bendaki
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 952
- 346
Ipo CCMNyerere ilikuwa na Azimio la Arusha, na ipo CCMMateka (Mtandao) Ina Azimio la Zanzibar. Ya kwanza muda wote iliweka mbele maslahi ya watz. Ya pili inaangalia maslahi ya mafisadi wachache waliojiunda kutoka ile ya kwanza zikiwa koo kadhaa ktk utendaji wa ya kwanza, wahindi wezi na waafrika kadhaa wala rushwa. Wamewatelekeza na kuwaone watanzania kwa uharisia wao wa elimu duni, kipato duni, fikra duni hata afya zao za mashaka. Kwa kuijua njaa yao watanunua kadi zao za kupigia kura. Watawagawia vyakula vya siku moja, kofia, kanga, tshirt, nk. Watawahadaa kubakizwa madarakani halafu wawatupe. Watawawekea madeni makubwa kulipa wao na vitukuu kwa kuboresha miundombinu ya kuimarisha zaidi mali zao (barabara za lami) na kudhoofisha miundombinu ya kuimarisha zaidi maisha ya walala hoi (reli). Wamehodhi uongozi ktk chama, serikali na taasisi zake. Kodi zatumika kujiimalisha ili baba, mama, mtoto vitukuu waendelee kukaa juu zaidi ya Watz wengine. Atakae tetea Watz wengine nguvu itatumika kumudhibiti.