CCM yabagua wananchi

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
[h=2]Na Victor Bariety, Geita - Mtanzania[/h]
*Mwenyekiti wao asema hatapeleka maendeleo kata za CHADEMA
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Geita, Joseph Musukuma, jana aliwaacha hoi wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Nyawilimilwa, kilichopo Kata ya Kagu, baada ya kusema hatakuwa tayari kupeleka miradi ya maendeleo katika kata hiyo, kwa kuwa inaongozwa na diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Musukuma alitoa kauli hiyo mbele ya Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Moses Minga pamoja na Ofisa Mipango wa Wilaya hiyo, Frank Makonda, waliokuwa wamehudhuria kikao hicho kilichofanyika wakati akikagua miradi ya maendeleo ya kata hiyo.

“Nilitumia gharama kubwa sana wakati wa uchaguzi uliopita wa udiwani, lakini wananchi wa kata hii mkanisaliti na kumchagua Lukondo Mkukura wa CHADEMA.

“Mlifanya hivyo kwa sababu zenu wenyewe na hii ilitokana na ninyi wenyewe kuendekeza makundi na ukabila. Kwa hiyo, naomba mkome kabisa na hayo ndiyo matunda ya kuchagua upinzani.

“Kutokana na tabia mliyoifanya, niko tayari kumzuia mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya, asiwaletee fedha za ruzuku zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya shughuli za maendeleo, ili liwe fundisho kwa watu wengine wanaoacha kuchagua CCM na kuchagua vyama vya siasa vya upinzani hususan CHADEMA.

“CHADEMA hawana uwezo wa kuwaletea maendeleo katika kata hii na ni vigumu pia na mimi kuwaletea maendeleo ama kuruhusu miradi ya maendeleo ije kwenu.

“Huenda nifanye hivyo kwa huruma tu ya chama changu, kwa sababu nyinyi wenyewe mlichagua shetani, acheni mkome,” alisema Musukuma.

Soma zaidi hapa


Je hizi ni sera za chama au ni mtu binafsi mwenye uelewa finyu?
 
kulikuwa na polisi wengi nini kwanini wasimpige mawe !
Teh teh, si unawajua watanzania walivyo? si ajabu walianza kutetemeka kwamba mambo yao yameshaharibika kutokana na kumchagua kiongiz wa CHADEMA. Na usishangae walipotoka hapo walianza kulaumiana kwa kuchagua kiongozi wa CHADEMA.
 
Teh teh, si unawajua watanzania walivyo? si ajabu walianza kutetemeka kwamba mambo yao yameshaharibika kutokana na kumchagua kiongiz wa CHADEMA. Na usishangae walipotoka hapo walianza kulaumiana kwa kuchagua kiongozi wa CHADEMA.

Wasukuma wanaogopa sana ccm siyo kwamba wanaipenda ila hako kajamaa kamewatishia vile wao hawajui tofauti ya chama na serikali. Wanajua hata balozi wa ccm kwao ni boss wa kuogopwa. Na hata wakati wa kupiga kura wanatishiwa na mabalozi wa ccm na wao wanafyata mkia bila hata kujua kuwa kura ni siri!

Kwa ujumla wasukuma ni waoga na watatulidisha nyuma maana wao ndo wengi nch hii!
 
Maendeleo siyo ombi kwake ni lazima kwasababu ni haki yetu kama watanzania na walipa kodi, huyo shetani wa malipizi, visasi alie mjaa ashindwe...Kikwete nakuchukia wewe na CCM yako kuliko hata shetani...
 
Wasukuma wanaogopa sana ccm siyo kwamba wanaipenda ila hako kajamaa kamewatishia vile wao hawajui tofauti ya chama na serikali. Wanajua hata balozi wa ccm kwao ni boss wa kuogopwa. Na hata wakati wa kupiga kura wanatishiwa na mabalozi wa ccm na wao wanafyata mkia bila hata kujua kuwa kura ni siri!

Kwa ujumla wasukuma ni waoga na watatulidisha nyuma maana wao ndo wengi nch hii!
Hilo si tatizo la wasukuma peke yao. Ni tatizo la watanzania walio wengi katika maeneo mbalimbali ya nchi. Ndiyo maana wanaishabikia CDM, lakini ukifika uchaguzi wanaipigia kura CCM. Kwa kuhofia kwamba labda kijiji chao kitakosa misaada iwapo watachagua upinzani.
 
Hilo si tatizo la wasukuma peke yao. Ni tatizo la watanzania walio wengi katika maeneo mbalimbali ya nchi. Ndiyo maana wanaishabikia CDM, lakini ukifika uchaguzi wanaipigia kura CCM. Kwa kuhofia kwamba labda kijiji chao kitakosa misaada iwapo watachagua upinzani.
Nchi hii kuna wasukuma na wagogo hawa ni zaidi ya maiti ambao ukiwaambia hata walipie pumzi na usingizi watakubali hata kama hawana kitu mfukoni ni aina mbaya ya wanaukombozi japo wanajitahidi ukilinganisha na wahaya...Kunahaja ya kuwaelimisha ili watu hawa wakiamka tulikomboe taifa hata kwa damu yangu niko tayari...Nailaani Ccm na wote wanaoiunga mkono mungu awaumize kadiri amuuzavyo shetani
 
Hayo ni mawazo ya viongozi Wa CCM lakini wakumbuke pesa za maendeleo Ni kodi zetu wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama.

kwa nchi yenye demokrasia Huyu aliyetoa kauli Kama hii anatakiwa achukuliwe harua za kinidhamu Na kufukuzwa uongozi.
 
Huyo ametoboa siri sasa,hiyo ni ajenda ya siri ya CCM hata majimbo yanayoongozwa na wabunge wa upinzani hayapelekewi fedha za maendeleo kwa wakati ili waonekane hawawezi kuongoza.Katika kumbukumbu kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mhe.Mbowe aliwahi kuhoji kama huo ndo mpango wa serikali wa kuwanyima fursa watanzania wanaochagua upinzani...kama kawaida Mzee Pinda alijiuma uma tu then ikaishia lakini ni swala ambalo lipo!
 
Waache kulipa kodi na TRA isiende kukusanya kodi katika maeneo hayo maana hawana faida na kodi zao kweli Ccm ni mbumbumbu mzungu wa reli manyang'au wasiosoma alama za nyakati
 
Hizo ndizo sera za ccm. Afadhali huyu katamka, wengine wanatekelezaga kimya kimya. Halafu mnasema ccm inadumisha democrasia, amani na utulivu. Kweli?

Hawa Watanzania kwa sababu ya uelewa wa kiwango kisichotosha, wanatishiwa ili wasije kuchagua kionogozi nje ya ccm.

Labda nitoke katika ngazi ya wanakijiji na kiongozi wao.

Katiba ya nchi inasemaje kwa kiongozi kama huyu anayetamka hadharani matusi, ubaguzi, ukandamizaji, ubwanyenye whether ni wake ama wa chama chake ccm?

Sheria ya Anti-discrimination inamlindaje mtu anapotangaza unyanyasaji na ubaguzi wa jinsi hii mchana kweupe tena hadharani?

Lakini pia, pengine huyu mtu anatakiwa kupimwa akili ili afya ya akili yake ijulikane ili kuona kama bado anasifa ya kushikda nafasi aliyonayo.

CCM, mnafahamu kwamba huduma za maendeleo ya wananchi siyo misaada mnayowapa kutoka katika mifuko yenu binafsi ama budget yenu ya ccm kama chama? Mnaweza kuzungumziaje suala la matumizi ya kodi za wananchi ambazo zinalipwa na kila mmoja wetu bila kujali itikadi za vyama?

Ndugu Watanzania wenzangu, hadi hapo, tunaweza kuona sasa ni jinsi gani ccm inavyokiuka katiba na kutengeneza mazingira ya uvunjifu wa amani?

Hadi hapo, kwa ubabe, kiburi, dhuruma, hujuma, kukosa uadilifu na maovu yote ya ccm kwa wananchi, bado tunaona ni chama kinachobeba sifa za kuendelea kuongoza nchi? Tunaweza kuona kwa mbali kidogo, kama hali itaendelea hivi,hadi tunafika 2015, hali itakuwaje TZ?

Kwa kashfa hizi na nyingine nyingi, mimi nadhani ccm itatupeleka katka machafuko makubwa mno ifikapo 2015. Hebu tushauriane, nini tufanye watanzania? Hiki si chama cha kuongoza nchi tena.
 
...Kwa ujumla wasukuma ni waoga na watatulidisha nyuma maana wao ndo wengi nch hii!
Aisee wee mkware Ngonini acha kuwaponda wasukuma. Uoga sio tatizo la kabila flani au kabila flani. Ni tabia ya watz wengi tu. Wabongo wanatabia ya uoga, kuchangaya na wewe vile vile.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom