TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
Hiki ni kituko jamani,chama cha mapinduzi(ccm) wametoa mpya kwa wananchi baada ya kupita na gari lao la watangazo wakiwatangazia wananchi ya kwamba wajitokeze katika eneo la shule ya msingi majengo kumsikiliza dr slaa ambaye atahutubia tena katika eneo hilo,ikumbukwe eneo hilo ndio ambalo dr slaa alihutubia juz maelfu ya wanasongea,lakin ukwel dr slaa alikuwa hautubii teno ktk eneo hilo bali mgombea ubunge wa ccm Emmanuel Nchimbi ndiye aliyekuwa anamkutano ktk eneo hilo.watu walioamin ya kwamba dr atakuwa hapo walienda na walipofika ktk eneo la tukio walikuta ngoma zikipigwa huku kukiwa na bendera nyingi za ccm basi walitukana na kuondoka kwa hasira.Baadhi ya akina mama na akinabibi ambao ndio walikuwa wahudhuliaji wakuu wa mkutano huo ulioanza majira ya saa 6 za mchana had saa 12 jioni walikutwa wakilalamika ktk maeneo ya mkutano baada ya maroli ambayo yaliwatoa kutoka maeneo ya pembeni ya mji na kuwaleta kwenye mkutano huu,kutoonekana baada yamkutano kuisha ili ya warudishe ktk maeneo yao hali iliyosababisha watembee kwa miguu kutoka katikati ya mji had maeneo yao waliyotoka ambayo mengine ni zaid ya kilometa 20 had 25..huku wakizomewa njia mzima na wananchi wakaz wasongea mjin ambao walikuwa wanawaona walivyokuwa wanalalamika tena wengine wakisema ya kuwa wamekalishwa na njaa siku mzima na wanarud kwa miguu baada ya marol kuwarudisha watu kwa upendeleo..