balaa na kumkosea heshima mwenzio.Tujifunze yaliyo mema jamani,mwaweza kufurahia tendo kwa ubunifu wenu na mapatano yenu,si mpaka muangalie zilizoectiwa na porn stars!!
 
Cd za ngono ni mbaya sana kwa wenye ndoa, maana mwanaume kuna vitendo vingine ataona halafu mkewe hawezi kuvifanya ataamua awatafute wanawake wa nje ili afanye kwa vitendo. Hatukatai kujifunza kwa ajili ya kuboresha ndoa lakini nyingi zimejaa vitendo vya aibu na kinyume cha maadili.
 
Kuna mambo ni makubaliano. kama mkeo ange kua hana neno na hiyo mikanda sawa ila kama haitaki basi hamna haja ya kuwa nayo. Nia yako ya kuwa nazo si wote mfurahie? Sasa kama hafurahii what's the point? Ila mkuu kama kweli hauwezi kuachana nazo naku shaui uka tafute msaada maana kuna addiction to porn labda una tatizo hilo. My advise follow what the lady wants on this one because she has the right.
 
Kwakweli CD za Ngono ni Mbaya sana tena zinachochea ngono ya mara kwa mara, maana ya tendo la ndoa ni kwa ajili ajili ya reproduction na tunafanya makosa tukizani ni mchezo wa kujiburudisha! Ni sawasawa na kujisaidia tu. Huwezi kusema unafanya mazoezi ya kujisaidia! Unaweza!!!

Ni Mawazo tu.

nimeona kwenye wikipedia article inayozungumzia sex for pleasure, inaweza ikawa inakinzana na wazo lako nililolihighlight hapo juu. naquote
'It is a common myth that animals do not (as a rule) have sex for pleasure, or alternatively that humans, pigs (and perhaps cats, dolphins and one or two species of primate) are the only species which do. This is sometimes formulated "animals mate only for reproduction".

kumbe basi humans and pigs huwa wanafanya mapenzi kwa kujiburudisha ikiwa ni pamoja na reproduction
 
Sidhani kama hiyo ni tabia nzuri acha kabisa mi ningekushauri uende kwa watoa ushauri wakupe cancelling utakuwa na matatizo.
 
usitafute matatizo kijana, kwenye zile cd kuna wanaume wana mipingo kama mwiko, mke wako akiiona ataitafuta nje.

try to be natural kama mababu zetu maisha yanaendelea maisha sio ngono, katika ndoa wataalam wanasema ngono uchukua dakika 20 ya masaa 24!
 
Move on mkuu kama wapenda we angalia tu...kama mkeo hata weka kwenye laptop yako hide folder hilo siku ukiwa na feel kucheck wewe check....kisha unakwenda piga besheni some is safe sana....
 
Nimekuja kugundua kuwa hayo mambo si haki. Iweje unaeangalia isiwe dhambi? Mungu hapendi
 

CD za ngono ni dhambi kwenye ndoa?
Jamani nipo kwenye ndoa zaidi ya miaka 10, nilikuwa na package ya cd mbali za ngono na tulikuwa tunafurahia na mywife. Jana nimezikuta zimesagwasagwa...eti zinanichochea niwe na wanawake wengi, je wakuu sijapokonywa haki yangu?

Ndugu mimi nitajaribu kujibu swali lako kwa mujibu wa kichwa cha habari husika. Unapouliza kama ni dhambi, hii moja kwa moja inapelekea, kwenye zile imani zenye kuamini kuwepo kwa dhambi na Thawabu. Yaani ni kitendo kibaya au chema.

Kama Wewe Ni Muislam

Kwa wale wenye kuamini Dini ya Kiislam ni madhambi kwa Muislamu mwanamme au mwanamke kukaa kwenye runinga (TV) na kuanza kuangalia vipindi vya ngono au kinyume na maadili. Huwe mwenye ndoa au si mwana ndoa.
M'Mungu ametukataza hilo pale aliposema:

“Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya”
Q17: 32

Jambo lolote ambalo litakukaribisha na mambo zinaa pia ni zinaa.
Unapokaa mbele ya TV na kuanza kuangalia vipindi au Video/Dvd/Vcd visivyo na adabu utakuwa una makosa. Ni makosa kwa Muislamu kutazama uchi wa mwenziwe akiwa ni wa jinsiya moja au tofauti.
Uchi ulioruhusiwa kuutazama ni mume kumtazama mkewe na mke kumtazama mumewe basi.

Hapa nakubaliana na wachangiaji wengi walio pita, kwa kusema kwao kuwa uenda kwa kuangalia kwako hiyo mikanda, kukakuperekea wewe kutamani kuiga yale yanayofanywa, na hao porn star (!?) Na ikatokea kuwa mwenza wako si mahiri wa hao unayoyatamani, mwishowe utaamua kwenda kujaribu nje...

Kwa kutunza ndoa zetu inatakiwa tujiepushe na mambo ambayo yanaweza kutupelekea kufanya zinaa yenyewe kama hivyo unavyofanya.

Bila kuwa ni matamanio si kuzini lakini ikiwa utatazama TV yenye uchafu huo na ukapata matamanio utaandikiwa madhambi.

Kama Wewe Ni Mkristo:
Je unapotazama hizo Video hutamani? Kutamani mtu asiye mume au mke wako nikuzini katika Mathayo 5:27-30 tunasoma maneno hayaa:

"Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;
Lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
Jicho lako la kuume likikukosesha, ling'oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum..
"

Soma vizuri andiko hilo hapo juu, unapotazama filamu za ngono, jicho lako huangalia na kukaribisha matamanio kwa mke au mume si wako (Jicho lako la kuume likikukosesha). Kwa mujibu wa andiko ilo utahesabiwa kuwa umezini.

Kisha baada yakutazama, mikono yako itatekelea kile ambacho macho yameona ili kukamilisha matamanio yako. (Na mkono wako wa kuume ukikukosesha)

Nimapenzi ya Mungu tusizini. Imeandikwa katika Wathesalonike wa kwanza 4:3
"Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, muepukane na usherati."

Basi kumbe hata kutazama tu kwa kutamani ni kuzini pia.

Tafadhali husichoke kunisoma, ila napenda kumalizia kwa kumnukuu Paulo alipokuwa anwaasa wakorintho:

“Yakini habari imeenea kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika mataifa….. Mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo….. Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi. Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyanganyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. Lakini mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyanganyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye
1 Wakorintho 5:1,2-11

Je vipi ukiwa wewe ni mkristo unakaribisha filamu za ngono na uzinzi chumbani kwako?
 
Jamani nipo kwenye ndoa zaidi ya miaka 10, nilikuwa na package ya cd mbali za ngono na tulikuwa tunafurahia na mywife. Jana nimezikuta zimesagwasagwa...eti zinanichochea niwe na wanawake wengi, je wakuu sijapokonywa haki yangu?

...kwa kuongezea, hata kama wewe na mkeo mtajirekodi hilo 'tendo la ndoa', halafu muwe mnajiangalia pia ni dhambi! :(
 
Mkuu piga mzigo tu check CD then zama kwenye PRACTICAL hihi hamna noma hapo mkuu na wala sio dhambi kabisa....ila cha muhimu kuna movie zingine ni za vishawishi so angalia sana usije ukavunja ndoa!!
 
Love making is something natural. You should be creative and learn how to give your partiner maximum pleasure. Watching porn videos is disastrous to your marriage. It will end up breaking your marriage. Ask your partiner which turns him/her on.
 
Ndugu mimi nitajaribu kujibu swali lako kwa mujibu wa kichwa cha habari husika. Unapouliza kama ni dhambi, hii moja kwa moja inapelekea, kwenye zile imani zenye kuamini kuwepo kwa dhambi na Thawabu. Yaani ni kitendo kibaya au chema.

Kama Wewe Ni Muislam
Kwa wale wenye kuamini Dini ya Kiislam ni madhambi kwa Muislamu mwanamme au mwanamke kukaa kwenye runinga (TV) na kuanza kuangalia vipindi vya ngono au kinyume na maadili. Huwe mwenye ndoa au si mwana ndoa.
M'Mungu ametukataza hilo pale aliposema:

“Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya”
Q17: 32

Jambo lolote ambalo litakukaribisha na mambo zinaa pia ni zinaa.
Unapokaa mbele ya TV na kuanza kuangalia vipindi au Video/Dvd/Vcd visivyo na adabu utakuwa una makosa. Ni makosa kwa Muislamu kutazama uchi wa mwenziwe akiwa ni wa jinsiya moja au tofauti.
Uchi ulioruhusiwa kuutazama ni mume kumtazama mkewe na mke kumtazama mumewe basi.

Hapa nakubaliana na wachangiaji wengi walio pita, kwa kusema kwao kuwa uenda kwa kuangalia kwako hiyo mikanda, kukakuperekea wewe kutamani kuiga yale yanayofanywa, na hao porn star (!?) Na ikatokea kuwa mwenza wako si mahiri wa hao unayoyatamani, mwishowe utaamua kwenda kujaribu nje...

Kwa kutunza ndoa zetu inatakiwa tujiepushe na mambo ambayo yanaweza kutupelekea kufanya zinaa yenyewe kama hivyo unavyofanya.

Bila kuwa ni matamanio si kuzini lakini ikiwa utatazama TV yenye uchafu huo na ukapata matamanio utaandikiwa madhambi.

Kama Wewe Ni Mkristo:
Je unapotazama hizo Video hutamani? Kutamani mtu asiye mume au mke wako nikuzini katika Mathayo 5:27-30 tunasoma maneno hayaa:

"Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;
Lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
Jicho lako la kuume likikukosesha, ling'oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.."

Soma vizuri andiko hilo hapo juu, unapotazama filamu za ngono, jicho lako huangalia na kukaribisha matamanio kwa mke au mume si wako (Jicho lako la kuume likikukosesha). Kwa mujibu wa andiko ilo utahesabiwa kuwa umezini.

Kisha baada yakutazama, mikono yako itatekelea kile ambacho macho yameona ili kukamilisha matamanio yako. (Na mkono wako wa kuume ukikukosesha)

Nimapenzi ya Mungu tusizini. Imeandikwa katika Wathesalonike wa kwanza 4:3
"Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, muepukane na usherati."

Basi kumbe hata kutazama tu kwa kutamani ni kuzini pia.

Tafadhali husichoke kunisoma, ila napenda kumalizia kwa kumnukuu Paulo alipokuwa anwaasa wakorintho:

“Yakini habari imeenea kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika mataifa….. Mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo….. Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi. Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyanganyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. Lakini mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyanganyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye
1 Wakorintho 5:1,2-11

Je vipi ukiwa wewe ni mkristo unakaribisha filamu za ngono na uzinzi chumbani kwako?


You made my weekend, kumbe mkuu unafaa kabisa kuwekwa waziri wa dini ,mahusiano na adabu!
 
Back
Top Bottom