Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,886
- 6,883
WAITUMIA TAKUKURU SALAMU
CCM kimesema kuwa fedha zilizogawanywa miongoni mwa wajumbe wake katika kura za maoni Jimbo la Igunga hazikuwa za rushwa, bali zilitolewa na chama.
Maelezo hayo yametolewa na chama hicho kufuatia taarifa za wanachama wake watatu kushikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) katika eneo la ukumbi wa mkutano wa kura za maoni na baadaye kuachiwa.
Mwigulu aliwataka maofisa wa Takukuru kuwa makini katika kutekeleza majukumu yake kwa kufuata kanuni na taratibu zao za kazi.
Mwigulu alisema Takukuru inapaswa kutambua kuwa CCM inapowaita wajumbe kutoka sehemu mbalimbali kwa ajili ya mikutano na vikao, gharama za uendeshaji ni juu ya chama na ndicho kilichofanyika katika mkutano huo. "Sisi kama Chama Cha Mapinduzi tunapoita wajumbe kutoka sehemu mbalimbali hatutarajii wajumbe wetu wajitegemee, ni CCM inayoingia gharama zote kuanzia kusafiri, kula na kulala hadi mkutano utakapokwisha," alisema Mwigulu.
Alisisitiza kuwa hicho ndicho kilichofanyika Igunga kwa kuwapa wajumbe fedha baada ya kufika mkutanoni. "Ninasikia ni kuwa TAKUKURU waliwakuta mkutanoni hapo na si kwinginepo," alisisitiza. Mwigulu alisema Takukuru na vyombo vingine watambue kuwa fedha hizo hazikuwa za wagombea bali ni mfuko wa chama.
Alisema: "Taasisi itambue kuwa vipo vikundi vya uhamasishaji ambavyo vinakusanywa kwa ajili ya maandalizi, ni wajibu wa CCM kuandaa na kugharimia safari zao na malazi hivyo ni wajibu wa taasisi (Takukuru) kupata maelezo kuhusiana na hilo isijekutokea wakadhani kuwa wanapewa rushwa."
Aidha, akizungumzia uchaguzi huo, Mwigulu alisema wakati vyama vya siasa vikikimbilia kuchukua fomu, CCM inajipanga kwa ajili ya ushindi mkubwa na wa kishindo.
"Ninachotaka kuwaambia kuhusiana na uchaguzi ujao ni kwamba, ushindi uko wazi kwa CCM kwa kuona mtaji mkubwa uliopo na hasa vijijini," alisema. Alisema kuwa vyama vinapaswa kujipima na bora kujitoa mapema kuliko kuanza malalamiko na kukimbilia Takukuru.
IPPMedia
CCM kimesema kuwa fedha zilizogawanywa miongoni mwa wajumbe wake katika kura za maoni Jimbo la Igunga hazikuwa za rushwa, bali zilitolewa na chama.
Maelezo hayo yametolewa na chama hicho kufuatia taarifa za wanachama wake watatu kushikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) katika eneo la ukumbi wa mkutano wa kura za maoni na baadaye kuachiwa.
Mwigulu aliwataka maofisa wa Takukuru kuwa makini katika kutekeleza majukumu yake kwa kufuata kanuni na taratibu zao za kazi.
Mwigulu alisema Takukuru inapaswa kutambua kuwa CCM inapowaita wajumbe kutoka sehemu mbalimbali kwa ajili ya mikutano na vikao, gharama za uendeshaji ni juu ya chama na ndicho kilichofanyika katika mkutano huo. "Sisi kama Chama Cha Mapinduzi tunapoita wajumbe kutoka sehemu mbalimbali hatutarajii wajumbe wetu wajitegemee, ni CCM inayoingia gharama zote kuanzia kusafiri, kula na kulala hadi mkutano utakapokwisha," alisema Mwigulu.
Alisisitiza kuwa hicho ndicho kilichofanyika Igunga kwa kuwapa wajumbe fedha baada ya kufika mkutanoni. "Ninasikia ni kuwa TAKUKURU waliwakuta mkutanoni hapo na si kwinginepo," alisisitiza. Mwigulu alisema Takukuru na vyombo vingine watambue kuwa fedha hizo hazikuwa za wagombea bali ni mfuko wa chama.
Alisema: "Taasisi itambue kuwa vipo vikundi vya uhamasishaji ambavyo vinakusanywa kwa ajili ya maandalizi, ni wajibu wa CCM kuandaa na kugharimia safari zao na malazi hivyo ni wajibu wa taasisi (Takukuru) kupata maelezo kuhusiana na hilo isijekutokea wakadhani kuwa wanapewa rushwa."
Aidha, akizungumzia uchaguzi huo, Mwigulu alisema wakati vyama vya siasa vikikimbilia kuchukua fomu, CCM inajipanga kwa ajili ya ushindi mkubwa na wa kishindo.
"Ninachotaka kuwaambia kuhusiana na uchaguzi ujao ni kwamba, ushindi uko wazi kwa CCM kwa kuona mtaji mkubwa uliopo na hasa vijijini," alisema. Alisema kuwa vyama vinapaswa kujipima na bora kujitoa mapema kuliko kuanza malalamiko na kukimbilia Takukuru.
IPPMedia