MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,264
Wananchi wakiwa wamembeba kwa furaha mgombea wa Ubunge jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, kwa tiketi ya CCM, Godfrey Mgimwa, wakati wa mkutano wa kufunga kampeni uliofanywa na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi, kwenye Uwanja wa Mnada, Kijiji cha Kidamali, Kata ya Nzihi, leo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Naibu Katibu Mkuu (Bara) Mwigulu Nchemba na Mgombea wa CCM jimbo la Kalenga, Godfrey Mgimwa wakisalimia wananchi baada ya kuwasili kwenye mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akimnadi Mgimwa kwenye mkutano huo wa kufunga kampeni
Naibu Katibu Mkuu(Bara), Mwigulu Nchemba akihutubia umati wa wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni
Mgimwa akihutubia maelfu ya wananchi kwenye mkutano huo wa kufunga kampeni
Mgimwa akiionyesha hadhara mkewe Robi, kwenye mkutano huo wa kufunga kampeni za CCM.
Umati wa wananchi wakinyoosha mikono kuafiki kumchagua mgombea wa CCM, Godfrey Mgimwa kesho.