Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
• CHENGE ABEBESHWA MZIGO KUWASILISHA HOJA BINAFSI
na Mwandishi wetu
SIKU moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, kueleza mkakati wa kutaka kuwaondoa bungeni wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), chama hicho tawala sasa kinajiandaa kuleta hoja binafsi kuwaondoa wabunge wa CHADEMA, Tanzania Daima Jumapili imeelezwa.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata kutoka ndani ya CCM, zilisema chama hicho kimetoa maagizo kwa wanasheria wake ili waandae hoja binafsi itakayowasilishwa bungeni na mwanasheria, Andrew Chenge, kisha kupiga kura ya kutaka wabunge hao waondolewe bungeni.
"Mchezo uliopangwa kufanyika ni kama ule aliofanyiwa Zitto Kabwe alipotoa hoja ya Buzwagi. Licha ya utetezi wake mzuri, aliondoka. Safari hii kazi hii atapewa Chenge, tumepania lazima wabunge wa CHADEMA waondoke bungeni hadi hapo watakaposema wanamtambua rais," alisema mmoja wa makada wa CCM.
Kwa mujibu wa habari hizo, mpango huo unasubiri baraka za Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, ambaye alitarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam jana baada ya kuwa nje ya ofisi yake kikazi.
Kada huyo alipohojiwa ni kifungu gani cha Katiba au cha kanuni za Bunge kilichovunjwa, alishindwa kujibu, lakini alisisitiza kuwa chini ya mkakati huo, CCM itahakikisha inamtumia spika wake mtiifu, Anne Makinda, kuhakikisha wabunge wa CHADEMA wanashughulikiwa.
"Hakuna kitu kilichomuumiza rais kama kitendo cha wabunge wa CHADEMA kusimama na kuondoka kwa dharau. Bora wasingekuja bungeni na katika hilo chama kimedhamiria, Bunge lijalo moto utawaka," alisema mpashaji habari huyo.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Benno Malisa, amelaami kitendo hicho na kusema ni ishara ya utovu wa nidhamu kwa wapiga kura waliowachagua.
Hata hivyo, uamuzi huu wa CHADEMA kususa matukio yanayomhusisha rais umemfadhaisha na kumsumbua rais mwenyewe na CCM mbele ya umma na macho ya kimataifa.
Source: Tanzania Daima
My Take
Iwapo CCM watatekeleza mpango huu, nafikiri wanaweza kuwa wamejichimbia kaburi kwa kuwa CHADEMA hawataongelea bungeni tena bali watakwenda kwa wananchi. Kitendo cha kuitisha mikutano na wananchi na kuwaeleza ni namna gani serikali iliyopo madarakani inadhulumu haki ya watanzania, kitaamusha hasira miongoni mwa wananchi na kuweza kupelekea kuvunjika kwa amani. CCM wafikirie upya juu ya mkakati wanaotaka kuuchukua, maana unaweza ukawagharimu, wakajikuta wanashindwa kuongoza nchi.
na Mwandishi wetu
SIKU moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, kueleza mkakati wa kutaka kuwaondoa bungeni wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), chama hicho tawala sasa kinajiandaa kuleta hoja binafsi kuwaondoa wabunge wa CHADEMA, Tanzania Daima Jumapili imeelezwa.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata kutoka ndani ya CCM, zilisema chama hicho kimetoa maagizo kwa wanasheria wake ili waandae hoja binafsi itakayowasilishwa bungeni na mwanasheria, Andrew Chenge, kisha kupiga kura ya kutaka wabunge hao waondolewe bungeni.
"Mchezo uliopangwa kufanyika ni kama ule aliofanyiwa Zitto Kabwe alipotoa hoja ya Buzwagi. Licha ya utetezi wake mzuri, aliondoka. Safari hii kazi hii atapewa Chenge, tumepania lazima wabunge wa CHADEMA waondoke bungeni hadi hapo watakaposema wanamtambua rais," alisema mmoja wa makada wa CCM.
Kwa mujibu wa habari hizo, mpango huo unasubiri baraka za Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, ambaye alitarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam jana baada ya kuwa nje ya ofisi yake kikazi.
Kada huyo alipohojiwa ni kifungu gani cha Katiba au cha kanuni za Bunge kilichovunjwa, alishindwa kujibu, lakini alisisitiza kuwa chini ya mkakati huo, CCM itahakikisha inamtumia spika wake mtiifu, Anne Makinda, kuhakikisha wabunge wa CHADEMA wanashughulikiwa.
"Hakuna kitu kilichomuumiza rais kama kitendo cha wabunge wa CHADEMA kusimama na kuondoka kwa dharau. Bora wasingekuja bungeni na katika hilo chama kimedhamiria, Bunge lijalo moto utawaka," alisema mpashaji habari huyo.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Benno Malisa, amelaami kitendo hicho na kusema ni ishara ya utovu wa nidhamu kwa wapiga kura waliowachagua.
Hata hivyo, uamuzi huu wa CHADEMA kususa matukio yanayomhusisha rais umemfadhaisha na kumsumbua rais mwenyewe na CCM mbele ya umma na macho ya kimataifa.
Source: Tanzania Daima
My Take
Iwapo CCM watatekeleza mpango huu, nafikiri wanaweza kuwa wamejichimbia kaburi kwa kuwa CHADEMA hawataongelea bungeni tena bali watakwenda kwa wananchi. Kitendo cha kuitisha mikutano na wananchi na kuwaeleza ni namna gani serikali iliyopo madarakani inadhulumu haki ya watanzania, kitaamusha hasira miongoni mwa wananchi na kuweza kupelekea kuvunjika kwa amani. CCM wafikirie upya juu ya mkakati wanaotaka kuuchukua, maana unaweza ukawagharimu, wakajikuta wanashindwa kuongoza nchi.