CCM yasikitishwa Rais Jakaya kuhusishwa na ufisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
CCM yasikitishwa Rais Jakaya kuhusishwa na ufisadi
Mwandishi Wetu
Daily News; Wednesday,March 12, 2008 @00:03

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesikitishwa na kauli ya kumtuhumu Rais Jakaya Kikwete kuhusika na ufisadi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu (BoT) na kuvitaka vyama vya siasa kuacha kutumia kashfa hiyo kwa malengo ya siasa.

Taarifa yake iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi ya CCM, John Chiligati, ilisema kauli hiyo ya Mbowe aliyoitoa kwenye kongamano la akinamama wa Chadema ina lengo la kumchafua Rais Kikwete na kuwataka Watanzania kupuuza na kuzikataa njama hizo.

“CCM tunayo kila sababu kuamini kashfa ya EPA imeanza kutumiwa kwa malengo ya siasa ya kudhoofisha kazi nzuri inayofanywa na Rais Kikwete katika kushughulikia ufisadi na mafisadi kumdhoofisha aonekane hajafanya jambo lolote la maana, njama hizi siyo za kiungwana ni mchezo mchafu,” alisema Chiligati katika taarifa yake.

Alisema Rais Kikwete anastahili pongezi na si lawama, kwani yeye ndiye aliyeamuru EPA ikaguliwe na wakaguzi wa nje. Aliunda kamati kuchunguza ufisadi huo, kuchukuliwa hatua za sheria na fedha kurejeshwa na baada ya tume ya uchunguzi kukamilisha kazi, Rais Kikwete atawachukulia hatua waliohusika, alisema.

“…lakini kabla Tume haijawasilisha taarifa ya uchunguzi, Rais anaanza kubebeshwa lawama na shutuma nzito, kwamba anawalinda watuhumiwa na anashindwa kuwachukulia hatua za kuwapeleka mahakamani.

Lawama hizi siyo sahihi, siyo wakati wake na zina lengo la kutimiza malengo ya siasa ya kulipaka matope jina la Rais machoni mwa umma. Hali hii haiwezi kukubalika machoni mwa jamii ya waungwana kama Watanzania tulivyo.

“CCM ingependa tujenge utamaduni wa kukosoana kwa lugha ya staha na uungwana, siyo lugha ya dharau, kejeli na ya kuudhi, kwa mfano kusema rais anafanya ‘uhuni’ siyo lugha ya kistaarabu,” alisema.

Chama hicho kimewataka Watanzania wawe macho na siasa za kuchafuana majina na wazikatae, ikiwamo kuwabeza na kuwapuuza viongozi wanaoendesha siasa hizo chafu. Hata hivyo, chama hicho kiliwataka Watanzania kuwa na subira hadi uchunguzi wa EPA ukamilike na Rais atakapochukua hatua za kisheria.

Kampuni ya Ernst & Young ilibaini upotevu wa Sh bilioni 133 kutoka akaunti ya EPA, hali ambayo ilisababisha Rais Kikwete kumfukuza kazi Gavana Dk. Daudi Ballali na nafasi yake kujazwa na Profesa Beno Ndulu.

Pia aliunda tume kuchunguza makampuni 22 yaliyohusika na ufisadi huo na kutakiwa kukamilisha kazi ndani ya miezi sita, ikiwamo kuwachukulia hatua wote waliohusika na ufisadi huo.

Hadi sasa tume hiyo imeshafanikisha kurejeshwa kwa Sh bilioni 50 kutoka kwa waliohusika na ufisadi huo pamoja na kutambua mali zilizonunuliwa na fedha hizo za EPA. Tume hiyo leo itazungumza na wahariri Dar es Salaam kufafanua kazi yake hadi sasa.
 
Jamani tuwekeeni hapa alichokisema Mbowe tuone propaganda za Chiligati.

Mbowe alisema Kikwete na kamati yake wanaficha mambo kuhusu EPA kwa kuwa kuna mambo yalihusika na kampuni yake. Alimtaka Kikwete ajisafishe kwa kuweka mambo yote hadharani. Pia alilaumu kwa Kikwete kuchunguza EPA pekee wakati kuna ufisadi mwingine mwingi uliofanyika BOT. Kikwete anajua kabisa kuwa sehemu ya fedha za Kagoda, Deep Green, Meremeta, Tangold nk zilikwenda kwenye kampeni zake. Ni Kikwete alijua ufisadi wa IPTL. Kikwete alijua ufisadi wa kwenye madini.

Mtakumbuka Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994. Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo, SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada. Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.
 
Chiligati hauna nyimbo,kama na wewe ndio unalipa fadhila za kupewa uwaziri suala hili usiliingilie ni vizuri ungekaa kimya,kwanza hata CCM ni fisadi,hoja hii ilipoibuliwa bungeni wabunge wa CCM mlimuona SLAA kama mwehu leo mnataka kutuambia nini,hii inaonyesha wazi kwamba mlijua kila kinachoendelea BOT

Naomba mtu yeoyote mwenye hoja za msingi ajitokeze kukanusaha kwamba JK sio fisadi.
 
Jamani tuwekeeni hapa alichokisema Mbowe tuone propaganda za Chiligati.

Mbowe alisema Kikwete na kamati yake wanaficha mambo kuhusu EPA kwa kuwa kuna mambo yalihusika na kampuni yake. Alimtaka Kikwete ajisafishe kwa kuweka mambo yote hadharani. Pia alilaumu kwa Kikwete kuchunguza EPA pekee wakati kuna ufisadi mwingine mwingi uliofanyika BOT. Kikwete anajua kabisa kuwa sehemu ya fedha za Kagoda, Deep Green, Meremeta, Tangold nk zilikwenda kwenye kampeni zake. Ni Kikwete alijua ufisadi wa IPTL. Kikwete alijua ufisadi wa kwenye madini.

Mtakumbuka Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994. Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo, SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada. Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.


JK anahusishwa na hili kwa mazingira yaliyopo na yeye amekaa kimya anapima uelewa wa watu wa Tanzania .Kauli za JK na kila mara Tume na mara wanaanz akurudisha pesa kimya kimya nk lazima tuhoji.Utetezi wake wa Lowasa kwamba ni mchapa kazi na yaliyo mpata ni ajali kazini .Ajali ipi ? Aseme .JK anauhusima kama anasema yeye ni msafi afanye kweli .Mbona akina Hosea na Mwanyika bado wanapeta ? Mbona mafisadi kibao kama Chenge kawarudisha kazini ?
 
JK anahusishwa na hili kwa mazingira yaliyopo na yeye amekaa kimya anapima uelewa wa watu wa Tanzania .Kauli za JK na kila mara Tume na mara wanaanz akurudisha pesa kimya kimya nk lazima tuhoji.Utetezi wake wa Lowasa kwamba ni mchapa kazi na yaliyo mpata ni ajali kazini .Ajali ipi ? Aseme .JK anauhusima kama anasema yeye ni msafi afanye kweli .Mbona akina Hosea na Mwanyika bado wanapeta ? Mbona mafisadi kibao kama Chenge kawarudisha kazini ?

Kuna mambo mengi ya kujioji ya kumweka au kumwondoa mtu mkubwa kwenye Kitanzi.
1.0 Urafiki wake na RA ulianzia wapi?
2.0 Ni kwa nini alimteuwa EL kuwa waziri mkuu licha ya wananchi kutokupendezwa naye tangu 1995? Lakini kwa nini hakujihoji ni nini kilichopelekea Mwl. kuhoji mipesa ya EL hasa baada ya kujilimbikizia mali muda mfupi baada ya kuingia pale AICC?
3.0 Mkataba wa madini Nzega Golden Pride uliyosainiwa na mkuu wakati ule kule Nzega ulifanikishwa na nani?
4.0 Je, watambua kuwa Igunga anakowakilisha RA ni karibu na machimbo ambayo Mh. white house alisign?
5.0 Je, watambua kuwa RA alikiri kuwatambua DOWSONS (jina-kampuni iliyoirithi Richmond) kwa kuwa wako sehemu moja/wanafanya kazi pamoja na kampuni yake CASPIAN?
6.0 Je, watambua kuwa wafanyakazi wawili wa CASPIAN ndiyo walihusika na kusajili Kagoda Agriculture wale wababe wa EPA?
7.0 Je, wajua kuwa kampuni ya CASPIAN ipo kwenye migodi ususani kwenye mgodi uliyosigniwa na Mh. Mkuu huko Nzega Golden Pride? Kama ulivyotajwa na Dr. Slaa kwenye orodha ya mafisadi.
8.0 Je, wajua kuwa inadaiwa fedha hizi ziliisaidia CCM kwenye Kampeni za uchaguzi wa 2005. Fedha za EPA na Zile zingine za Deep solution?
9.0 Je, wajua kuwa wadadisi wanadai fedha hizi wakati zinaingia kwenye Chama kuelekea kwa walengwa Mh. Katibu wa CCM enzi hizo hakujua na alikanusha kutokujua lolote?
10.0 Je, umeshawai kujiuliza kuwa kama Katibu wa Chama hakujua, je vipi Kuhusu Mweka hazina wa chama?
11.0 Je, watambua kuwa baada ya Kikosi kuingia madarakani RA aliteuliwa kuwa Mweka Hazina wa Chama na Ng Mkuu wa mkoa wetu miaka ile kupewa Ukatibu? (Huyu bwana siku mh. ameteuliwa Dom na chama chake alidaiwa kutoweka ktk Gari la mkuu huyu)
12.0 Je, umeshawai kujioji ni kwa nini Mweka hazina wa wakati ule ambaye angejua lolote juu ya mapesa ya Kampeni ni kwa nini alienguliwa wadhifa wake, na yuko wapi leo hii kutusaidia sisi watanzania kuhusu fedha za kampeni kuhusishwa na Kagoda na Deep?
13.0 Je, wajua kuwa imedaiwa kuwa ile kampuni hewa ya deep solution iliyochota mapesa mengi BOT ilisajiliwa na wanasheria wenye Kampuni ijulikanayo kama IMMMA?
14.0 Je, wajua kuwa waziri wa mambo ya Ndani mh. Lawrence Masha kijana toka Sengerema (Mtoto wa Dr. Masha yule wa UDP aliyekuwa akiibiwa kura na CCM kule sengelema. Dr. William Shija ndo alikuwa mbunge wa jimbo hili lakini mpinzani wa Mh. Bush wetu kwenye mchakato wa CCM)ni mmoja wa watu wanene pale IMMMA?
15.0 Je, wajua Masha alipelekwa sengelema mahususi kumwengua Dr. Shija na kupanua wigo wa mtandao? (This time Baba hakugombea lakini alipewa ulaji fulani japo sikumbuki lakini alisaidiwa na CCM, may be mbunge wa EA or else. Lakini cheki Cheo-bwana Mapesa na yule Bibie wa UDP aliyehoji mfuko wa Mama Mkapa bungeni Teddy Kasela Bantu walivyopewa ulaji. Cheo umsifia sana Kikweta for WHAT?)
16.0 Je, umejioji juu ya Masha kupewa wadhifa from no where na Kijana wa Mkuu kuwa mmoja wa staff wa IMMMA. Si mbaya lakini kwa nini IMMMA, mtoto, deep na waziri hapa hapa?
17.0 Je, watambua kuwa wakati wa BM mwanasheria aliyekuwa anakamata dau la selikali ni mzee wetu wa Musoma Vijijini ambaye aliingia bungeni na kupiku wadau wengine, je, kwa nini chombo kingine cha sheria Bungeni wakati wa term hii ya Bush yaani waziri? wote wamehusishwa na mapesa ya BOT.

Sasa CCM watuambiye huyo mtu msafi yuko wapi? Kura za watanzania hazina macho lakini haimaanishi ndiyo tulimweka msafi wakati alikuwa anafanya kazi kwenye jiko lenye masizi akiwa amevaa nguo nyeusi. Hatuoni masizi lakini nguo inanuka uvundo.
 
Kuna mambo mengi ya kujioji ya kumweka au kumwondoa mtu mkubwa kwenye Kitanzi.
1.0 Urafiki wake na RA ulianzia wapi?
2.0 Ni kwa nini alimteuwa EL kuwa waziri mkuu licha ya wananchi kutokupendezwa naye tangu 1995? Lakini kwa nini hakujihoji ni nini kilichopelekea Mwl. kuhoji mipesa ya EL hasa baada ya kujilimbikizia mali muda mfupi baada ya kuingia pale AICC?
3.0 Mkataba wa madini Nzega Golden Pride uliyosainiwa na mkuu wakati ule kule Nzega ulifanikishwa na nani?
4.0 Je, watambua kuwa Igunga anakowakilisha RA ni karibu na machimbo ambayo Mh. white house alisign?
5.0 Je, watambua kuwa RA alikiri kuwatambua DOWSONS (jina-kampuni iliyoirithi Richmond) kwa kuwa wako sehemu moja/wanafanya kazi pamoja na kampuni yake CASPIAN?
6.0 Je, watambua kuwa wafanyakazi wawili wa CASPIAN ndiyo walihusika na kusajili Kagoda Agriculture wale wababe wa EPA?
7.0 Je, wajua kuwa kampuni ya CASPIAN ipo kwenye migodi ususani kwenye mgodi uliyosigniwa na Mh. Mkuu huko Nzega Golden Pride? Kama ulivyotajwa na Dr. Slaa kwenye orodha ya mafisadi.
8.0 Je, wajua kuwa inadaiwa fedha hizi ziliisaidia CCM kwenye Kampeni za uchaguzi wa 2005. Fedha za EPA na Zile zingine za Deep solution?
9.0 Je, wajua kuwa wadadisi wanadai fedha hizi wakati zinaingia kwenye Chama kuelekea kwa walengwa Mh. Katibu wa CCM enzi hizo hakujua na alikanusha kutokujua lolote?
10.0 Je, umeshawai kujiuliza kuwa kama Katibu wa Chama hakujua, je vipi Kuhusu Mweka hazina wa chama?
11.0 Je, watambua kuwa baada ya Kikosi kuingia madarakani RA aliteuliwa kuwa Mweka Hazina wa Chama na Ng Mkuu wa mkoa wetu miaka ile kupewa Ukatibu? (Huyu bwana siku mh. ameteuliwa Dom na chama chake alidaiwa kutoweka ktk Gari la mkuu huyu)
12.0 Je, umeshawai kujioji ni kwa nini Mweka hazina wa wakati ule ambaye angejua lolote juu ya mapesa ya Kampeni ni kwa nini alienguliwa wadhifa wake, na yuko wapi leo hii kutusaidia sisi watanzania kuhusu fedha za kampeni kuhusishwa na Kagoda na Deep?
13.0 Je, wajua kuwa imedaiwa kuwa ile kampuni hewa ya deep solution iliyochota mapesa mengi BOT ilisajiliwa na wanasheria wenye Kampuni ijulikanayo kama IMMMA?
14.0 Je, wajua kuwa waziri wa mambo ya Ndani mh. Lawrence Masha kijana toka Sengerema (Mtoto wa Dr. Masha yule wa UDP aliyekuwa akiibiwa kura na CCM kule sengelema. Dr. William Shija ndo alikuwa mbunge wa jimbo hili lakini mpinzani wa Mh. Bush wetu kwenye mchakato wa CCM)ni mmoja wa watu wanene pale IMMMA?
15.0 Je, wajua Masha alipelekwa sengelema mahususi kumwengua Dr. Shija na kupanua wigo wa mtandao? (This time Baba hakugombea lakini alipewa ulaji fulani japo sikumbuki lakini alisaidiwa na CCM, may be mbunge wa EA or else. Lakini cheki Cheo-bwana Mapesa na yule Bibie wa UDP aliyehoji mfuko wa Mama Mkapa bungeni Teddy Kasela Bantu walivyopewa ulaji. Cheo umsifia sana Kikweta for WHAT?)
16.0 Je, umejioji juu ya Masha kupewa wadhifa from no where na Kijana wa Mkuu kuwa mmoja wa staff wa IMMMA. Si mbaya lakini kwa nini IMMMA, mtoto, deep na waziri hapa hapa?
17.0 Je, watambua kuwa wakati wa BM mwanasheria aliyekuwa anakamata dau la selikali ni mzee wetu wa Musoma Vijijini ambaye aliingia bungeni na kupiku wadau wengine, je, kwa nini chombo kingine cha sheria Bungeni wakati wa term hii ya Bush yaani waziri? wote wamehusishwa na mapesa ya BOT.

Sasa CCM watuambiye huyo mtu msafi yuko wapi? Kura za watanzania hazina macho lakini haimaanishi ndiyo tulimweka msafi wakati alikuwa anafanya kazi kwenye jiko lenye masizi akiwa amevaa nguo nyeusi. Hatuoni masizi lakini nguo inanuka uvundo.

Ndugu Agao madai mazito haya .Yanaleta hisia nzito .Kwa kukusaidia tu ni kwamba ni Deep Green na si deep Solution.Asante sana kwa hoja zako .CCM wanacheza na watanzania
 
Ndugu Agao madai mazito haya .Yanaleta hisia nzito .Kwa kukusaidia tu ni kwamba ni Deep Green na si deep Solution.Asante sana kwa hoja zako .CCM wanacheza na watanzania

YOU MADE THE POINT !!THATS REALLY TRUE. WENGINE WANAWACHEZEA WATANZANIA !
 
Jamani tuwekeeni hapa alichokisema Mbowe tuone propaganda za Chiligati.

Mbowe alisema Kikwete na kamati yake wanaficha mambo kuhusu EPA kwa kuwa kuna mambo yalihusika na kampuni yake. Alimtaka Kikwete ajisafishe kwa kuweka mambo yote hadharani. Pia alilaumu kwa Kikwete kuchunguza EPA pekee wakati kuna ufisadi mwingine mwingi uliofanyika BOT. Kikwete anajua kabisa kuwa sehemu ya fedha za Kagoda, Deep Green, Meremeta, Tangold nk zilikwenda kwenye kampeni zake. Ni Kikwete alijua ufisadi wa IPTL. Kikwete alijua ufisadi wa kwenye madini.

Mtakumbuka Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994. Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo, SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada. Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.

Kuna watu wanadhani kuwa vitu kama hivi havionekani na havijulikani kwa watanzania. Wakati ccm wakiendelea kuhangaika na issue ya Mbowe, wana JF kama kawaida yetu tunaendeleza miziki hapa mpaka ikulu kieleweke!

Kikwete ameshindwa kushughulikia ufisadi kwa vile yeye ni part and parcel ya ufisadi na katika hili nakushukuru da Asha kwa maneno mazito haya.
 
Naona Bwana Ngurudoto ama Kaiza Twalipo ameamua "kumwaga radhi" kabisa, katuonesha hadi uchi wake wa ubongoni na tumeona kilichopo ni EMPTY SET!
 
14.0 Je, wajua kuwa waziri wa mambo ya Ndani mh. Lawrence Masha kijana toka Sengerema (Mtoto wa Dr. Masha yule wa UDP aliyekuwa akiibiwa kura na CCM kule sengelema. Dr. William Shija ndo alikuwa mbunge wa jimbo hili lakini mpinzani wa Mh. Bush wetu kwenye mchakato wa CCM)ni mmoja wa watu wanene pale IMMMA?

Lawrence Masha, ni mbunge wa Nyamagana Mwanza, sio Sengerema, na yes aliwahi kuwa patner pale IMMA, je kuna sheria iliyovunjwa mkuu?

15.0 Je, wajua Masha alipelekwa sengelema mahususi kumwengua Dr. Shija na kupanua wigo wa mtandao?

Masha, hakupelekwa Sengerema, kwanza aligombea ujumbe wa baraza la vijana mkoa wa Mwanza na kushinda, baadaye akagombea ubunge wa Nyamagana na kumtoa Mbunge wa zamani Mh. Kazi, kwa hiyo hayo ya Sengerema na Shija ni uongo wa mchana mkuu!

(This time Baba hakugombea lakini alipewa ulaji fulani japo sikumbuki lakini alisaidiwa na CCM, may be mbunge wa EA or else.

Dr. Kagya Masha, ni makamu wa mwenyekiti wa UDP ndiye baba wa Waziri Masha, yes aligombea bunge wa Afrika Mashariki na kuupata, eti kuna dhambi gani hapo au kuna kitu nina-miss?
 
Swala kubwa la wananchi ni hili hapa:-

Aliunda kamati kuchunguza ufisadi huo, kuchukuliwa hatua za sheria na fedha kurejeshwa na baada ya tume ya uchunguzi kukamilisha kazi, Rais Kikwete atawachukulia hatua waliohusika, alisema.

“…lakini kabla Tume haijawasilisha taarifa ya uchunguzi, Rais anaanza kubebeshwa lawama na shutuma nzito, kwamba anawalinda watuhumiwa na anashindwa kuwachukulia hatua za kuwapeleka mahakamani.


Kinachonishangaza hapa ni kwamba mbona vitu vinafanywa kinyume?....Kwa nini swala hili liwe na sheria tofauti na zile zinazotumika duniani kote kiasi kwamba neno Kuchukuwa hatua za Kisheria lina maana ya kutumia mahakama zetu. haiwezekani tume fulani ndiyo ipewe wajibu wa kuunda sheria mpya ambayo kwanza inakusanya fedha zilizoibiwa kisha ndio watuhumiwa wachukuliwe hatua na rais... hapa iko wapi nafasi ya mahakama ikiwa kamati ndio wakusanyaji wakitumia mwongozo wa sheira gani?.. kisha rais kuchukua hatua dhidi ya wahusika baada ya kurudishwa fedha hii pia ni sheria gani?
 
Naona Bwana Ngurudoto ama Kaiza Twalipo ameamua "kumwaga radhi" kabisa, katuonesha hadi uchi wake wa ubongoni na tumeona kilichopo ni EMPTY SET!

KITHUKI, SENTESI YAKO NI JINA + KASHFA + FISADI HAMNA ZAIDI!!! HUJUI KINGINE WEWE...
 
Jakaya hatufahamu kama ni Fisadi au laa. Lakini tuna maswali machache sana kwake.
1. Kwa nini Rostam Aziz alifinance kampeni ya Uraisi wa Mh. Kikwete kwa percentage kubwa sana?

2. Jee kwa nini alimuweka Lowasaa kuwa waziri mkuu wakati watanzania wengi walipinga swala hilo. Jee alisahau maneno ya mwalim J.K Nyerere kuhusu Lowassa.

3. Jee ni kweli Mh. Kikwete hafahamu kuhusu Richmond wakati best friend wake amemuoa mtoto wa mkurugenzi wa DOWANS. Jee ni kweli best wake akumwambia kuhusu kiini macho cha Richmond wakati best friend wake ni mkazi wa Houston, Texas. Na best wake alimkaribisha Gire kwenye moja ya shere za watoto wake. Jee kweli JK alikuwa hana habari kwamba Gire ni mpiga photocopy na sio mtaalam wa umeme?

4.Jee kwa nini Mh.J. Kikwete alimkingia kifua mmiliki wa mabasi ya Scandnavia limited pindi bank husika ilipotaka kufreez mali za mfanyabiashara huyo kutokana na kuchelewa kumake payment.

5.Jee kwa nini Mh. J.Kikwete hajaweka report ya enerst & Young mpaka sasa kwenye website ya Ikulu so kila mlipa kodi akaona jinsi fedha zetu zilivyofujwa.

6. Jee scandal ya kununua rada kwa million kibao haikufanyika wakati Mh.J. Kikwete akiwa mambo ya nje? Jee yeye alifanya nini kuwaarifu wananchi kwamba tumeliwa? Jee Mh.Jakaya Kikwete tangu alipoingia mdarakani amechukua atua gani kuhakikisha Pesa zetu za rada zinarudishwa, na waliohusika wanakwenda ndani.

7. Huu ni mwaka wa tatu tangu JK ameingia madarakani. Jee amefanya juhudi gani za kuwatia kizimbani waliofuja mali za serikali wakati wa awamu ya tatu. Watu kama Mkapa na mkewe mama Anna Mkapa, Sumaye, Daniel Yona, Basil Mramba na wengine wengi. Jee Jk amechukua measures gani kuretain our assets.

Sasa kabla hujaanza kumtetea kwamba JK ni safi please answer those questions. Sijasema Jakaya ni fisadi, lakini ninachosema ni kwamba, Jakaya hajaisaidia Tanzania kwa asilimia hata 10% mpaka sasa katika miaka 3 aliyokuwa madarakani. Haswa haswa yeye na team yake wametuingiza kwenye mtego wa Richmond, na mikataba hewe kupitia Karamangi.

I think Jakaya ana good personality, lakini we need more than boyz II men in the white house. Please stop Jakaya 2010.
 
Unajua mtu kama Chiligati na wana CCM wenzake wanazani watanzania wa leo ni kama wa enzi zile za Ujamaa na kujitegemea.

Hawajui ya kuwa watz wa leo ni wasomi na wako update.

Ifike wakati wajue fika kuwa siasa si suala la usanii tuu,kuburuza watu,it is a serious profession/displine unlike currently in Tz siasa imekuwa ni usanii leo mtu anasema iki kesho anaamka na kile-hopeless.

Nani asiyejua mkuu wa kaya ni fisad!!!!!!!!!!!???????????

Labda waseme tusahau yaliyopita na tugange yajayo tena kwa kuomba msamaha sio ivi ivi tuu-hopeless.Alafu mtu mweneyewe ni Kampteni wa jeshi analeta ubabe wa jeshi kuforce watu kuelewa somo la kichina apa!!!!!!!!!! ebo...........wanaccm mgeuke mjue mnadeal na watu wenye akili zao timamu
 
POINT BLANK-EPA scam: Those returning the loot should be arrested soonest

Nkwazi
THIS DAY

IF anything, small draughts read revelations of nonsensical and suicidal deals that thieves behind economic profligacy by so-called thieves are returning the External-Payment-Account loots to the Bank of Tanzania.

It is said they are doing it secretly, the mighty power-that-be, this should read the central bank, is receiving the money returned silently! Surely, such action is shameful, to say the least.

It is a cardinal sin in the first place! Some are saying. But may I ask you folks: Do you want the power-that-be to burn their own fingers? I say nay, nobody is ready to kill his own kids.

One person has sarcastically said ’’ Under any law under the sun this is but bloody theft even if it is committed by the high and mighty. How can the power-that-be commit such a financial sacrilege so to speak? I have heard that they have suspended the chief architects of this scam. But they have not hauled them to court.

Today I am not saying much. After gulping some liquor I have the temerity to say: ’’What adds up to this abracadabra is the fact that even the names of the thieves behind this crime are being concealed? So too is the amount and the dates of return of the cash! Gosh!

’’If this is the murky way we are doing things, time will come when the culprits will iron out things with their victims! If not they too will be suspended in lieu of being brought to book! This looks like jungle justice per excellence!’’

Who are those being concealed? One is tempted to ask: Are they a government within a government? JK told us point blank: His is a government purely made by him. No allies. No shareholders, even us, the stakeholders.’’

’’If what JK said was right, and we have no reason to doubt him for, after all he is at the helm of our country. Then where does this returned loot come from? Was it hidden under various mattresses or pots, awaiting things to cool down before it was taken back to the bank in Tanzania or in off-shore banks?

Another Bongoman says ’’The braggarts behind the curtains are big men and women with big influence in the power-that-be circles. But let’s face it single-handedly: How long will this deceit last if at all we want to know everything?’’

Let me put it point blank. I am not supporting these EPA undertakings altogether. Phew! Stop dilly-dallying and arrest those who are returning our money soonest.’’

Today things are hotter. Bettie the liquor seller says: ’’Return our money. Those implicated must face the music along with forfeiture of their ill-gotten property. Because they have committed a sin.

Bettie, the liquor seller, keeps saying: ’’We still need Ballali, the ex-BoT governor, to face the music as well. We shall never stop making loud noises so that he lands in the cooler once proven guilty.’’

She adds point blank. ’’If I got it right, I remember. The president has been asking us to help him by producing the names of the corrupt fellows in our midst. Now those behind EPA scam are known, what else is the president waiting for?’’

As Bettie pauses to quaff a little bit, Vyombo adds: ’’Does he philosophically mean we should go and attack them wherever they are in our republic? It can’t be!’’

Such behaviour would only create chaos in our country that is famous for keeping law and order.

As our meeting was about to delve deeper into EPA’s looting, the police stormed in to arrest us for drinking bootleg liquor instead of pursuing EPA’s looters using techniques they learned from Scotland Yard or the Federal Bureau of Investigation!

nkwazigatsha@yahoo.com
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom