CCM yaanza kujipanga kunyakua Ilemela, Nyamagana

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

22 NOVEMBER 2011

Na Moses Matthew, Mwanza

KAMATI ya Habari na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza, imekamilisha kazi ya kupata maoni mbalimbali kutoka kwa
wananchi ngazi ya Kata kujua sababu zilizosababisha chama hicho kupoteza majimbo mawili ya Ilemela na Nyamagana katika uchaguzi Mkuu uliopita.

Kamati hiyo iliyoanzishwa mwezi Mei na kuanza kazi rasmi mwezi wa saba mwaka jana, imebaini sababu kubwa nne zilizosababisha CCM kushindwa katika majimbo hayo mawili ikiwemo urasimu na ukandamizaji kwa baadhi ya watendaji, walimu kutopewa haki zao kwa wakati, uratatibu wa kura za maoni na migogoro ya ardhi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Jijini hapa, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. Musa Magabe, alisema lengo kuu la kamati yao kufanya ziara kwenye kata zote za wilaya hiyo ilikuwa kujua kwa undani kero mbalimbali za wananchi wa kada zote wakiwemo wafanyakazi zilizosababisha CCM kunyimwa kura mwaka jana ili ziwasilishwe kwenye kamati ya Siasa ya wilaya na kufanyiwa maamuzi ya utatuzi kwa manufaa ya taifa.

Alisema ili kufikia lengo waligawa kazi hiyo kwa makundi makubwa mawili. Kundi la kwanza ikiwa ni la wananchi na la pili ikijumlisha viongozi wote wa CCM waliokuwa wapigadebe na wasimamizi wakati wa uchaguzi uliopita ili waweze kubaini wapi walipokosea na kujirekebisha mapema.

Akitaja matokeo ya kazi hiyo kwa upande wa wafanyakazi alisema, watumishi wa serikali ngazi za Kata Kamati iligundua udhaifu mkubwa kwa baadhi ya Maofisa wa ngazi ya juu kwenye Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuwanyanyasa walio chini yao hivyo kuwafanya waichukie CCM na serikali yake.

Alitoa mfano kwa watumishi wa sekta ya elimu na kuweka wazi kuwa kamati yake imebaini walimu kukasirishwa na kucheleweshewa mafao yao, malipo yao ya likizo, kupandishwa madaraja na fedha za kujikimu kwa walimu wanaoanza kazi.

Alisema walibaini wananchi wengi wakiwemo wafanyakazi kulalamikia ukiritimba kwa baadhi ya watendaji katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza hivyo kuwafanya waichukie CCM hatimaye kukiadhibu chama hicho kwa kukinyima kura katika uchaguzi mkuu uliopita hususan katika majimbo hayo mawili.

Kwa mujibu wa katibu huyo kero zingine zilizobainishwa na kamati hiyo ni Maofisa watendaji wa kata kutopewa fedha za kuendesha Ofisi na ucheleweshaji wa fedha za maendeleo ikiwemo ukarabati katika sekta za afya, elimu na kero mbalimbali za kijamii.

Kuhusu migogoro ya ardhi alisema kamati hiyo ilibaini wananchi kuchukizwa na kero hiyo kukithiri na kuwapa wakati mugumu katika kata zao na kwamba hawaoni dalili ya wazi kushughulikia tatizo hilo na kwamba waliwekwa wazi kuwa hicho ndicho chanzo cha CCM kushindwa kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 Jiji la Mwanza.

Akizungumzia viongozi wa CCM ngazi za kata alisema kilio chao kikubwa kilikuwa chama hicho kiliwasahau mabalozi wa nyumba 10 ambao ndiyo uti wa mgongo na uhai wa chama pamoja na mfumo wa utaratibu wa kura za maoni kutosimamiwa vizuri hivyo kuzaa makundi.

Kuhusu suluhisho la matatizo hayo baada ya kazi hiyo Bw. Magabe alisema kuundwa kwa kamati hiyo na kubaini chanzo cha CCM kukosa ushindi wa ubunge na baadhi ya kata ni suluhisho la kwanza kwa kuwa maoni hayo yatawasilishwa sehemu husika na wananchi wataanza kuona mabadiliko.

"Chama cha Mapinduzi hakipindui serikali, kinajipindua chenyewe ndiyo maana unasikia dhana ya kujivua gamba, wananchi watarajie mabadiliko makubwa maana tumeshajua chanzo cha tatizo", alisema Bw. Magabe.

"Dhana ya kujivua gamba siyo geni, wakati wa Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere, alitumia dhana hiyo kwa jina la tujisahihishe katika jitihada za kuweka mambo sawa," alisema.










 
Wenje na CHADEMA makao makuu watafute copy ya matokeo ya hiyo research na kuyafanyia kazi. Simple!
 
Wenje na CHADEMA makao makuu watafute copy ya matokeo ya hiyo research na kuyafanyia kazi. Simple!

mkuu wala usiumize kichwa hakuna reserch yoyote iliyofanywa na magamba, uliona wapi hawa jamaa wakafanya reserch??
 

22 NOVEMBER 2011

Na Moses Matthew, Mwanza

KAMATI ya Habari na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza, imekamilisha kazi ya kupata maoni mbalimbali kutoka kwa
wananchi ngazi ya Kata kujua sababu zilizosababisha chama hicho kupoteza majimbo mawili ya Ilemela na Nyamagana katika uchaguzi Mkuu uliopita.

Kamati hiyo iliyoanzishwa mwezi Mei na kuanza kazi rasmi mwezi wa saba mwaka jana, imebaini sababu kubwa nne zilizosababisha CCM kushindwa katika majimbo hayo mawili ikiwemo urasimu na ukandamizaji kwa baadhi ya watendaji, walimu kutopewa haki zao kwa wakati, uratatibu wa kura za maoni na migogoro ya ardhi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Jijini hapa, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. Musa Magabe, alisema lengo kuu la kamati yao kufanya ziara kwenye kata zote za wilaya hiyo ilikuwa kujua kwa undani kero mbalimbali za wananchi wa kada zote wakiwemo wafanyakazi zilizosababisha CCM kunyimwa kura mwaka jana ili ziwasilishwe kwenye kamati ya Siasa ya wilaya na kufanyiwa maamuzi ya utatuzi kwa manufaa ya taifa.

Alisema ili kufikia lengo waligawa kazi hiyo kwa makundi makubwa mawili. Kundi la kwanza ikiwa ni la wananchi na la pili ikijumlisha viongozi wote wa CCM waliokuwa wapigadebe na wasimamizi wakati wa uchaguzi uliopita ili waweze kubaini wapi walipokosea na kujirekebisha mapema.

Akitaja matokeo ya kazi hiyo kwa upande wa wafanyakazi alisema, watumishi wa serikali ngazi za Kata Kamati iligundua udhaifu mkubwa kwa baadhi ya Maofisa wa ngazi ya juu kwenye Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuwanyanyasa walio chini yao hivyo kuwafanya waichukie CCM na serikali yake.

Alitoa mfano kwa watumishi wa sekta ya elimu na kuweka wazi kuwa kamati yake imebaini walimu kukasirishwa na kucheleweshewa mafao yao, malipo yao ya likizo, kupandishwa madaraja na fedha za kujikimu kwa walimu wanaoanza kazi.

Alisema walibaini wananchi wengi wakiwemo wafanyakazi kulalamikia ukiritimba kwa baadhi ya watendaji katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza hivyo kuwafanya waichukie CCM hatimaye kukiadhibu chama hicho kwa kukinyima kura katika uchaguzi mkuu uliopita hususan katika majimbo hayo mawili.

Kwa mujibu wa katibu huyo kero zingine zilizobainishwa na kamati hiyo ni Maofisa watendaji wa kata kutopewa fedha za kuendesha Ofisi na ucheleweshaji wa fedha za maendeleo ikiwemo ukarabati katika sekta za afya, elimu na kero mbalimbali za kijamii.

Kuhusu migogoro ya ardhi alisema kamati hiyo ilibaini wananchi kuchukizwa na kero hiyo kukithiri na kuwapa wakati mugumu katika kata zao na kwamba hawaoni dalili ya wazi kushughulikia tatizo hilo na kwamba waliwekwa wazi kuwa hicho ndicho chanzo cha CCM kushindwa kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 Jiji la Mwanza.

Akizungumzia viongozi wa CCM ngazi za kata alisema kilio chao kikubwa kilikuwa chama hicho kiliwasahau mabalozi wa nyumba 10 ambao ndiyo uti wa mgongo na uhai wa chama pamoja na mfumo wa utaratibu wa kura za maoni kutosimamiwa vizuri hivyo kuzaa makundi.

Kuhusu suluhisho la matatizo hayo baada ya kazi hiyo Bw. Magabe alisema kuundwa kwa kamati hiyo na kubaini chanzo cha CCM kukosa ushindi wa ubunge na baadhi ya kata ni suluhisho la kwanza kwa kuwa maoni hayo yatawasilishwa sehemu husika na wananchi wataanza kuona mabadiliko.

"Chama cha Mapinduzi hakipindui serikali, kinajipindua chenyewe ndiyo maana unasikia dhana ya kujivua gamba, wananchi watarajie mabadiliko makubwa maana tumeshajua chanzo cha tatizo", alisema Bw. Magabe.

"Dhana ya kujivua gamba siyo geni, wakati wa Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere, alitumia dhana hiyo kwa jina la tujisahihishe katika jitihada za kuweka mambo sawa," alisema.












asante mkuu nyoka_bndm.JPG
 
Viti vyote Mwanza pamoja na ile Ilemela hapati mtu mpaka tujuzwe kwanza MKE WA KWANZA kifo chake kilitokeaje huko miaka ya nyuma kidogo; watu lazima kwanza wajisafishe tangu majumbani ndipo watoke nje kwenda kugombea viti huko.
 
binafsi niliongea na mbunge wa Ilemela kupitia CHADEMA nikampa tips za jinsi ya kuimarisha kuungwa mkono na wananchi wa Ilemela,mpaka leo miezi 4 hakuna lolote aliloshughulikia kati ya yale niliyomtajia. Nina uzoefu wa kutosha katika maeneo yale,miaka 6 ninatoa huduma za kijamii katika jimbo hili,nafahamu sehemu ambazo hata kwa efforts kidogo ukizishughulikia matokeo utayaona haraka, tatizo la wanasiasa wengi ni kutofanya vitu kisayansi.

Hebu jiulize,wauguzi,madaktari, walimu n.k wenye migogoro na mkurugenzi wa jiji wakiamua kuvurunda makazini mwao impact yao itakuwaje kwa wapiga kura? Ccm walishindwa kwa mchezo huo pamoja na kero nyingine
 
Mke wa nani tena jamani? naomba utupe information
Viti vyote Mwanza pamoja na ile Ilemela hapati mtu mpaka tujuzwe kwanza MKE WA KWANZA kifo chake kilitokeaje huko miaka ya nyuma kidogo; watu lazima kwanza wajisafishe tangu majumbani ndipo watoke nje kwenda kugombea viti huko.
 
Ni jambo jema kwa ccm kujitafakari na hatimaye kuja na majibu ya kile kilichowavuruga
 
Back
Top Bottom