CCM watakuja na gia gani 2020?

ibesa mau

JF-Expert Member
Sep 17, 2015
2,109
1,692
Kilichowapa mvuto ccm ni siasa za kumchafua mgombea wa ukawa kuwa ni mgonjwa na pointi ya pili mgombea huyo ni fisadi . Hii hoja ya ugonjwa ndio waliishikia bango sana. ..

Sasa watu wenye ufahamu tunajiuliza ikiwa Lowasa Mungu atamuweka hai hadi 2020 ile hoja ya ugonjwa ambayo iliwapa nguvu kwa 70% itakuwa haina nguvu tena. Lakini hoja ya pili ya ufisadi ambayo ilihubiriwa sana kwamba mahakama ya kifisadi itamfunga Lowasa na mpaka sasa imeshaonekana dhahili uwezekano wa kumfungulia mashtaka Lowasa haupo , hoja hiyo nayo itakuwa imekwisha nguvu.

Je unafikiri ccm wanaweza kuwini influence kwa mbinu gani.
 
Wataendelea kuiba kura kama walivyozoea.

Hata wasipopiga kampeni kabisa na uchaguzi ukafanyika, lazima washinde.

Tume yao, polisi lao, jeshi lao, bunge lao, mahakama yao.
 
Wapinzani washughulikie mambo ya msingi kabla ya hiyo 2020 ambayo ni Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Wakiweza hivyo, wategemee ushindi wa kishindo.

Wasipofanya hayo, hata hao wabunge waliowapata watapotea wote..
 
Wataendelea kuiba kura kama walivyozoea.

Hata wasipopiga kampeni kabisa na uchaguzi ukafanyika, lazima washinde.

Tume yao, polisi lao, jeshi lao, bunge lao, mahakama yao.
HATA WASIPOSHIRIKI UCHAGUZI WAO KUSHINDA NI 22/7
 
Tumeweka mazingira mazuri ya wawekezaji kujenga viwanda, tupeni nafasi tuvijenge sasa
 
Mkurugenzi wa tume si ameshateuliwa? Hiyo ndo kazi ya ccm......Tunaulizana maswali mengi wkt tumeona kinachofanyika zenji chaguzi 3 zilizopita na yanayofanyika zenji yote yanaratibiwa bara
 
Kilichowapa mvuto ccm ni siasa za kumchafua mgombea wa ukawa kuwa ni mgonjwa na pointi ya pili mgombea huyo ni fisadi . Hii hoja ya ugonjwa ndio waliishikia bango sana. ..

Sasa watu wenye ufahamu tunajiuliza ikiwa Lowasa Mungu atamuweka hai hadi 2020 ile hoja ya ugonjwa ambayo iliwapa nguvu kwa 70% itakuwa haina nguvu tena. Lakini hoja ya pili ya ufisadi ambayo ilihubiriwa sana kwamba mahakama ya kifisadi itamfunga Lowasa na mpaka sasa imeshaonekana dhahili uwezekano wa kumfungulia mashtaka Lowasa haupo , hoja hiyo nayo itakuwa imekwisha nguvu.

Je unafikiri ccm wanaweza kuwini influence kwa mbinu gani.
Tatizo sio kuwa hai,bali ni uwezo wa kufanya mambo magumu kama Rais, tumeona tu kwenye kampeni amefanya mikutano mingapi, na akiongea anaongea dakika mbili tu, Mara aseme a agombea ubunge, hicho ndio cha kukiwaza, je 2020 atakuwa fit kiasi gani kupambana na JPM ambae tayari atakuwa na uzoefu wa kutosha wa ikulu na kupambana na wapinzani wake?, think big, sio mnashangilia tu. Je kwa wakati huo nchi irakuwa imepiga hatua kiasi gani kimaendeleo ili tupate cha kuongea na wananchi?, je tutaendelea kubaki na wafuasi hawa walituunga mkono mwaka 2015 au watakuwa wamebadili muelekeo baada ya kuona hatuna jipya?
 
Haina haja ya kubadili gia wala nini mwendo ni ule ule hatujafikia hatua ya kuwapa watu nchi wafanyie majaribio fanyeni mambo mengine ikulu ni baada ya miaka 50 mbele ndiyo wapinzani mtakuwa mmejitambua na kujua watanzania sio wa kuburuzwz
 
Shaka letu kubwa ni nani atagombea Urais Ukawa? Maana EL mradi wake wa kugawa hela umeisha na Mbowe anawaza atapiga hela kwa nani awamu hii.
Kilichowapa mvuto ccm ni siasa za kumchafua mgombea wa ukawa kuwa ni mgonjwa na pointi ya pili mgombea huyo ni fisadi . Hii hoja ya ugonjwa ndio waliishikia bango sana. ..

Sasa watu wenye ufahamu tunajiuliza ikiwa Lowasa Mungu atamuweka hai hadi 2020 ile hoja ya ugonjwa ambayo iliwapa nguvu kwa 70% itakuwa haina nguvu tena. Lakini hoja ya pili ya ufisadi ambayo ilihubiriwa sana kwamba mahakama ya kifisadi itamfunga Lowasa na mpaka sasa imeshaonekana dhahili uwezekano wa kumfungulia mashtaka Lowasa haupo , hoja hiyo nayo itakuwa imekwisha nguvu.

Je unafikiri ccm wanaweza kuwini influence kwa mbinu gani.
 
Back
Top Bottom