CCM yampongeza Richard

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,338
12,904
Nimeipa heshima Tanzania - Richard

2007-11-13 09:33:15
By Fred Ogot, Johannesburg


Richard Bizubenhout ameeleza anafurahia kuipa heshima Tanzania katika medani ya kimataifa baada ya kuibuka kidedea kwenye shindano la televisheni la Big Brother Africa 2 lililomalizika hapa, juzi usiku.

Akizungumza na waandishi wa habari, Richard alisema ushindi huo haukuwa wake pekee bali sifa ilikuwa inapaswa kwenda kwa Watanzania wote.

Kwa ushindi huo aliweza kuondoka na kitita cha Dola 100,000 (zaidi ya Sh. milioni 100). Aliweza kuwapiku mshiriki kutoka Nigeria, Ofuneka na mrembo kutoka Angola, Tatiana waliofanikiwa kuingia fainali.

Ofuneka ndio alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kushinda na kuambulia nafasi ya pili na Tatiana anayesadikika kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Richard, alikamata nafasi ya tatu.

``Kwa kweli ninajivunia sana ushindi na hasa Watanzania waliochangia kura za ushindi wangu,`` alisema Richard kwenye mkutano na waandishi.

Pia aliomba radhi kama kuna watu wowote aliowakosea katika kipindi chote alipokuwa akishiriki kwenye Big Brother.

Watu wengi walifika kwa ajili ya kumshangilia Richard, akiwamo Dada yake, Linda na Kaka Louis.

Alipoulizwa kuhusiana na uhusiano na mpenzi wake Tatiana alijibu; ``Ninampenda na nitamwoa ikiwa nitavunja ndoa na mke wangu. Ninasikia amerejea kwao Canada, sijui kitu gani kimetoa,`` alieleza.

Kuhusiana na milioni 120, alizopata alidai kuwa anajipanga kuanzisha kampuni ya kutengeneza filamu.

Alisema pia atatafuta watu wa kumshauri kuweza kutumia fedha hizo.

Washiriki wengine walikuwa Max (Zambia), Kwaku (Ghana), Jeff (Kenya), Justine (Botswana), Moureen (Uganda), Code (Malawi) na Bartha (Zimbabwe).

Wakati huo huo, Chama cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza Richard kwa kufanikiwa kulivaa taji la Big Brother.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati ilisema kuwa ushindi huo ulitokana na malezi mazuri wanayopata vijana wa Kitanzania na hasa kwa kuzingatia sera nzuri za CCM.
SOURCE: Nipashe
 
ccm inaupora ushindi wa richard na kuufanya wake mbona haiwafanyii hivyohivyo mamiss wakirejea missworld? huu ni unyanyapaa na kujikweza. ukifilisika kifikra unakuwa kama gari bovu kilimani....
 
Haya sasa,ina maana hta wale waliokua wanamponda Rich kwa uzinzi pia hili nalo walitupie macho kwani kama Rich alipata huo ushindi kwa Uzinzi it means CCM ndio zaidi kwa kujifunga kibwebwe kumshangilia.Wabongo tuacheni unafiki na unazi.

Mbona hawa watu wanajua kudandia kila kitu? Kwa hiyo hata mamiss wote waliofail miss world ni sera mbovu za CCM,taifa stars sina hakika kama bado wanbatambulika kama JK boys au la,na njaa inayowakabili wahadzabe pia ni matokeo ya sera za CCM au sio?

Umaskini wetu uliokithiri unatokana sera za wapinzani au? Chama kilichoongoza kwa miaka 45 huku tukipigwa bao kiuchumi hata na nchi zilizokua kwenye vita kama Rwanda,Burund na Uganda iliyoporomoshwa kiuchumi na utawala wa Dikteta asiyekua na elimu Idd Amini leo hii wanatupita kiuchumi si aibu tupu na kinyaa ?

Kama tunaweza kukubaliana kwenye hayo mambo hapo juu basi dhamira ya CCM kumpongeza Rich ni ya kweli

Rich hongera kwa kuipeperusha bendera ya Tanzania bora uinvest hizo hela utoe ajira kwa vijana wetu umaskini huu upungue.Hao vilaza waaache kujigamba sasa wajafdili mambo ya msingi.Sasa wasiache kuijadili Richmond leo,waanze kufikiria kukupokea na kukuita bungeni.

Itakua tusi kwetu sisi wananchi
 
Huu ni upumbavu kabisa, yaani anapongezwa kwa kuonyesha uwezo wake wa kufanya ngono hadharani? Hii BBA ni upuuzi ambao tumeuiga kutoka nchi za Magharibi kwa hiyo Watanzania na Waafrika kwa ujumla hakuna kitu cha maana tunachojifunza hapo.

Bora mamiss wetu angalau wana nidhamu kwenye mashindano yao
 
Nchi hii inaongozwa na CCM, ushindi wa mtanzania yeyote ni WETU.

CCM hoyeee kwa malezi bora!
 
Mhh,hii sasa inaonyesha dalili za ccm kufa kwani kama hata Chiligati niliyekuwa namwona yuko serious na ana tofauti kubwa na Makamba kumbe ni wale wale tuu.

Nampongeza Richard, ila kuna haja ya kubadilisha mtindo wa kufanya mashindano hayo kwani hakuna utamaduni wa kitanzania unaosema kuwa watu wawili wanaume na mwanamke wakae pamoja na kuoga pamoja tena mbele ya hadhara , kama haya ndio malezi ya ccm tuendako kamwe hatutafika.

Pili ,hakuna utamaduni wa kufanya ngono hadharani hapa Tanzania, kama hayo ndio malezi ccm inataka yaigwe na kila mtanzania tunakwenda kuua taifa hili.

Tatu, kumbe CCM haina dhamira ya kupambana na ukimwi, kwani ingewataka waandaaji wa BBA kuwapima kwanza washiriki ndipo wawekwe na kuruhusiwa kufanya ngono na huwa sijawahi kumwona mmoja wao akiwa na kondom ama akiulizia kondomu hata siku moja ,kama hayo ndio malezi ya ccm basi Tanzania bila ukimwi kamwe haiwezekani.

Hongera Richard, ila usimtese mkeo na familia yako kwa sababu ya kupata milioni mia ,kwani hiyo itakuwa ni laana kwako na hizo pesa pia, mtafute mkeo na umwombe radhi naamini ni binadamu na ataweza kukusamehe.
 
Na kesho atakapokuja atapokelewa na waziri, kisha akiwa kwenye gari la wazi atapelekwa ikulu kupumzika. Yote hayo ili vibaka wasipate nafasi ya kuzifikia dola zake mia.

Kisha watampa pongezi kwa kuzingatia malezi bora ya CCM yaliyomuondolea mtu hofu, hadi kuvua nguo mbele ya kamera na dunia ikishuhudia.

Kidumu chama cha mapinduzi!
 
huyu kijana anaonekana amateur sana kwenye issue kama sio kila kitu...eti nitamwoa tatiana kama mke wangu akiniacha na hana huruma kabisa kwa mke wake,nafikiri ni puppy love inamsumbua lakini kama mama wa kizungu kakasirika na jamaa atarudi Canada one sure thing i know he is goin to pay heavy price kwa huyo mzungu kutokana na hiyo humiliation aliyomfanyia mke wake
 
I don't want to be speculator, lakini huyu kijana uwezo wa mawazo unaonyesha mdogo sana. Yaani unasema kama utamuacha mkeo then utaowa kimada.... what kind of nonsense? you can't manage family affair will you be able to manage business. give me a brake.
 
Ashakum si matusi , hivi yakifanyika mashindano ya porno na yakatangazwa vizuri na vyombo vikubwa vya habari hapa duniani , na ikatokea bahati mtanzania akashinda jee vyama vya siasa hapo nchini vitampongeza ?

Ni hilo tuu by the way mwenye macho aambiwi ...
 
Nchi hii inaongozwa na CCM, ushindi wa mtanzania yeyote ni WETU.

CCM hoyeee kwa malezi bora!

i love this! ni vizuri kumiliki ushindi na kujivunia ushindi wa chama chetu. Kwa vile mambo yote mazuri lazima yahusishwe na CCM kama tulivyoifunga Burkinabe.. naona ni vizuri kuufurahia ushindi huu kama ushindi wa chama tawala na tabia iliyoonesha na kijana huyo kama malezi ya CCM.

Tunapomiliki mafanikio ya namna hii ni lazima tuwe tayari kumiliki mapungufu yetu pia kama chama.. mikataba mibovu, uongozi mbovu n.k yote ni mali ya CCM. Nitafurahi siku moja watawala wetu watakapokuwa na ujasiri wa kumiliki mapungufu yote yanayotokea nchini kwani wao ndio wanaongoza nchi! Iweje leo suala la kadhi lirushiwe Mrema, ubovu bodi ya mikopo lawama kwa wanafunzi, ajali barabarani makosa ya abiria?
 
Una damu ya kijani nini FD, kila kitu ya CCM ni perfect, is it?

i love this! ni vizuri kumiliki ushindi na kujivunia ushindi wa chama chetu. Kwa vile mambo yote mazuri lazima yahusishwe na CCM kama tulivyoifunga Burkinabe.. naona ni vizuri kuufurahia ushindi huu kama ushindi wa chama tawala na tabia iliyoonesha na kijana huyo kama malezi ya CCM.

Tunapomiliki mafanikio ya namna hii ni lazima tuwe tayari kumiliki mapungufu yetu pia kama chama.. mikataba mibovu, uongozi mbovu n.k yote ni mali ya CCM. Nitafurahi siku moja watawala wetu watakapokuwa na ujasiri wa kumiliki mapungufu yote yanayotokea nchini kwani wao ndio wanaongoza nchi! Iweje leo suala la kadhi lirushiwe Mrema, ubovu bodi ya mikopo lawama kwa wanafunzi, ajali barabarani makosa ya abiria?


Mzee, Mimi binafsi ninakubali kukosolewa kwa CCM. Na penye raha huwa pia nasherehekea!

Kumbukeni ninatazama pande zote za shilingi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom