KOMBAJR
JF-Expert Member
- Nov 15, 2011
- 5,827
- 1,271
Heshima kwenu Wanabodi, Nilikuwa naperuzi Gazeti la Mwananchi nikakutana na hii Habari, Ebu tuisome kisha tuijadili ukiisoma hii habari unapata kujua kiwango na uwezo wa kufikiri wa viongozi na Makada wa CCM.Yaan utafikiri wakati wanaojiwa wanakuwa wametoka usingizini!
Akizungumza na gazeti hili kwenye mahojiano maalum yaliyofanyika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda alisema kuwa, licha ya Lema kuwasumbua katika kipindi chote cha uchaguzi na ubunge wake, hawezi kushinda hata akisimama kwa mara nyingine.
Lema mtoto wa mjini kweli kweli, aliweza kutusumbua tangu kwenye kampeni hadi kwenye kipindi cha ubunge, lakini sasa hivi hata akisimama tena hawezi kushinda, kwa sababu amekiuka sharia na taratibu za kanuni za uchaguzi, alisema Chatanda.
Aliongeza kutokana na hali hiyo chama hicho kimejipanga upya ili kuhakikisha kuwa jimbo hilo linarudi mikononi mwao jambo ambalo litaweza kuwavunja nguvu wanachama wa Chadema mkoani humo.
Alisema CCM iko makini licha ya kuwepo kwa tofauti za hapa na pale ambazo zimeweza kuwaondoa baadhi ya wanachama wa chama hicho mkoani humo, lakini ni mwendelezo wa kuwaondoa wanachama wanaokwenda kinyume na sharia za chama chao, jambo ambalo limewafanya baadhi yao kujiondoa wenyewe.
Sio hao tu, kuna wengine nao wako njiani wanaweza kuondoka wakati wowote, lakini mkakati wetu utabaki pale pale, ni kuhakikisha kuwa, majimbo ya CCM ya mkoa wa Arusha ambayo yamechukuliwa na upinzani yanarudi, aliongeza.
Source:Mwananchi!
Akizungumza na gazeti hili kwenye mahojiano maalum yaliyofanyika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda alisema kuwa, licha ya Lema kuwasumbua katika kipindi chote cha uchaguzi na ubunge wake, hawezi kushinda hata akisimama kwa mara nyingine.
Lema mtoto wa mjini kweli kweli, aliweza kutusumbua tangu kwenye kampeni hadi kwenye kipindi cha ubunge, lakini sasa hivi hata akisimama tena hawezi kushinda, kwa sababu amekiuka sharia na taratibu za kanuni za uchaguzi, alisema Chatanda.
Aliongeza kutokana na hali hiyo chama hicho kimejipanga upya ili kuhakikisha kuwa jimbo hilo linarudi mikononi mwao jambo ambalo litaweza kuwavunja nguvu wanachama wa Chadema mkoani humo.
Alisema CCM iko makini licha ya kuwepo kwa tofauti za hapa na pale ambazo zimeweza kuwaondoa baadhi ya wanachama wa chama hicho mkoani humo, lakini ni mwendelezo wa kuwaondoa wanachama wanaokwenda kinyume na sharia za chama chao, jambo ambalo limewafanya baadhi yao kujiondoa wenyewe.
Sio hao tu, kuna wengine nao wako njiani wanaweza kuondoka wakati wowote, lakini mkakati wetu utabaki pale pale, ni kuhakikisha kuwa, majimbo ya CCM ya mkoa wa Arusha ambayo yamechukuliwa na upinzani yanarudi, aliongeza.
Source:Mwananchi!