CCM yawataka Wawakilishi wake kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Sep 6, 2020
663
430
CCM YATAKA WAWAKILISHI WAKE KUWA KARIBU NA WANANCHI

Songea, Ruvuma
19 Septemba, 2021

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama hicho kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka.

Shaka amewataka wawakilishi wa wananchi kupitia CCM wakiwemo wenyeviti wa vitongoji, vijiji, mitaa, madiwani na wabunge watekeleze wajibu waliouomba kikamilifu ikiwemo kufanya mikutano ya wananchi, kuhamasisha maendeleo na kushughulikia kero za wananchi pamoja na kuzitafutia ufumbuzi kwa wakati.

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka.

Alilazimika kutoa maelekezo hayo kufuatia malalamiko yaliyotolewa kwake na wananchi wa mtaa wa Mlelewa kata ya Mletele ambao walidai tangu wamchague diwani wao Ndg Maurisi Lungu hajawahi kufanya mkutano katika mtaa wao.

Akiwa katika Ziara yake Manispaa ya Songea aliweza kukagua mradi wa machinjio ya kisasa uliogharimu shilingi bilioni 5.523 mpaka ulipofikia huku ukihitaji kiasi cha shilingi bilioni 3.798 kukamilika ili kutoa huduma kama ilivyokusudiwa. Machinjio hayo yanachinja ng'ombe 300 kwa siku ikiwa imetoa ajira za kudumu 35 na vibarua 40.

Shaka alisema "Mradi huu ni sehemu ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati kiuchumi yenye kulenga kuzalisha ajira, kuongeza thamani ya mazao ya mifugo kwa uchakataji nyama kwa ajili ya mahitaji ya ndani na usafirishaji nje ya nchi hivyo kuipatia nchi yetu fedha za kigeni. Ujenzi wa machinjio haya ya kisasa ni utekelezaji wa ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 40(x). Nawapongeza wote waliohusika katika utekelezaji wa mradi huu kwani wamemuunga mkono kwa vitendo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anamedhamiria kufanya mageuzi makubwa ya kiuchumi."

Aidha Shaka aliongeza kuwa mwakani kutafanyika uchaguzi ndani ya CCM hivyo wale wenye sifa za kuwania nafasi mbalimbali waachwe wawanie nafasi hizo ili kuendelea kukijenga na kukiimarisha pamoja na kukipatia chama ushindi katika chaguzi za 2024/2025.

Katika kuhitimisha hotuba yake kwa wananchi wa shina namba tatu, tawi la Mlelewa aliwahamasisha wananchi wananchi kujitokeza kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwaka 2022 kwani kushiriki kwao kutaiwezesha serikali kupata taarifa sahihi kwa ajili ya mipango ya maendeleo ya Nchi yetu.

Shaka yupo wilaya ya Songea Mjini mkoani Ruvuma alipowasili leo akitokea mkoani Mtwara na kuanza ziara ya uhamasishaji uhai wa chama mashinani, kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi, kuhamasisha sensa na kusikiliza kero za wananchi ikiwa ni muendelezo wa ziara ya Sekretarieti ya CCM Taifa inayoongozwa na Katibu Mkuu Ndg Daniel Chongolo katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Njombe.

IMG-20210919-WA0093.jpg
 
Na Mwandishi Wetu,
Songea, Ruvuma.
19 Septemba, 2021.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama hicho kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka.

Shaka amewataka wawakilishi wa wananchi kupitia CCM wakiwemo wenyeviti wa vitongoji, vijiji, mitaa, madiwani na wabunge watekeleze wajibu waliouomba kikamilifu ikiwemo kufanya mikutano ya wananchi, kuhamasisha maendeleo na kushughulikia kero za wananchi pamoja na kuzitafutia ufumbuzi kwa wakati.

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka

Alilazimika kutoa maelekezo hayo kufuatia malalamiko yaliyotolewa kwake na wananchi wa mtaa wa Mlelewa kata ya Mletele ambao walidai tangu wamchague diwani wao Ndg Maurisi Lungu hajawahi kufanya mkutano katika mtaa wao.

Akiwa katika Ziara yake Manispaa ya Songea aliweza kukagua mradi wa machinjio ya kisasa uliogharimu shilingi bilioni 5.523 mpaka ulipofikia huku ukihitaji kiasi cha shilingi bilioni 3.798 kukamilika ili kutoa huduma kama ilivyokusudiwa. Machinjio hayo yanachinja ng'ombe 300 kwa siku ikiwa imetoa ajira za kudumu 35 na vibarua 40.

Shaka alisema "Mradi huu ni sehemu ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati kiuchumi yenye kulenga kuzalisha ajira, kuongeza thamani ya mazao ya mifugo kwa uchakataji nyama kwa ajili ya mahitaji ya ndani na usafirishaji nje ya nchi hivyo kuipatia nchi yetu fedha za kigeni. Ujenzi wa machinjio haya ya kisasa ni utekelezaji wa ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 40(x). Nawapongeza wote waliohusika katika utekelezaji wa mradi huu kwani wamemuunga mkono kwa vitendo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anamedhamiria kufanya mageuzi makubwa ya kiuchumi."


Aidha Shaka aliongeza kuwa mwakani kutafanyika uchaguzi ndani ya CCM hivyo wale wenye sifa za kuwania nafasi mbalimbali waachwe wawanie nafasi hizo ili kuendelea kukijenga na kukiimarisha pamoja na kukipatia chama ushindi katika chaguzi za 2024/2025.

Katika kuhitimisha hotuba yake kwa wananchi wa shina namba tatu, tawi la Mlelewa aliwahamasisha wananchi wananchi kujitokeza kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwaka 2022 kwani kushiriki kwao kutaiwezesha serikali kupata taarifa sahihi kwa ajili ya mipango ya maendeleo ya Nchi yetu.

Shaka yupo wilaya ya Songea Mjini mkoani Ruvuma alipowasili leo akitokea mkoani Mtwara na kuanza ziara ya uhamasishaji uhai wa chama mashinani, kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi, kuhamasisha sensa na kusikiliza kero za wananchi ikiwa ni muendelezo wa ziara ya Sekretarieti ya CCM Taifa inayoongozwa na Katibu Mkuu Ndg Daniel Chongolo katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Njombe.

IMG-20210919-WA0051.jpg
IMG-20210919-WA0048.jpg
IMG-20210919-WA0050.jpg
IMG-20210919-WA0045.jpg
IMG-20210919-WA0046.jpg
 
Nawasalimu katika jina la JMT,

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama na serikali kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka,

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka

VIVA SHAKA VIVA || VIVA CCM VIVA

IMG-20210916-WA0049.jpg
 
Simlaumu Shaka. Amekuzwa kwenye mfumo ambao haujui nini kinatakiwa kufanywa kwa ajili ya nchi. Ili tutoke kwenye shida, je tunataka tufanye nini? Hilo ndilo swali muhimu.

Otherwise tutakuwa tunakwenda hatua kumi mbele, 25 nyuma. Tukifahamu hilo, hutasikia habari za wamachinga kuhama au kuruhusiwa kufanya biashara sehemu ambazo siyo zao. Nchi ya matamko haifiki popote. CCM hebu njooni na scientific plan ya kuisimamia serikali. Achaneni na utoto utoto
 
Niliwahi kusema narudia tena Shaka ni msaada mkubwa sana kwa chama changu cha CCM na Serikali yake,

Shaka tunakukaribisha kanda ya ziwa,

Tunataka kuona mikutano ya Viongozi wa chama na serikali,

Tuone mkutano wa Mkt wa kitongoji,
Tuone mkutano wa Mkt wa kijiji
Tuone mkutano wa Mkt wa Mtaa
Tuone mkutano wa Diwani,
Tuone mkutano wa mtendaji wa kijiji|kata
Tuone mkutano wa Mbunge,
Tuone mkutano wa DED,
Tuone mkutano wa DC
Tuone mkutano wa RC

TUNATAKA KUONA MIKUTANO TUPATE MAPATO NA MATUZI YA FEDHA ZETU,


Hongera sana Shaka kwa hili,


Nawasalimu katika jina la JMT,


Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama na serikali kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka,

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka

VIVA SHAKA VIVA || VIVA CCM VIVA

View attachment 1945777
iliwahi kusema narudia tena Shaka ni msaada mkubwa sana kwa chama changu cha CCM na Serikali yake,

Shaka tunakukaribisha kanda ya ziwa,

Tunataka kuona mikutano ya Viongozi wa chama na serikali,

Tuone mkutano wa Mkt wa kitongoji,
Tuone mkutano wa Mkt wa kijiji
Tuone mkutano wa Mkt wa Mtaa
Tuone mkutano wa Diwani,
Tuone mkutano wa mtendaji wa kijiji|kata
Tuone mkutano wa Mbunge,
Tuone mkutano wa DED,
Tuone mkutano wa DC
Tuone mkutano wa RC

TUNATAKA KUONA MIKUTANO TUPATE MAPATO NA MATUZI YA FEDHA ZETU,


Hongera sana Shaka kwa hili,
 
Nashauri peleka maoni yako moja kwa moja kwa muhusika, unazo hoja za msingi but acha kulalamika nchi yetu sote hii,


Simlaumu Shaka. Amekuzwa kwenye mfumo ambao haujui nini kinatakiwa kufanywa kwa ajili ya nchi. Ili tutoke kwenye shida, je tunataka tufanye nini? Hilo ndilo swali muhimu. Otherwise tutakuwa tunakwenda hatua kumi mbele, 25 nyuma. Tukifahamu hilo, hutasikia habari za wamachinga kuhama au kuruhusiwa kufanya biashara sehemu ambazo siyo zao. Nchi ya matamko haifiki popote. CCM hebu njooni na scientific plan ya kuisimamia serikali. Achaneni na utoto utoto
 
Nawasalimu katika jina la JMT,


Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama na serikali kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka,

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka

VIVA SHAKA VIVA || VIVA CCM VIVA

View attachment 1945777


Ila CCM inahazina kubwa ya viongozi aise,

Baada ya Polepole kuondolewa tukadhani Chama kitasinzia kumbe Mungu kamuandaa Elisha kuchukua mikoba ya Elia,

Asante Polepole, Hongera sana Shaka,
 
Nawasalimu katika jina la JMT,


Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama na serikali kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka,

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka

VIVA SHAKA VIVA || VIVA CCM VIVA

View attachment 1945777

Waende field wakati serikali yako haijawapa mafuta ya gari? Au unataka waende kwa miguu?
 
CCM ina misingi imara sana, mtaji-watu wa kutosha, wanachama wenye imani

Na muhimu zaidi hakuna mkubwa kuliko chama kwao

Wanaposema KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI huwa wanamaanisha
 
Kuitisha mikutano ili kujua kero za wananchi ni matumizi mabovu ya kodi na inaonyesha jinsi gani kuna upuuzi unaendelea.

Mkoa una wabunge.

Una serikali za mitaa zenye wawakilishi mpaka level ya chini kabisa.

Hawa wawili wanaweza kuwasilisha hizo kero kwa RC (Kama RC hajui kero za mTanzania) bila kutumia pesa nyingi pasipo ulazima.
 
Kuitisha mikutano ili kujua kero za wananchi ni matumizi mabovu ya kodi na inaonyesha jinsi gani kuna upuuzi unaendelea.

Mkoa una wabunge.

Una serikali za mitaa zenye wawakilishi mpaka level ya chini kabisa.

Hawa wawili wanaweza kuwasilisha hizo kero kwa RC (Kama RC hajui kero za mTanzania) bila kutumia pesa nyingi pasipo ulazima.


HAPANA HUELEWI HII CHAIN OF COMAND,

kila ngazi inaumuhimu wake ndio maana Rais akienda mkoa wowote kuna kero atapewa na wananchi,
Kwanini wanampa wanaamini katika mamlaka aliyonayo,

Ndio hivyo kwa RC, DC na wengine,
 
kweli kuongea na wananchi ni muhimu

changamoto ni kaulimbiu ya mkutano, ikiwa kisiasaa ni changamoto
 
Nawasalimu katika jina la JMT,


Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka viongozi wa chama na serikali kushughulikia matatizo ya wananchi badala ya kufanya vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kutafuta madaraka,

"Ili CCM iendelee kukubalika na kuaminiwa na wananchi na kuendelea kupewa ridhaa ya kuunda serikali na kuongoza Nchi yetu, ni lazima wawakilishi wetu na viongozi serikalini kuwa karibu na wananchi. Hivyo natoa maelekezo kwa wawakilishi wetu hawa nchi nzima wafanye mikutano ya wananchi ili kuhamasisha maendeleo, kusikiliza kero zao na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. Pamoja na kuendelea kuwa wasemaji na watetezi wa wananchi wote. Haya ni maelekezo ya ilani yetu ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 255 ambayo ni lazima chama tuyasimamie ili kuendelea kuaminiwa." Alisema Shaka

VIVA SHAKA VIVA || VIVA CCM VIVA

View attachment 1945777
Vivaaa

SIEMPRE JMT
 
Niliwahi kusema narudia tena Shaka ni msaada mkubwa sana kwa chama changu cha CCM na Serikali yake,

Shaka tunakukaribisha kanda ya ziwa,

Tunataka kuona mikutano ya Viongozi wa chama na serikali,

Tuone mkutano wa Mkt wa kitongoji,
Tuone mkutano wa Mkt wa kijiji
Tuone mkutano wa Mkt wa Mtaa
Tuone mkutano wa Diwani,
Tuone mkutano wa mtendaji wa kijiji|kata
Tuone mkutano wa Mbunge,
Tuone mkutano wa DED,
Tuone mkutano wa DC
Tuone mkutano wa RC

TUNATAKA KUONA MIKUTANO TUPATE MAPATO NA MATUZI YA FEDHA ZETU,


Hongera sana Shaka kwa hili,



iliwahi kusema narudia tena Shaka ni msaada mkubwa sana kwa chama changu cha CCM na Serikali yake,

Shaka tunakukaribisha kanda ya ziwa,

Tunataka kuona mikutano ya Viongozi wa chama na serikali,

Tuone mkutano wa Mkt wa kitongoji,
Tuone mkutano wa Mkt wa kijiji
Tuone mkutano wa Mkt wa Mtaa
Tuone mkutano wa Diwani,
Tuone mkutano wa mtendaji wa kijiji|kata
Tuone mkutano wa Mbunge,
Tuone mkutano wa DED,
Tuone mkutano wa DC
Tuone mkutano wa RC

TUNATAKA KUONA MIKUTANO TUPATE MAPATO NA MATUZI YA FEDHA ZETU,


Hongera sana Shaka kwa hili,



Shaka atatuvusha salama kabisa,Nimekuelewa,
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom