CCM yashikwa kigugumizi kutoa maamuzi walioiba BoT

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994

Posted Date::3/31/2008

CCM yashikwa kigugumizi kutoa maamuzi walioba BoT

* Suala la mwafaka labaki kitendawili

* Yatumpia lawama Maalim Seif

* JK abaki na siri yake moyoni

Na Theodatus Muchunguzi, Butiama
Mwananchi

HALMASHAURI Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) , imeshindwa kutoa maamuzi mazito kama ilivyotarajiwa na Watanzania, kuhusiana na matukio yaliyotokea nchini hivi karibuni, ikiwamo kuwashugulikia wanachama wake, wanaohusishwa na kashfa ya ufisadi.

Vilevile, imeshindwa kushughulikia Muafaka wa kiasiasa visiwani Zanzibar baina ya ya CCM na Chama cha Wananchi (CUF) na badala yake, imerudisha mjadala wake kwa wananchi ili waweze kuamua kwa kupiga kura za maoni.

Watanzania wengi walikuwa na shauku na matumaini kuwa kikao cha NEC kilichofanyika Kijiji cha Butiama, alikozaliwa Baba wa Taifa, Hatati Mwalimu Julius Nyerere kuanzia Jumamosi hadi Jumapili iliyopita usiku, kingetoa maamuzi makubwa na muhimu kama hatua ya kujisafisha kwa umma, kutokana na kashfa hiyo kwa baadhi ya viongozi wake na wa serikali.

Baadhi ya kashfa hizo, ni ya kutoa zabuni kwa upendeleo kwa kampuni hewa ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond na kuisababishia serikali hasara ya mamilioni ya fedha.

Kashfa hiyo ilimlazimisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu na kufuatiwa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Afrika Mashariki , Dk Ibrahim Msabaha, Februari 7, mwaka huu, wakati wa kikao cha bungeni kilichofanyika mjini Dodoma.

Lowassa ni mjumbe wa NEC na alikuwa mjumbe wa Kamati Kuu kwa wadhifa wake wakati Karamagi ni mjumbe wa NEC wa Mkoa wa Kagera.

Suala lingine ambalo lililokuwa linasubiriwa kwa hamu kuamuliwa na NEC ni kuhusu makubaliano ya mwafaka baina ya CCM na CUF yaliyofikiwa hivi karibuni, baada ya kudumu kwa takribani miaka miwili chini ya makatibu wakuu wa vyama hivyo, Yusuf Makamba na Maalim Seif Sharrif Hamad.

NEC , pia ilisubiriwa kwa hamu, kuamua na kupitisha azimio kuhusu hoja ya kutaka kutenganisha shughuli za biashara na uongozi ikiwa ni hatua ya kudhibiti ukiukaji wa maadili ya uongozi, lakini haikufanya hivyo.

Akisoma tamko la kikao cha NEC kwa wajumbe wake na waandishi wa habari baada ya kumalizika majira ya saa 5:00 usiku juzi katika ukumbi wa Mikutano wa Joseph Kizurira Nyerere, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, alisema halmashauri hiyo, iliyakubali kimsingi mapendekezo yaliyomo katika taarifa ya mazungumzo ya muafaka baina ya makatibu wakuu hao.

Hata hivyo, alisema NEC imeazimia kuwa, ikiwa makubaliano hayo yatakubaliwa, yataleta mabadiliko makubwa katika mfumo wa utawala wa Zanzibar na kwa kuliangalia jambo hilo ni lazima wananchi wote wa Zanzibar washirikishwe kuamua kwa kura ya maoni.

Kutokana na hali hiyo, NEC imeigiza kamati ya muafaka ya CCM kurejea tena katika mazungumzo na wenzao wa CUF, ili kuamua jambo hilo.

Hata hivyo, tamko hilo limesema kuwa, NEC imesikitishwa na tabia ya CUF ya kutangaza makubaliano hayo kinyume na makubaliano kati ya vyama hivyo kwa kuwa lilitakiwa kufanywa kwa pamoja baada ya kufikia mwisho.

Kauli hiyo ya kukilalamikia CUF, imetokana na uamuzi wa Hamad kutangaza baada ya mazungumzo ya mwafaka kukamilika kuwa miongoni mwa mambo yaliyokubaliwa katika mazungumzo yao ni mgawanyo wa madaraka, kwa chama kitakachoshinda uchaguzi kuchukua nafasi ya urais na kingine wadhifa wa waziri kiongozi.

Wakati Hamad anatangaza makubaliano yaliyofikiwa kuhusu mwafaka, CCM kilisema suala hilo lingepelekwa katika kikao cha NEC kupata baraka na ni miongoni mwa ajenda zilizoandaliwa.

Kuhusu azimio la kutenganisha shughuli za biashara na siasa, NEC imeagiza serikali zote mbili kutunga sheria ya kufanya hivyo t kwa viongozi walioko ndani ya vyombo vya dola.

“Utaratibu wa kuchanganya nafasi za uongozi na biashara umekuwa ni chanzo cha migongano ya kimaslahi, na ukiukwaji wa maadili na miiko ya uongozi, hivyo Halmashauri Kuu ya Taifa imeazimia kuondoa upungufu huu, ” ilieleza sehemu ya tamko hilo na kusisitiza kuwa:

“ Halmashauri Kuu ya Taifa imezingatia kwamba uongozi katika chama si kazi ya kujipatia riziki, japo zipo baadhi ya kazi za uongozi zenye mishahara; hivyo imesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba kiongozi wa chama lazima awe na shughuli halali inayompatia kipato cha kuendesha maisha."

Tamko linaitaka CCM ijiimarishe katika taswira yake ya asili kama chama chenye viongozi waadilifu, kinachojali maslahi ya watu na hasa jukumu lake la kutetea wanyonge.

Msekwa, alisema viongozi watakaobainika kuvunja miiko ya uongozi wachukuliwe hatua mara moja na Kamati za Maadili za ngazi zote zitekeleze majukumu yake ipasavyo na kwa nguvu mpya.

Kikao cha NEC hakikutoa tamko lolote kuhusu hatua za kinidhamu dhidi ya watuhumiwa wa kashfa ya Richmond. Badala yake tamko hilo limesema halmashauri hiyo kwa kuzingatia hoja zilizojadiliwa bungeni kutokana na taarifa ya Kamati Teule iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe, imeona wananchi wanachukia maovu, hususan wizi, ubadhirifu na rushwa miongoni mwa viongozi na watumishi wa umma.

“Hivyo basi, Halmashauri Kuu ya Taifa imewasisitiza viongozi wa chama na serikali wasiwe sehemu ya maovu, kufanya hivyo kunajenga chuki kwa chama na serikali zake. Aidha, zichukuliwe hatua thabiti kupambana na maovu katika jamii mara yanapojitokeza.

Pamoja na hayo, NEC imesisitiza kuwa Bunge kama chombo cha kusimamia serikali katika utendaji wake, halina budi kuwa mstari wa mbele kukemea maovu yaliyofanywa na viongozi, watumishi wa umma na vyombo vya umma.

Msekwa aliongeza kusema kuwa, halmashauri hiyo imesisitiza kuwa, mfumo, utaratibu na madhumuni ya kuwapo kwa Kamati ya Wabunge wote wa CCM yazingatiwe na itumike kuzungumza na kuelewana hasa kuhusu masuala makubwa yanayowasilishwa Bungeni.

Tamko halikuzungumzia chochote kuhusu kashfa kuhusu ufisadi wa wizi wa Sh 133 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Wakati Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakata Kikwete akitangaza kumalizika kwa kikao hicho na kuwaita waandishi wa habari kuingia ukumbini kusikiliza tamko, wajumbe wa NEC walilipuka kwa nyimbo za kukisifia chama hicho na Kikwete.

Kikwete aliufunga mkutano huo kwa kuwaeleza wajumbe kuwa watakutana Mei, mwaka huu, kujadili jambo alilosema ni la siri aliyowaeleza Jumamosi. Hata hivyo hakufafranua.
 
Nilikuwa nimejiandaaa kumpigia bonge la debe Kikwete hapa JF, yaani kama angemtosa Chenge, Rostam, Mkono na mafisadi wengine kwa kutumia rungu la chama (kama ilivyokuwa inafanyika miaka ya nyuma kabla sijazaliwa) basi angepata my full support hapa JF.

Nilikuwa nimejiandaa na kupambana na kina Balile ambao kazi yao ni kujaribu kusafisha wale wanafukuzwa kazi kwa ufisadi (kama EL na wenzake). Kikwete umeniangusha buddy! sijui tena utapata wapi nafasi kama wakati hauna tena time out iliyosalia kwenye hii game
 
Hivi CCM ndio inawashughulikia hao mafisadi wa BOT au vyombo vyetu ambavyo havina chama vilivyoundwa kutokana na katiba yetu,yaani ni ubabaishaji kila kitu!
 
My question is...who paid for Prof. Ndullu's expenses to go to Butiama to address CCM while some of the people who stole from his institution were just sitting in the very same meeting? Is it CCM? Is it BOT?

Although I don't intend to answer my own question, it seems as though taxpayers' money was used which increase my impatience to CCM and JK. I'm trying to imagine if Hon. Mbowe and CHADEMA decide to have their meeting at Mtei's or Makani's birthplace and summon the governor...not going to happen, unless, of course, governor Ndullu proves me wrong!
 
Waungwana,

Nyeti nilizopata zasema kuwa Wajumbe wa CCM na baadhi ya watendaji walitaka hiki kikao cha "kumfunda" Ndulu kuwafunda CCM kuhusu mwelekeo wa Uchumi kilipiwe na BOT!

Wajanja walidai eti kwa kuwa BOT ndio facilitator wa Seminar, basi BOT I-foot expenses zote pamoja na mapochopocho.

Jambo hili lilipowasilishwa kwa "Beno" Gavana Ndulu akawauliza "jamani BOT zichotwe mara ngapi...?"

Kwa wale waliokuwa wakidai kuwa Ndulu anawajibika kwenda Butiama kuhutubia, tafakarini kilichotakika kufanyika, BOT ilipie gharama za Sinema (sic) ya Kufundana!
 
Mie nilisema tangu mwanzo, mwizi atamkaripiaje mwizi mwenzake? Serikali ya huyo JK ilitanganzia wananchi kuwa wasinunue mali za MAFISADI maana ziko njiani kutaifishwa. Tukasikia kuwa ime-freeze bank accounts za wana ndugu 2. Sasa leo hii ndani ya chama chake anadiriki kuwatangazia MAFISADI wenzake kuwa wasiwe na wasiwasi kwani Chama na serikali yake hawana nia wala mpango wa kutaifisha mali zao. Sasa hii siyo double standard?????? Yaani hiki chama kimejaa usanii tele tena ule wa MKWEPU. Hakuna cha kumuenzi Mwl wala nini, nyie SISIEMU ni MA-FISI WALAFI. Yaani mnanitia hasira S**~@#** zenu. Watanzania inabidi tuwakomalie hawa walafi ili wasipate tena kura.
 
Mie nilisema tangu mwanzo, mwizi atamkaripiaje mwizi mwenzake? Serikali ya huyo JK ilitanganzia wananchi kuwa wasinunue mali za MAFISADI maana ziko njiani kutaifishwa. Tukasikia kuwa ime-freeze bank accounts za wana ndugu 2. Sasa leo hii ndani ya chama chake anadiriki kuwatangazia MAFISADI wenzake kuwa wasiwe na wasiwasi kwani Chama na serikali yake hawana nia wala mpango wa kutaifisha mali zao. Sasa hii siyo double standard?????? Yaani hiki chama kimejaa usanii tele tena ule wa MKWEPU. Hakuna cha kumuenzi Mwl wala nini, nyie SISIEMU ni MA-FISI WALAFI. Yaani mnanitia hasira S**~@#** zenu. Watanzania inabidi tuwakomalie hawa walafi ili wasipate tena kura.

Nguvu zimeniishia kabisa kama maneno ya Kishoka na Indume ni kweli basi tuna hali mbaya sana .Lakini CCM wanadhani wataendelea namna kama wanadhani hivyo basi ni kosa kubwa .
 
Kutoa Maamuzi Ni Wajibu Wa Serikali Sio Chama Cha Mapinduzi

Serikali Yenyewe Ya Watanzania Imeshindwa Kutoa Maamuzi Sasa Ndio Ccm Ijiingize Kati ? Hiyo Haiwahusu Wao Wanadeal Na Mambo Yanayohusu Chama Cha Mapinduzi
 
Kutoa Maamuzi Ni Wajibu Wa Serikali Sio Chama Cha Mapinduzi

Serikali Yenyewe Ya Watanzania Imeshindwa Kutoa Maamuzi Sasa Ndio Ccm Ijiingize Kati ? Hiyo Haiwahusu Wao Wanadeal Na Mambo Yanayohusu Chama Cha Mapinduzi
Nina mashaka sana na uwezo wa ubongo wako Shy ! maana hata kama ni kununuliwa mh! huku kwako kumezidi hata ule utii kwa Mume
 
Waungwana,

Nyeti nilizopata zasema kuwa Wajumbe wa CCM na baadhi ya watendaji walitaka hiki kikao cha "kumfunda" Ndulu kuwafunda CCM kuhusu mwelekeo wa Uchumi kilipiwe na BOT!

Wajanja walidai eti kwa kuwa BOT ndio facilitator wa Seminar, basi BOT I-foot expenses zote pamoja na mapochopocho.

Jambo hili lilipowasilishwa kwa "Beno" Gavana Ndulu akawauliza "jamani BOT zichotwe mara ngapi...?"

Kwa wale waliokuwa wakidai kuwa Ndulu anawajibika kwenda Butiama kuhutubia, tafakarini kilichotakika kufanyika, BOT ilipie gharama za Sinema (sic) ya Kufundana!

Kikwete anaweka historia ya incompetence katika nafasi ya juu kabisa ya uongozi wa nchi. By the time this guy anamwogopa MUNGU na kuamua kuachia madaraka basi hiyo nchi itakuwa inahitaji the whole new make over of the presidency!

Aibu tupu huko state house!
 
Nilikuwa nimejiandaaa kumpigia bonge la debe Kikwete hapa JF, yaani kama angemtosa Chenge, Rostam, Mkono na mafisadi wengine kwa kutumia rungu la chama (kama ilivyokuwa inafanyika miaka ya nyuma kabla sijazaliwa) basi angepata my full support hapa JF.

Nilikuwa nimejiandaa na kupambana na kina Balile ambao kazi yao ni kujaribu kusafisha wale wanafukuzwa kazi kwa ufisadi (kama EL na wenzake). Kikwete umeniangusha buddy! sijui tena utapata wapi nafasi kama wakati hauna tena time out iliyosalia kwenye hii game


Pole sana dada yangu ila niliposoma matarajio yako na mama yako kuhusu kikao cha Butiama nilifikiri kuwa hamukuona campain ya Kikwete gharama ilizotumia ambazo zilikuwa bilioni za kutosha.Kwa kifupi pesa zalizochotwa BOT zinamuhusu yeye kwa kiasi kikubwa na ndio yeye aliyetoa mwanya kwa wengine kuchota nao kivyao .Haya ndio maneno yaliyosemwa na Mwl.kwamba "mtu anatumia pesa kwenye uchanguzi kazipata wapi?kama kakopa atazilipaje lipaje?"
Sifa moja ambayo Rais anatikiwe awenayo sasa hivi ni kwamba awe kama dume la nyani achore mstari kwamba kama yaliyotoke anashitwa ku rectify kwa kuwa na yeye yumo,basi awaambie vijana wake no more mess no more drama na amaanishe hivyo.Ikulu si mahala pa mzaha wala kuiza sura.
 
Hivi vyama vya upinzani haviwezi kushirikiana na kuishitaki Serikali na pia kufungua madai ya Katiba katika mahakama ili kieleweke kwani kwenda nao majukwaani inaweza ikachukua miaka nenda miaka rudi na wao wanapokezana vijiti tu. Yaani hio Mei Mosi anayoingojea Mh.Kikwete hata isifike serikali yake ipandishwe kizimbani .
 
Tusishangae kigugumizi cha CCM

Moja wa wezi wa Account ya EPA ni CCM kama chama.

Sijui ni vipi mkutano wa CCM unaweza tangaza wezi wa BOT wakati kitendo hicho ni sawa na kujisomea hukumu ya kifo?

CCM wameiteka kazi ya Polisi,uzuri wa utekaji wa kazi isiyo wahusu ni mmoja, imewashinda kuitekeleza.

Kwanza si kazi ya chama kutangaza wezi wa aina yeyote ile hata kama wezi hao wameiba fedha za account za CCM yenyewe.

Pili kupeleleza na kutangaza matokeo ya upelelezi wa wizi wowote ule ni kazi ya Polisi.

CCM siyo polisi wala serikali.

Kama nilivyo wahi kusema hapo awali kwamba kabla ya 2010 tutashuhuduia mengi na shuhudio la mwisho likiwa ni anguko kuu la CCM katika uchaguzi wa wabunge.

Nyufa zinazo tokea ndani ya CCM ni muhimu sana kwa maendeleo ya uchumi wa taifa.
Nyufa pekee yake kamwe hazibomoi nyumba ila zinaifanya nyumba dhaifu dhidi ya dhoruba yeyote, hata dhoruba ndogo kama ya kimbunga cha ngoma ya mdundiko.

Ni vizuri kwetu Watanzania kwamba CCM wanaendelea kujidanganya kwamba ni wamoja na umoja wao una nguvu ya kulinda wezi, wanyang'anyi na wauaji.

Umoja huu dhaifu wa CCM ukiendelea hadi wakati wa uchaguzi utasaidia kuleta mabadiliko ya kweli endapo vyama vya upinzani vitautumia udhaifu huo vizuri.

Watanzania ni vema wajifunze matukio ya Kenya na kujenga umoja wa kitaifa dhidi ya wezi na wauaji hawa, yaani CCM.

Umoja ni umoja tu.

Kumbuka, Wazungu wa Ulaya wenye nguvu na maarifa kuliko sisi wanaungana na kuleta umoja wa nchi za ulaya.Wazungu hawa waliwahi ungana zamanai kugawana bara la Afrika na kulitawala kwa karibu karne nzima. Sasa wanaungana kujenga taifa moja kubwa lenye nguvu nyingi mno za ajabu zitakazo shinda taifa kubwa la Marekani.

Watu wenye nguvu wanaungana, sisi tusio na nguvu tunang'aa macho na kushindwa kuungana kudai haki hata pale tunyang'anywapo tonge mdomoni.

Sasa tuna sababu za kuungana kuking'oa CCM madarakni kuliko wakati wowote ule katika historia ya nchi yetu.

Kwa sababu Chama tawala kimeanza kujaa nyufa hadi sehemu nyeti ni vema wananchi tujiulize mara mbili je kuna umuhimu wowote wa kuendelea kukihifadhi chama hiki chenye kila dalili za kufa?

Mmoja wetu angefanikiwa kuipata taarifa ya uchunguzi wa BOT na list ya wezi wote wa BOT, na hasa Waheshimiwa Mawaziri wakurugenzi wa wizara makatibu na watendaji wakuu wengine wa chama na serikali, na kuimwaga hapa jamvini JF, basi Vibwengo wote wa CCM ni lazima wangejitafuna ndimi na mikia yao hadi wajimalize.
 
Kikwete anaweka historia ya incompetence katika nafasi ya juu kabisa ya uongozi wa nchi. By the time this guy anamwogopa MUNGU na kuamua kuachia madaraka basi hiyo nchi itakuwa inahitaji the whole new make over of the presidency!

Aibu tupu huko state house!


Ni uozo mtupu kuanzia JK, Makamba, Msekwa, Pinda na wengineo wote walio chini yao. Hivi huko hakuna mtu hata wa kuwashtua jamani tunavyofanya sivyo!? Nchi inaelekea kubaya tugeuze huu mwelekeo kwa manufaa ya Watanzania na badala ya kuendelea kuwakumbatia mafisadi na wahuni ndani ya chama na sirikali? Duh!
 
Mmoja wetu angefanikiwa kuipata taarifa ya uchunguzi wa BOT na list ya wezi wote wa BOT, na hasa Waheshimiwa Mawaziri wakurugenzi wa wizara makatibu na watendaji wakuu wengine wa chama na serikali, na kuimwaga hapa jamvini JF, basi Vibwengo wote wa CCM ni lazima wangejitafuna ndimi na mikia yao hadi wajimalize.

Tafuteni huu muziki tuucheze hapa. Pia kuna nyeti kwamba ripoti ya ukaguzi ilichezwa na mkaguzi wa sirikali, si mnakumbuka alikaa nayo kipindi eti alikuwa akiifanyia mchakato. Wanaogopa kuiweka hadharani maana Ernst & Young wataulizwa je hii ndiyo ripoti yenu mliyoiandika? Jibu likiwa hapana basi kitakuwa ni kizaa zaa kingine kwa hii siri kali isiyokuwa na credibility yoyote kwa Watanzania na pia kwa nchi wafadhili.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom