CCM waweke wazi mapato na matumizi ya chama

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Kuna Mwanaccm hapa anapenda sana kusifia ushindi wa ccm katika chaguzi zote kuanzia mwaka 1995 hadi leo kama dalili ya kuwa chama hicho kinapendwa na watanzania.

Nilikuwa Tanzania uchaguzi wa mwaka 95 na 2000 ambako nilishuhudia mamilioni ya pesa yakitolewa na wagombea uchaguzi wa ccm. Nilishuhudia kanga na vitenge vyenye picha za Mkapa vikitolewa kama Njugu kwa wananchi wa Mwanza na Bukoba bure.

Mwanachama wa CCM mzee Butiku alilalamika kwa Mkapa mwaka 2005 jinsi ambavyo baadhi ya wana ccm (Kikwete akiwemo) walivyokuwa wanatumia mamilioni (ya Rostam Azizi) kufanya kampeni za kumpata mgombea wa ccm

Report iliyovuja toka BOT inaonyesha jinsi ambavyo mabilioni ya pesa yalichotwa benki kuu ili kugharimia uchaguzi wa mwaka 2005.

Nadhani imefika wakati CCM ikaweka wazi vyanzo vya mapato ya pesa ambazo zimetumia na wagombea wake kwa chaguzi zote tatu.
Inabidi pia taarifa ya pesa na matumizi hayo iwekwe wazi kila mwezi au kila miezi mitatu ili wananchi wote waisome.

Hapa Marekani, kuna udhibiti mkubwa sana kwa wanasiasa kuhusu mapato na matumizi ya pesa kwenye chaguzi. Haijalishi chama gani kiko madarakani lakini vyama vyote vinatakiwa kutoa report kila miezi mitatu ya matumizi na mapato yanayotumika kwenye uchaguzi.

Nina hakika kuwa hili likifanyika, huyo anayesifia ushindi wa ccm hapa atakosa cha kusifia muda si mrefu.

Asante.
 
Utoto mwingine bwana,

Vyama vyote vya siasa vinatoa report zao kwa msajili wa vyama kwani hiyo haitoshi hadi unataka uwekewe report kwenye gazeti la mwanahalisi au Tanzania Daima? CCM inashinda chaguzi kihalali. Hayo ya kutoa rushwa ni visingizio tu vyenu wapinzani kwa kushindwa uchaguzi. Sio kila siku lazima uandike kitu hapa. Wakati mwingine inabidi ukae kimya na uache wengine waandike.
 
Utoto mwingine bwana,

Vyama vyote vya siasa vinatoa report zao kwa msajili wa vyama kwani hiyo haitoshi hadi unataka uwekewe report kwenye gazeti la mwanahalisi au Tanzania Daima? CCM inashinda chaguzi kihalali. Hayo ya kutoa rushwa ni visingizio tu vyenu wapinzani kwa kushindwa uchaguzi. Sio kila siku lazima uandike kitu hapa. Wakati mwingine inabidi ukae kimya na uache wengine waandike.

Naona wewe hujaacha kunifuatilia.

Swali ni kwamba, je wewe unataka msajili wa vyama peke yake ndiye apewe report au wananchi wote wanatakiwa kujua vile pesa ya ruzuku (zinazotokana na kodi) zinatumika.

Kwa nini hutaki pesa na vyanzo vya mapato ya ccm viwekwe wazi hapa? Wakati mwingine inahitaji effort kidogo tu kujua kile kilichomweka Kikwete madarakani na sababu inayomfanya awe na mafisadi kwenye uongozi wa chama na baraza lake.
 
Utoto mwingine bwana,

Vyama vyote vya siasa vinatoa report zao kwa msajili wa vyama kwani hiyo haitoshi hadi unataka uwekewe report kwenye gazeti la mwanahalisi au Tanzania Daima? CCM inashinda chaguzi kihalali. Hayo ya kutoa rushwa ni visingizio tu vyenu wapinzani kwa kushindwa uchaguzi. Sio kila siku lazima uandike kitu hapa. Wakati mwingine inabidi ukae kimya na uache wengine waandike.

Wewe ndiyo unatakiwa ukae kimya kama huna la kusema. Nani amekwambia kuwa ruzuku ya vyama ni pesa za msajili? Unashindwa kuelewa hata suala la msingi kuhusu pesa yako ya kodi inatumikaje. Halafu unaunyaunya kuuliza na nidhamu yako ya uoga. Inaelekea umeridhika status yako ya kutawaliwa na wakoloni.
 
Mkuu wangu, again ulitakiwa uombe katiba iongezewe hii ya vyama vya siasa kutoa mahesabu yao, hata huko US huwa serikali inahusika na hela zilizotolewa na serikali, na zile zilizochangwa na PACs, otherwise Bloomberg, alipotumia dola millioni 70 kule NY kupata u-Mayor hakuna aliyemuuliza zilitumikaje,

the ishu hapa inatakiwa iwe marekebisho ya katiba on matumizi ya vyama mkuu!
 
Kwani CCM hawana miradi inayowaingizia fedha...? Hivi Uhuru na Mzalendo wanayagawa bure...?
 
I dunno...but it won't make sense for them to still be in business while operating at a loss....if doesn't make dollars (Tshs.) then it doesn't make sense

Zingine hizi ni huduma (propaganda machine) zinazogharimiwa na pesa yako bila kujua. Usiniulize evidence...sina. Lakini naamini ujumbe umefika.
 
Kama huna "evidence" ni bora ukae kimya basi la sivyo kila mtu ataanza kusema yake na mwisho tutapoteza lengo...
 
Kuna Mwanaccm hapa anapenda sana kusifia ushindi wa ccm katika chaguzi zote kuanzia mwaka 1995 hadi leo kama dalili ya kuwa chama hicho kinapendwa na watanzania.

Nilikuwa Tanzania uchaguzi wa mwaka 95 na 2000 ambako nilishuhudia mamilioni ya pesa yakitolewa na wagombea uchaguzi wa ccm. Nilishuhudia kanga na vitenge vyenye picha za Mkapa vikitolewa kama Njugu kwa wananchi wa Mwanza na Bukoba bure.

Mwanachama wa CCM mzee Butiku alilalamika kwa Mkapa mwaka 2005 jinsi ambavyo baadhi ya wana ccm (Kikwete akiwemo) walivyokuwa wanatumia mamilioni (ya Rostam Azizi) kufanya kampeni za kumpata mgombea wa ccm

Report iliyovuja toka BOT inaonyesha jinsi ambavyo mabilioni ya pesa yalichotwa benki kuu ili kugharimia uchaguzi wa mwaka 2005.

Nadhani imefika wakati CCM ikaweka wazi vyanzo vya mapato ya pesa ambazo zimetumia na wagombea wake kwa chaguzi zote tatu.
Inabidi pia taarifa ya pesa na matumizi hayo iwekwe wazi kila mwezi au kila miezi mitatu ili wananchi wote waisome.

Hapa Marekani, kuna udhibiti mkubwa sana kwa wanasiasa kuhusu mapato na matumizi ya pesa kwenye chaguzi. Haijalishi chama gani kiko madarakani lakini vyama vyote vinatakiwa kutoa report kila miezi mitatu ya matumizi na mapato yanayotumika kwenye uchaguzi.

Nina hakika kuwa hili likifanyika, huyo anayesifia ushindi wa ccm hapa atakosa cha kusifia muda si mrefu.

Asante.

Wezi hawa hawawezi kufanya hivyo!. Hata wakitamka wanafanya haisaidii kitu kwa sababu hesabu za chama hazikaguliwi! Kwanza sijui hata kama hizo hesabu wanazo. Kama utakumbuka Balozi wa Marekani aliwasemea hovyo kuhusu kampuni yao inayosimamia ujenzi wa bomba la mafuta toka Dar. Aliwaambia nyinyi kama chama tawala hamuwezi kuwa na kampuni ambayo chochote itakachofanya kampuni hiyo kitakuwa kimejaa mikingamo na mizengwe ambayo haitaeleweka kwa wananchi, lakini jamaa wamenyamaza kimya hadi leo hawajasema chochote kuhusiana na tuhuma hizo.

Kuna haja ya kufanya kampeni kali kuhakikisha vyama vyote vinakuwa na mahesabu ili kuonyesha mapato na matumizi yao, ambayo yanakaguliwa kila mwaka. Hili litasaidia sana kupunguza wizi unaofanywa na CCM wa pesa za walipa kodi. BOT kuna pesa nyingi tu zilikuwa zinatoka kiajabu ajabu na kuingia kwenye akaunti ya kampuni ya chama (nimesahau jina lake) karibu na uchaguzi mkuu wa 2005. Bank account ya kampuni hiyo ilifunguliwa j'pili siku ambayo mabenki hayafanyi kazi. Halafu wenyewe wanajiita CCM nambari one! Ni nambari one kwa ufisadi, kupokea rushwa, uroho wa utajiri wa haraka haraka na kuiangamiza Tanzania.
 
Kuna haja ya kufanya kampeni kali kuhakikisha vyama vyote vinakuwa na mahesabu ili kuonyesha mapato na matumizi yao, ambayo yanakaguliwa kila mwaka. FULL STOP!

Mkuu Bubu,

Heshima mbele mkuu, unajua kati ya kumi bora wa hii forum wewe ni mmoja wao pia no question kabisaa!
 
Nashukuru sana Mkuu kwa kunipa hesima kubwa kama hiyo. Wote tuko hapa kuchangia mawazo yetu ili kuiboresha nchi yetu na hatimaye maisha ya Watanzania wote. Hatumchukii mtu yeyote ndani ya serikali wala CCM, bali tunachochukia na maamuzi yao mbali mbali ambayo mengi yanafanyika kwa kificho na mara nyingi hayana maslahi kwa nchi yetu.
 
Binti kila chama kina utaratibu wake mnataka mjue zimetumika wapi so that mkopi?kama unataka ujue matumizi ya ccm anagalia network ya ccm utajua ruzuzku inataumikaje pia report ya mapato na matumizi ya ccm hua tunajua wana ccm kama hujui basi ur not amaong US.

Pia naona kuna terminology mpya MAFISADI kila mkiandika sentesi nyie watu wenye mawazo kama ww Fisadi lazima litamkwe mnajua maana ya fisadi?au bcs slaa na triangilar mind wenzie wametamka then na ww unatamka?

CCM ipo responsible kutoa maelezo kwa wana ccm ambao wanalipia ADA za uanacham only na matumizi yake yanajulikana we dont need to weka ktk public.

KIDUMA CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Zingine hizi ni huduma (propaganda machine) zinazogharimiwa na pesa yako bila kujua. Usiniulize evidence...sina. Lakini naamini ujumbe umefika.

Ushahidi uko wazi. Hawa jamaa wanatumia kodi yangu kuendeshea UHURU. Gazeti gani haliuzi hata nakala elfu 5 lakini linapata matangazo karibu yote ya serikali? Kwa kawaida matangazo si yanapaswa kuwekwa kwenye magazeti yenye wasomaji wengi? Sasa ya nini kupeleka matangazo UHURU? Huku ni kutumia kodi yangu kufanya propaganda za CCM

Asha
 
Kuna conflict of interest ya wazi kabisa Chama tawala kinapokuwa na biashara na serikali. Si halali serikali kutoa tenda au kutoa contract kwa chama chake. Serikali yetu ni Serikali ya CCM. Ni kosa serikali ya CCM iingie mikataba ya kiuchumi na CCM.

Siku za nyuma kulikuwa na SUKITA. Tunajua mapesa ya uma yalimalizikia pale. Inafilisiwa kwa sasa, na nadhani bado inameza, kwa siri kubwa, fedha za serikali
.
Huko nyuma, wakati wa chama kimoja, kuna wakati watu waliuliza iweje CCM itengewe fedha nyingi hivyo za uma. Mzee Kawawa alijibu zilikuwa ni fedha za consultancy. Yaani serikali ilibidika kulipa consultancy fees kwa chama chake.

Fedha zilizochukuliwa na CCM kupitia BoT ni kama shilingi moja kati ya kila shilingi 10 za bajeti. Zilikuwa fedha nyingi kiasi cha kutisha. Kwa hivyo, hizo hongo nyingi walizopewa wananchi kama alivyosema Mwafrika wa Kike, zilitokana na fedha za wananchi. Yaani CCM inachukua kwa nguvu (au kwa njia za wizi) fedha za wananchi kisha inazitumia kununua kura za wananchi.

Kumbukeni kwamba kuna wakati hata viwanja vikuu vya michezo vilidaiwa na CCM kwamba ni mali yake. CCM ina historia ya kupora mali ya wananchi. Haiwezekani kabisa CCM ikubali kuwatangazia wananchi, kwa ukweli, mapato na matumizi yake. Mapato ya kuchota kiasi cho chote upendacho Hazina utayatangazaje?

Hatuwezi kutegemea msaada toka kwa Msajili wa Vyama kwenye jambo hili. Kwani anachaguliwa kwa ushirikiano na vyama vyote? Kwa mpango uliopo, Msajili wa Vyama lazima awe mwana CCM (overtly or covertly).

Mwafrika wa Kike: well done. Lakini jua kabisa hali ya Tanzania itabaki kuwa ya mipango mibaya hadi CCM watakapowekwa upinzani kwa angalau kipindi kimoja au viwili. Mawazo yako mazuri lakini umegonga mwamba.
 
Mzizi wa matatizo yote wanayoyapata vyama vya upinzani unaanzia hapa - kwenye uwezo wa pesa. Inafaa wapinzani walichukulie hili jambo kwa umhimu unaolistahili, na hasa kabla ya chaguzi za 2010. CCM inachuja, na sio sera zake zinazoiwezesha ipate kura nyingi za wananchi. Siasa yao imekingama zaidi kwenye matumizi ya pesa nyingi wanazozipata kwa njia mbalimbali, nyingine zikiwa si kwa njia iliyo halali; hasa zile wanazochangiwa na matajiri wanao invest for future gain.
Kwa uhakika, the playing field is not level at all!

Wapinzani, fanyeni utafiti wa kina kuhusu jambo hili kama mwanzo wa kuelewa jinsi mnavyofungwa magoli ya mikono mara kwa mara, ili baadae muweke tahadhari. Hamtaweza kushindana, hata muwe na sera nzuri namna gani, kama mshindani wenu yeye ananunua favors za wananchi, na kuuza sera kwa matangazo.

Ni jambo lililo bayana, mwenye uwezo (fedha) wa kujitangaza hufanikiwa. Waulizeni wauza bidhaa ni kwa vipi hutumia pesa nyingi kuzitangaza bidhaa hizo. Siasa na wanasiasa sasa imekuwa ni bidhaaa.
 
Bimdogo, changamoto yako hii hawakuifanyia kazi. Naungana na wewe, wakati umefika ili CCM siyo tu iseme kuwa ni "safi" basi ijioneshe kuwa ni safi kwa kuweka mapato na matumizi yake yote ya 2005/2006 hadharani ili kuziba kizabizabina.

Inashangaza kuona chama kichanga kama Chadema kimeweka mahesabu yake hadharani.. wakati chama kikongwe kama CCM kinaenda "nyalinyali"..
 
Bimdogo, changamoto yako hii hawakuifanyia kazi. Naungana na wewe, wakati umefika ili CCM siyo tu iseme kuwa ni "safi" basi ijioneshe kuwa ni safi kwa kuweka mapato na matumizi yake yote ya 2005/2006 hadharani ili kuziba kizabizabina.

Inashangaza kuona chama kichanga kama Chadema kimeweka mahesabu yake hadharani.. wakati chama kikongwe kama CCM kinaenda "nyalinyali"..

Nimesubiria sana dear kwa hili kutokea bila majibu. Kuna sehemu nilisoma kuwa ccm inapokea ruzuku karibu bilioni moja za madafu kila mwezi. Kama hizi pesa haziwekwi wazi ikajulikana zinakwenda wapi, basi ni makosa sana kushangaa kwa nini pesa za BoT hazina maelezo kuwa zimekwenda wapi!

Kwa hili bado nasubiria majibu!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom