CCM watashindwa kwa kishindo uchaguzi mdogo arusha-tusishangae,sababu hizi hapa Watanzania wenzangu

MMASSY

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
290
193

Kwanini CCM watakosa udiwani kwa kata zote za arusha?hili najua kwa wale tulioko hapa Arusha si swala geni lakini naandika kuufahamisha ulimwengu kuhusu kuondoka kwa CCM rasmi Arusha na madhambi yao yote.Kampeni za uchaguzi hapa zinaendelea na mambo kimsingi ni magumu kwa CCM kuliko kawaida.Kwenye kata zote nne wamekuwa wakishindwa kufanya mikutano na kuahirisha mara kwa mara kutokana na mahudhurio hafifu.Kata ya Elerai ngoma ni nzito mno,kata ya Kaloleni juzi Mwigulu Nchemba alizomewa na hii ilitokana na utamaduni wake wa kutumia masaa mawili na nusu kumtukana Leman na kusahau kwamba anatakiwa kumwombea kura diwani wa ccm.Baada ya mkutano alizomewa vibaya na wamama na wanawake walioonekana kumchukia sana kutokana na matusi yake huku wakilalamika kuwa amewapotezea muda wao.Kule kata ya Temi walileta siasa za udini na ukabila mwisho wa siku zikawageukia na sasa hawawezi hata kufanya mkutano wa watu kumi.Kata zote hapa ni mwiba mkali kwa CCM na dalili ni kwamba wataondoka kwa aibu kubwa kuliko ya mwaka 2010.Sasa nieleze ni kwanini watakosa udiwani arusha

Moja,CCM kupitia Meya wa Kichina(Gaudence Lyimo)na madiwani wa CCM walitumia kura ya Veto katika halmashauri na kuidhinisha kiasi cha sh.Milioni 365.6 kutumika katika mbio za Mwenge hapa Arusha,hili Chadema wamelitumia vizuri kwa kuwaeleza wananchi namna madiwani wa CDM walivyopinga kitendo hiki lakini CCM kwa wingi wao wakapitisha kiasi hiki kikubwa kabisa cha fedha kwa ajili ya kukimbiza mwenge ambao hoja ya Chadema ni kuwa mwenge unatakiwa ujengewe jengo la ukumbusho na uwekwe huko kama kuna anayetaka kuuona kwenda huko na kuuona.Ikumbukwe kuwa hapa arusha katika hospitali ya Mount Meru hakuna vitanda vya kutosha kuwahudumia wakina mama wanaotaka kujfungulia,Zahanati ya Levolosi imezidiwa na wagonjwa,Kuna shule ambazo hazina madawati wala walimu wa kutosha mathalani shule ya sekondari arusha day ambayo wanafunzi wanaingia kwa shift.Diwani wa kata ya Daraja mbili CHADEMA alieleza kwa kina katika mikutano ya hadhara namna ambavyo mama mmoja alivyofariki muda mfupi baada ya kupelekwa Hospitali ya Levolosi na trekta kwenda kujifungua takribani kilomita 20.Madaktari wa Levolosi alithibitisha kwamba mama huyo alitikiswa sana kitu kilichopelekea kupoteza maisha yake nay a mtoto wake akiwa tumboni.Katika mazingira haya,akina mama na wababa watakaotoa kura kwa ccm ni wale wenye maisha mazuri na wasiokumbwa na shida kama hizi ambao ni wachache sana na au ikibidi wasiwe na akili nzuri.

Pili,Kupigwa,kujeruhiwa na kuteswa na wafuasi wa CHADEMA,Katika kampeni hizi mara nyingi tumeona na kusikia kuwa vijana wa CCM wa ulinzi wajulikanao kama Green Guards wamekamatwa katika mikutano ya CHADEMA wakiwa na mashoka,visu,mishale na vitu vyenye ncha kali.Kama haitoshi,katika kata ya Themi na Elerai ngoma ni nzito kupita maelezo na CCM bila kujua wameanza kutumia mbinu chafu za kuteka,kupiga na kujeruhi wanachama wa CHADEMA.Katika kata ya Kimandolu huko CCM wanazomewa kila kona na hata ninavyoandika uchambuzi rafiki yangu mmoja mwaminifu kanieleza kuwa kuna wamama wameonekana tu wamevaa mavazi ya kijani wakazomewa hadi kiasi cha fedheha lakini hawakudhuriwa na wananchi.Kwa siasa hii ya mashoka,visu,sime na "vitu vyenye ncha kali",kumefanya CCM waendelee kujijengea taswira mbaya ya ugaidi na kuonekana chama hatari sana kwa mustakabali wan chi na wakazi wa Arusha na kwa hiyo wamejenga chuki mbaya sana ya wananchi dhidi yao kiasi cha kufanya kura zao kufikia au kuwa pungufu ya namba za kiatu.

Tatu,Kunyayasa wamachinga mjini.Katika kipindi cha kuanza kuzindua jiji la arusha hadi sasa,wamachinga,wamama kwa vijana wanaouza bidhaa zao kwa kuzunguka mjini na hata kuegesha mahali,wamekuwa hawapumziki kwa kusumbuliwa na mgambo wa jiji.Mara nyingi mgambo hawa wakikamata mzigo wa machinga wanakamata mzigo wa mtu wanyemhisi kuwa mwanachama wa Chadema na hata kwa bahati mbaya wakikamata mali ya mwana ccm anarudishiwa mara moja.Hili limeongeza chuki mara dufu kwa chama cha ccm na kwa kuwa wapiga kura karibia wote wa kata hizi hasa ile ya Elerai na Kaloleni ni machinga/wachuuzi wa biashara ndogondogo hapa mjini.Kwa hoja hii ni vigumu na haitawaingia wana wa arusha kupiga kura kwenye dole gumba manake kwa kufanya hivyo wanaamini wamemchagua adui yao kuwa kiongozi wao.

Nne,Soko la NMC,Eneo hili linajulikana na National Milling Corporation nab ado ni la mali ya NMC ila lilichukuliwa kisiasa na kufanywa soko kwa nia ovu ya kuwanyima Chadema eneo la kukutana na umati wao mkubwa wa wananchi ambapo palikuwa eneo lao la kukutana pale wanataka kukutana na mbunge wao na/au viongozi wengine wa chama ngazi za juu.Eneo hili mimi nilikuwa shahidi baada ya Chadema mwaka jana kutaka kukutana na wanchi wake kwa nia ya kueleza yaliyokuwa yanajiri katika kesi ya Lema,palijengwa ndani ya usiku mmoja na kesho yake wamachinga wakatakiwa kuhamia huko.Ililazimika nguvu kubwa sana kuhakikisha eneo hili linageuzwa kuwa soko.Tatizo hapa CCM na RC wao walishindwa kusoma alama za nyakati.Chadema kwa uadilifu walitumia kete hii vizuri sana kupata uungwaji mkono kwani wao walikubali eneo hili kuwa moja ya maeneo ya wamachinga lakini lilikuwa nab ado linabaki kuwa si eneo salama sana kwa kuwa mvua ikinyesha maji yote machafu ya jiji yanatuama hapo.Lakini wakafaulu zaidi kwa kunasa mbinu za CCM katika kuwapatia maeneo ya kufanyia biashara kwa kuzingatia itikadi zao.Hii ilitokea pale ambapo wananchi walielezwa kwenda kujishikia maeneo wenyewe hali iliyosababisha wananchi kuumizana wenyewe kwa wenyewe wakigombania maeneo sokoni hapo.Lakini haikuisha muda ikaja orodha inayotoa majina ya machinga waliosajiliwa kwa mkuu wa wilaya/halmashauri kwamba tayari walikuwa wameshapewa baadhi ya meneo ambayo wananchi walikuwa wameshagawanywa.Baada ya wananchi kuyaona majina yale,wakabaini kuwa ni wamachinga wenzao lakini wanachama wa CCM na kwa hiyo wakaamini kuwa wao wanafukuzwa kwa kuwa ni wana wa CHADEMA.Katika hali hii kwa sisi wenye kuelewa siasa ni nini bila kujali itikadi zetu,ni ngumu sana kwa Mmachinga yeyote,au ndugu yake,au rafiki yake aliyepata kusikia kadhia hii kuipa kura CCM Manake kauli za kuwaondoa machinga mjini na kuwapeleka NMC ilikuwa kusafisha jiji.N a kwa maana hiyo Machinga ni uchafu,lakini leo watawala wanategemea uchafu huu huu uwapigie kura.Hapana,nasema hapana kwa kuwa hata kura kama hizo bado zitakuwa chafu tu.Haziwezi kamwe kusafishika!!

Tano,rushwa na ufisadi uliokithiri halmashauri.Kwa mwaka mmoja tu katika jiji la arusha,kuna upotevu wa fedha kiasi cha Tsh.15 Billioni,katika hali hii wananchi wameelimishwa vya kutosha juu ya upotevu huu mkubwa na matumizi ya anasa ya fedha za walipa kodi maskini wan chi hii.Hakuna mwenye majibu ya fedha hizi isipokuwa Chama tawala na Meya wao Bw.Gaudence Lyimo,madiwani wa CCM na mkurugenzi wa Jiji.Wao CCM walidhani ni siri kwa kuwa wanaongoza halmashauri lakini CHADEMA kwa kutumia mtandao mkali walenasa ufisadi huo na wameelimisha vizuri wananchi na hasa namna fedha hizo zingetumika kuwasaidia kuondokana na umaskini,wameelimisha umma namna fedha zao zilivyochezewa,na wameonyesha mfano kwa kupiga marufuku michango ya madawati,chakula na michango ya ujenzi katika shule kwa kuwa fedha zipo nyingi halmashauri.Katika mazingira haya,hata kama ni kipofu ametumwa kwenda kupiga kura ataweka bayana kuwa ni wapi pa kupiga kati ya ukweli na uongo,kati ya nuru na giza.Matokeo ya kipindi hiki Arusha yatakifundisha somo moja kubwa CCM na watanzania kuwa wananchi wa sasa wanasikia na kufikiri sa sawa.


Sita
,siasa za matusi,majivuno,dharau na kejeli.CCM kwa mara nyingine wamefanya kosa kubwa kisiasa Arusha,Mwigulu Nchemba,Juliana Shonza na Mtela Mwampamba wamekuja Arusha kwa gia ya matusi,vijembe,kejeli na Mkwara.Kama vile hawana kumbukumbu kwamba kule Arumeru mashariki walitumia mbinu hii na kuadhibiwa vikali na wazee,vijana na wamama wa kimeru.Wamekuja kufanya mikutano waliyokuwa wanatukana wananchi wanaoipenda Chadema na Lema pamoja na viongozi wengine wa Chama hiki.Ukiachia mbali vijana hawa(Juliana na Mtela)Mwigulu ni msomi tena mzuri tu lakini sio wa siasa(isiwe tatizo).Ameshindwa kutumia Intelectual capacity yake kuwaomba kura wana Arusha badala yake akajikuta akishusha mitusi,lawama na kejeli kwa Chadema na Lema ambao kimsingi wanapendwa kuliko CCM hapa Arusha.Arusha kuna wacha Mungu,wapenda haki,wavuta bangi,wanywa viroba,wezi,majangili,watu wema na wengine kama ilivyo sehemu nyinginezo nchini na duniani.Unapokuwa jukwaani unatakiwa kufahamu diversity hii katika jamii na kutumia jukwaa vizuri kuwaunganisha watu hawa wote wakukubali wewe.Lakini ninaanza kuwa na wasi wasi na Elimu ya Mwigulu kushindwa kutumia elimu yake vizuri na inawezekana hata kupatikana kwa elimu hii kulikuwa na namna.Amekuja arusha kuonyesha mwananchi aliyemwagiwa tindikali katika uchaguzi wa Igunga(of which is past event)na kusema kuwa hiyo ni kazi ya Chadema.Inawezekana ikawa kweli lakini kufanya hivyo kwa Mwigulu ni sawa na kwamba sasa anaomba huruma ya wananchi.Inajulikana wazi nchi hii mtu akifanya kosa kama la kumwagia tindikali mtu anapelekwa mahakamani.Sasa kama utaratibu wa ndani ya chama na serikali inayoongoza Tanzania umebadilika ni vizuri Mwigulu Nchemba akaeleza wananchi na ni lini tulibadilisha katiba ikasomeka hivyo.Wananchi wa Arusha wanaelewa adui wao ni mmoja tu,CCM.Wanaamini huyundiye anayeweza kuwamwagia tindikali,ndiye anayeweza kuwakata mashoka,visu na mishale.Wanaamini ni huyu adui wao anayeweza kuwango'a kucha,macho,kope na hata meno bila ganzi.Hawaamini kamwe kama adui yao atakuwa CHADEMA Ambaye wamemwamini na kuishi naye kirafiki kwa miaka kadhaa sasa.Kwa hiyo,ujio wa akina Mwigulu Nchemba,Juliana Shonza na Mtela Mwampamba Arusha hakujainusuru CCM bali kumezidi kuwachimbia kaburi zaidi na kupunguza kura zao hadi kufikia namba ya kiatu.

Saba,
Kodi zisizo na mashiko katika masoko ya hapa Arusha mjini.Hapa mjini kuna masoko kadhaa kama vile Kilombero,Soko kuu,na mengineyo mengi.Sio wanaume wala wanawake wanaelewa utaratibu maalumu wa kozi zinazotozwa kwenye haya masoko.Kuna fedha zinakusanywa kwa wamama na wababa zisizo na maelezo.Haieleweki kwamba fedha hizo zinaenda wapi.Wakala anayekusanya anakanwa na serikali kwamba hawana mkataba,huku serikali nayo ikikusanya za kwake kwa utaratibu usio rasmi.Ikumbukwe kuwa kila unapokuwa unanunua bidhaa kwa bei ya jumla/rejareja kwa mtu tayari umelipa kodi,bado unaenda sokoni unalipia kodi ya eneo unapofanyia biashara(pango),hujapumzika anakuja wakala wa ushuru anataka ushuru wa kila siku(hauna maelezo),kama vile unataka kupumzika anakuja mwingine anataka ushuru wa usafi n.k.Katika hali hii ni kama vile tunaishi kwenye jiji lisilo na wenyewe.Wafanyabiashara wanatumika kama shamba la bibi.Wanasiasa wa upinzani hususani CHADEMA wamefanikiwa kuwaeleimisha wananchi namna wanavyotozwa kodi zaidi ya kumi na ndio maana sababu biashara hazisongi mbele kabisa.Wamewaelewa sana Chadema na tusishangae ushindi wa kishindo utakaofuata jumapili ya kesho kutwa.CCM hawana ubavu wala ujasiri wa kuondokana na dhambi hii kwa kuwa muda wa kurekebisha haya ulishapita nao ulikuwa kabla ya uchaguzi huu kutangazwa.Kwa sasa hawawezi tena.Kuna msemo kwenye Biblia unasema Kesheni kwa sababu hamjui siku wala saa atakapokuja Mwana wa Mungu".CCM chukueni hiyo.

Nane,matatizo ya vyuoni na ukosefu wa ajira.Haujaisha muda mrefu tangu zitokee vurumai hapa chuo cha Uhasibu Arusha.Katika sakata lile Mkuu wa Mkoa alijitoza kichwa kichwa na kumtuhumu Lema kuwa ndiye chanzo.Wote tulishuhudia na kwa kuwa lipo mahakamani na kwa kuwa mimi pia ni mwanasheria nisizungumzie sana hili.Lakini sheria hainizuii kuzungumzia athari za tukio lile kisiasa kwa kuwa sitaingila mwendelezo wa kesi(Legal Proceeding).Cd zimesambazwa mtaani na wananchi wa Arusha wameona namna mkuu wa mkoa na mbunge Lema walivyoenda Njiro.Kila mwenye macho anaona nani mwenye kosa kati ya Lema na Mulongo.Ni dhahiri kwamba hata watawala wameona namna ambavyo wamepata hasara ya kisiasa kwa kupambana na Lema badala ya kumtafuta muuaji wa mwanafunzi kule Njiro.Kama haitoshi huku mtaani na kwenye hizi kata kuna wanafunzi na ndugu wa wanafunzi wanaosoma Njiro.Wameapa kukiadhibu chama cha Mapinduzi kwa kura.Ajira ni tatizo linaloizika CCM sasa hapa nchini,vijana wengi wapo mjini hawana ajira,wanajaribu bahati zao sehemu mbalimbali na wengine wanafanya kazi ya siasa kwa kiwango cha hali ya juu.Vijana wanatoa elimu ya mageuzi ya kiutawala,kiuchumi na hata kijamii.Muda wote vijana wako kazini kuhakikisha wale watu wanaowatetea wao wanakuwa viongozi katika jamii.Wako mitaani kuhakikisha kuwa Chama ambacho kwao ni rafiki kinashika hatamu.Katika baadhi ya sehemu nilizotembelea hapa Arusha vijana wanaapa kwamba CCM kushinda uchaguzi huu ni sawa na matusi makubwa kwao,wazazi na walezi wao.Wameapa kukiangamiza chama hiki katika uchaguzi wa jumapili kwa kura.Wanajitolea kufanya kazi za siasa usiku na mchana na hawataki hata kujulikana na kupewqa nafasi wala heshima katika Chadema.Wameapa kwamba hata wakiokota shilingi mia au hamsini wataichangia Chadema ili ishinde uchaguzi huu.Kuna vijana walioko kazini nao wanatumia muda wao wanaoupata kuhakiksha kuwa wazee,wamama na vijana wanapata elimu ya kutosha kabisa kuchagua mabadiliko.

Tisa,uwepo wa viongozi wa Chadema wenye ushawishi mkubwa,Kama chama kilicho serious na kazi zake,Chadema kinapanga mashambulizi kulingana na eneo mtu anakokubalika.Kuna maeneo ambayo Lema anapangiwa kwa sababu maalumu kama vile kata ya Temi,Elerai na kwingineko,lakini pia kuna maeneo yaliyotembelewa na Mbowe,Nassari,Natse, na viongozi wengine wenye ushawishi mkubwa.Ukiangalia kwa umakini utabaini kuwa Chadema kimetumia mbinu zaidi(Strategies)kukikaba Chama Cha Mapinduzi ambacho hadi sasa kimeshindwa kuwafikia wananchi wengi zaidi.Nasema haya kwa kuwa wakati CCM wamejinasibu kuwafikia wanachama na wananchi majumbani na hongo(rushwa) tena usiku,Chadema kinakwenda nyumbani kwa wananchi asubuhi na mchana na bila kubeba hongo yoyote,kinatembea hatua kwa hatua,kitongoji kwa kitongoji,mtaa kwa mtaa,kijiji kwa kijiji na hata kata kwa kata.Hii imefanikiwa kwa kuwa wanapendwa na wananchi kwa kuwa wanasema yale wananchi wanayoyapenda,hawako mbali na jamii wala hawaishi Dar na kusiemea arusha hapana,kila kukicha wako na wananchi kwenye shida na raha.Wameweza kugawana vizuri majukumu kati ya viongozi wenyeji,wageni na wananchi pamoja na wanachama wao na dalili hapa ushindi ni lazima.

Kumi,Ulinzi wa kura wa hali ya juu,hadi naandika waraka huu,mbinu mbalimbali za wizi ambazo zimepangwa na CCM kushinda angalau kata moja kati ya nne zimenaswa na Chadema.Tayari tangia mwanzo wa kampeni wananchi wamekuwa wakielezwa mikakati ya CCM kuhujumu huu uchaguzi na kinachoonekana Chadema na Wananchi wamejipanga kikamilifu.CCM walipanga kununua kadi za kupigia kura na tayari wamenaswa,walipanga kuwanunulia viroba vijana wao na kuwavalisha mavazi na skafu za Chadema ili walete vurugu na kusingizia Chadema tayari wamenaswa,walipanga kuwajeruhi ama kuwauwa viongozi wa Chadema na wanachama walioonekana kuwa Mwiba kwao tayari wameumbuliwa na katibu wao wa fedha tayari amefunguliwa mashitaka ya kutishia na bunduki mbele ya OCD.Wamepanga mbinu nyingi na hapa sitasema zile ambazo hazijatajwa na viongozi wa Chadema manake hadi zipelekwe kwanza usalama ndio tuziseme hapa.Kwa sasa CCM wamerudisha silaha nyuma kujipanga manake juzi wamepita wakigawa sukari maeneo ya Ilboru ili wapewe kura,wamepita wakihonga kati ya 20000/= na 100000/= ili wauziwe kadi za kupiga kura.Kinachoshangaza ulimwengu ni kwamba wakati rushwa ikitembea waziwazi,Makao makuu ya TAKUKURU yapo kwenye kwenye kata mojawapo ya uchaguzi na sii nyingine bali ni kata ya Kaloleni.Hili bado linatuingiza Tanzania katika maajabu ya dunia.Mpango uliopo sasa na ambao tayari umekwama ni kwamba CCM wamejipanga kununua sukari nyingi siku moja kabla ya huu uchaguzi na kuichanganya na mchanga mweupe(kama sukari)Watavaa mavazi ya Chadema na watatumia sare na salamu za Chadema kuwagawia baadhi wa wapiga kura majumbani mwao wakisema ni Chadema inaomba kura.Sasa hii sukari lazima watakaogawiwa watapikia chai siku ya kura asubuhi,watakapokuta imechanganyikana na mchanga watailaumu Chadema na kuona kama imewakejeli na kwa hiyo hawataichagua Chadema.Hiyo ndiyo CCM bhana,wazee wa Intelligensia mpo hapo?Chadema wamefanikiwa kuwaelimisha sana wananchi kuhusu mbinu hizi na nyinginezo chafu.Na pia kupitia kanda ya kaskazini,Chadema wameagiza walinzi wa kura toka mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Manyara kwa nia ya kuimarisha ulinzi wa kura na uwakala.Hapa kazi inayoendelea sasa ni namna gani ya kulinda kura na si vinginevyo!! Nimeandika haya kwa muono wangu na uhalisia wa mambo ulivyo hapa Arusha.Kwa wale mliopo mbali na hapa msije mkasikia CCM wamepata kura sawa na namba ya kiatu mkafikiri ni bahati mbaya,hapana,wananchi wameamua na ni lazima wasikilizwe. Ni hayo tu
 

Kwanini CCM watakosa udiwani kwa kata zote za arusha?hili najua kwa wale tulioko hapa Arusha si swala geni lakini naandika kuufahamisha ulimwengu kuhusu kuondoka kwa CCM rasmi Arusha na madhambi yao yote.Kampeni za uchaguzi hapa zinaendelea na mambo kimsingi ni magumu kwa CCM kuliko kawaida.Kwenye kata zote nne wamekuwa wakishindwa kufanya mikutano na kuahirisha mara kwa mara kutokana na mahudhurio hafifu.Kata ya Elerai ngoma ni nzito mno,kata ya Kaloleni juzi Mwigulu Nchemba alizomewa na hii ilitokana na utamaduni wake wa kutumia masaa mawili na nusu kumtukana Leman na kusahau kwamba anatakiwa kumwombea kura diwani wa ccm.Baada ya mkutano alizomewa vibaya na wamama na wanawake walioonekana kumchukia sana kutokana na matusi yake huku wakilalamika kuwa amewapotezea muda wao.Kule kata ya Temi walileta siasa za udini na ukabila mwisho wa siku zikawageukia na sasa hawawezi hata kufanya mkutano wa watu kumi.Kata zote hapa ni mwiba mkali kwa CCM na dalili ni kwamba wataondoka kwa aibu kubwa kuliko ya mwaka 2010.Sasa nieleze ni kwanini watakosa udiwani arusha Moja,CCM kupitia Meya wa Kichina(Gaudence Lyimo)na madiwani wa CCM walitumia kura ya Veto katika halmashauri na kuidhinisha kiasi cha sh.Milioni 365.6 kutumika katika mbio za Mwenge hapa Arusha,hili Chadema wamelitumia vizuri kwa kuwaeleza wananchi namna madiwani wa CDM walivyopinga kitendo hiki lakini CCM kwa wingi wao wakapitisha kiasi hiki kikubwa kabisa cha fedha kwa ajili ya kukimbiza mwenge ambao hoja ya Chadema ni kuwa mwenge unatakiwa ujengewe jengo la ukumbusho na uwekwe huko kama kuna anayetaka kuuona kwenda huko na kuuona.Ikumbukwe kuwa hapa arusha katika hospitali ya Mount Meru hakuna vitanda vya kutosha kuwahudumia wakina mama wanaotaka kujfungulia,Zahanati ya Levolosi imezidiwa na wagonjwa,Kuna shule ambazo hazina madawati wala walimu wa kutosha mathalani shule ya sekondari arusha day ambayo wanafunzi wanaingia kwa shift.Diwani wa kata ya Daraja mbili CHADEMA alieleza kwa kina katika mikutano ya hadhara namna ambavyo mama mmoja alivyofariki muda mfupi baada ya kupelekwa Hospitali ya Levolosi na trekta kwenda kujifungua takribani kilomita 20.Madaktari wa Levolosi alithibitisha kwamba mama huyo alitikiswa sana kitu kilichopelekea kupoteza maisha yake nay a mtoto wake akiwa tumboni.Katika mazingira haya,akina mama na wababa watakaotoa kura kwa ccm ni wale wenye maisha mazuri na wasiokumbwa na shida kama hizi ambao ni wachache sana na au ikibidi wasiwe na akili nzuri. Pili,Kupigwa,kujeruhiwa na kuteswa na wafuasi wa CHADEMA,Katika kampeni hizi mara nyingi tumeona na kusikia kuwa vijana wa CCM wa ulinzi wajulikanao kama Green Guards wamekamatwa katika mikutano ya CHADEMA wakiwa na mashoka,visu,mishale na vitu vyenye ncha kali.Kama haitoshi,katika kata ya Themi na Elerai ngoma ni nzito kupita maelezo na CCM bila kujua wameanza kutumia mbinu chafu za kuteka,kupiga na kujeruhi wanachama wa CHADEMA.Katika kata ya Kimandolu huko CCM wanazomewa kila kona na hata ninavyoandika uchambuzi rafiki yangu mmoja mwaminifu kanieleza kuwa kuna wamama wameonekana tu wamevaa mavazi ya kijani wakazomewa hadi kiasi cha fedheha lakini hawakudhuriwa na wananchi.Kwa siasa hii ya mashoka,visu,sime na “vitu vyenye ncha kali”,kumefanya CCM waendelee kujijengea taswira mbaya ya ugaidi na kuonekana chama hatari sana kwa mustakabali wan chi na wakazi wa Arusha na kwa hiyo wamejenga chuki mbaya sana ya wananchi dhidi yao kiasi cha kufanya kura zao kufikia au kuwa pungufu ya namba za kiatu. Tatu,Kunyayasa wamachinga mjini.Katika kipindi cha kuanza kuzindua jiji la arusha hadi sasa,wamachinga,wamama kwa vijana wanaouza bidhaa zao kwa kuzunguka mjini na hata kuegesha mahali,wamekuwa hawapumziki kwa kusumbuliwa na mgambo wa jiji.Mara nyingi mgambo hawa wakikamata mzigo wa machinga wanakamata mzigo wa mtu wanyemhisi kuwa mwanachama wa Chadema na hata kwa bahati mbaya wakikamata mali ya mwana ccm anarudishiwa mara moja.Hili limeongeza chuki mara dufu kwa chama cha ccm na kwa kuwa wapiga kura karibia wote wa kata hizi hasa ile ya Elerai na Kaloleni ni machinga/wachuuzi wa biashara ndogondogo hapa mjini.Kwa hoja hii ni vigumu na haitawaingia wana wa arusha kupiga kura kwenye dole gumba manake kwa kufanya hivyo wanaamini wamemchagua adui yao kuwa kiongozi wao. Nne,Soko la NMC,Eneo hili linajulikana na National Milling Corporation nab ado ni la mali ya NMC ila lilichukuliwa kisiasa na kufanywa soko kwa nia ovu ya kuwanyima Chadema eneo la kukutana na umati wao mkubwa wa wananchi ambapo palikuwa eneo lao la kukutana pale wanataka kukutana na mbunge wao na/au viongozi wengine wa chama ngazi za juu.Eneo hili mimi nilikuwa shahidi baada ya Chadema mwaka jana kutaka kukutana na wanchi wake kwa nia ya kueleza yaliyokuwa yanajiri katika kesi ya Lema,palijengwa ndani ya usiku mmoja na kesho yake wamachinga wakatakiwa kuhamia huko.Ililazimika nguvu kubwa sana kuhakikisha eneo hili linageuzwa kuwa soko.Tatizo hapa CCM na RC wao walishindwa kusoma alama za nyakati.Chadema kwa uadilifu walitumia kete hii vizuri sana kupata uungwaji mkono kwani wao walikubali eneo hili kuwa moja ya maeneo ya wamachinga lakini lilikuwa nab ado linabaki kuwa si eneo salama sana kwa kuwa mvua ikinyesha maji yote machafu ya jiji yanatuama hapo.Lakini wakafaulu zaidi kwa kunasa mbinu za CCM katika kuwapatia maeneo ya kufanyia biashara kwa kuzingatia itikadi zao.Hii ilitokea pale ambapo wananchi walielezwa kwenda kujishikia maeneo wenyewe hali iliyosababisha wananchi kuumizana wenyewe kwa wenyewe wakigombania maeneo sokoni hapo.Lakini haikuisha muda ikaja orodha inayotoa majina ya machinga waliosajiliwa kwa mkuu wa wilaya/halmashauri kwamba tayari walikuwa wameshapewa baadhi ya meneo ambayo wananchi walikuwa wameshagawanywa.Baada ya wananchi kuyaona majina yale,wakabaini kuwa ni wamachinga wenzao lakini wanachama wa CCM na kwa hiyo wakaamini kuwa wao wanafukuzwa kwa kuwa ni wana wa CHADEMA.Katika hali hii kwa sisi wenye kuelewa siasa ni nini bila kujali itikadi zetu,ni ngumu sana kwa Mmachinga yeyote,au ndugu yake,au rafiki yake aliyepata kusikia kadhia hii kuipa kura CCM Manake kauli za kuwaondoa machinga mjini na kuwapeleka NMC ilikuwa kusafisha jiji.N a kwa maana hiyo Machinga ni uchafu,lakini leo watawala wanategemea uchafu huu huu uwapigie kura.Hapana,nasema hapana kwa kuwa hata kura kama hizo bado zitakuwa chafu tu.Haziwezi kamwe kusafishika!! Tano,rushwa na ufisadi uliokithiri halmashauri.Kwa mwaka mmoja tu katika jiji la arusha,kuna upotevu wa fedha kiasi cha Tsh.15 Billioni,katika hali hii wananchi wameelimishwa vya kutosha juu ya upotevu huu mkubwa na matumizi ya anasa ya fedha za walipa kodi maskini wan chi hii.Hakuna mwenye majibu ya fedha hizi isipokuwa Chama tawala na Meya wao Bw.Gaudence Lyimo,madiwani wa CCM na mkurugenzi wa Jiji.Wao CCM walidhani ni siri kwa kuwa wanaongoza halmashauri lakini CHADEMA kwa kutumia mtandao mkali walenasa ufisadi huo na wameelimisha vizuri wananchi na hasa namna fedha hizo zingetumika kuwasaidia kuondokana na umaskini,wameelimisha umma namna fedha zao zilivyochezewa,na wameonyesha mfano kwa kupiga marufuku michango ya madawati,chakula na michango ya ujenzi katika shule kwa kuwa fedha zipo nyingi halmashauri.Katika mazingira haya,hata kama ni kipofu ametumwa kwenda kupiga kura ataweka bayana kuwa ni wapi pa kupiga kati ya ukweli na uongo,kati ya nuru na giza.Matokeo ya kipindi hiki Arusha yatakifundisha somo moja kubwa CCM na watanzania kuwa wananchi wa sasa wanasikia na kufikiri sa sawa. Sita,siasa za matusi,majivuno,dharau na kejeli.CCM kwa mara nyingine wamefanya kosa kubwa kisiasa Arusha,Mwigulu Nchemba,Juliana Shonza na Mtela Mwampamba wamekuja Arusha kwa gia ya matusi,vijembe,kejeli na Mkwara.Kama vile hawana kumbukumbu kwamba kule Arumeru mashariki walitumia mbinu hii na kuadhibiwa vikali na wazee,vijana na wamama wa kimeru.Wamekuja kufanya mikutano waliyokuwa wanatukana wananchi wanaoipenda Chadema na Lema pamoja na viongozi wengine wa Chama hiki.Ukiachia mbali vijana hawa(Juliana na Mtela)Mwigulu ni msomi tena mzuri tu lakini sio wa siasa(isiwe tatizo).Ameshindwa kutumia Intelectual capacity yake kuwaomba kura wana Arusha badala yake akajikuta akishusha mitusi,lawama na kejeli kwa Chadema na Lema ambao kimsingi wanapendwa kuliko CCM hapa Arusha.Arusha kuna wacha Mungu,wapenda haki,wavuta bangi,wanywa viroba,wezi,majangili,watu wema na wengine kama ilivyo sehemu nyinginezo nchini na duniani.Unapokuwa jukwaani unatakiwa kufahamu diversity hii katika jamii na kutumia jukwaa vizuri kuwaunganisha watu hawa wote wakukubali wewe.Lakini ninaanza kuwa na wasi wasi na Elimu ya Mwigulu kushindwa kutumia elimu yake vizuri na inawezekana hata kupatikana kwa elimu hii kulikuwa na namna.Amekuja arusha kuonyesha mwananchi aliyemwagiwa tindikali katika uchaguzi wa Igunga(of which is past event)na kusema kuwa hiyo ni kazi ya Chadema.Inawezekana ikawa kweli lakini kufanya hivyo kwa Mwigulu ni sawa na kwamba sasa anaomba huruma ya wananchi.Inajulikana wazi nchi hii mtu akifanya kosa kama la kumwagia tindikali mtu anapelekwa mahakamani.Sasa kama utaratibu wa ndani ya chama na serikali inayoongoza Tanzania umebadilika ni vizuri Mwigulu Nchemba akaeleza wananchi na ni lini tulibadilisha katiba ikasomeka hivyo.Wananchi wa Arusha wanaelewa adui wao ni mmoja tu,CCM.Wanaamini huyundiye anayeweza kuwamwagia tindikali,ndiye anayeweza kuwakata mashoka,visu na mishale.Wanaamini ni huyu adui wao anayeweza kuwango’a kucha,macho,kope na hata meno bila ganzi.Hawaamini kamwe kama adui yao atakuwa CHADEMA Ambaye wamemwamini na kuishi naye kirafiki kwa miaka kadhaa sasa.Kwa hiyo,ujio wa akina Mwigulu Nchemba,Juliana Shonza na Mtela Mwampamba Arusha hakujainusuru CCM bali kumezidi kuwachimbia kaburi zaidi na kupunguza kura zao hadi kufikia namba ya kiatu. Saba,Kodi zisizo na mashiko katika masoko ya hapa Arusha mjini.Hapa mjini kuna masoko kadhaa kama vile Kilombero,Soko kuu,na mengineyo mengi.Sio wanaume wala wanawake wanaelewa utaratibu maalumu wa kozi zinazotozwa kwenye haya masoko.Kuna fedha zinakusanywa kwa wamama na wababa zisizo na maelezo.Haieleweki kwamba fedha hizo zinaenda wapi.Wakala anayekusanya anakanwa na serikali kwamba hawana mkataba,huku serikali nayo ikikusanya za kwake kwa utaratibu usio rasmi.Ikumbukwe kuwa kila unapokuwa unanunua bidhaa kwa bei ya jumla/rejareja kwa mtu tayari umelipa kodi,bado unaenda sokoni unalipia kodi ya eneo unapofanyia biashara(pango),hujapumzika anakuja wakala wa ushuru anataka ushuru wa kila siku(hauna maelezo),kama vile unataka kupumzika anakuja mwingine anataka ushuru wa usafi n.k.Katika hali hii ni kama vile tunaishi kwenye jiji lisilo na wenyewe.Wafanyabiashara wanatumika kama shamba la bibi.Wanasiasa wa upinzani hususani CHADEMA wamefanikiwa kuwaeleimisha wananchi namna wanavyotozwa kodi zaidi ya kumi na ndio maana sababu biashara hazisongi mbele kabisa.Wamewaelewa sana Chadema na tusishangae ushindi wa kishindo utakaofuata jumapili ya kesho kutwa.CCM hawana ubavu wala ujasiri wa kuondokana na dhambi hii kwa kuwa muda wa kurekebisha haya ulishapita nao ulikuwa kabla ya uchaguzi huu kutangazwa.Kwa sasa hawawezi tena.Kuna msemo kwenye Biblia unasema Kesheni kwa sababu hamjui siku wala saa atakapokuja Mwana wa Mungu”.CCM chukueni hiyo. Nane,matatizo ya vyuoni na ukosefu wa ajira.Haujaisha muda mrefu tangu zitokee vurumai hapa chuo cha Uhasibu Arusha.Katika sakata lile Mkuu wa Mkoa alijitoza kichwa kichwa na kumtuhumu Lema kuwa ndiye chanzo.Wote tulishuhudia na kwa kuwa lipo mahakamani na kwa kuwa mimi pia ni mwanasheria nisizungumzie sana hili.Lakini sheria hainizuii kuzungumzia athari za tukio lile kisiasa kwa kuwa sitaingila mwendelezo wa kesi(Legal Proceeding).Cd zimesambazwa mtaani na wananchi wa Arusha wameona namna mkuu wa mkoa na mbunge Lema walivyoenda Njiro.Kila mwenye macho anaona nani mwenye kosa kati ya Lema na Mulongo.Ni dhahiri kwamba hata watawala wameona namna ambavyo wamepata hasara ya kisiasa kwa kupambana na Lema badala ya kumtafuta muuaji wa mwanafunzi kule Njiro.Kama haitoshi huku mtaani na kwenye hizi kata kuna wanafunzi na ndugu wa wanafunzi wanaosoma Njiro.Wameapa kukiadhibu chama cha Mapinduzi kwa kura.Ajira ni tatizo linaloizika CCM sasa hapa nchini,vijana wengi wapo mjini hawana ajira,wanajaribu bahati zao sehemu mbalimbali na wengine wanafanya kazi ya siasa kwa kiwango cha hali ya juu.Vijana wanatoa elimu ya mageuzi ya kiutawala,kiuchumi na hata kijamii.Muda wote vijana wako kazini kuhakikisha wale watu wanaowatetea wao wanakuwa viongozi katika jamii.Wako mitaani kuhakikisha kuwa Chama ambacho kwao ni rafiki kinashika hatamu.Katika baadhi ya sehemu nilizotembelea hapa Arusha vijana wanaapa kwamba CCM kushinda uchaguzi huu ni sawa na matusi makubwa kwao,wazazi na walezi wao.Wameapa kukiangamiza chama hiki katika uchaguzi wa jumapili kwa kura.Wanajitolea kufanya kazi za siasa usiku na mchana na hawataki hata kujulikana na kupewqa nafasi wala heshima katika Chadema.Wameapa kwamba hata wakiokota shilingi mia au hamsini wataichangia Chadema ili ishinde uchaguzi huu.Kuna vijana walioko kazini nao wanatumia muda wao wanaoupata kuhakiksha kuwa wazee,wamama na vijana wanapata elimu ya kutosha kabisa kuchagua mabadiliko. Tisa,uwepo wa viongozi wa Chadema wenye ushawishi mkubwa,Kama chama kilicho serious na kazi zake,Chadema kinapanga mashambulizi kulingana na eneo mtu anakokubalika.Kuna maeneo ambayo Lema anapangiwa kwa sababu maalumu kama vile kata ya Temi,Elerai na kwingineko,lakini pia kuna maeneo yaliyotembelewa na Mbowe,Nassari,Natse, na viongozi wengine wenye ushawishi mkubwa.Ukiangalia kwa umakini utabaini kuwa Chadema kimetumia mbinu zaidi(Strategies)kukikaba Chama Cha Mapinduzi ambacho hadi sasa kimeshindwa kuwafikia wananchi wengi zaidi.Nasema haya kwa kuwa wakati CCM wamejinasibu kuwafikia wanachama na wananchi majumbani na hongo(rushwa) tena usiku,Chadema kinakwenda nyumbani kwa wananchi asubuhi na mchana na bila kubeba hongo yoyote,kinatembea hatua kwa hatua,kitongoji kwa kitongoji,mtaa kwa mtaa,kijiji kwa kijiji na hata kata kwa kata.Hii imefanikiwa kwa kuwa wanapendwa na wananchi kwa kuwa wanasema yale wananchi wanayoyapenda,hawako mbali na jamii wala hawaishi Dar na kusiemea arusha hapana,kila kukicha wako na wananchi kwenye shida na raha.Wameweza kugawana vizuri majukumu kati ya viongozi wenyeji,wageni na wananchi pamoja na wanachama wao na dalili hapa ushindi ni lazima. Kumi,Ulinzi wa kura wa hali ya juu,hadi naandika waraka huu,mbinu mbalimbali za wizi ambazo zimepangwa na CCM kushinda angalau kata moja kati ya nne zimenaswa na Chadema.Tayari tangia mwanzo wa kampeni wananchi wamekuwa wakielezwa mikakati ya CCM kuhujumu huu uchaguzi na kinachoonekana Chadema na Wananchi wamejipanga kikamilifu.CCM walipanga kununua kadi za kupigia kura na tayari wamenaswa,walipanga kuwanunulia viroba vijana wao na kuwavalisha mavazi na skafu za Chadema ili walete vurugu na kusingizia Chadema tayari wamenaswa,walipanga kuwajeruhi ama kuwauwa viongozi wa Chadema na wanachama walioonekana kuwa Mwiba kwao tayari wameumbuliwa na katibu wao wa fedha tayari amefunguliwa mashitaka ya kutishia na bunduki mbele ya OCD.Wamepanga mbinu nyingi na hapa sitasema zile ambazo hazijatajwa na viongozi wa Chadema manake hadi zipelekwe kwanza usalama ndio tuziseme hapa.Kwa sasa CCM wamerudisha silaha nyuma kujipanga manake juzi wamepita wakigawa sukari maeneo ya Ilboru ili wapewe kura,wamepita wakihonga kati ya 20000/= na 100000/= ili wauziwe kadi za kupiga kura.Kinachoshangaza ulimwengu ni kwamba wakati rushwa ikitembea waziwazi,Makao makuu ya TAKUKURU yapo kwenye kwenye kata mojawapo ya uchaguzi na sii nyingine bali ni kata ya Kaloleni.Hili bado linatuingiza Tanzania katika maajabu ya dunia.Mpango uliopo sasa na ambao tayari umekwama ni kwamba CCM wamejipanga kununua sukari nyingi siku moja kabla ya huu uchaguzi na kuichanganya na mchanga mweupe(kama sukari)Watavaa mavazi ya Chadema na watatumia sare na salamu za Chadema kuwagawia baadhi wa wapiga kura majumbani mwao wakisema ni Chadema inaomba kura.Sasa hii sukari lazima watakaogawiwa watapikia chai siku ya kura asubuhi,watakapokuta imechanganyikana na mchanga watailaumu Chadema na kuona kama imewakejeli na kwa hiyo hawataichagua Chadema.Hiyo ndiyo CCM bhana,wazee wa Intelligensia mpo hapo?Chadema wamefanikiwa kuwaelimisha sana wananchi kuhusu mbinu hizi na nyinginezo chafu.Na pia kupitia kanda ya kaskazini,Chadema wameagiza walinzi wa kura toka mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Manyara kwa nia ya kuimarisha ulinzi wa kura na uwakala.Hapa kazi inayoendelea sasa ni namna gani ya kulinda kura na si vinginevyo!! Nimeandika haya kwa muono wangu na uhalisia wa mambo ulivyo hapa Arusha.Kwa wale mliopo mbali na hapa msije mkasikia CCM wamepata kura sawa na namba ya kiatu mkafikiri ni bahati mbaya,hapana,wananchi wameamua na ni lazima wasikilizwe. Ni hayo tu

Halafu wee ni kijana nenda kasome jinsi ya uandishi Mzuri wa habari. Hata paragraph hujuwi? Wee ni CDM? Jifunze ndugu yangu acha kuandika riwaya ya KULI humu wakati uandishi hujuwi. Nipo tayari kukuchangia unatuabisha vijana wenzako. Kazi kuandika majungu na kushabikia Lichasema nenda kasome computer ndugu yangu
 
Ha ha ha ha ha ha haaaa ndugu yangu Shelui,kwa taarifa yako sikusoma kimagumashi kama wewe na shule zenu za kata.Ninayo elimu ya kumzidi Mwenyekiti wa CHAMA chako,Ni mwalimu pia wa Kompyuta tena kwa taaluma na experience,ninafahamu siasa kuanzia ya kule kwenu shelui hadi the great nations.Lakini usipoteze pia lengo na mada manake nyie ndio mnatumwa na wawakilishi wa Lumumba kuja kugeuza mada zinazowaumiza mwisho wa siku mnalipwa vibuku saba mnalala na kaubwawa tumboni
 
Halafu wee ni kijana nenda kasome jinsi ya uandishi Mzuri wa habari. Hata paragraph hujuwi? Wee ni CDM? Jifunze ndugu yangu acha kuandika riwaya ya KULI humu wakati uandishi hujuwi. Nipo tayari kukuchangia unatuabisha vijana wenzako. Kazi kuandika majungu na kushabikia Lichasema nenda kasome computer ndugu yangu

Wewe ndio mwehu una quote gazeti zima ni kwa nini usifute 90% halafu ukaacha jina la mleta uzi tukakuelewa? Inamaana gani kureplay kama ilivyo?
 
Umejitahidi kijana. Ila bado makwasukwasu yapo ktk post yako, lazima ujue wasomaji nao ni wafuatiliaji wa mambo haya.
 
MMassy that is a well detailed information,thank you sir , please MACCM munayafahamu yanapenda tukose wote kazeni boot
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom