CCM yawatosa Watuhumiwa bila Ushahidi!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Wakati serikali ya CCM ikidai kuwa watuhumiwa wasichukuliwe hatua yoyote au kuhukumiwa kwa namna yoyote hadi vyombo vya sheria vitimize kazi yake, habari zinazoingia KLH News ni kuwa Kamati Kuu imeamua kuwatosa waliokuwa wa Bunge wa Mkoani Arusha ambao walikuwa wanakabiliwa na TUHUMA ZA RUSHWA. Chama hicho tawala, hakikutaka kusubiri maamuzi ya mahakama au kuacha mchakato wa sheria ufuate mkondo wake na badala yake imeamua kuwa mtoa taarifa, hakimu, polisi, na Mnyongaji!!

Taarifa zaidi baadaye....
 
Hii mpya na kali. ukiona kukurupuka usingizini ndiko huku, enewei tuone kitakachojiri....
 
hayooooooo...

yanawatokea puani na double standard zao!
Mbona wasisubiri mahakama na vyombo vya sheria vifanye kazi?
 
Those are sacrificial lambs hoping that will appease the masses that something is being done on the whole "ufisadi". Now let us wait for the reaction from the very masses.
 
Hivi si juzi tu 'muungwana mwendo mdundo' kaleta stori kule Arusha?? sasa hii ni nini tena....anataka kumkoroga nani?
 
Chetu ni chao na chao ni chao.. Kwenye "Shamba la Wanyama" kuna sheria zinazohusu wanyama wote, lakini kuna sheria nyingine haziwahusu wote kwani kuna wanyama wengine ambao wana haki zaidi kuliko wengine.

Kada.. ndiyo habari za hivi sasa... kama watageuza kibano hilo jingine.. ila ndiyo hivyo tena..
 
Chetu ni chao na chao ni chao.. Kwenye "Shamba la Wanyama" kuna sheria zinazohusu wanyama wote, lakini kuna sheria nyingine haziwahusu wote kwani kuna wanyama wengine ambao wana haki zaidi kuliko wengine.

Kada.. ndiyo habari za hivi sasa... kama watageuza kibano hilo jingine.. ila ndiyo hivyo tena..

Mzee wa kijiji, hapa sijakupata vema, kwamba wamefukuzwa uanachama? ama wamesimamishwa ubunge? fafanua kidogo mkuu.. ama habari bado ziko jikoni sana?

Na kikao kipi kime fanya maamzi hayo mbona ile k/kuu ilisema wataendelea na ubunge hizo ni tuhuma tu?
 
Rwabugiri tangia jana kuna kikao cha Kamati Kuu ambacho kilikuwa kinaandaa mkutano wa Halmashauri Kuu ambao utaangalia mipango ya Mkutano Mkuu. Sasa habari ni kuwa kikao cha Kamati Kuu kimeamua kuwavua Uanachama and hence wanapoteza Ubunge mara moja, kwani Kamati Kuu haiwezi kuwavua Ubunge!
 
Wanajaribu kufukia mashimo ya Buzwagi na BOT.Wamesahau kwamba "la kuvunda halina ubani, hata wakiendelea kupaka manemane litaendelea kunuka tu".
 
Rwabugiri tangia jana kuna kikao cha Kamati Kuu ambacho kilikuwa kinaandaa mkutano wa Halmashauri Kuu ambao utaangalia mipango ya Mkutano Mkuu. Sasa habari ni kuwa kikao cha Kamati Kuu kimeamua kuwavua Uanachama and hence wanapoteza Ubunge mara moja, kwani Kamati Kuu haiwezi kuwavua Ubunge!

Asante Mkijiji,

Hapo kazi imeanza vyama mbadala inabidi vifanye kweli... taratiiibu kuja kufika 2010 mambo hayatakuwa haba!. na haya majimbo kuyachukua ni rahisi sana, kwani hao wabunge wana support kubwa ya watu wao nao wanadai wameonewa!! kwahiyo ni rahisi kusaidia upande wa pili.. na hasira ya wale wanao ungana nao kwamba wameonewa inaweza malizikia kwa kuwapa mbadala...

oh.. lovely!
 
SISIEMU lazima washikiwe Bango wasilete zao.

Hata Fisi kwa Uroho wake wa nyama hali Nyama ya Fisi mwenzie ni kweli aweza mkata gino la tako lakini si kula nyama yake.

SISIEMU wameanza kulana wenyewe bila kufuata Utaratibi Kanuni na Sheria.

Jamaa wakishinda Kesi waipeleke SISIEMU Mahakamani kupinga kufukuzwa.
 
Wakati serikali ya CCM ikidai kuwa watuhumiwa wasichukuliwe hatua yoyote au kuhukumiwa kwa namna yoyote hadi vyombo vya sheria vitimize kazi yake, habari zinazoingia KLH News ni kuwa Kamati Kuu imeamua kuwatosa waliokuwa wa Bunge wa Mkoani Arusha ambao walikuwa wanakabiliwa na TUHUMA ZA RUSHWA. Chama hicho tawala, hakikutaka kusubiri maamuzi ya mahakama au kuacha mchakato wa sheria ufuate mkondo wake na badala yake imeamua kuwa mtoa taarifa, hakimu, polisi, na Mnyongaji!!

Taarifa zaidi baadaye....

Kwa speed hii itakuwa vizuri kama Muungwana akiwatosa Karamagi, Meghji, Balali, Msolla, Magufuli, Mramba na wengineo wote ambao hawana credibility machoni mwa Watanzania ili kusafisha awamu yake. Vinginevyo itakuwa yale yale ya usanii. Kwa wengine sheria inatumika kwa speed kali sana wakati huo huo kwa wana mtandao na washkaji hawaguswi na wanaendelea kupeta.
 
Nadhani kama sisiemu wamechukua hatua hiyo, sio haki kwa watuhumiwa, kwa sababu kesi yao bado iko mahakamani, wangesubiri. Na iwapo uchaguzi wa majimbo ya hawa wabunge utafanyika, huenda kura nyingi zikaenda kwa wapinzani, maana Tanzania ya 2007 haitabiriki.
 
Ukiwa mnafiki na fisadi hata siku moja huwezi kubadilika. Kila siku tulikuwa tunasema gavana wa benki kuu asimamishwe ili uchunguzi ufanyike walisema ni majungu lakini leo kwa sababu wengine ni binadamu zaidi ya Watanzania wengine hiyo ni sawa kuwasimamisha bila ushahidi.

Tunataka watu ambao wamefanya makosa ya uhujumu wa uchumi kama Karamavi na timu yote iliyohusika na mkataba wa Buzwagi wafukuzwe mara moja na uchunguzi zaidi ufanyike kwenye makampuni yote ya madini na mikataba yote ambayo haina faida ifutwe. MBONA JK ANAONA KIGUGUMIZI KWA HILI?
 
2007-10-11 16:35:21
Na Mwandishi Wetu, Arusha


Sakata la tuhuma za ufisadi zilizoshikiwa bango na kambi ya upinzani limeingia katika sura mpya baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Jakaya Kikwete kuanza rasmi kushusha rungu lake zito dhidi ya mafisadi wa kweli katika Serikali yake.

Akizungumza katika hafla ya kuchangia ujenzi wa hoteli ya Kanisa la KKKT Jijini Arusha jana, Rais Kikwete amesema Serikali yake itawashughulikia vikali wale wote watakathibitika kuwa ni mafisadi.

Aidha, katika tamko lake hilo ambalo linadaiwa kuwatia presha baadhi ya vigogo Serikalini, Rais Kikwete amesema katika kushughulikia suala hilo, kamwe Serikali yake haitajali nafasi ya mtu katika jamii na badala yake, sheria zitachukua mkondo wake.

Kufuatia tamko hilo, chanzo chetu kimoja ndani ya Serikali kimedai kuwa tayari baadhi ya vigogo walio na kashfa za kweli katika ufisadi wameanza kuhaha huku na kule.

`Maneno ya Rais yalikuwa mazito? siku zote amekuwa mstari wa mbele katika kukomesha rushwa na kwa sababu hiyo, aliposema tuhuma zote zinafanyiwa kazi na wahusika watachukuliwa hatua zimewafanya baadhi yao kuanza kujihesabia siku za kushikilia mamlaka waliyo nayo,` kimesema chanzo chetu hicho.

Aidha, katika maelezo yake hiyo jana, pia Rais Kikwete amesema taarifa zote zinazotolewa kuhusu tuhuma za rushwa zinachunguzwa na mamlaka husika na baadaye zitatolewa uamuzi.

`Kila taarifa inayohusu rushwa au tuhuma za rushwa itachunguzwa na mamlaka husika na si vinginevyo na atakayethibitishwa na mamlaka halali atachukuliwa hatua za kisheria bila kujali nafasi yake,` amessema Rais Kikwete.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete aliwaonya wanaowatuhumu wenzao kwa ufisadi bila ya kuwa na uthibitisho kwa kuwaeleza kuwa hatua hiyo si sahihi.

Akasema si vyema watu wakajipa mamlaka ya kuwa polisi, wapelelezi, waendesha mashtaka na pia watoaji wa hukumu.

Badala yake, Rais Kikwete akataka kila mmoja kuzingatia sheria za nchi.

SOURCE: Alasiri

nadhani hii ameitoa huko arusha na akaamua kuwa hao wabunge watoswe as mfano ingawa sie wananchi tunaona baaaado kweli kweli. Kama akimtosha white head na RA pamoja na vicheche wengine walah tutaona angalau atapata kura moja in 2010.

`Kila taarifa inayohusu rushwa au tuhuma za rushwa itachunguzwa na mamlaka husika na si vinginevyo na atakayethibitishwa na mamlaka halali atachukuliwa hatua za kisheria bila kujali nafasi yake,` amessema Rais Kikwete.

...haya maneno nakumbuka nilishawahi kuyasikia akisema siku fulani mwanzoni mwa utawala wake, tena akasema anawajua kwa majina halafu kikapita kimya mpaka sasa....


Akasema si vyema watu wakajipa mamlaka ya kuwa polisi, wapelelezi, waendesha mashtaka na pia watoaji wa hukumu.

....Naye anawalaumu kina slaa kistaili. Akumbuke kuwa hiyo ndiyo impact ya kuishtaki serikali kwa wananchi, walidhani ni mchezo, angalau wangekubali kuundwa kwa tume bungeni lakini kwa kuwa hawajui majira ya vuli na masika basi wanaambulia fedheha.... Sisi wananchi tunaamua ktk sanduku la kura.

Tena hapo juu naona muungwana amekwenda mbali kidogo maana akina slaa hawajatoa hukumu bali wameshtaki kwa wananchi ambapo nasi hatujatoa hukumu mpaka siku ya uchaguzi ifike. Na je alitegemea kuwa watoa tuhuma wasifanye upelelezi?? Naamini kuwa wanapaswa wajiridhishe kuwa taarifa wanazotoa kwa umma ni sahihi na usahihi huu lazima waangalie rangi halisi ya carpert baada ya kulifunua.
Namshauri muungwana awatimue washauri wake maana wamekosea kumshauri ktk hili.
 
Back
Top Bottom