VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Tangu jana hapa Ofisi Ndogo za CCM,Lumumba kuna furaha. Furaha ya kichama inahusu sarakasi zilizoanzishwa nasi juu ya Rasimu ya Katiba na wengine kuziiga. Makada waandamizi wa chama hapa Lumumba wanaziona sarakasi hizo kama zenye uwezo wa kuchelewesha uandikwaji wa Katiba mpya na hivyo kuifanya iliyopo kuendelea kufanya kazi.
Wanatamani mabishano yapambe moto na kuendelea na chama chetu kizidi kushika hatamu.'Rasimu ya Muungano tu hivi,je ikianza ya Tanganyika?' aliuliza Afisa mmoja wa Idara ya Uenezi.
‘Mwaka 2015 uchaguzi utafanyika kwa Katiba ya sasa. Mambo yatakuwa vilevile kama zamani.Cha kufanya ni kuendelea kupinga sehemu kubwa ya Rasimu hii.' aliongeza Afisa huyo anayejiita 'Tsunami'. Je,wanaamini katika kweli?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam