Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Habari zinanukia na kusema kuwa ili kujisafisha na kuondoa sura ya madoa ya EPA, RADA, Kiwira na dalili zozote za kuitwa Chama Cha Mafisadi, CCM imeanza kampeni za usajili wa wagombea Udiwani na Uchaguzi 2009 & 2010!
Habari za upenuni zinasema dhumuni la Usajili huu ni kwanza kuwang'oa wabunge Machachari wa CCM ambao wamekuwa wakiukoroema ufisadi, na pili kwa kuwa baadhi ya Watuhumiwa wa Ufisadi wanaweza kuombwa waachiee ngazi, basi kunahitajika Wabunge wasio na madoa ambao wakiingia Bungeni, kazi yao itakuwa ni kukilinda CCM na hao Fisi wenye madoa madoa ambao wanatuhumiwa kuwa mafisadi!
Usajili huu unafanywa kwenye taasisi za elimu ya juu na CCM imedhamiria kusakanya wasomi, iwe Mzumbe, SUA, UDSM, au kwingineko kunakoitwa chuo. Dhamira ni kuleta vijana ambao wataonekana ni safi na wapya ili kuondoa ukungu unaotanda ambao unadhihirisha kuwa CCM inaweza kuanguka.
Kikubwa na cha kutisha ni danganya toto ya kutaka kuleta ufalme wa milele wa CCM na kulidna maslahi ya Mafisadi. Ikiwa CCM itashinda kwa kishindo kwa hizi sura mpya ambazo hazijapata madoa, itakuwa ni rahisi kwa CCM kuliongoza bunge kwa upinzani mdogo sana kutoka kwa Vyama vya Upinzani au wengine wote wanaopigia kelele udhaimu na mabavu ya CCM.
Habari za kuaminika ni kuwa wale ambao wamekuwa watii wa vikao vya usajili na viongozi hawa wa CCM, wameahidiwa "Ufalme Mpya" na "usafi" wao utakingiwa kifua.
Bado tuko mitamboni tukitafuta habari zaidi!
Habari za upenuni zinasema dhumuni la Usajili huu ni kwanza kuwang'oa wabunge Machachari wa CCM ambao wamekuwa wakiukoroema ufisadi, na pili kwa kuwa baadhi ya Watuhumiwa wa Ufisadi wanaweza kuombwa waachiee ngazi, basi kunahitajika Wabunge wasio na madoa ambao wakiingia Bungeni, kazi yao itakuwa ni kukilinda CCM na hao Fisi wenye madoa madoa ambao wanatuhumiwa kuwa mafisadi!
Usajili huu unafanywa kwenye taasisi za elimu ya juu na CCM imedhamiria kusakanya wasomi, iwe Mzumbe, SUA, UDSM, au kwingineko kunakoitwa chuo. Dhamira ni kuleta vijana ambao wataonekana ni safi na wapya ili kuondoa ukungu unaotanda ambao unadhihirisha kuwa CCM inaweza kuanguka.
Kikubwa na cha kutisha ni danganya toto ya kutaka kuleta ufalme wa milele wa CCM na kulidna maslahi ya Mafisadi. Ikiwa CCM itashinda kwa kishindo kwa hizi sura mpya ambazo hazijapata madoa, itakuwa ni rahisi kwa CCM kuliongoza bunge kwa upinzani mdogo sana kutoka kwa Vyama vya Upinzani au wengine wote wanaopigia kelele udhaimu na mabavu ya CCM.
Habari za kuaminika ni kuwa wale ambao wamekuwa watii wa vikao vya usajili na viongozi hawa wa CCM, wameahidiwa "Ufalme Mpya" na "usafi" wao utakingiwa kifua.
Bado tuko mitamboni tukitafuta habari zaidi!