Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,494
Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Wilaya ya Ubungo, Mbaruku Masudi wakati akiongea na waandisha wa habari amedai kuwa kwa sasa wameanza kuondoa changamoto mbalimbali ndani ya chama hicho kuhakikisha wanashinda na kukomboa mitaa na Kata ambazo zipo chini ya wapinzani.
"Tutahakikisha katika changuzi zozote zilizopo mbele yetu kama ule wa Saranga uchaguzi mdogo ni kuhakikisha tunarudisha mitaa iliyobaki na Kata zilizobakia" alisisitiza Mbaruku
Katika uchaguzi mdogo wa marudio uliofanyika Novemba 26, 2017 uliwapa ushindi Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Kata ya Saranga Ubungo na kuweza kukomboa Kata hiyo ambayo awali ilikuwa chini ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Muungwana