Wadau nilikuwa naangalia habari ITV saa mbili jioni, imeonyeshwa vyama vyote vya siasa vimeshusha bendera nusu mlingoti, ikiwa ni pamoja na bendera ya taifa,isipokuwa CCM. Je hii inakaaje? ina maana CCM wanamaanisha nini? Wakati watanzania tuna msiba mkubwa namna hii?
@Sidhani kama wameamua kudharau wito wa maombolezo, Nafikiri wahusika kwenye ofisi za CCM watakuwa wamejisahau tu, maana wengi wako busy sana na shughuli zao binafsi. @Lakini wapo wengine wanapeperusha bendera ya CCM kwenye mazingira yao kama utamaduni, au kuficha biashara haramu zinazofanywa kwenye mazingira yao, au kukwepa usumbufu wa polisi na maafisa wa kodi. Kwa ujumla wengi wao sio wanaCCM halisia hivyo hawana muda na mchango wowote kwa chama chao, kwa hivyo suala la kupeperusha bendera nusu mlingoti ni msamiati na zoezi gumu sana kwao.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.