engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Haya tena kamati ya siasa ya mkoa wa DSM imemwomba Dr. Magufuli kuwaomba radhi wananchi wa DSM kuwa kauli yake ni ya kuwadharau wananchi.
=======
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dar es Salaam kimemtaka Waziri wa Ujenzi, John Magufuli aache kufanya kazi kwa jazba, dharau na maneno ya kejeli.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, alisema jana kuwa hawakufurahishwa na lugha ya kibabe aliyotoa Magufuli alipozungumzia sakata la kupanda kwa nauli za kivuko cha Kigamboni.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Guninita alisema kuwa kauli aliyoitoa Magufuli kwa mbunge wa Kigamboni Faustine Ndungulile na wananchi ya kuwataka kupiga mbizi na kwamba mbunge wa Kigamboni kama anawaonea huruma wananchi anunue boti itakayoitwa kwa jina lake au chama chake ni kauli inayotia hofu na inaweza kupoteza wanachama, na chama hicho kimkoa kimemtaka awaombe radhi wananchi kutokana na kauli yake hiyo.
“Kuna haja viongozi wachague kauli ya kusema na sheria zimetungwa na kutengenezwa na watu na zinazungumzika, ukifananisha vivuko vya Ziwa Victoria na hiki cha Kigamboni ni tofauti kubwa na neno ‘marufuku’ si neno jema hivyo ni busara kuomba radhi,” alisema Guninita.
Guninita alisema kauli hiyo ya Magufuli haijengi mshikamno na ushirikiano kati ya viongozi wa CCM, serikali ya mkoa na wananchi, na kwamba kama malalamiko ya wananchi hao hawezi kuyasikiliza, asingetumia maneno aliyoyasema.
Aidha Guninita alisema kuwa CCM mkoa wa Dar es Salaam, imeipokea kwa masikitiko kauli hiyo na imewaomba wananchi kuwa na subira wakati uongozi wa chama ukiendelea na jitihada za kuzungumza na serikali ili kutatua tatizo hilo kwani umesikia kilio chao cha kupanda kwa nauli na unawathibitishia kutatua tatizo hilo.
via Tanzania Daima
==========
My Take:
Mimi ninavyoelewa kazi za kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya CCM ya mkoa ni hizi hapa
1. Kutoa uongozi wa siasa ktk mkoa
2. Kueneza itikadi na siasa ya CCM ktk mkoa
3. Kuandaa mikakati ya kampeni za uchaguzi na kampeni nyinginezo ktk mkoa
4. Kusimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za CCM na maamuzi yote ya CCM chini ya uongozi wa H/ KUU ya CCM MKOA
5. Kupanga mipango ya kukipatia chama mapato,kusimamia kwa dhati utekelezaji wa mipango hiyo,kudhibiti mapato na kusimamia matumizi bora ya fedha na mali za chama ktk mkoa
Sasa hili tamko lao la kumtaka Waziri wa Ujenzi aombe radhi mbona si moja ya kazi zilizopo hapo juu?
Kazi ipo jamani
Siasa ktk kazi hadi lini?
=======
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dar es Salaam kimemtaka Waziri wa Ujenzi, John Magufuli aache kufanya kazi kwa jazba, dharau na maneno ya kejeli.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, alisema jana kuwa hawakufurahishwa na lugha ya kibabe aliyotoa Magufuli alipozungumzia sakata la kupanda kwa nauli za kivuko cha Kigamboni.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Guninita alisema kuwa kauli aliyoitoa Magufuli kwa mbunge wa Kigamboni Faustine Ndungulile na wananchi ya kuwataka kupiga mbizi na kwamba mbunge wa Kigamboni kama anawaonea huruma wananchi anunue boti itakayoitwa kwa jina lake au chama chake ni kauli inayotia hofu na inaweza kupoteza wanachama, na chama hicho kimkoa kimemtaka awaombe radhi wananchi kutokana na kauli yake hiyo.
“Kuna haja viongozi wachague kauli ya kusema na sheria zimetungwa na kutengenezwa na watu na zinazungumzika, ukifananisha vivuko vya Ziwa Victoria na hiki cha Kigamboni ni tofauti kubwa na neno ‘marufuku’ si neno jema hivyo ni busara kuomba radhi,” alisema Guninita.
Guninita alisema kauli hiyo ya Magufuli haijengi mshikamno na ushirikiano kati ya viongozi wa CCM, serikali ya mkoa na wananchi, na kwamba kama malalamiko ya wananchi hao hawezi kuyasikiliza, asingetumia maneno aliyoyasema.
Aidha Guninita alisema kuwa CCM mkoa wa Dar es Salaam, imeipokea kwa masikitiko kauli hiyo na imewaomba wananchi kuwa na subira wakati uongozi wa chama ukiendelea na jitihada za kuzungumza na serikali ili kutatua tatizo hilo kwani umesikia kilio chao cha kupanda kwa nauli na unawathibitishia kutatua tatizo hilo.
via Tanzania Daima
==========
My Take:
Mimi ninavyoelewa kazi za kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya CCM ya mkoa ni hizi hapa
1. Kutoa uongozi wa siasa ktk mkoa
2. Kueneza itikadi na siasa ya CCM ktk mkoa
3. Kuandaa mikakati ya kampeni za uchaguzi na kampeni nyinginezo ktk mkoa
4. Kusimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za CCM na maamuzi yote ya CCM chini ya uongozi wa H/ KUU ya CCM MKOA
5. Kupanga mipango ya kukipatia chama mapato,kusimamia kwa dhati utekelezaji wa mipango hiyo,kudhibiti mapato na kusimamia matumizi bora ya fedha na mali za chama ktk mkoa
Sasa hili tamko lao la kumtaka Waziri wa Ujenzi aombe radhi mbona si moja ya kazi zilizopo hapo juu?
Kazi ipo jamani
Siasa ktk kazi hadi lini?