Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
CCM yaibuka na ushindi mnono
Monday, 31 January 2011 19:35 administrator
NA SOLOMON MWANSELE, MBEYA
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Mbeya mjini, kimeibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi mdogo wa serikali za Mitaa na wajumbe, kwa kunyakua mitaa sita kati ya saba iliyofanya uchaguzi, Januari 30, mwaka huu.
Sambamba na hilo, CCM imefanikiwa pia kushinda nafasi 12 za ujumbe, kati ya 14 zilizokuwa zinawania katika mitaa mbalimbali mjini hapa.
Katibu wa CCM wilayani hapa, Bahati Makalanzi, akizungumza jana, alisema matokeo hayo yanaonyesha kuwa wananchi wengi bado wana imani na Chama, hali iliyopelekea maeneo mengine wagombea wake kupita bila kupingwa.
Alisema uchaguzi huo umefanyika kufuatia baadhi ya wenyeviti kujiuzulu kwa kuchaguliwa katika nafasi za udiwani na katika mitaa mingine, kufariki.
Bahati aliitaja mitaa mitatu kati ya saba ambayo wagombea wa nafasi ya Uenyekiti kwa tiketi ya CCM wamepita bila kupingwa na kata yake ikiwa kwenye mabano ni Paul Sangu wa mtaa wa Kanda ya chini (Iduda).
Mingine ni mtaa wa Jacaranda (Sisimba) ambapo mgombea Alinanga Kamwela alipita bila kupingwa na mtaa wa Kagera (Ilomba), Anyosisye Mwambona amepita bila kupingwa.
Katibu huyo wa CCM wilaya ya Mbeya mjini, alisema Chama kimefanikiwa kuibuka kidedea kwa wagombea wake waliosimamishwa katika mitaa ya Ghana magharibi (Ghana), ambapo Sudi Kipande, alimshinda mgombea wa CHADEMA kwa kujizolea kura 137 dhidi ya 18 za mpinzani wake.
Katika mtaa wa Kiwanja Ngoma (Maendeleo), mgombea uenyekiti aliyesimamishwa na CCM, Richard Mwakoba, aliibuka mshindi kwa kujizolea kura 120 dhidi ya 21 alizozipata mgombea wa CUF.
Pia CCM imeibuka mshindi katika mtaa wa Nsalaga (Nsalaga), ambapo mgombea wake Peter Ngonde, alimshinda mgombea aliyekuwa amesimamishwa na CHADEMA, kwa kupata kura 252. Mtaa wa Ndeje (Iwambi), umechukuliwa na CHADEMA.
Kwa upande wa nafasi za ujumbe zilizokuwa zinagombewa kwa wilaya ya Mbeya mjini ni 14, ambapo CCM kimefanikiwa kushinda nafasi 12, huku moja ikichukuliwa na CHADEMA.
Katibu Bahati, alisema uchaguzi wa kumtafuta mjumbe wa mtaa wa Nkuyu, uliopo kata ya Isanga, utarudiwa baada ya wagombea ujumbe kupitia CCM na CHADEMA kulingana kwa kura.
Aliongeza kuwa, katika uchaguzi huo mdogo, CCM imefanikiwa pia kuirudisha mitaa ya Nsalaga na Kagera ambayo awali ilikuwa inashikiliwa na wenyeviti kutoka CHADEMA, ambao safari hii wameshindwa vibaya.
Monday, 31 January 2011 19:35 administrator
NA SOLOMON MWANSELE, MBEYA
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Mbeya mjini, kimeibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi mdogo wa serikali za Mitaa na wajumbe, kwa kunyakua mitaa sita kati ya saba iliyofanya uchaguzi, Januari 30, mwaka huu.
Sambamba na hilo, CCM imefanikiwa pia kushinda nafasi 12 za ujumbe, kati ya 14 zilizokuwa zinawania katika mitaa mbalimbali mjini hapa.
Katibu wa CCM wilayani hapa, Bahati Makalanzi, akizungumza jana, alisema matokeo hayo yanaonyesha kuwa wananchi wengi bado wana imani na Chama, hali iliyopelekea maeneo mengine wagombea wake kupita bila kupingwa.
Alisema uchaguzi huo umefanyika kufuatia baadhi ya wenyeviti kujiuzulu kwa kuchaguliwa katika nafasi za udiwani na katika mitaa mingine, kufariki.
Bahati aliitaja mitaa mitatu kati ya saba ambayo wagombea wa nafasi ya Uenyekiti kwa tiketi ya CCM wamepita bila kupingwa na kata yake ikiwa kwenye mabano ni Paul Sangu wa mtaa wa Kanda ya chini (Iduda).
Mingine ni mtaa wa Jacaranda (Sisimba) ambapo mgombea Alinanga Kamwela alipita bila kupingwa na mtaa wa Kagera (Ilomba), Anyosisye Mwambona amepita bila kupingwa.
Katibu huyo wa CCM wilaya ya Mbeya mjini, alisema Chama kimefanikiwa kuibuka kidedea kwa wagombea wake waliosimamishwa katika mitaa ya Ghana magharibi (Ghana), ambapo Sudi Kipande, alimshinda mgombea wa CHADEMA kwa kujizolea kura 137 dhidi ya 18 za mpinzani wake.
Katika mtaa wa Kiwanja Ngoma (Maendeleo), mgombea uenyekiti aliyesimamishwa na CCM, Richard Mwakoba, aliibuka mshindi kwa kujizolea kura 120 dhidi ya 21 alizozipata mgombea wa CUF.
Pia CCM imeibuka mshindi katika mtaa wa Nsalaga (Nsalaga), ambapo mgombea wake Peter Ngonde, alimshinda mgombea aliyekuwa amesimamishwa na CHADEMA, kwa kupata kura 252. Mtaa wa Ndeje (Iwambi), umechukuliwa na CHADEMA.
Kwa upande wa nafasi za ujumbe zilizokuwa zinagombewa kwa wilaya ya Mbeya mjini ni 14, ambapo CCM kimefanikiwa kushinda nafasi 12, huku moja ikichukuliwa na CHADEMA.
Katibu Bahati, alisema uchaguzi wa kumtafuta mjumbe wa mtaa wa Nkuyu, uliopo kata ya Isanga, utarudiwa baada ya wagombea ujumbe kupitia CCM na CHADEMA kulingana kwa kura.
Aliongeza kuwa, katika uchaguzi huo mdogo, CCM imefanikiwa pia kuirudisha mitaa ya Nsalaga na Kagera ambayo awali ilikuwa inashikiliwa na wenyeviti kutoka CHADEMA, ambao safari hii wameshindwa vibaya.