CCM yakatakaza wagombea wake kuonekana TBC1, Tido Mhando ataarifiwa

CCM bado kinajiendesha kama chama cha Kikomunisti. Msisahau uhusiano uliopo kati ya CCM na wakomunisti mahali pengi duniani. CCM wameshindwa kufanya ukomunisti Tanzania lakini hawajakosa mbinu kadhaa kutoka vyama vya kikomunisti walizozibeba ambazo wanaendelea kuzitumia.

Mojawapo ya mbinu ya kikomunisti ni hili la chama kuchukua hatamu na serikali na vyombo vyake kubaki kama mawakala wa vyama vya kikomunisti. Kwa kawaida chama cha kikomunisti huwa hakihitaji nguvu ya umma, kinahitaji waaminifu waliolishwa kiapo rasmi ndani ya chama ambao huwa ndo nguvu ya chama. Watu hao ndo huingia serikalini kufanya kazi za chama. Kwa ujumla ni vigumu sana kutenganisha chama cha Kikomunisti na serikali ndo maana unaona mwenyekiti wa chama ndiye rais. Matamko ya viongozi wa chama siku zote huwa ni amri kwa serikali.

Sasa CCM wameona midahalo inawafunua jinsi walivyo na wagombea dhaifu wanaopewa nguvu na chama dola. Wagombea hao katika mazingira ya kawaida wasingeweza kushinda. Ila nguvu ya chama dola itatumika kuwasimika madarakani utake usitake. Midahalo hii inawaweka wazi kwa watu kuwa hawana uwezo. Kwa hiyo amri ya chama ya kuwataka CCM wasishiriki midahalo ni amri kwa chombo cha umma TBC kufuta midahalo hiyo. Subirini mtaona yatakayofuata, kipindi kitaondolewa, au kubadilishwa ili kukosa mwelekeo.

Kutenganisha chama na serikali ni mojawapo ya mafanikio ya mifumo ya kidemokrasia popote duniani. Mahali ambapo hakuna demokrasia, serikali na chama hubaki kuwa kama kitu kimoja. Hali hii ndo ipo hapa Tanzania.
 
Watu wa media kuna haja ya kuwajulisha watanzania kuwa CCM inahitaji ridhaa yao kuwaongoza lakini haiko tayari kuvumilia wazo lolote toka kwao. Itawaongoza kama inavyoona yenyewe vema na sio kama wao wananchi wanavyotaka!!!!!:glasses-nerdy:
 
CCM kuogopa mdahalo ina maana hawataki kura zetu? wanategemea mabango ndiyo yatawapa kura? ninaomba vyama vingine muendelee na midaharo ili wanachi waweze kusikiliza sera zenu. Kati ya viongozi watakaoiangusha CCM ni pamoja na Makamba sijui kwa nini CCM wamemng'ang'ania. SHAME ON YOU MAKAMBA!

MZALAMO
Ni nani ataviruhusu hivyo vya upinzani viendelee na huo mdahalo? kwa amri ya nani? na kwa sababu zipi na kama MUME WETU CCM kajitoa? Tumia akili , ZINDUKA.

MZALAMO, wewe kama wewe wanakuhesabu kama mpiga kelele na wanajua hauna mchango wowote ule katika maamuzi katika Taifa lako wakisema wao(CCM) basi basi tena, TIDO hawezi kufanya kinyume.
 
ukweli ni kwamba wakati wagombea "MASKINI " wasiokuwa na pea wa chadema wakiwa kila siku wapo mbele ya camera kutengeneza movie! wenzao wa CCM wapo majimboni ambapo asilimia kubwa hawana TV, wakijaribu kuwapa sera wananchi watawasaidia vipi kila mmoja awe na Laptop + internet kama wakiwapa kura zao. at the same time wakiwapa kura chadema basi miaka 5 ya kwanza kodi zao zinapotea vipi kwa ajili ya kuimarisha chama. Pia mavasi yao ya kikomunist inaonesha wazi wakipewa madaraka hawatong`atuka! mchungaji slaa IF akipa ikulu basi aesabu miaka mi 4 atapinduliwa na ZITO kutokana na kwamba zito ameshaanza kuonesha NIA mapemaaa!
 
Makamba awaweka pabaya wagombea CCM
Thursday, 09 September 2010 07:23

“Akizungumza na gazeti hili jana, Makamba alisisitiza akisema: "Hatutaki. Tumekataa ndio. Sisi yetu ni mikutamo ya hadhara. Tutaeleza huko malengo, ilani yetu na sera zetu kwa wananchi. Hatuoni sababu ya kukaa katika chumba kidogo na kuwapa nafasi ya ushiriki watu wachache."

Chumba kidogo sawa Ma-Rope, but wanaoangalia ni wengi! Hicho ni kipindi cha television, nadhani ni vyema tukajiuliza ni watanzania wangapi wanaangalia TV? Huko vijijini kuna TV pia. Kwa hesabu ya haraka haraka nadhani karibu asilimia 20 ya wapiga kura wana access na TV, na most ni independent, wasiokuwa na vyama. Hii ni idadi kubwa sana. Wakati wa kombe la dunia it was very obvious jinsi watu waliokuwa wanaona TV, yumkini hata wakati huu wa uchaguzi pia!!

Kama TV sio issue, mbona TBC1 walikatiza matangazo yao wakati wa mkutano wa Chadema wakati Marando anakata issue kwa maelekezo ya CCM?

Kuna haja ya mdahalo kuingizwa kwenye sheria za uchaguzi. Hili litasaidia kuwapima wagombea in their true color, sio wakiwa na written remarks au speeches kweney mikutano ambapo hawajibu maswali magumu. Wanatakiwa wajibu maswali magumu, hata kama wakipewa maswali before, is OK, kuna zile follow up questions kama bungeni vile wanasema swali al nyongeza.
 
CCM vigeugeu sana hizi sababu wanazotoa zinafanana na zilizowahi kutolewa na wapinzani mwaka 2010, au tuseme CCM wameanza kujifunza maisha ya upinzani?
 
Back
Top Bottom