CCM yawakosha wa Congo na Warundi... sijui huko kwingine I hope ni the same

msumeno

JF-Expert Member
Aug 3, 2009
2,827
1,729
Wakati mchakato ukiendelea kule Dodoma jamaa zangu hapa DRC hawakua nyuma kuufuatilia, kuna jamaa yangu mmoja alinitembelea kwangu na kukuta nafuatilia recorded video ya mchakato wa CCM wa kumpata mgombe wa urais ,,, tuliangalia mwanzo mpaka mwisho. Mcongoman huyu kwa masikikitiko akasema ''natamani na sisi tungekuwa kama ninyi watanzania''. Alifurahia kila tukio na kusema hii ndio democrasia ya kweli na nchi zote Africa zinapashwa kujifunza toka kwenu. Huyu bwana aliniuliza pia kama kuna vyama vya upinzani vingi na kama wana uhuru wa kufanya shuguli za kiasa.. kwa kweli nilimjibu ndio na wako huru kisiasa na nikamwambia na wao viongozi wao wanapatikana kwa kura.

Leo wakati nikichungulia FB, nimekutana na post ya jamaa yangu mmoja wa Burundi, huyu jamaa kasema mengi sana akisifia democrasia ya CCM, nikiweza nitaipost hiyo post ya huyu jamaa, iko kwa kifaransa na kiigereza. mchakato wa CCM ulifuatiliwa sana hasa hapa DRC.

Nilichotaka kusema ni kwamba Democrasia yetu inasifika sana nchi zingine.
 
Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza.
Utamu wa ngoma ingia ndani uicheze.
 
Viongozi wetu ni sasa kuwa makini kulinda huo utamaduni ili ukomae, na kikubwa wasilale kwa Mataifa makubwa ambayo yanataka kuendelea kututawala indirect. Hasa suala la gasi, wote sasa wageni ni mate yanawatoka na madini.Mbona ulaya hakuna yote hayo, kikubwa ukiangalia Ulaya wao wanaita mfano ziwa kumbe kadimbwi.Sisi Ziwa Victoria linaweza kubeba Robo ya ulaya hata Robo tatu na bado miundo mbinu karibu na ziwa hilo ni zero.Na maziwa mengine.Take care.
 
Back
Top Bottom