CCM yazidi kuhaha katika uchaguzi mkuu wa 2015

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
Katika Chama shenye wasi wasi na wakati mgumu sana hivi sasa ni Chama cha mapinduzi Ccm.

Hofu kubwa imeingia katika chama cha ccm kutokana na kuhamwa na wimbi kubwa la viongozi wao na wanachama wake, kuna tetesi za kikao cha siri kilicho fanyika Zanzibar kikijumuisha vigogo wa ccm wa pandezote mbili Tanzania Bara na Visiwani.

Katika habari zilizo patikana nikuwa yamezungumzwa mengi lakini zaidi ilikuwa nimbinu gani za kukimarisha chama ili 2015 kisipoteze madaraka yake ya kuongoza Serekali kwenye gazi ya urais na Bunge.

Hali hii ili changiwa sana kwa malumbano ya kushtumiana wenyewe kwa wenyewe kusherewa kukimirisha chama mpaka hali imekuwa ngumu na yakutisha, kuna fununu zimepenya kuwa wako badhi ya vigogo kwa kuhofia hali ya sasa kujiweka pembeni au kukihama chama kabisa, swala lao kubwa ni hali ya uchaguzi wa 2015 hali itakuwa vipi?.

Utulivu katika vikao vya ccm hivi sasa si washuari baada ya kushtumiana wenyewe kwa wenyewe kukizofisha chama kwa mgawanyika wa makundi ndani ya chama , imesema kuna kumbuana kwa kutumia fedha kwa walio naza na kupikiana fitina na majungu.

Hali hii imesema inakipeleka chama pabaya na kukipa wakati mgumu katika uchaguzi wa 2015, vigogo wengi kutoka Zanzibar wakichangiwa na kutoka upande wa Tanzania Bara walimtaka Rais kikwete asiwe mwepesi na mwenye kuvumilia mazambi ya wale ambao wanashutumia kufanya ufisadi wa fedha za umma na wale wote wenye kusababisha uzofikaji wa chama wachukuliwe hatuwa za mara moja ili kurudisha imani ya wanachama katika chama chao.

Walisema bila ya kufanya hivyo basi chama kitakuwa kiko hatarini na itakuwa vigumu 2015 kuchinka nguvu ya dola na Baadae itadondoka kwa wapinzani na chama kitakosa muelekeo. kwa upande wa vigogo wa Zanzibar wa ccm walisema hali ikiwa ngumu kwa Tanzania Bara inaweza kuwa ngumu vile vile kwa visiwani.

Walisema hivi sasa ccm nivigumu kutumia pesa kiholela holela au kutumia madaraka kizembe kwa vile tunaweza kuleta asari kwa chama chetu na kusababisha mbinu za vyama vya upinzani kupata vyanzo vya kutuhukumu kwa mazambi tutakayo yafanya kwa jamii.

Rais kikwete alisema sipendelei kuondoka katika Badaraka huku chama changu kimesambaratika na vile vile sipendelei kuacha maafa huko nyuma itakuwa sote tumehusika kwa njia hii au ile kukiuwa chama, huu sio wakati tena wakulindana kwa machafu, mtu afanye madudu yake halafu chama kimstahamilie ,hii nikukiuwa chama na kupoteza wafuasi.
 
Mkuu abdulahsaf, mzizi wa matatizo ya ccm ni kiongozi wake mkuu-JK, kama wanaweza wamtoe kwenye icho kiti. Pia, wanapaswa watambua now its toooo late!!! Wajiandae kuwa chama pinzani, pia inawapasa waboreshe hali ya magereza nchini kwani watajaa humo...
 
Mkuu abdulahsaf, mzizi wa matatizo ya ccm ni kiongozi wake mkuu-JK, kama wanaweza wamtoe kwenye icho kiti. Pia, wanapaswa watambua now its toooo late!!! Wajiandae kuwa chama pinzani, pia inawapasa waboreshe hali ya magereza nchini kwani watajaa humo...
Mkuu mimi nimesha-book chumba ukonga.
 
abdulahsaf

Kwa wewe mfuatiliaji wa siasa za tatu kasorobo unaona kama vile hilo ni jambo la ajabu. Kwa taarifa yako hata vyama ambayo ni vikongwe kukutana na kunyoosheana vidole kama namna ya kujipanga kwa mapambano ya mbele ni kitu cha kawaida.

Sasa kama wewe hujui kwamba hata kile chama chenu cha kifamilia wamekuwa wakifanya hivyo hivyo basi ujijue kwamba una tatizo la msingi la kukosa ufahamu wa mambo.
 
Last edited by a moderator:
Ccm imeshazikwa zamani,wananchi wamesanuka..tunamshukuru EL kuleta sekondari za kata..somehow wameelimisha.
 
Kwa wewe mfuatiliaji wa siasa za tatu kasorobo onaona kama vile hilo ni jambo la ajabu. Kwa taarifa yako hata vyama ambayo ni vikongwe kukutana na kunyoosheana vidole kama namna ya kujipanga kwa mapambano ya mbele ni kitu cha kawaida. Sasa kama wewe hujui kwamba hata kile chama chenu cha kifamilia wamekuwa wakifanya hivyo hivyo basi ujijue kwamba una tatizo la msingi la kukosa ufahamu wa mambo.

Ujijue kwamba unatatizo la kukosa ufahamu wa mambo.
 
Abdul......
Kaka hata gharika enzi ya sodoma na gomora iliwakuta watu wakiwa hawaaamini kuwa inakuja gharika. Sikushangai maana na wewe hutakuwa pekee yako ila wenye maono wameanza kuchukua hatua ili waingie katika safina.
Kazi kwako
action time
 
Abdul......
Kaka hata gharika enzi ya sodoma na gomora iliwakuta watu wakiwa
hawaaamini kuwa inakuja gharika. Sikushangai maana na wewe hutakuwa
pekee yako ila wenye maono wameanza kuchukua hatua ili waingie katika
safina.
Kazi kwako
action time

Gharika ilikuwa wakati wa Nuhu ndugu yangu! Sodoma na Gomora waliteketezwa kwa moto.
 
Back
Top Bottom